Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Nipo Saudi Arabia. Nchi ya kiislamu ambayo ndipo ndugu zetu waislam wanakuja kutimiza moja ya nguzo kuu za uislamu.
Habari ya mji hapa ni mji wa kisasa wa kiteknolojia na starehe unaojengwa kutokana na mawazo ya Prince Mohammed Bin Salman ambaye hapa Saudi yeye ndo Crown Prince yaani Mkuu wa Serikali (Waziri Mkuu). Mji huu unaitwa Neom.
Mji huu unajengwa kuwa mji wa kipekee wa starehe na teknolojia na ndani yake kutakuwa na mahoteli makubwa, Casinos, Parks na Artificial Beach kwa ajili tu ya kuvutia watu kwenda kufanya starehe. Ndani ya mji huu mtu utakuwa huru kustarehe unavyotaka yeye na hakuna cha hijabu wala mavazi ya staha.
Dhumuni la Saudia kujenga mji huu ni kukuza utalii. Na wanategemea kuingiza trillions of money kupitia watu watakaoenda kutembelea mji huu kwa ajili ya kufanya starehe tu.
Hapa Tanzania tuna jiji linaitwa Dar es Salaam. Kwa takwimu za viwanja vya ndege sasaivi utalii umeshuka sana na kiwanja cha ndege cha Dar ndo cha mwisho kwa kupokea watalii saivi kikiwa nyuma na Uwanja wa Zanzibar na KIA. jiji hili pamoja na kuwa na fukwe nzuri za kutosha na maeneo mengi ambayo yangetumika vizuri ila bado hatujaona jitihada zozote za Serikali katika kulifanya kuwa kama Jiji la kipekee.
Kituko zaidi ni unapogundua sisi ujinga ndo unatufanya kuwa maskini kupitia matamko yanayotolewa na Viongozi wa Serikali.
Juzi Mkuu wa Mkoa wa Dar Chalamila ametoa maelekezo ya kufungiwa sehemu za massage. Huu ni uthibitisho kuwa ngozi nyeusi tuna shida katika kufikiri kwetu.
Pamoja na mkoa wake sasa kuzidiwa na Zanzibar badala apambane kutumia ubunifu kulifanya jiji lake kuw na sifa ya kuvutia wageni wengi zaidi ili kuongeza mapato yeye anapambana kufungia sehemu za massage. Hawajui inawezekana wakaja watu hapa Tanzania na Dar kwa sababu tu ya hizo sehemu za massage na kuongeza idadi kubwa sana ya Watalii.
Ushamba na Ujinga wetu uko kwenye sisi kujiona na tuna maadili na dini kuliko jamii nyingine. Na tunajiona pia kama sisi ndo tunamjua Mungu kuliko watu wengine. Na kwa ushamba huu tumejikuta tunaifanya nchi yetu kutokufanya mambo ambayo yanaweza kuihakikishia nchi kupata mapato mazuri na kufanya maendeleo kwa wananchi.
Napenda kumaliza kwa Kusema tuna safari ndefu sana.
Lord Denning
Saudi Arabia
Habari ya mji hapa ni mji wa kisasa wa kiteknolojia na starehe unaojengwa kutokana na mawazo ya Prince Mohammed Bin Salman ambaye hapa Saudi yeye ndo Crown Prince yaani Mkuu wa Serikali (Waziri Mkuu). Mji huu unaitwa Neom.
Mji huu unajengwa kuwa mji wa kipekee wa starehe na teknolojia na ndani yake kutakuwa na mahoteli makubwa, Casinos, Parks na Artificial Beach kwa ajili tu ya kuvutia watu kwenda kufanya starehe. Ndani ya mji huu mtu utakuwa huru kustarehe unavyotaka yeye na hakuna cha hijabu wala mavazi ya staha.
Dhumuni la Saudia kujenga mji huu ni kukuza utalii. Na wanategemea kuingiza trillions of money kupitia watu watakaoenda kutembelea mji huu kwa ajili ya kufanya starehe tu.
Hapa Tanzania tuna jiji linaitwa Dar es Salaam. Kwa takwimu za viwanja vya ndege sasaivi utalii umeshuka sana na kiwanja cha ndege cha Dar ndo cha mwisho kwa kupokea watalii saivi kikiwa nyuma na Uwanja wa Zanzibar na KIA. jiji hili pamoja na kuwa na fukwe nzuri za kutosha na maeneo mengi ambayo yangetumika vizuri ila bado hatujaona jitihada zozote za Serikali katika kulifanya kuwa kama Jiji la kipekee.
Kituko zaidi ni unapogundua sisi ujinga ndo unatufanya kuwa maskini kupitia matamko yanayotolewa na Viongozi wa Serikali.
Juzi Mkuu wa Mkoa wa Dar Chalamila ametoa maelekezo ya kufungiwa sehemu za massage. Huu ni uthibitisho kuwa ngozi nyeusi tuna shida katika kufikiri kwetu.
Pamoja na mkoa wake sasa kuzidiwa na Zanzibar badala apambane kutumia ubunifu kulifanya jiji lake kuw na sifa ya kuvutia wageni wengi zaidi ili kuongeza mapato yeye anapambana kufungia sehemu za massage. Hawajui inawezekana wakaja watu hapa Tanzania na Dar kwa sababu tu ya hizo sehemu za massage na kuongeza idadi kubwa sana ya Watalii.
Ushamba na Ujinga wetu uko kwenye sisi kujiona na tuna maadili na dini kuliko jamii nyingine. Na tunajiona pia kama sisi ndo tunamjua Mungu kuliko watu wengine. Na kwa ushamba huu tumejikuta tunaifanya nchi yetu kutokufanya mambo ambayo yanaweza kuihakikishia nchi kupata mapato mazuri na kufanya maendeleo kwa wananchi.
Napenda kumaliza kwa Kusema tuna safari ndefu sana.
Lord Denning
Saudi Arabia