Inauma: 'Alisema tusimpige picha'... Angesema mvue nguo!!

Inauma: 'Alisema tusimpige picha'... Angesema mvue nguo!!

Kwanza mimi naona aibu kuwachukulia walioshiriki katika press conference hiyo kama "waandishi wa habari" They are nothing but MAKANJANJA!!! Kwa sababu kupiga picha ni moja kati ya njia muhimu sana za ukusanyaji habari!!!! They say a picture can speak a thousand words!!! Leo hii jitu linawaambia msipige picha na wao wanakubali kirahisi!!!.... Hivi kweli wewe ni mkulima halafu mtu anakuambia njoo shamba lakini ukifika usipalilie.... kuna ujinga kama huo!!! What's the point in going????!!!! Hamna kitu Makanjanja hayo!!!!....
 
Hoja nzuri ila imeletwa na wrong person ambaye credibility yake inayoyoma. Na ungeendelea tu kidogo ungeishia kusema hao waandishi wa habari ni CDM! Poor Waberoya!
Acha siasa za maji taka wewe!
Tunaongelea maswala ya msingi unaleta bifu zako za kisiasa hapa. nani kaongelea CCM na CDM hapa?
Au na wewe ni mmoja wao nini? Viumbe wengine wanaboa sana! you included.
 
I was shocked niliposoma hiyo habari. Yaani mtu kawaambia wasimpige picha, yaani kawaambia cha kufanya, halafu kesho yaake ile habari ilikuwa ndo leading headlines katika magazeti ya wote waliohudhuria hicho wanachoita press conference. Mie naamini hata hiyo press conference haikuwepo ila walipewa tu habari ya kuandika wakaambiwa "kaandikeni hivi".

Ilikuwa haiingii akilini kwamba watu hawa hawa wanaojiita mhimili wa nne ndo hao hao walioambiwa wazime kamera kwanza kabla ya kuingia kwenye hicho chumba kinachoitwa chumba cha conference room. Aaa hapa ni kulambishwa tu. Ufisadi naona ni mkubwa kuliko tunavyofikiria!

Naona yule aliyesema "ni heri kuishi nchi isiyo na serikali ila yenye vyombo huru vya habari, kuliko kuishi kwenye nchi yenye serikali bila vyombo huru vya habari" hakukosea.

Kwa hili vyombo vyote vya habari vilivyoingizwa mkenge huu, lazima tuviangalie mara mbili. Hakuna la kujibaraguza!
 
upupu,tafuta lingine la kusema!mnakera na ma-thread ya kijinga!

Ana hoja tena ya msingi kwelikweli waandishi wanaambiwa wasipige picha nao wanakubali wangetoka nje. Tatizo wengi walikuwa wa type ya Kibonde.
 
Hoja nzuri ila imeletwa na wrong person ambaye credibility yake inayoyoma. Na ungeendelea tu kidogo ungeishia kusema hao waandishi wa habari ni CDM! Poor Waberoya!

Sijawahi kuwa na credibility inayo yoyoma inatokea wapi, kumbe unapenda credibility? mpaka sasa mimi ni ghost unawaza credibility! ya kwako ngapi ili ikianza kushuka tujue inashuka kwa kasi kiasi gani? hao uliowaita hawana credibility wana supporters kibao, bahati mbaya sina credibility ya kufuata mikumbo,so usinipendelee kwa kusema inayoyoma sina KABISA and am proud of that!
 
Hao si waandishi bali makuwadi wa mafisadi, jamani jamani bahasha hizo zitaliangamiza taifa letu.
 
Ukombozi/uhuru utakamilika pale tu utumwa wa fikra utakapoisha!
Safari bado inaendelelea kutoka utumwani.

Well said! na utumwa huu wa fikra sio kwa wakoloni wazungu tu, bali hawa weusi na waarabu, wahindi na wachina! mwenye fedha Mungu mtu, anaweza kusema lolote lile, kama hili limefanywa na waandishi je, mapolisi, ma-nurse, wanajeshi na waalimu wanafanya hayo kwa mapana kiasi gani? na taifa letu linaathirika kiasi gani
 
Tena inawezekana walidharirishwa na kusachiwa kama vile wanataka kupaa.

Baada ya tukio hili nimeanza kujiuliza waandishi wa UWAZI,IJUMAAA na hawa wa haya magazeti tunayotegemea nani mwenye akili zaidi

jibu ijumaa uwazi wanaongoza wengine wengine wanafuata
 
Tena inawezekana walidharirishwa na kusachiwa kama vile wanataka kupaa.

Baada ya tukio hili nimeanza kujiuliza waandishi wa UWAZI,IJUMAAA na hawa wa haya magazeti tunayotegemea nani mwenye akili zaidi

jibu ijumaa uwazi wanaongoza wengine wengine wanafuata

Sure magazeti ya 'udaku' yanaonyesha yana waandishi bora sana kuliko haya magazeti ya wenye 'akili'
 
nawashangaa sana wanaosema hii thread ni ya kijinga na haina maana, ina lots of sense. sijui watu tuna matatizo gani kama tunashindwa kuelewa anachokisema waberoya hapa.
 
Upo sahihi kabisa Waberoya, hawa waandishi wetu wameonyesha udhaifu mkubwa sana, mbaya zaidi eti ni wahariri!!!!
 
Wlipewa meeting alowance ndiyo maana..! Nasikia waliopiga kamera zao ziliporwa na picha kufutwa. Shame on you
 
nawashangaa sana wanaosema hii thread ni ya kijinga na haina maana, ina lots of sense. sijui watu tuna matatizo gani kama tunashindwa kuelewa anachokisema waberoya hapa.


ukisoma heading tu unajua ujumbe mzito alionao mtoa mada. kwani wangempiga picha angewafanya nini? yaani tapeli atoke zake india aje kuchimba mkwara tanzania, na bado mwandishi anajishebedua kuandika eti nilikatazwa kupiga picha!?

nahisi wahariri nao wana mgawo wao huko kwenye mabilioni ya JK (sorry Dowans)
 
nawashangaa sana wanaosema hii thread ni ya kijinga na haina maana, ina lots of sense. sijui watu tuna matatizo gani kama tunashindwa kuelewa anachokisema waberoya hapa.
Huenda ndio haohao waandishi na wahariri waliokutana na huyo al-haradai.
 
Alafu kesho yake wanaenda kumuwinda pale Tanesco, alipokuwa mbele yenu mkashindwa..shame shame shame..hawa ndio wasaliti wakubwa..wanajiita mhimili wa nne lakini mafedhuli na wala rushwa tu.. RA aliwakatia MSHIKO wasilete za kuleta hapa.
 
Webs!

Nakuunga mkono kwa hili tupo pamoja kabisa. Watu hawa wahariri wa magazeti ni watu wa ajabu sioni tofauti na wasaliti ama yule Chifu Mangungo wa Usagara! Kuna watu makini sijui ni umasikini wa akili, Ngoja nimtafute Bakari Machumu wa Citizen nijue ameuguwa lini ugonjwa wa akili. Wangekuwa wahariri wa habari leo, Uhuru ama Daily News nisingalikuwa na wasi wasi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom