Inasikitisha: Hali ya miundombinu baadhi ya majengo Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja, Zanzibar

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
1695239767379.png
Awali niliona uzi humu JF kuhusu Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja iliyopo Unguja, Zanzibar, sikuamini kama ni kweli, lakini juzi(Novemba 13, 2023) nilifika hospitalini hapo ukweli ni kuwa hali ya miundombinu katika baadhi ya maeneo si nzuri.

Nilishindwa kupiga picha lakini miundombinu mingi haipo sawa kwa maana ya ubora, vitu vingi vinaonekana vimechoka, ni kama vile hospitali imetelekezwa.

Mbali na huduma nyingine kuendelea kama kawaida kwa maana ya Watoa huduma kufanya shughuli zao na kusafisha mazingira kwa kufagia lakini wanaangushwa na miundombinu ambayo imechoka, kuanzia kwene ukuta, viti na vifaa vingine mbalimbali.

Pia sehemu ya vyoo nako hali si nzuri, mabomba na miundombinu mingine ipo hoi.

Hivi viongozi wetu wako wapi? Hawajui hiki kinachoendelea au wanafanya makusudi? Serikali ya Zanzibar ifanye kitu katika hili.

Hela zinazotolewa na Serikali kuboresha na kuendesha Taasisi hiyo zinaelekea wapi? Nani anahusika na jukumu la kuangalia ubora wa miundombinu na vifaa? Hatua zichukuliwe.

Sehemu ya kutolea huduma ya afya nayo inakuwa si salama kwa afya.

Pia soma: Inasikitisha: Tazama hali ya miundombinu Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja, Unguja, Zanzibar
 
Kuna taarifa nilisikia wataboresha ubora wa majengo but sadly mpaka sasa kupo vile vile yani 0 progress.

Na hapo hospitali inapakana na ikulu. Bado viongozi hawaoni? Inasikitisha kwa kweli!

Ukiingia ndani ya hosp kwenye department moja moja ndio balaa, vifaa muhimu vimekua aghalabu. How come ICU inakosa kifaa cha kupima ABG?
Ukizunguka mawodini, monitors ni za kuazima..

Mimi nilipita tu lakini nilichokiona ni kwamba serikali inachukulia mazoea, yani business as usual. Lakini mambo hayako hivyo, viongozi wanahitaji kubadilika.
 
Back
Top Bottom