JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Kocha huyo raia wa Ubelgiji ambaye pia amewahi kuzifundisha Free State Stars na Polokwane City za Afrika Kusini, Oktoba 2022 alishinda kesi ya kuvunjiwa mkataba na Yanga bila kufuata utaratibu.
Klabu ya Yanga ilipewa maelekezo ya kumlipa Kocha huyo jumla ya dola za Marekani 152,000 kufuatia kumfuta kazi pasipo kufuata taratibu miaka miwili iliyopita.
Baadae klabu ya Yanga ilipanga kulipa kiasi hicho kwa awamu tano (5) ambapo awamu ya kwanza alipaswa kuwa Oktoba 2022.
Kwa mujibu wa FARPost, Yanga ililipa deni hilo kwa awamu mbili, Oktoba na Novemba 2022.
Kwa maana hiyo, Yanga bado wanadaiwa na Eymael dola za Marekani 99,000 pamoja na ada ya adhabu ambayo ni dola za Marekani 5,000.