Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Klabu ya Young Africans iliyo Ligi Kuu ya NBC imefungiwa kusajili mpaka itakapomlipa mchezaji Gael Bigirimana.
Uamuzi huo umefanywa na Shirikisho la Kimataifa la Mira wa Miguu (FIFA) baada ya mchezaji huyo kushinda kesi ya madai dhidi ya klabu hiyo.
Birigimana alifungua kesi FIFA kuhusiana na malipo ya ada ya usajili (sign on fee).
Klabu hivo ilitakiwa iwe imemlipa ndani ya siku 45 tangu uamuzi huo ulipotolewa, lakini haikutekeleza hukumu hiyo.
Wakati FIFA imeifungia klabu hiyo kufanya uhamisho wa wachezaji kimataifa, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeifungia kufanya uhamisho wa ndani.
TFF inazikumbusha klabu kuheshimu mikataba ambayo zimeingia na wachezaji pamoja na makocha ili kuepuka adhabu mbalimbali ikiwemo kufungiwa kusajili.
Iwapo klabu inataka kuvunja mkataba na mchezaji au kocha, inatakiwa kufanya hivyo kwa kuzingatia taratibu.
===
Pia soma
Yanga yafutiwa adhabu ya kutosajili baada ya kumlipa Bigirimana