Ubinadamu unatangulia dini. Hivyo watu wote tuko sawa kama binadamu. Dini ni uamuzi wa mtu. Mimi kama ni muislamu huo ni uamuzi wangu binafsi, labda na familia yangu. Na mkristo ni uamuzi wake binafsi labda na familia yake. Hivyo ninarudia, kama kuna mkristo au muislamu amevunja sheria za nchi, ambazo zinatuunganisha bila kuzingatia itikadi za kidini, ni lazima sheria ichukue mkondo. Kama polisi wamefanya makosa katika utekelezaji wa sheria, huyo muadhirika ni lazima atetewe, lakini sio kwa kuingiza udini ndani. Ninasisitiza kama huyo mtuhumiwa wa ugaidi ameteswa na kusababisha kifo hilo ni kosa la hao polisi na hakuna mpango wa kuuwa waislamu. Acheni kuleta uchochezi wa kidini hapa jamvini. Tujadili maendeleo na kila mtu ana haki ya kufuata dini anayotaka na hakuna sababu ya kuita binadamu wenzio makafiri.
Nijibu kama sio mkakati kwanini wanao uliwa na kuteswa na kulawitiwa wawe waislam tu ? Kwa nini yule mkristo aliekamatwa red hand wakati kanisa lilipo ripoliwa arusha hakuteswa wala kuuliwa ?
Kwa nini ponda ananyimwa dhamana kwa kesi za madai bakwata?
Kwanini masheikh wale wa zanzubar wakamatwe znz waje kuteswa bongo na kufanyiwa ushenzi ?
Kwanini yule Sensei apigwe risasi za tumbo akiwa chini ya ulinzi wa polisi?
Waislam ni watanzania wana haki sawa kama mtanzania mwengine. Mtuhumiwa wowote ni innocent mpaka atapotiwa hatiani hii ni kwa mujibu wa katiba yetu na ni haki ya kila Mtanzania.
Lakini kwa nini watuhumiwa hawa waislam wa ugaidi polisi wanawahukumu kifo kabla ya kutiwa hatiani ?
Wwislan ni binaadamu tuna hisia na pia kila muislam inamuuma kuona haya mambo yanaendelea na kuna wakristo wengi wanafurahia polisi wanapo vunja haki za msingi za raia wa waislam.
Hali hii sio ya kujivunia katika nchi yenye tabaka mbili kubwa za dini.
Ni vitendo vya kukemewa .
Raia yoyote akiuliwa na polisi akiwa chini ya uamgalizi wao ni lazima ifanyike inquest kujua chanzo cha kifo chake.
Na inawezekana kuwa serikali haina sera hii chafu dhidi ya raia wake lakini tunatilia shaka na vikosi vya kupambana na waislam a.k.a ugaidi kuwa vimeingiliwa na mataifa yenye chuki za kuupiga vita uislam.hawa wamepewa mafunzo marekani au na instructors wa huko na hawa hawana nia nzuri na hawapendi nchi hizi zitulie hivyo kuna shaka vikosi hivi baadhi ni moles na ni double agents . Wanafanya kazi ya kuwagombanisha watanzania kutumia dini kwa kuua waislam japo low targets ili kupandisha hasira.
Tuangalie kenya leo imefika wapi hawana raha wako sawa na somali tu.
Marekani walishindwa kuzuia ugaidi mkubwa kufanywa ndani ya nchi yao sio mara moja wala mbili leo wao ndio wawe walimu ? Tafakari