Ubinadamu unatangulia dini. Hivyo watu wote tuko sawa kama binadamu. Dini ni uamuzi wa mtu. Mimi kama ni muislamu huo ni uamuzi wangu binafsi, labda na familia yangu. Na mkristo ni uamuzi wake binafsi labda na familia yake. Hivyo ninarudia, kama kuna mkristo au muislamu amevunja sheria za nchi, ambazo zinatuunganisha bila kuzingatia itikadi za kidini, ni lazima sheria ichukue mkondo. Kama polisi wamefanya makosa katika utekelezaji wa sheria, huyo muadhirika ni lazima atetewe, lakini sio kwa kuingiza udini ndani. Ninasisitiza kama huyo mtuhumiwa wa ugaidi ameteswa na kusababisha kifo hilo ni kosa la hao polisi na hakuna mpango wa kuuwa waislamu. Acheni kuleta uchochezi wa kidini hapa jamvini. Tujadili maendeleo na kila mtu ana haki ya kufuata dini anayotaka na hakuna sababu ya kuita binadamu wenzio makafiri.