Imaging Africa kitendo chenu cha kukata miti usiku Bamaga Mwenge ni cha kihuni, na ni uharibifu wa mazingira, hakikubaliki

Aug 15, 2022
19
46
Kampuni ya matangazo ya Imaging Africa usiku wa jumamosi tarehe 24.06.2023 walifanya uharibifu mkubwa wa kimazingira kwa kukata miti iliyooteshwa pembezoni mwa barabara.

Imaging Africa imefyeka miti hiyo ambayo hawakushiriki kuiotesha wala kuitunza.

Wamefyeka miti ili ubao wao wa matangazo ya biashara uonekane. Ubao huu wameufunga mwaka huu, lakini miti hii ina miaka isiyopungua mitatu.

TREE OF LIFE FOUNDATION tunakemea vikali kitendo hiki, na tunawaonya Imaging Africa waache mara moja vitendo vya ukataji miti kwani ni ukatili dhidi ya mazingira yetu.
 
Kampuni ya matangazo ya Imaging Africa usiku wa Jumamosi tarehe 24.06.2023 walifanya uharibifu mkubwa wa kimazingira kwa kukata miti iliyooteshwa pembezoni mwa barabara.

Imaging Africa imefyeka miti hiyo ambayo hawakushiriki kuiotesha wala kuitunza.

Wamefyeka miti ili ubao wao wa matangazo ya biashara uonekane. Ubao huu wameufunga mwaka huu, lakini miti hii ina miaka isiyopungua mitatu.

TREE OF LIFE FOUNDATION tunakemea vikali kitendo hiki, na tunawaonya Imaging Africa waache mara moja vitendo vya ukataji miti kwani ni ukatili dhidi ya mazingira yetu.
 
Aibu kubwa sana hii kwa kampuni kubwa ya matangazo. Kampuni kubwa ziko busy na utunzaji wa mazingira hawa ndio wanaharibu.

Hebu wajulisheni NEMC wawawajibishe japo kidogo
 
uttoh2002, miti inekatwa Jumamosi usiku, je ni manispaa gani hufanya shughuli zake usiku?

Tayari tumewajulisha wenzetu wa Baraza la Mazingira NEMC na pia leo jumatatu tutaonana na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kinondoni.
 
uttoh2002, miti inekatwa Jumamosi usiku, je ni manispaa gani hufanya shughuli zake usiku?

Tayari tumewajulisha wenzetu wa Baraza la Mazingira NEMC na pia leo jumatatu tutaonana na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kinondoni.
Mkurugenzi kabariki hayo,washachukua hela ya bango,sema wanatambua ni kosa ndiomaana wamekata usiku 🙏
 
Tuambieni kwamba munawashtaki,miti tunapanda kwa kujitolea,tunamwagilia kwa vidumu kama wanafunzi wa kata,leo wao wanakata bila kupanda mbadala,tena hata mbadala wanapaswa wasubiri ikue au wapande mikubwa waipepelee,ebo!.
 
Kasumba ya kuleta info za kufikiria imekuwa sugu.

Picha ingesindikiza ama kutujengea imani kuwa uyasemayo ni kweli. Inawezekana wamefyeka matawi kama wafanyavyo chama cha siasa cha Tanesco ambapo miti itaendelea kukua.

Mimi nipo Igunga huku, naithibitishaje taarifa yako?
 
Back
Top Bottom