Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Huwa nawaza sana tulifikaje hapa tulipo leo,

Hivi ilikuwaje taifa lenye wasomi wazuri kabisa likaamua kufanya maamuzi ya kipumbavu ambayo hata Waroma wa kale walioishi miaka 2000 iliyopita wasingeyafanya. Hivi katika maksudi kabisa, taasisi nyeti za Tanzania ziliamini kabisa kwamba wao wangeweza kuifanya Tanzania nchi tajiri bila kushirikiana na dunia : Hivi ilikuwaje kabisa wataalamu wetu ambao wameenda shule, wanafahamu mifumo ya dunia ya kiuchumi, kiulinzi na kisiasa na wako kule USALAMA, BENKI KUU na MAMBO YA NJE wakakubaliana na huu upumbavu na kuanza kuutekeleza kabisa?

Mpangilio wa dunia yetu ya sasa uliwekewa msingi mwaka 1814 kule Vienna baada ya miaka 25 ya vita za mfalme Napoleon Bonaparte. Mwanamfalme Von Matternich alifahamu kabisa ili dunia isirudie kuingia kwenye songombingo la vita au kadhia yoyote ile, basi ni lazima watengeneze mfumo ambao uko kama utandu wa bui-bui: Kwamba maamuzi ya nchi moja yakifanyika lazima yaathiri nchi zote, hivyo nchi lazima zikubaliane kwenye baadhi ya mambo muhimu yanayowagusa wote. Ndiyo nadharia ya MZANI WA NGUVU (Balance of Power) ikazaliwa.

Mfumo wa dunia ya yetu hii tunayoishi leo hii umejengwa na matukio yaliyotokea miaka ya 1913, 1914, 1918, 1920, 1927, 1928, 1933, 1935, 1939, 1941, 1944, 1945, 1947, 1948, 1971 na 2001 . Kiufupi mlolongo wa matukio haya yafuatayo ndiyo yanatoa mwelekeo mzima wa mwenendo wa dunia yetu ya leo : Nashauri tufanya utafiti wa ndani kuhusu hili.

Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.

Mtaalamu yoyote yule wa Uchumi, Diplomasia, Ulinzi na Sheria ni lazima afahamu fika kuhusu haya ninayoyasema hapa. Kwamba dunia nzima tuko ndani ya utandu moja wa bui-bui. Huwezi kufanya jambo lolote lile ukiwa nje ya hapo. Ndani ya huu utandu wa bui-bui kuna kila aina ya watu: Wema na wabaya, Huru na watumwa, Masikini na tajiri, Wenye matumaini na wasio na matumaini, Wababe na dhaifu na Waamini Mungu na Maadui wa Mungu.

Huu ndiyo mfumo wa dunia (The World Order), huwezi kufanya maajabu yoyote yale ukiwa nje: Hata mataifa makubwa yenye nguvu duniani yanaheshimu huu mfumo kwasababu yanafahamu siku mfumo huu unaharibika basi ndiyo utakuwa mwisho wao. Hivyo kuna baadhi ya sheria hata yenyewe yatazifuata tu kwasababu zina manufaa kwao. Mwandishi George Orwell kwenye The ANIMAL FARM aliwahi kusema "All animals are equal, but some are more equal than others" hivyo hata kama tunataka usawa kuna wale waliotutangulia watakuwa mbele yetu kwenye baadhi ya mambo tu.

Sasa kinachoumiza wasomi wa Tanzania wenye PhD za sheria, uchumi na diplomasia. Huku wengine wakiwa na shahada kwenye masomo ya ulinzi, usalama na sayansi za vita wakiwa na akili timamu kabisa, wakaamua kuwa wapumbavu. Wakatundika elimu zao nyuma ya milango na kuanza kutekeleza jambo ambalo hata watu wa kale walioishi miaka 2000 hawakuwahi kuliwaza. Tanzania ina matatizo mengi, lakini ilikuwa inarekebishika vizuri tu kwasababu waliofikisha nchi yetu hapa wanafahamika na tunakula na kunywa nao kila siku.

Kuanza kulaumu mabeberu peke yake haisaidii kwasababu kuna wenzetu ambao wamefanikiwa kutumia mifumo hii-hii ya mabeberu kuwashinda mabeberu kiuchumi, kiulinzi na kisiasa. Ukweli ni kwamba huu mfumo umejengwa na mabeberu lakini hata walioujenga hawaundeshi wanavyotaka wao. Mataifa ya Magharibi ndiyo waanzilishi wa World Trade Organization (WTO) lakini leo hii, WTO imemnufaisha Uchina kuliko tangu alivyojiunga nao mwaka 2001 na mpaka sasa wanajutia kumkaribisha.

Nchi kama Singapore, India, Korea-Kusini na Brazil wamewezaje kucheza vizuri kwenye huu mfumo wa mabeberu hadi kufikia kuwango cha kuwashinda mabeberu kwenye baadhi ya mambo ??? Inahitaji akili ya ziada kutoka kwa Mungu ili kuweza kucheza kwenye huu mfumo. Raisi Donald Trump alijaribu kuitoa Marekani kwenye huu mfumo wa Vienna, lakini pamoja na maguvu yote ya Marekani alifanikiwa ???

Lakini leo hii kuna watu wako ndani ya IDARA ZA USALAMA ZA TANZANIA waliamini kabisa kwamba Tanzania inaweza kujitenga na dunia bila kupata madhara. Yaani waliamini kabisa na wengine bado wanaamini kabisa. Kuna wengine bado wanaamini kwamba mfumo wa Kileninisti na Kimaksisti (Marxist-Leninism) unaweza kutumika kuikomboa Tanzania. Sawa, lakini hata walioutuletea huu mfumo Warusi na Wachina, wamebadilisha sana baadhi ya hizi falsafa.

Dunia ya nchi moja kutawala wengine (Uni-Polar World) au nchi mbili kuamulia dunia nini kifanyike (Bi-Polar World) unakufa taratibu, ndiyo maana Marekani na Urusi wanapata shida kukubaliana na huu ukweli. Wao kama mataifa hawaanguki na bado wana nguvu, ila tu ni kwamba mataifa yale madogo na masikini kama Vietnam, Poland, Mexico yamekuwa makubwa yenye uchumi unaokua kwa kasi sana.

Tanzania tuliachiwa mtaji mkubwa sana kidiplomasia, ambao ulitujengea SOFT-POWER na INFLUENCE ambayo ilifanikisha ulinzi na usalama wa Tanzania kikanda na kidunia kwa kiwango kikubwa sana. Tuliingia sehemu ambazo hata nchi kubwa hazikuweza kuingia, tulipata taarifa nyeti kabla hata baadhi ya mataifa makubwa hayajazipata, tulipewa heshima ya kipekee (Special Treatment) ambayo mataifa mengine yenye uchumi mkubwa kuliko sisi barani Afrika hayakupewa.

Tuliogelea bwawa moja na mababeru, wakomunisti, wajahidina na wazayuni lakini tulitoka salama, kesho tena tukarudi kuogelea. We were a Shrimp among Whales, lakini bado tuliheshimika mno. Lakini leo hii hebu angalia, ile nguvu yote ambayo Mzee Nyerere na Raisi Mkapa walitutengenezea, imemomonyoka kisa kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uelewa mpana wa mahitaji ya nchi yetu na nafasi yetu hapa ulimwenguni.

Binafsi naamini ili tuweze kutoka hapa tulipo ni lazima NYUMBA ISAFISHWE aidha mbele ya majirani au kisiri. Mambo ya UHAINI, KUHODHI MADARAKA, KUPANGA KUUA MARAISI WASTAAFU,KUSHIRIKIANA NA MAADUI WA TAIFA na KUWINDANA KWA KUTUMIA MAKUNDI NDANI YA TASISI ZA KIUSALAMA (Cloack and Dagger Diplomacy) tulikuwa tunayasikia nchi jirani tu: Kwetu sisi yalikuwa ni MWIKO KABISA. Vitendo vya kihaini tulishaachana navyo awamu ya kwanza. Lakini leo kuna kakundi kalifikiri kabisa kangeweza kutupangia sisi Watanzania nani awe Mkuu wa nchi kweli?

Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).

Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....
To be honest i admire your reasoning. Umeandika vyema.

I believe 'diplomacy is an art of compromise'

Sasa kwa magufuli hili lisingewezekana hawezi 'kucompromise' maana deep down kiasili yeye ni mtu wa kuamini anachokiamini yeye tu, hashauriki na hili amelisema mara kadhaa ata hadharani kwamba 'mimi ni jiwe' , 'siyumbishwi' , 'sishauriki' , 'tena mkijaribu kunishauri ndo mnakua mnaharibu kabisa' . Vitu vingi katika international scale kaviharibu kabisa na it will take time kuvirepair, kaua soko la korosho, kavunja mikataba mingi kiholela, ndege zimekamatwa nje, nchi imefunguliwa kesi nyingi za madai kwenye mahakama na wawekezaji waliofukuzwa au kuvunjiwa mikataba yao bila kufuata utaratibu, wakati dunia ikijitahid kupambana na janga la korona ye anakwambia korona haipo hiyo ni michezo tu ya wazungu, n.k. n.k

Mtu yeyote yule anayekataa au anayebisha kwamba Magufuli hajairudisha nyuma Nchi katika nyanja na sera za uhusiano wa kimataifa basi huyo atakua tu naye ni mbishi wa kiasili kama magufuli na hatuna budi bali inabidi tumpuuze

Sasa turudi kwenye hoja yako ya msingi ambayo ningependa pia wachangiaji wanaofuta wajikite nayo ni kwamba 'vichwa vyetu au think tanks wa nchi hii kwenye vyombo vyetu nyeti vya ulinzi na usalama vilikua wapi wakati haya yote yanatendeka???'
Hapa ndipo kuna hoja ya msingi inayohitaji majibu ya kina. Na kama walikaa kimya na mpaka leo wapo kwenye nafasi zao hata kama Uongozi wa juu umebadilika tutawaamini vipi kama wataweza kutuvusha salama sisi kama taifa.
 
Hivi mtoa mada unadhani kabisa hayo mambo uliyoyaandika hapo juu jiwe angeyajua kweli?

Yeye nje ya mabarabara hakua anajua chochote kile khs Mambo ya diplomasia, uchumi, usalama etc
Trust me JPM was no fool. He was very intelligent. Alijua kujenga hoja. Kwa namna ya kipekee kabisa alijua pia namna ya kuwaaminisha watu yale aliyotaka watu wayaamini. He was well informed. He had access to every inch of information you can imagine of. He was a hard worker. Alisoma sana kila taarifa aliyopewa na wasaidizi wake. He always slept late. A very hard working man. The question is why did he act the way he acted while he knew all that was required to be done yet he did the exact opposite.
 
Trust me JPM was no fool. He was very intelligent. Alijua kujenga hoja. Kwa namna ya kipekee kabisa alijua pia namna ya kuwaaminisha watu yale aliyotaka watu wayaamini. He was well informed. He had access to every inch of information you can imagine of. He was a hard worker. Alisoma sana kila taarifa aliyopewa na wasaidizi wake. He always slept late. A very hard working man. The question is why did he act the way he acted while he knew all that was required to be done yet he did the exact opposite.

Hahahah hivi ni kazi ya rais kusema eti nalala na ma file kitandani na unakuja kusema hadharani?Ili uonekane hard worker?Unajua maana ya segregation of duties?Unajua maana ya ku-delegate?

Zaidi ya kujua KM za barabara kwny mambo mengine alikua mweupe.Naked truth.
 
Ukitaja kujua tuliongukia mikono mwa matapeli washamba, msikilize Kabudi akielezea mirabaha kwenye madini, sijui tutapata 50/ 50 laki wakati huo huo tuna shares 16%. Halafu huo utapeli hawataki mtu ahoji bali ni ww kusifia tu, eti nchi mkononi kwa mzalendo! Ila Mungu amtuepusha na yule kiongozi muovu, acheni Mungu aitwe Mungu.
Amekuepushia na kiongozi muovu bila kumwaga damu!

Vipi sasa mko vizuri sana uovu umeisha, madini mna share za 50/50? Hamuibiwi tena, nchi sasa iko mikononi mwa wazalendo. Mko vizuri ee?
 
Watu hawakuwa wanaamini ule utapeli, bali ilikuwa ni shuruti. Na ilikuwa ukionyesha kwenda kinyume na ule utapeli unatekwa, kuuwawa au kubambikiwa kesi. Yaani tulipata kiongozi muovu, hisia zake akawa anatulazimisha tuziamini!
Usilalamike sasa!

Mshukuru mungu wako sasa hivi uko vizuri sana
 
Ben mkapa alifanya nchi yetu first class diplomacy
Alichotakiwa ku fanya Magu pamoja ma ku renovate weakness hakutakiwa kugombana na investors
Tumeonankipinf chake aki close mikataba mbalimbali bila sababu za maana
Like gas, bagamoyo
Afu anaenda ku invest charity na burigi what a shame
Kwa hiyo mkataba hata kama ni mbovu wa kinyonyaji unatakiwa kuchekelea tu? Ndio diplomacy hiyo?
 
Hahahah hivi ni kazi ya rais kusema eti nalala na ma file kitandani na unakuja kusema hadharani?Ili uonekane hard worker?Unajua maana ya segregation of duties?Unajua maana ya ku-delegate?

Zaidi ya kujua KM za barabara kwny mambo mengine alikua mweupe.Naked truth.
Mambo mengine kama yapi?

Hao waliokuwa wanajua mambo mengine walikufikisha wapi kama nchi?
 
Populism ipo lakini haitakiwi ivuke mipaka na kuathiri sera ya mambo ya nje na diplomasia ya nchi. Ukisoma sana Diplomasia utakutana na kitu kinaitwa COMPARTMENTALIZATION OF FOREIGN POLICY AND NATIONAL DIPLOMACY. Kwamba utakuwa na ujinga wako ndani ya nchi au utakuwa na uadui na taifa fulani, lakini lazima mshirikiane nalo kwenye mambo muhimu.

Sasa mtu usipofahamu jinsi mfumo wa dunia unafanya kazi unaweza kuyapeleka yale ya ndani ya nchi nje ya mipaka yako na yakakuletea madhara. Hili ndilo liliiukuta Tanzania yetu, tumepata madhara makubwa. Hebu angalia hapa:

1. Uchina na Marekani ni maadui wakubwa - Lakini ndiyo mataifa yenye mahusiano makubwa kibiashara.
2. Uchina na Japan ni maadui wakubwa - Lakini wanahusiana sana kwenye ulinzi na usalama wa Pasifiki.
3. Uchina na Australia wameanza kuwa maadui- Lakini biashara ya Real Estate Uchina ina mkono wa Australia.
4. Urusi na Marekani ni maadui - Lakini wanashirikiana sana kwenye teknolojia na usalama wa Mashariki ya Kati.
5. Urusi na Ukraine ni maadui - Lakini juzi Ukraine wameomba kuuziwa gesi na Urusi baada ya uhaba kutokea Ulaya.

Hujiulizi kwanini haya mataifa makubwa hayasusi au kuzira kama mataifa ya kiafrika, huku mkijivuna kwamba sisi ni matajiri na tunajenga kwa pesa za ndani. Mara hatuwahitaji hawa wanyonyaji, tunaweza kufanya wenyewe. Hizi kauli hata mtu binafsi huwezi kuzisema kwa jirani zako. Lakini watanzania wakaingia mkenge, ona leo sasa.....

Hahahah hivi ni kazi ya rais kusema eti nalala na ma file kitandani na unakuja kusema hadharani?Ili uonekane hard worker?Unajua maana ya segregation of duties?Unajua maana ya ku-delegate?

Zaidi ya kujua KM za barabara kwny mambo mengine alikua mweupe.Naked truth.
Alipenda kusema vile ili kupata public sympathy ni dalili ya mtu muoga ambae hajiamini jinsi anavyotekeleza wajibu wake. Anachokisema Malcolm wachangiaji wengine hawajamuelewa na hawataki kutulia kusoma ili waelewe. Kwe lugha nyepesi "diplomasia" ni upatanishi ambao unaanzia ndani mpaka nje ya mipaka ya nchi na ndio msingi wa uhusiano wa kimataifa. Kwenye anga za diplomasia sisi tulikuwa vizuri Sana kwa sababu kwanza Umoja wetu wakitaifa ulikuwa imara na pili tuliweza kushirikiana vizuri na nchi zingine kwenye mambo mbalimbali hata kutatua migogoro.

Tanzania tulikuwa vinara kwenye upatanishi (diplomasia) tuliweza kusimamia maridhiano ya Burundi, Kenya hata kuleta amani kwenye visiwa vya anjuani kumuondoa kanali Bakari. Kwenye biashara zakimataifa tulikuwa vizuri sana tuliweza kufanya biashara ya mazao na malighafi zetu vizuri japo changamoto hazikosi. Mwaka 2012 dola ya marekani ilikuwa sawa na 1500 ya Tanzania nchi ilikuwa na hela ndio maana Kikwete aliajiri Sana, alipandisha madaraja kila mwaka watumishi wa umma waliweza kujenga nchi ilifunguka watu waliuza mpaka mbaazi nje kwa bei nzuri. Tatizo JPM alikuwa mshamba na Muoga sana kujivisha uzalendo wa hovyo aliamini kwenye mabarabara akasahau umoja wa kitaifa na upatanishi wakimataifa
 
Mambo mengine kama yapi?

Hao waliokuwa wanajua mambo mengine walikufikisha wapi kama nchi?
Wewe unaona umefika wapi kama nchi, acha kuwa mjinga basi Taifa lolote duniani ni kama mtoto anakuwa taratibu, Nyerere alipoishia mwinyi alianzia pale. JPM hakuwa malaika alifanya fyongo tu na wala nchi haijafika popote. Sema niwatanzania Wangapi wamekuwa lifted from poverty line. Uongozi wenye makelele mengi ya propaganda kutumia media bias matokeo yake ndio haya, nchi yetu imetoka mbali sana kama hujui tunu yetu kubwa tangu Taifa hili linazaliwa ni (diplomasia) upatinishi ndio Taifa kama msumbiji linatueshimu Sana. Jiulize kwanini mkapa aliwekeza sana kwenye jeshi, Sisi tulikuwa tunauwezo wakuchezea majirani tunavyotaka hata Rais nkrunzinza wa Burundi tuna mkono wetu kwa hiyo ilikuwa rahisi kuingiza chumvi yetu ya uvinza kutoka kigoma, tulienda Congo kumfurusha Kagame maana hao niwatoto wetu, mseveni wa uganga alikuwa hawezi kujamba mbale yetu tunachapa kiboko. Acha ushamba wewe, ulishafika udom ukaona uwekezaji wa serikalii, chuo Nelson Mandela, hospital ya mloganzira na Benjamin mkapa. Najua bado mtoto ukikua utaacha ujinga nchi iliingia mkosi kupata Rais mjinga
 
Huwa nawaza sana tulifikaje hapa tulipo leo,

Hivi ilikuwaje taifa lenye wasomi wazuri kabisa likaamua kufanya maamuzi ya kipumbavu ambayo hata Waroma wa kale walioishi miaka 2000 iliyopita wasingeyafanya. Hivi katika maksudi kabisa, taasisi nyeti za Tanzania ziliamini kabisa kwamba wao wangeweza kuifanya Tanzania nchi tajiri bila kushirikiana na dunia : Hivi ilikuwaje kabisa wataalamu wetu ambao wameenda shule, wanafahamu mifumo ya dunia ya kiuchumi, kiulinzi na kisiasa na wako kule USALAMA, BENKI KUU na MAMBO YA NJE wakakubaliana na huu upumbavu na kuanza kuutekeleza kabisa?

Mpangilio wa dunia yetu ya sasa uliwekewa msingi mwaka 1814 kule Vienna baada ya miaka 25 ya vita za mfalme Napoleon Bonaparte. Mwanamfalme Von Matternich alifahamu kabisa ili dunia isirudie kuingia kwenye songombingo la vita au kadhia yoyote ile, basi ni lazima watengeneze mfumo ambao uko kama utandu wa bui-bui: Kwamba maamuzi ya nchi moja yakifanyika lazima yaathiri nchi zote, hivyo nchi lazima zikubaliane kwenye baadhi ya mambo muhimu yanayowagusa wote. Ndiyo nadharia ya MZANI WA NGUVU (Balance of Power) ikazaliwa.

Mfumo wa dunia ya yetu hii tunayoishi leo hii umejengwa na matukio yaliyotokea miaka ya 1913, 1914, 1918, 1920, 1927, 1928, 1933, 1935, 1939, 1941, 1944, 1945, 1947, 1948, 1971 na 2001 . Kiufupi mlolongo wa matukio haya yafuatayo ndiyo yanatoa mwelekeo mzima wa mwenendo wa dunia yetu ya leo : Nashauri tufanya utafiti wa ndani kuhusu hili.

Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.

Mtaalamu yoyote yule wa Uchumi, Diplomasia, Ulinzi na Sheria ni lazima afahamu fika kuhusu haya ninayoyasema hapa. Kwamba dunia nzima tuko ndani ya utandu moja wa bui-bui. Huwezi kufanya jambo lolote lile ukiwa nje ya hapo. Ndani ya huu utandu wa bui-bui kuna kila aina ya watu: Wema na wabaya, Huru na watumwa, Masikini na tajiri, Wenye matumaini na wasio na matumaini, Wababe na dhaifu na Waamini Mungu na Maadui wa Mungu.

Huu ndiyo mfumo wa dunia (The World Order), huwezi kufanya maajabu yoyote yale ukiwa nje: Hata mataifa makubwa yenye nguvu duniani yanaheshimu huu mfumo kwasababu yanafahamu siku mfumo huu unaharibika basi ndiyo utakuwa mwisho wao. Hivyo kuna baadhi ya sheria hata yenyewe yatazifuata tu kwasababu zina manufaa kwao. Mwandishi George Orwell kwenye The ANIMAL FARM aliwahi kusema "All animals are equal, but some are more equal than others" hivyo hata kama tunataka usawa kuna wale waliotutangulia watakuwa mbele yetu kwenye baadhi ya mambo tu.

Sasa kinachoumiza wasomi wa Tanzania wenye PhD za sheria, uchumi na diplomasia. Huku wengine wakiwa na shahada kwenye masomo ya ulinzi, usalama na sayansi za vita wakiwa na akili timamu kabisa, wakaamua kuwa wapumbavu. Wakatundika elimu zao nyuma ya milango na kuanza kutekeleza jambo ambalo hata watu wa kale walioishi miaka 2000 hawakuwahi kuliwaza. Tanzania ina matatizo mengi, lakini ilikuwa inarekebishika vizuri tu kwasababu waliofikisha nchi yetu hapa wanafahamika na tunakula na kunywa nao kila siku.

Kuanza kulaumu mabeberu peke yake haisaidii kwasababu kuna wenzetu ambao wamefanikiwa kutumia mifumo hii-hii ya mabeberu kuwashinda mabeberu kiuchumi, kiulinzi na kisiasa. Ukweli ni kwamba huu mfumo umejengwa na mabeberu lakini hata walioujenga hawaundeshi wanavyotaka wao. Mataifa ya Magharibi ndiyo waanzilishi wa World Trade Organization (WTO) lakini leo hii, WTO imemnufaisha Uchina kuliko tangu alivyojiunga nao mwaka 2001 na mpaka sasa wanajutia kumkaribisha.

Nchi kama Singapore, India, Korea-Kusini na Brazil wamewezaje kucheza vizuri kwenye huu mfumo wa mabeberu hadi kufikia kuwango cha kuwashinda mabeberu kwenye baadhi ya mambo ??? Inahitaji akili ya ziada kutoka kwa Mungu ili kuweza kucheza kwenye huu mfumo. Raisi Donald Trump alijaribu kuitoa Marekani kwenye huu mfumo wa Vienna, lakini pamoja na maguvu yote ya Marekani alifanikiwa ???

Lakini leo hii kuna watu wako ndani ya IDARA ZA USALAMA ZA TANZANIA waliamini kabisa kwamba Tanzania inaweza kujitenga na dunia bila kupata madhara. Yaani waliamini kabisa na wengine bado wanaamini kabisa. Kuna wengine bado wanaamini kwamba mfumo wa Kileninisti na Kimaksisti (Marxist-Leninism) unaweza kutumika kuikomboa Tanzania. Sawa, lakini hata walioutuletea huu mfumo Warusi na Wachina, wamebadilisha sana baadhi ya hizi falsafa.

Dunia ya nchi moja kutawala wengine (Uni-Polar World) au nchi mbili kuamulia dunia nini kifanyike (Bi-Polar World) unakufa taratibu, ndiyo maana Marekani na Urusi wanapata shida kukubaliana na huu ukweli. Wao kama mataifa hawaanguki na bado wana nguvu, ila tu ni kwamba mataifa yale madogo na masikini kama Vietnam, Poland, Mexico yamekuwa makubwa yenye uchumi unaokua kwa kasi sana.

Tanzania tuliachiwa mtaji mkubwa sana kidiplomasia, ambao ulitujengea SOFT-POWER na INFLUENCE ambayo ilifanikisha ulinzi na usalama wa Tanzania kikanda na kidunia kwa kiwango kikubwa sana. Tuliingia sehemu ambazo hata nchi kubwa hazikuweza kuingia, tulipata taarifa nyeti kabla hata baadhi ya mataifa makubwa hayajazipata, tulipewa heshima ya kipekee (Special Treatment) ambayo mataifa mengine yenye uchumi mkubwa kuliko sisi barani Afrika hayakupewa.

Tuliogelea bwawa moja na mababeru, wakomunisti, wajahidina na wazayuni lakini tulitoka salama, kesho tena tukarudi kuogelea. We were a Shrimp among Whales, lakini bado tuliheshimika mno. Lakini leo hii hebu angalia, ile nguvu yote ambayo Mzee Nyerere na Raisi Mkapa walitutengenezea, imemomonyoka kisa kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uelewa mpana wa mahitaji ya nchi yetu na nafasi yetu hapa ulimwenguni.

Binafsi naamini ili tuweze kutoka hapa tulipo ni lazima NYUMBA ISAFISHWE aidha mbele ya majirani au kisiri. Mambo ya UHAINI, KUHODHI MADARAKA, KUPANGA KUUA MARAISI WASTAAFU,KUSHIRIKIANA NA MAADUI WA TAIFA na KUWINDANA KWA KUTUMIA MAKUNDI NDANI YA TASISI ZA KIUSALAMA (Cloack and Dagger Diplomacy) tulikuwa tunayasikia nchi jirani tu: Kwetu sisi yalikuwa ni MWIKO KABISA. Vitendo vya kihaini tulishaachana navyo awamu ya kwanza. Lakini leo kuna kakundi kalifikiri kabisa kangeweza kutupangia sisi Watanzania nani awe Mkuu wa nchi kweli?

Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).

Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....
A good read
 
Mimi Malcom Lumumba nitasema ukweli daima, fitna kwangu mwiko. Raisi Magufuli kuna mambo mengi sana aliyafanya vizuri lakini mambo ya nje na diplomasia haviko kwenye hiyo orodha. Dunia yetu ya leo siyo ile ya karne ya 18 na 19 ambayo ulikuwa unaweza kujifungia tu (Isolationism) halafu mambo yakawa yanaenda tu. Tunaishi kwenye ulimwengu wa utandawazi, hivyo ni lazima tunavyojenga ndani na nje tujenge: Lazima kuwe na uwiano mzuri......
Sasa mjomba ni kweli huwezi endelea bila kujihusisha na dunia sija bisha lakini mm nimekwambia unabidii uanze kujenga kwanza ndani ndiyo ufwate hivi hukuona like jambo la kwenda uchumi wa kati lingeleta tija Katika uwekezaji. By the way magufuli hatunaye Tena Sasa turudi kwa waliopo Sasa hivi unadhani viongozi wanavyo zunguka ni kuijenga uhusiano wa dunia ni kuleta tija mtu unazunguka nchi za watu kwako umeme ni shida, maji ni shida hafu utaleta uwekezaji ni mwekezaji chizi pekee atakae wekeza kwa ajili ya hasara. Yaani beberu yeye ni mtu wa 1 profit, 2 profit,3 profit huwezi enda na pua yako kwa beberu akategemea kuwini. Hivi hujawahi ishi na mtu kakuzidi kiuchumi mbali lakini akakuheshimu kwa jambo moja ambalo ni dogo kwakuwa yeye haliwezi. Ndio hivyo Tanzania inabidii sisi tutambue nini tunaweza na Nini hatuwezi kile tuchoweza tunakifanya ambavyo hatuviwezi tunashirikiana na wengine hichi ndio ambacho jpm aliweza kutaka mtanzani afikiri anaweza. Sasa kuzunguka zunguka kwa kuomba misaada na kuona Kama wananchi ni visiki hatuwezi chochote.
 
Alipenda kusema vile ili kupata public sympathy ni dalili ya mtu muoga ambae hajiamini jinsi anavyotekeleza wajibu wake. Anachokisema Malcolm wachangiaji wengine hawajamuelewa na hawataki kutulia kusoma ili waelewe. Kwe lugha nyepesi "diplomasia" ni upatanishi ambao unaanzia ndani mpaka nje ya mipaka ya nchi na ndio msingi wa uhusiano wa kimataifa. Kwenye anga za diplomasia sisi tulikuwa vizuri Sana kwa sababu kwanza Umoja wetu wakitaifa ulikuwa imara na pili tuliweza kushirikiana vizuri na nchi zingine kwenye mambo mbalimbali hata kutatua migogoro.

Tanzania tulikuwa vinara kwenye upatanishi (diplomasia) tuliweza kusimamia maridhiano ya Burundi, Kenya hata kuleta amani kwenye visiwa vya anjuani kumuondoa kanali Bakari. Kwenye biashara zakimataifa tulikuwa vizuri sana tuliweza kufanya biashara ya mazao na malighafi zetu vizuri japo changamoto hazikosi. Mwaka 2012 dola ya marekani ilikuwa sawa na 1500 ya Tanzania nchi ilikuwa na hela ndio maana Kikwete aliajiri Sana, alipandisha madaraja kila mwaka watumishi wa umma waliweza kujenga nchi ilifunguka watu waliuza mpaka mbaazi nje kwa bei nzuri. Tatizo JPM alikuwa mshamba na Muoga sana kujivisha uzalendo wa hovyo aliamini kwenye mabarabara akasahau umoja wa kitaifa na upatanishi wakimataifa
I couldn't agree more mkuu!:
 
Kichwa cha mada yake tu ni upotoshaji. Umemjibu vizuri sana.Yaani wao wanaamini kushirikiana na dunia ni kuwapa madini na kupokea neti na Condoms. Ukisema hapana nataka niuze madini mwenyewe na niende dukani kununua neti mwenyewe tayari unakua hutaki kushiriki na dunia.Hili jukwaa Kuna muda watu wanaoonekana wana akili TIMAMU huwa wanapost vitu vya ovyo sana.
Hayo yote yamefanyika kwasababu ya nchi kua na viongozi wabovu.Na kwavile Ccm ndo chama kilichoongoza nchi toka uhuru huwezi kutenganisha ccm na huo ujinga wakutoa madini na kupewa condoms.Kwahiyo tatizo ni sisi wenyewe.Unapokubali kudanganywa na kuibiwa tatizo ni wewe sio muibaji,tena hawaibi bali tunawapa kupitia mikataba tunayosaini wenyewe chumbani.
 
Hivi ni nani aliyekwambia kwamba Diplomasia ya nchi inafanywa na mabalozi peke yake ???

Balozi ni kitaalamu ni Diplomatic Agent/Legate/Envoy yeye hufanya kazi kama wakala au muwakilishi wa nchi na sera zake. Wao hawafanyi kazi nje ya TOR ambazo hupewa baada ya teuzi na kutumwa nje ya nchi. Sasa kama unafikiri mabalozi ndiyo wanaendesha diplomasia ya nchi au lazima mtua aende nje ya nchi ili awe mwana diplomasia, UMECHELEWA BASI (You've missed a bus) mkuu.

Nadhani sasa kuna haja turudishe ule utaratubu wa zamani vijana wote wa UVCCM, Viongozi wa umma, TISS na JWTZ na makada wengine wa UVCCM lazima tuwapeleke Kurasini kinguvu au wasome vyuo vya itikadi kwa lazima: Hiki kiwango chenu cha ujinga is beyond ordinary comprehension. Yaani wewe SWEETTABLET nilikuwa nakuona walau ziko kichwani kumbe na wewe ni mweupe hivi ??? SMH
Hao uliowataja ndo waliofikisha hii nchi kua ovyo hivi ilivyo.hakuna kitu humo.
 
Hivi unategemea nani akuendeleze dunia ya leo? We ujajua kwamba bila afrika mzungu ni masikini mwafrika akijitambua na kuacha kulialia anaweza kujitegemea hii ndiyo mtizamo wa walioleta uhuru. Misaada haijawahi saidia popote ukienda ulaya tunaitwa omba2 tumalizane hewa ya dunia bure hatuna faida na kuna watawala wanatamani kutufuta kabisa kwenye uso wa dunia. Usiwe unaandika tangazo la kuchosha kwa mtizamo hasi ulionao, jambo hili linataka mjadala wa kitaifa usifikiri kuondoa umasiki ni lelemama!
Kipi kinamfanya au kumzuia mwafrika asijitambue badala yake amebaki kulia lia huku akiwa maskini?
 
Kwa hiyo mkataba hata kama ni mbovu wa kinyonyaji unatakiwa kuchekelea tu? Ndio diplomacy hiyo?

Kwani dhalimu alifanya nini, au zile brainwash za kwenye TV ndio uliona kapatia? Zile $192 alizoongopa tunawadai Barrick mlilipwa. Kile kushika uchumba cha $300m kimeshalipwa chote?
 
Back
Top Bottom