Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Mkuu hii thread kuanzia kichwa tu umeandika upuuz. Hakuna sehemu Magufuli hakutaka kushirikiana na dunia. Swala ni maslai ya Tz mbele.Kuanza kufumua mikataba ya ovyo tayari ni kukataa kushirikiana na dunia?Kukataa Lockdown au Chanjo tayari hataki kushirikiana na dunia?
Mtu anakuja kuwekeza unamuita beberu
Diplomasia ya wapi
 
Mmmmmh! Tulijitenga na dunia lini? Mbona tuliongea na Rwanda na Uganda kuhusu kuonganisha nchi zetu na (SGR). Mbona mkutano wa sadac ulifanyika Tanzania. Mbona balozi zetu hazikufungwa nchi jirani na duniani.Mbona wageni/watalii walifika nchini.Mbona viwanda vya wageni hususani ni waChina vimeongezeka.

Au kuwa karibu na dunia nikujenga bandari ya bagamoyo kwa masharti ya kipumbavu na kubinafsisha Tanesco. Au kusaini bogus treaty

Je umesema kuhusu leagal of nation je kwanini ujerumani aliona ni uboya akawageuka. Nakusuhu UN kwanini Patrice lumumba aliomba jeshi kutoka UN ili kuwaondoa wabelgiji wezi wa shaba congo baadala yake wanajeshi wa UN wakaanza kuwasupport wabelgiji. Huuu ndio uhusiano na dunia? jihusishe na dunia lakini chunga chako kwasababu hakuna wakutupa zaidi ya mungu lazima tuheshimu zawadi hii.

Nasikitika Sana mtoa maada umekuja na kapoint uchwara sijui ka diplomasia sijui naahisi ndo hicho ukijuacho kwenye maendeleo foreign policy hayo ni mambo ya mwisho maendeleo yanaanza ndani tengeneza mazingira ya ndani kwanza. Hizo nchi China na wenzake zimewin sio kwasababu ya blabla unazosema wewe ni kwa kufanya kazi kwa bidii na kutengeneza mazingira ya uwekazaji.
Hivi Rwanda ni dunia
Fdi au Fci kutoka Rwanda na uganda ni asilimia ngap
 
Yawezekana hujamwelewa Lumumba, yeye amejikita zaidi katika awamu ya tano...

Ndio maana naamini kabla na baada ya awamu ya tano, nyinyi wataalamu mlipewa nafasi na makafanya kazi

Swali langu, kabla na baada ya Magufuli mmeisaidiaje Tanzania katika vipengele alivyotaja Malcom?

Asante.
Hawezi kukujibu tena ongezea awataje ata watatu then atueleze walifanya yapi ao watatu?

Ayo majina hutokosa la January, Membe na Nape hapo ndo utajua kweli hatuna watu nchii hii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu hawakuwa wanaamini ule utapeli, bali ilikuwa ni shuruti. Na ilikuwa ukionyesha kwenda kinyume na ule utapeli unatekwa, kuuwawa au kubambikiwa kesi. Yaani tulipata kiongozi muovu, hisia zake akawa anatulazimisha tuziamini!
Hapa ndio kauliza
Those people we call elite walikua wapi
TICC na vyombo vingine walikua wapi
 
Naamini Tanzania inaweza kuendelea bila kutegemea misaada bali ikabaki tu kuheshimiana na kushirikiana kwenye maendeleo...

Wakubwa wa dunia wanaamini kwenye umafia kwa kuendelea kufanya wengine masikini kwa kutumia baadhibya tools zai kila mahala..Wakubwa wadunia wakigundua una mtazamo tofauti wakuwatoa watu kwenye utumwa wa kiuchumi basi hutumia tools zao na vibaraka waliopandikizwa kila mahala kukumaliza..... WaAfrica tujaribu kuwa real na Uafrica wetu tusishupaze shingo na kubabaika sana na hawa pua ndefu....
Tanzania itaendeleaje hata hatuna Uwekezaji kwenye technology..?
Umeona wapi serikali ilopita ikipeleka vijana kwa ajili ya ujasus wa kitekinolojia
Uliona wap tukifanya sampling ya technology ..??
Sisi n mazuzu
Ili tupate maendeleo lazima serikal iwekeze kwenye ujasus wa kitekinolojia na ujasus wa kiuchumi sio kutisha investors
 
Hawezi kukujibu tena ongezea awataje ata watatu then atueleze walifanya yapi ao watatu?

Ayo majina hutokosa la January, Membe na Nape hapo ndo utajua kweli hatuna watu nchii hii

Sent using Jamii Forums mobile app
Ben mkapa alifanya nchi yetu first class diplomacy
Alichotakiwa ku fanya Magu pamoja ma ku renovate weakness hakutakiwa kugombana na investors
Tumeonankipinf chake aki close mikataba mbalimbali bila sababu za maana
Like gas, bagamoyo
Afu anaenda ku invest charity na burigi what a shame
 
Kuna njia ipi mbadala ambazo nchi za Afrika zitatumia kulinda masilahi yake? Huoni aliyoyapa Gadaffi? Labda utasaidie hata kidogo, nchi kama Tanzania itawezaje kulinda rasilimali zake kwa njia ya urafiki na mabeberu?
Nchi kama Singapore na Korea-Kaskazini ambazo ni ndogo kuliko Tanzania ziliwezake kuwa tajiri huku zikiendelea kushirikiana na mabeberu kama Marekani, Uingereza na Uchina ??? Lakini pia, ni lazima ufahamu kwamba kushambuliwa Muhammar Qhadaffy kuna historia ndefu sana. Hivi mnaikumbuka michezo yake lakini :

-The Lockerbie Incident ???
Majasusi wa Libya mwaka 1988 walilipua ndege ambayo ilikuwa na inatoka ujerumani na kuua abiria zaidi ya 200.
Unapoanza michezo hatari kama hii ni lazima uhakikishe kwamba unaweza kuicheza mpaka mwisho, maana hawa wenzetu wanaweza kukuwekea kiporo hata miaka 100. Ndiyo maana Mwalimu Nyerere aliwaambia watanzania wanaopigania uhuru kwamba Mabeberu hawa nikuwasema na kuwaabisha tu, kupambana nao kijeshi hatuwezi.

  • Kuwaunga mkono waasi wa Tuareg
  • Kuwaunga mkono PLO na UGANDa kwenye uvamizi wa Tanzania

Yeye Muhammar Qhadaffy alikuwa anajitanabaisha kwamba yeye ni mtoto wa Gamal Abdi Nasser wa Misri, hivyo akawa anaiga karibia kila tabia ya Nasser. Sasa Mzee alifanikiwa sana katika kuijenga nchi yake na kuleta maendeleo, lakini ukichagua kuishi maisha kama ya Nasser, Ayatollah, Kim n.k ni lazima uwe makini sana sanaaa. Kuna mengi unaweza kukutana nayo ambayo yatakugharimu..

Hoja ni kwamba unaweza kufanikiwa kulinda maslahi ya nchi yako bila kusababisha kadhia na taharuki, mbona Lee Kuan Yew aliweza jamani ??? Haya mambo ya kusingizia mabeberu kwenye kila kitu yataligharimu hili bara letu
 
Malcom Lumumba naamini wewe ni mtaalamu mzuri wa diplomasia

Na mwana diplomasia kama wewe ni lazima utakua unawafahamu wajuvi wenzako wa diplomasia ndani ya nchi hii

Swali langu...

Tuambieni watanzania, utaalamu wenu wa diplomasia ulitusaidiaje kama nchi kujikomboa na janga la umasikini?(before&after magu, maana kwa mujibu wako huyu ni sufuri kwenye diplomacy)
Hivi Nyakubonga kuna Raisi ambaye alifanikiwa kukuza uchumi wa Tanzania kwa kupitia Diplomasia kama Mzee Mkapa ??? Japo alikuwa na makosa yake mengi tu, lakini alitumia vizuri mtaji ulioachwa na Mzee Nyerere. Unakumbuka baada kwenda G8 nini kilitokea: Hivi unakumbuka uwekezaji ulivyokuwa nchini na madeni mengi ya nje kufutwa ???

Tena naona mnasahau kuhusu changamoto za kiusalama zilizokuwepo huu ukanda wetu mnamo miaka ya 1995-2003, nchi nyingi ziliingia kwenye matatizo makubwa lakini unafahamu kwanini Tanzania ilitoka salama ??? Tanzania ilikuwa inaangaliwa katika jicho la kipekee sana linapokuja suala zima la siasa za Afrika. Leo hii nini kimetokea ??? Binafsi siamini kabisa kama Tanzania ina msuli ule iliyokuwa nao miaka hiyo......

Halafu leo Raisi Magufuli alitaka kutuaminisha kwamba hawa watangulizi wake hawakufanya chochote wala lolote kwa nchi hii: Ilhali mifumo yote ambayo ilimfanikisha hata yeye kuvuruga nchi yetu ameikuta imejengwa na wao. Sisi kama nchi bado tuna safari ndefu sana, lakini njia na mbinu za watu kama Magufuli ni hatari mno na zimeturudisha nyuma miaka 25. Kurudi kwenye ile nafasi yetu, inawezekana lakini itachukua muda sana na nguvu ya ziada.

NB: Mimi ninachouliza iliwezekanaje nchi ikawa ikavurugwa hivi, ilhali kuna taasisi nyeti zenye wasomi na wataalamu ambao walikuwa wanafahamu fika nchi ilikotoka. Kwanini washiriki utekelezaji wa mauti ya taifa letu halafu leo hii wanaachwa bila hata kupigwa kitanzi au kunyongwa kwa uhaini ili wapuuzi wengine wasidiriki kabisa kurudia jambo kama hili ???
 
Mpinge kwa hoja ndoo tutakuona mwanaume

Sasa hapo unataka nipinge kwa hoja gani wakati bandiko lake lenyewe limejengwa juu ya msingi potofu?

mwambie kwanza aweke ushahidi wa audio au video ili kuthibitisha kwamba JPM alikuwa anajaribu kuitenga Tanzania na Mataifa mengine(Dunia)


halafu akishafanya hivyo tutajadili hoja zake,kinyume na hapo hakuna cha kujadili hapa!!
 
Ushirikiano ni muhimu sana. Lakini ushirikiano kwa namna ulivyo sasa hatutakuja kuendelea kamwe, tutabaki maskini siku zote. WTO wanahimiza soko huria, vikampuni toka nchi maskini vikashindane kwa usawa sokoni na makampuni makubwa ya matajiri. Hao IMF na WB wanalazimisha nchi zifuate sera za kichumi ambazo zinadumaza maendeleo ya nchi maskini. Sera ambazo nchi tajiri hazikuzitumia kujipatia maendeleo.

Hata nchi tajiri zenyewe mambo yakiziendea kombo zinaachana na makubaliano ya kimataifa. US kuipiga pin Huawei ni mfano mmoja wapo. Ushirikiano ni muhimu lakini kwa namna uliopo hautufai.
Nakubaliana kabisa na wewe, lakini mkakati wa kujikwamua kutoka kwenye hiyo mifumo ya kibeberu ni ipi ???
Unaufahamu mchezo wa CHESS ??? Siku zote anayemshinda ni yule mwenye kusoma vizuri na kutabiri hatua za adui.
 
Anhaa, kwahiyo mkuu unataka kusema kwamba sera ya mambo ya nje ya Tanzania ilitekelezwa ipasavyo kwasababu ya SGR, mkutano wa SADC, kuongezeka kwa viwanda vya wachina na watalii SI NDIYO ??? Lakini, vipi kuhusu utekelezaji wa International Commitments at Regional and International Levels ambazo tuliziweka kisiasa na zile ambazo ziko kisheria ???

Kuna matatizo mangapi ambayo nchi iliingizwa kwasababu za kutokuwa makini katika kuheshimu hizi international Commitments ??? Kuhusu mambo ya Bilateral Investment Treaties (BIT's) ni mara ngapi tulijiingiza kwenye shida zisizokuwa na ulazima kisa tu kiburi cha mtu mmoja ??? Haya ni baadhi ya mambo ambayo inabidi tuyazungumzie, lakini sioni mtu hata mmoja akiyaleta hapa.


Hakuna nchi inayolazimishwa kusaini mikataba endapo inahisi mikataba hiyo haina manufaa kwa taifa lake. Kila taifa ni Sovereign na Signin of Treaties falls within a scope of sovereign prerogatives. Pia hata kujitoa kwenye mikataba nayo ni Sovereign Prerogative, nchi inaweza kuamua kujitoa. Sisi tunachokataa ni kujitoa bila kuwa na mkakati, kudanganya umma au kutaka umaarufu.

Katika kusoma kwangu kote hata nchi kama Serikali za nchi kama Uingereza huwa hazishindi kesi dhidi ya wawekezaji endapo pale serikali imeamua kujitoa bila kufuata mkakati maalumu. Kama tunaikataa hii mikataba basi lazima tuje na mkakati na siyo kukurupuka hapa, mwishowe tunakuja kupata madhara kama yale yaliyotukuja kisa tulivunja baadha ya BIT kwa kukurupuka.


Daaah, hili swali huwa nilikuwa nakutana nalo kila nilipokuwa nafundisha International Law kwa wanafunzi wa mwaka wa pili. Ntakujibu kwa kufupi kabisa: International Relations cross-cuts many issues other than peace and security, it touches investment issues, health issues, international monetary systems, markets, culture etc.

Kilichotokea kwa Lumumba siyo kitu kuzuri hata kidogo, na kilidhihirisha udhaifu wa mfumo wetu wa dunia ambao uko mpaka leo hii. Lakini busara ni ipi, tuendelee kujitenga na kujificha au sisi kama bara la nchi masikini tuungane ili kusaidiana kubadilisha mifumo ya dunia ambayo inatukandamiza ??? Tanzania ilipoteza pesa nyingi sana katika kusaidia nchi za Afrika kupata Uhuru, lakini unafahamu faida za kiusalama ambazo nchi ilizipata kutokana na ule uwekezaji ???

Swali la msingi kijiuliza: Kikwete na Mkapa walifanikiwa sana kuendeleza hii tunu tulioachiwa na Baba wa Taifa. Je Raisi Magufuli alifanikiwa kufanya hivyo au alishindwa ???

Kaa chini fikiri.....


Dunia hii ya leo huwezi kutengeneza ya ndani bila kutengeneza ya nje pia, maana kila kitu ambacho kinakuja ndani ya nchi hutoka nje. Kiasilia, taifa ambalo huwa tajiri ni lile ambalo linafanikiwa sana kuuza bidhaa zake nje ya nchi kwa kiwango kikubwa, na lile ambalo linafanikiwa kuvutia mitaji ya nje kwa kupitia uwekezaji. Sasa ili ufanikiwe katika hili ni lazima uwe unafahamu fika mfumo mzima wa masoko ya dunia na michezo michafu ambayo mabeparu hucheza.

Nikikuuliza Sera ya uwekezaji na viwanda ya Tanzania kwa miaka mitano iliyopita ilikuwa ni ipi hutanijibu kabisa. Mkakati ambao ulitekelezwa vizuri ni ujenzi wa miundo mbinu, katika hili lazima tukubali kwamba Raisi Magufuli alijitahidi sana , lakini huko kwingineko hebu mnifundishe zaidi
mkuu inawezekana jamaa kiukweli hakuwavizuri nyanja zote. Lakini isiwe sababu ya kuondoa sifa kubwa alizokua nazo kwa kuanza kumtukana na kuonesha jamaa alikuwa hatendi mazuri. Na pia tusitupilie macho yetu yote kwenye kitu kimoja Kama wewe unavyouweka uhusiano na dunia Kama ndio chanzo cha maendeleo ambacho jpm hufanya nakuona yale aliyo yafanya ni zero. Na pia umesema unatakiwa ujenge ndani na nje ni sahihi lakini sidhani Kama unaweza ukaanza na nje hafu ukafwata ya ndani ni wapuzi tu Hawa wa Sasa ndio mawazo yao. Lakini njia sahihi ni kuimalisha kwanza ya ndani ya nje huja yenyewe sio lazima uzunguke. hebu niambie Kama nyerere dam ambalo lilikuwa ndoto ya mda mrefu likikamilika litavutia wawekezaji wangapi? Naona umeitaja China na marekani kuwa ni maadui na pia Zinafanya biashara nikweli lakini uhusiano alionao China kwa mmarekani sio wakujipendekeza Kama wakwetu ambao mwisho ni unyonyaji mchina aliweka nchi yake Katika mazingira ya uwekazaji mmarekani akavutiwa kwa uwekeza japo walikuwa ni maadui na mbaka Sasa ni maadui lakini wanafanya biashara kutokana na uhitaji. Pia hata hapa kwetu Katika EAC hatukuwa vizuri na Kenya but Kenya wamenunua kwetu mazao kwasababu wanauhitaji. Kwa hiyo hii point yako ya kuangalia Sana uhusiano na dunia huku tukiwa mikono mitupu mm nadhani haiko sawa.
 
Huwa nawaza sana tulifikaje hapa tulipo leo,

Hivi ilikuwaje taifa lenye wasomi wazuri kabisa likaamua kufanya maamuzi ya kipumbavu ambayo hata Waroma wa kale walioishi miaka 2000 iliyopita wasingeyafanya. Hivi katika maksudi kabisa, taasisi nyeti za Tanzania ziliamini kabisa kwamba wao wangeweza kuifanya Tanzania nchi tajiri bila kushirikiana na dunia : Hivi ilikuwaje kabisa wataalamu wetu ambao wameenda shule, wanafahamu mifumo ya dunia ya kiuchumi, kiulinzi na kisiasa na wako kule USALAMA, BENKI KUU na MAMBO YA NJE wakakubaliana na huu upumbavu na kuanza kuutekeleza kabisa?

Mpangilio wa dunia yetu ya sasa uliwekewa msingi mwaka 1814 kule Vienna baada ya miaka 25 ya vita za mfalme Napoleon Bonaparte. Mwanamfalme Von Matternich alifahamu kabisa ili dunia isirudie kuingia kwenye songombingo la vita au kadhia yoyote ile, basi ni lazima watengeneze mfumo ambao uko kama utandu wa bui-bui: Kwamba maamuzi ya nchi moja yakifanyika lazima yaathiri nchi zote, hivyo nchi lazima zikubaliane kwenye baadhi ya mambo muhimu yanayowagusa wote. Ndiyo nadharia ya MZANI WA NGUVU (Balance of Power) ikazaliwa.

Mfumo wa dunia ya yetu hii tunayoishi leo hii umejengwa na matukio yaliyotokea miaka ya 1913, 1914, 1918, 1920, 1927, 1928, 1933, 1935, 1939, 1941, 1944, 1945, 1947, 1948, 1971 na 2001 . Kiufupi mlolongo wa matukio haya yafuatayo ndiyo yanatoa mwelekeo mzima wa mwenendo wa dunia yetu ya leo : Nashauri tufanya utafiti wa ndani kuhusu hili.

Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.

Mtaalamu yoyote yule wa Uchumi, Diplomasia, Ulinzi na Sheria ni lazima afahamu fika kuhusu haya ninayoyasema hapa. Kwamba dunia nzima tuko ndani ya utandu moja wa bui-bui. Huwezi kufanya jambo lolote lile ukiwa nje ya hapo. Ndani ya huu utandu wa bui-bui kuna kila aina ya watu: Wema na wabaya, Huru na watumwa, Masikini na tajiri, Wenye matumaini na wasio na matumaini, Wababe na dhaifu na Waamini Mungu na Maadui wa Mungu.

Huu ndiyo mfumo wa dunia (The World Order), huwezi kufanya maajabu yoyote yale ukiwa nje: Hata mataifa makubwa yenye nguvu duniani yanaheshimu huu mfumo kwasababu yanafahamu siku mfumo huu unaharibika basi ndiyo utakuwa mwisho wao. Hivyo kuna baadhi ya sheria hata yenyewe yatazifuata tu kwasababu zina manufaa kwao. Mwandishi George Orwell kwenye The ANIMAL FARM aliwahi kusema "All animals are equal, but some are more equal than others" hivyo hata kama tunataka usawa kuna wale waliotutangulia watakuwa mbele yetu kwenye baadhi ya mambo tu.

Sasa kinachoumiza wasomi wa Tanzania wenye PhD za sheria, uchumi na diplomasia. Huku wengine wakiwa na shahada kwenye masomo ya ulinzi, usalama na sayansi za vita wakiwa na akili timamu kabisa, wakaamua kuwa wapumbavu. Wakatundika elimu zao nyuma ya milango na kuanza kutekeleza jambo ambalo hata watu wa kale walioishi miaka 2000 hawakuwahi kuliwaza. Tanzania ina matatizo mengi, lakini ilikuwa inarekebishika vizuri tu kwasababu waliofikisha nchi yetu hapa wanafahamika na tunakula na kunywa nao kila siku.

Kuanza kulaumu mabeberu peke yake haisaidii kwasababu kuna wenzetu ambao wamefanikiwa kutumia mifumo hii-hii ya mabeberu kuwashinda mabeberu kiuchumi, kiulinzi na kisiasa. Ukweli ni kwamba huu mfumo umejengwa na mabeberu lakini hata walioujenga hawaundeshi wanavyotaka wao. Mataifa ya Magharibi ndiyo waanzilishi wa World Trade Organization (WTO) lakini leo hii, WTO imemnufaisha Uchina kuliko tangu alivyojiunga nao mwaka 2001 na mpaka sasa wanajutia kumkaribisha.

Nchi kama Singapore, India, Korea-Kusini na Brazil wamewezaje kucheza vizuri kwenye huu mfumo wa mabeberu hadi kufikia kuwango cha kuwashinda mabeberu kwenye baadhi ya mambo ??? Inahitaji akili ya ziada kutoka kwa Mungu ili kuweza kucheza kwenye huu mfumo. Raisi Donald Trump alijaribu kuitoa Marekani kwenye huu mfumo wa Vienna, lakini pamoja na maguvu yote ya Marekani alifanikiwa ???

Lakini leo hii kuna watu wako ndani ya IDARA ZA USALAMA ZA TANZANIA waliamini kabisa kwamba Tanzania inaweza kujitenga na dunia bila kupata madhara. Yaani waliamini kabisa na wengine bado wanaamini kabisa. Kuna wengine bado wanaamini kwamba mfumo wa Kileninisti na Kimaksisti (Marxist-Leninism) unaweza kutumika kuikomboa Tanzania. Sawa, lakini hata walioutuletea huu mfumo Warusi na Wachina, wamebadilisha sana baadhi ya hizi falsafa.

Dunia ya nchi moja kutawala wengine (Uni-Polar World) au nchi mbili kuamulia dunia nini kifanyike (Bi-Polar World) unakufa taratibu, ndiyo maana Marekani na Urusi wanapata shida kukubaliana na huu ukweli. Wao kama mataifa hawaanguki na bado wana nguvu, ila tu ni kwamba mataifa yale madogo na masikini kama Vietnam, Poland, Mexico yamekuwa makubwa yenye uchumi unaokua kwa kasi sana.

Tanzania tuliachiwa mtaji mkubwa sana kidiplomasia, ambao ulitujengea SOFT-POWER na INFLUENCE ambayo ilifanikisha ulinzi na usalama wa Tanzania kikanda na kidunia kwa kiwango kikubwa sana. Tuliingia sehemu ambazo hata nchi kubwa hazikuweza kuingia, tulipata taarifa nyeti kabla hata baadhi ya mataifa makubwa hayajazipata, tulipewa heshima ya kipekee (Special Treatment) ambayo mataifa mengine yenye uchumi mkubwa kuliko sisi barani Afrika hayakupewa.

Tuliogelea bwawa moja na mababeru, wakomunisti, wajahidina na wazayuni lakini tulitoka salama, kesho tena tukarudi kuogelea. We were a Shrimp among Whales, lakini bado tuliheshimika mno. Lakini leo hii hebu angalia, ile nguvu yote ambayo Mzee Nyerere na Raisi Mkapa walitutengenezea, imemomonyoka kisa kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uelewa mpana wa mahitaji ya nchi yetu na nafasi yetu hapa ulimwenguni.

Binafsi naamini ili tuweze kutoka hapa tulipo ni lazima NYUMBA ISAFISHWE aidha mbele ya majirani au kisiri. Mambo ya UHAINI, KUHODHI MADARAKA, KUPANGA KUUA MARAISI WASTAAFU,KUSHIRIKIANA NA MAADUI WA TAIFA na KUWINDANA KWA KUTUMIA MAKUNDI NDANI YA TASISI ZA KIUSALAMA (Cloack and Dagger Diplomacy) tulikuwa tunayasikia nchi jirani tu: Kwetu sisi yalikuwa ni MWIKO KABISA. Vitendo vya kihaini tulishaachana navyo awamu ya kwanza. Lakini leo kuna kakundi kalifikiri kabisa kangeweza kutupangia sisi Watanzania nani awe Mkuu wa nchi kweli?

Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).

Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....
Mkuu Asante kwa andiko lako, Kwanza nikupongeze kwa kutumia lugha halisi kwenye mazingira ya kiutafiti(ulioufanya)

Kunambo umeyaongea ukwel Ila Kuna mengine umepotosha...

Sasa niamze na ukwel, Ni kwel hatuwezi Kama nchi Kuendelea bila kushirikiana na nchi zingine, hila haliwezekani, na hakuna hata nchi moja ambayo inaweza ku survive, bila kuwa na utegemezi wa nchi nyingne, na kwa kuwa kwangu mtanzania sijawahi kuona awamu yoyote ile iliyojitenga na jamii za kimataifa, ndyo maana tunamabalozi karb nchi zote, na tuna mjumbe(balozi) katika general assembly, UN..

Sasa hoja ya pili kwamba nchi imeingia kubaya, sijui unazungumzia awamu ipi ila Kama ya JPM, hapana, maana Mwamba alitaka kuifanya nchi kujitegemea, kuwa sawa na kujari masilahi ya wananchi, hebu twende kwa mifano mkuu, nchi yetu ndo Kwanza tunaawamu ya 6 yaan tunarais wa 6, tukiwa tunamiak 60 ya Uhuru,je can we compared na nchi USA?? Ambayo inarais wa 47?? Inamiaka zaidi takriban 100+ ya Uhuru?? Je democracy ya kwetu inaweza kuwa sawa na wao??

Mkuu, huwezi kuwa masikini ukacompite na tajiri, hapana unachotakiwa Ni kuwa na akili ili ujikwamue kutoka hapo, na ndicho alichokuwa anakifanya Mwamba,

Sasa tatzo lilikuja wapi?? Ni kwenye mifumo, baada ya JPM kulala, kwa kuwa hatuna mpango wa maendeleo wa mda mrefu, (tuseme miaka 15-30) miladi yote ambayo iliibuliwa na miongozo yote, inawekwa kando taratb lakini kwa uhakika, Nini kinafuata, tunarudi nyuma kwa kasi ya ajabu kubwa na kwa sabab hatuna vision, and planning, for the long term, tunapiga maketime au kurud nyuma,

Itoshe tu kusema, JPM Wala raisi wa awamu yoyote hakuwahi kujitenga na dunia na Wala hatatokea Rais kwa sabb hyo Ni world order, ila kila1 ana application yake tofauti namna ya kuhusiana na mataifa, itoshe tu kusema hvi tz hii inahitaji mtu jasiri kabisa ambae siyo kwamba anaongea kwa karamu, ila anaongea kwa vyote, Tena in strongly voice, vinginevyo kunawatu wamepinda kuiba kwao Wala hawoni shida, kuona wenzao wanaishi Kama wakimbizi si shida, kuwahurumia akina mama wanaoteseka na maji na huduma za afya Wala hawaoni kuwa tatzo..

Mkuu tz itajengwa na wtz wenyewe ila si kwa kwa kulia Lia et msaada, masaada, na Ni dhambi kuomba kitu ambacho unauwezo nacho..

Mr B
 
Mimi hasa ningependa kufahamu mtazamo wako binafsi kuhusu utawala wa Magufuli ulikuwaje na ukoje hivi sasa? Unaweza kurejea michango yako hapa JF kama afanyavyo Pascal Mayalla.
Sijawahi kubadilisha msimamo wangu kuhusu Raisi Magufuli kwasababu naamini katika kweli, lakini pia nina miiko yangu ya maisha ambayo ndiyo mwongozo wangu. Lakini kikubwa ni kwamba nilianza kuwa adui wa watu wengi humu ndani baada ya kuanza kukosoa aina ya utawala wa Magufuli: Hivyo bila hata kufanya rejea kama bwana Mayalla I'M AN OUTCAST and I MUST ADMIT I LOVE THIS MONIKER,........
 
Naamini Tanzania inaweza kuendelea bila kutegemea misaada bali ikabaki tu kuheshimiana na kushirikiana kwenye maendeleo...

Wakubwa wa dunia wanaamini kwenye umafia kwa kuendelea kufanya wengine masikini kwa kutumia baadhibya tools zai kila mahala..Wakubwa wadunia wakigundua una mtazamo tofauti wakuwatoa watu kwenye utumwa wa kiuchumi basi hutumia tools zao na vibaraka waliopandikizwa kila mahala kukumaliza..... WaAfrica tujaribu kuwa real na Uafrica wetu tusishupaze shingo na kubabaika sana na hawa pua ndefu....
Nakubaliana kabisa na wewe, lazima Afrika tujifunze kujitegemea na naamini kabisa hili tunaliweza.
Lakini mbinu za kufika hapo haziwezi kuwa zile ambazo tulizijaribu miaka mitano iliyopita.
 
mkuu inawezekana jamaa kiukweli hakuwavizuri nyanja zote. Lakini isiwe sababu ya kuondoa sifa kubwa alizokua nazo kwa kuanza kumtukana na kuonesha jamaa alikuwa hatendi mazuri. Na pia tusitupilie macho yetu yote kwenye kitu kimoja Kama wewe unavyouweka uhusiano na dunia Kama ndio chanzo cha maendeleo ambacho jpm hufanya nakuona yale aliyo yafanya ni zero. Na pia umesema unatakiwa ujenge ndani na nje ni sahihi lakini sidhani Kama unaweza ukaanza na nje hafu ukafwata ya ndani ni wapuzi tu Hawa wa Sasa ndio mawazo yao. Lakini njia sahihi ni kuimalisha kwanza ya ndani ya nje huja yenyewe sio lazima uzunguke. hebu niambie Kama nyerere dam ambalo lilikuwa ndoto ya mda mrefu likikamilika litavutia wawekezaji wangapi? Naona umeitaja China na marekani kuwa ni maadui na pia Zinafanya biashara nikweli lakini uhusiano alionao China kwa mmarekani sio wakujipendekeza Kama wakwetu ambao mwisho ni unyonyaji mchina aliweka nchi yake Katika mazingira ya uwekazaji mmarekani akavutiwa kwa uwekeza japo walikuwa ni maadui na mbaka Sasa ni maadui lakini wanafanya biashara kutokana na uhitaji. Pia hata hapa kwetu Katika EAC hatukuwa vizuri na Kenya but Kenya wamenunua kwetu mazao kwasababu wanauhitaji. Kwa hiyo hii point yako ya kuangalia Sana uhusiano na dunia huku tukiwa mikono mitupu mm nadhani haiko sawa.
Mimi Malcom Lumumba nitasema ukweli daima, fitna kwangu mwiko. Raisi Magufuli kuna mambo mengi sana aliyafanya vizuri lakini mambo ya nje na diplomasia haviko kwenye hiyo orodha. Dunia yetu ya leo siyo ile ya karne ya 18 na 19 ambayo ulikuwa unaweza kujifungia tu (Isolationism) halafu mambo yakawa yanaenda tu. Tunaishi kwenye ulimwengu wa utandawazi, hivyo ni lazima tunavyojenga ndani na nje tujenge: Lazima kuwe na uwiano mzuri......
 
Nakubaliana kabisa na wewe, lazima tulinde rasilimali zetu kwa WIVU MKUBWA, lakini siyo kutumia ile njia ambayo kipenzi chenu alikuwa anaitumia. Amevuruga mambo na itifikati katika kiwango kikubwa sana,.....

amevuruga kitu gani!!!
mtu mpumbavu akikusoma anawezasema uko timamu kumbe unaumwa kichwa.

unalalamika watu kuchukia mama kusafiri,tukuulize ushirikiano ni kusafiri peke yake!!mtu yuko hewani akirudi makamu karuka lakini umeme na maji hakuna huku.
 
amevuruga kitu gani!!!
mtu mpumbavu akikusoma anawezasema uko timamu kumbe unaumwa kichwa.

unalalamika watu kuchukia mama kusafiri,tukuulize ushirikiano ni kusafiri peke yake!!mtu yuko hewani akirudi makamu karuka lakini umeme na maji hakuna huku.
Anhaa bwana Grinch upo,......???
 
Hivi mtoa mada unadhani kabisa hayo mambo uliyoyaandika hapo juu jiwe angeyajua kweli?

Yeye nje ya mabarabara hakua anajua chochote kile khs Mambo ya diplomasia, uchumi, usalama etc
 
Back
Top Bottom