Ili ufanye harusi au sherehe Moshi lazima ulipe Kodi za Manispaa Tsh. 230,000

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
13,599
22,529
IMG-20240522-WA0057.jpg


Manispaa ya Moshi chini ya Sheria ndogo za (ada na ushuruj ya Mwaka 2019, Tangazo in Serikali Na. 148 la Tarehe 15/02/2019, imeainisha ada na tozo mbalimbali katika kuendesha sherehe kwenye kumbi na maeneo ya starehe.

Mchanganuo wa ada na tozo hizo ni kama ifuatavyo;
  • Tshs. 60,000.00, Kibali cha kufanya sherehe
  • Malipo kutoka kwa mpambaji wa sherehe Tshs. 50,000.00 Tshs. 50,000.00
  • Malipo chakula na vinywaji Tshs. 30,000.00
  • Mshercheshaji wa sherehe (MC) Tsh. 30,000
  • Mpiga picha wa sherehe Tshs. 20,000.00
  • Muziki Tshs. 20,000,00
JUMLA KUU: Tshs 230,000.00

Fedha hizi zinatakiwa kulipwa na Mwenye sherehe ndipo apatiwe kibali cha kuendesha sherehe husika. Aidha mmiliki wa Ukumbi anapaswa kuhakikisha kwamba Mwenye sherehe anakupatia nakala ya kibali kabla ya kumruhusu kutumia Ukumbi. ANGALIZO: Iwapo wakala hatakuta kibali ukumbini, sherehe itazuiwa kufanyika kuanzia muda huo.

Kwa barua hii namtambulisha kwenu ULOFAMO AUCTIONEER AND COURT BROKERS LTD, wakala atakayehusika na usimamizi wa ukiukwaji wa ada na tozo tajwa kifungu cha 3 hapo juu.
 
Kaimu Mkurugenzi 😳

Mkurugenzi ni mteule wa Rais, Kaimu Mkurugenzi anateuliwa na nani na majukumu yake ni yameainishwa wapi?.

Na anashika madaraka hayo kwa muda au kipindi Gani?.

Je anaruhusiwa kusainishwa mikataba na nyaraka zipi akiwa kwenye nafasi hiyo?

Au ndio muda wa kupitisha magendo?
 
Hizo hela zinapelekwa wapi? Angechanganua vizuri sio kuwaacha watu kwenye sintofahamu ya ajabu ajabu unakusanya Pesa hausemi unazipeleka wapi nani atakuelewa?
 
Kwa kweli nchi ikikosa watu makini wenye ubunifu na malengo halisi ya kusaidia nchi haya ndio matokeo yake.
 
Mimi naona yuko sahihi.
Ndoa ni mpango wa Mungu ila haya maharusi (masherehe) ya kileo ni mpango wa Ibilisi.
 
Siku hizi taarifa za makusanyo katika Migodi, Mbuga, Misitu husikii
Full kutusumbua wahangaikaji.
 
Wana discourage watu wasioe. Tusubiri ongezeko la single moms
Hajakataza ndoa, kufunga ndoa hakuna gharama. Ni hharusi ndizo anataka mulipe tozo.
Hizi hharusi ni mpango wa shetani ili watu waogope kuoa kwasababu ya gharama zake . Vijana wanabaki wanaziniana tu mpaka nyuma wanapeana na hawaoani
 
Back
Top Bottom