Linguistic
JF-Expert Member
- Mar 16, 2021
- 3,671
- 8,237
Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni leo tarehe 20 Mei, 2021 atafanya ziara ya kikazi ya siku 1 hapa nchini kwa Mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Akiwa hapa nchini Mhe. Rais Museveni na Mhe. Rais Samia watashuhudia utiaji saini wa mikataba ya utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta la kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni za uwekezaji katika mradi huo (Host Government Agreement) utakaofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:00 asubuhi.
========
Shughuli inaanza kwa nyimbo za Taifa na wimbo wa Afrika Mashariki. Gerson Msigwa anaanza kwa kutoa ufafanuzi wa wingi wa mikataba inayosainiwa kwenye bomba hilo.
Msigwa amefafanua mkataba wa leo ni makubaliano kati ya nchi ya Tanzania na kampuni itakayotekeleza mradi, amesema miradi mikubwa kama huu wa mafuta unaohusisha zaidi ya pande moja huambatana na utiaji saini wa mikataba kadha kadha hivyo hakuna kujirudia kwa utiaji saini wa mikataba.
Mkataba wa bomba la mafuta umetiwa saini na waziri wa nishati, Medard Kalemani shuhuda akiwa mwanasheria mkuu wa Tanzania, Prof. Kilangi na kwa upande wa kampuni ya EACOPP ni mkuregunzi mkuu wa kampuni hiyo, Martin John na atashuhudiwa na rais wa utafiti na uzalishaji wa Total Afrika, Nicholaus Teraz.
Rais Samia Suluhu Hassan
“Rais Museveni sio Mgeni Tanzania, ameishi hapa, amepata Elimu yake ya Chuo Kikuu hapa na hata baadhi ya Watoto wake amepatia hapa kwahiyo huyu ni nusu Mtanzania na nusu Mganda, tunamkaribisha sana”
“Hayati Magufuli na Museveni walianza mchakato wa mradi huu wa ujenzi wa bomba la mafuta la Hoima - Tanga na Mimi nimekuja kuuendeleza, mradi huu una faida nyingi ikiwemo pia kuwapatia ajira Wananchi wetu”
“Nakushukuru Rais Museveni kwa kuja licha ya changamoto ya Corona, asante nilikuwa na wasiwasi ila umenithibitishia nyumbani ni nyumbani,najua umekuja kutokana na uzito wa mradi huu wa bomba la mafuta, Watanzania wamesikia maneno kwa miaka 5 tuache maneno tukatekeleze”
“Kuna mambo yanashangaza kulikuwa na sheria wote tusajili laini tuweke vidole ili Mtu akifanya utapeli ajulikane lakini utapeli wa mtandao unaendelea na Watu hawafikishwi Mahakamani, sasa ule usajili ulikuwa kiini macho au nini!? Maana wote tumesajili na majina yapo.
Yoweri Museveni
“Mimi naelewa kiswahili lakini nimesafiri na Wazungu weusi nilionao hapa kutoka Uganda wanajifanya hawaelewi Kiswahili na masikio yanawauma kwa vitu walivyoweka masikioni”
“Sekta muhimu nne ni Kilimo ambacho utapata chakula na utajiri, sekta ya pili ni viwanda, sekta ya tatu ni service (huduma), sekta ya nne ni ICT, sekta hizi zinataka miundombinu kama barabara, umeme, nishati na hizi sekta zote haziwezi kuendelea bila soko”
“Wananchi wa Uganda na Tanzania wasilewe na sekta ya mafuta na gesi wakasahau sekta nyingine kama kilimo, ICT, viwanda n.k, kwasababu mafuta yanaisha lakini kilimo, utalii vinaendelea kwahiyo tutumie rasilimali zenye ukomo kuendeleza rasilimali endelevu”
========
Pia soma
Akiwa hapa nchini Mhe. Rais Museveni na Mhe. Rais Samia watashuhudia utiaji saini wa mikataba ya utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta la kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni za uwekezaji katika mradi huo (Host Government Agreement) utakaofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:00 asubuhi.
========
Shughuli inaanza kwa nyimbo za Taifa na wimbo wa Afrika Mashariki. Gerson Msigwa anaanza kwa kutoa ufafanuzi wa wingi wa mikataba inayosainiwa kwenye bomba hilo.
Msigwa amefafanua mkataba wa leo ni makubaliano kati ya nchi ya Tanzania na kampuni itakayotekeleza mradi, amesema miradi mikubwa kama huu wa mafuta unaohusisha zaidi ya pande moja huambatana na utiaji saini wa mikataba kadha kadha hivyo hakuna kujirudia kwa utiaji saini wa mikataba.
Mkataba wa bomba la mafuta umetiwa saini na waziri wa nishati, Medard Kalemani shuhuda akiwa mwanasheria mkuu wa Tanzania, Prof. Kilangi na kwa upande wa kampuni ya EACOPP ni mkuregunzi mkuu wa kampuni hiyo, Martin John na atashuhudiwa na rais wa utafiti na uzalishaji wa Total Afrika, Nicholaus Teraz.
Rais Samia Suluhu Hassan
“Rais Museveni sio Mgeni Tanzania, ameishi hapa, amepata Elimu yake ya Chuo Kikuu hapa na hata baadhi ya Watoto wake amepatia hapa kwahiyo huyu ni nusu Mtanzania na nusu Mganda, tunamkaribisha sana”
“Hayati Magufuli na Museveni walianza mchakato wa mradi huu wa ujenzi wa bomba la mafuta la Hoima - Tanga na Mimi nimekuja kuuendeleza, mradi huu una faida nyingi ikiwemo pia kuwapatia ajira Wananchi wetu”
“Nakushukuru Rais Museveni kwa kuja licha ya changamoto ya Corona, asante nilikuwa na wasiwasi ila umenithibitishia nyumbani ni nyumbani,najua umekuja kutokana na uzito wa mradi huu wa bomba la mafuta, Watanzania wamesikia maneno kwa miaka 5 tuache maneno tukatekeleze”
“Kuna mambo yanashangaza kulikuwa na sheria wote tusajili laini tuweke vidole ili Mtu akifanya utapeli ajulikane lakini utapeli wa mtandao unaendelea na Watu hawafikishwi Mahakamani, sasa ule usajili ulikuwa kiini macho au nini!? Maana wote tumesajili na majina yapo.
Yoweri Museveni
“Mimi naelewa kiswahili lakini nimesafiri na Wazungu weusi nilionao hapa kutoka Uganda wanajifanya hawaelewi Kiswahili na masikio yanawauma kwa vitu walivyoweka masikioni”
“Sekta muhimu nne ni Kilimo ambacho utapata chakula na utajiri, sekta ya pili ni viwanda, sekta ya tatu ni service (huduma), sekta ya nne ni ICT, sekta hizi zinataka miundombinu kama barabara, umeme, nishati na hizi sekta zote haziwezi kuendelea bila soko”
“Wananchi wa Uganda na Tanzania wasilewe na sekta ya mafuta na gesi wakasahau sekta nyingine kama kilimo, ICT, viwanda n.k, kwasababu mafuta yanaisha lakini kilimo, utalii vinaendelea kwahiyo tutumie rasilimali zenye ukomo kuendeleza rasilimali endelevu”
========
Pia soma
- Marais Museveni na Magufuli wakubaliana kujenga bomba la mafuta
- Rais Magufuli na Museven kuzindua mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda wiki ijayo
- Chongoleani, Tanga: Rais Magufuli na Museveni waweka la jiwe la Msingi mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima - Tanga
- Ujenzi wa Bomba la Mafuta: Ziara ya Rais Museveni nchini Tanzania - Septemba 13, 2020
- Serikali za Tanzania na Uganda zatiliana saini mkataba wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta
- Tanzania yasaini mkataba wa ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima, Uganda
- Kampuni ya Uchimbaji mafuta Uganda yavunja Mkataba na TOTAL. Je, maslahi yetu kwenye Bomba la Mafuta yatakuwaje?
- Kampuni ya Uchimbaji mafuta Uganda yavunja Mkataba na TOTAL. Je, maslahi yetu kwenye Bomba la Mafuta yatakuwaje?