Chamoto
Platinum Member
- Dec 7, 2007
- 9,856
- 22,190
.Dar es salaam ni mji wa hovyo mchafu hakuna sehem ambazo ni smart kote uchafu mitaro hovyo taka zimejaa rambo zinazagaa mtaani pa1 na Gaborone kua na wakaz wachache ni moja ya town la maana,pia Francistown kumetulia sana.
Ila kufananisha investment ya mji wa watu 200k na 5M siyo sahihi kabisa. Dar es salaam mbona ulikuwa mji uliopangwa vizuri tuu na msafi? Ni baada ya viwanda mikoani kufa na watu wengi kukimbilia jijini ndiyo mambo yakaharibika.
.bali ni upeo aliokuwa nao huyo raisi wa kwanza Sir Seretse Khama
Ilikuwa rahisi kufanya mambo mazuri na kwa haraka kwasababu jamii yao kwa kiasi kikubwa ilikuwa moja (watsana 80%) na wengi wao wakiwa na imani moja. Watu kuwa wamoja teyari ni hatua kubwa ya maendeleo.
Pia imani ya uchifu ilisaidia, kwa kuwa chifu ni kama mungu mtu, akisema hivi hakuna wakubisha. Sasa sisi kwetu ilibidi tuanze kujenga 'Identity' mpya (waswahili) halafu tulitumia resources zetu nyingi kuwa komboa wengine na hivyo kupunguza shabaha ya maendeleo kwetu.
Nchi yao pia, miaka ya 60's haikuwa tishio katika ukanda wa kusini kwahiyo haikusumbuliwa na kuingiliwa na wakubwa.