Yule jamaa wa CUF amezungumza jambo moja la nsingi sana. PESA, siasa za kitanzania na kiafrika kwa ujumla ni pesa tu, wananchi wengi hasa hawa wa vijijini wana uelewa mdogo juu ya katiba na maendeleo kupiga kampeni kazi bure, unaweza kupata kura zao kwa kuwarubuni na vijizawadi vidogo-vidogo, hata buku kumi kumi wanakugaia kura.
Huo ndio ukweli na ndio strategy pekee inayofanya kazi kwa sasa. Hadi pale wananchi walio wengi watakapoelimishwa na wakafahamu sababu za umasikini wao nachelea kusema mambo yatakuwa yanajirudia hivi kila chaguzi.
Itachukua muda zaidi ya tunavyofikiria unless Chadema wakubali falsafa ya if you can't beat them join them nao waanze kampeni ya mapesa ama waanze kufanya kazi ya ziada kupeleka elimu ya maendeleo kwa wananchi wa mikoani na vijijini, venginevo hiyo 2015 mambo yatakuwa ni yale-yale
. Money Talk- Hata Rostam akisema arudi kugombea atashinda tena kwa vile ana hela na yuko tayari kuitumia, huo ndio ukweli.