The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,800
Tangu Rais Magufuli aingie madarakani kumekuwa na malalamiko ya chinichini miongoni mwa Watanzania kuhusu hali ya kiuchumi kuwa ngumu. Ugumu huo ulizaa msemo ‘’vyuma vimekaza’’, jambo lililokemewa vikali na Mheshimiwa wa ngazi za juu.
Sasa basi, kufuatia hali ya kiuchumi kuendelea kuwa ngumu, mwananchi mmoja huko wilayani Igunga Mkoani Tabora, kwa nafasi adimu na adhimu aliyoipata ya kumweleza jambo Rais, amewasilisha malalamiko ya wengi.
“Maisha ni magumu fedha hakuna watu wana hali mbaya; akina mama wananyang’anywa televisheni, friji kwa ajili ya mikopo. Tunaomba mheshimiwa tuachie fedha mengine yote hatuna tatizo na wewe,” amesema mjasiriamali huyo.
Baada ya kutoa majibu ya matatizo mengine yanayowakumba wanaIgunga, Rais akajibu:
“Usipofanya kazi hela zitaisha tu. Ukitaka hela fanya kazi. Wapo wanaolima mpunga sasa hivi na baada ya miezi kadhaa watapata hela. Sasa wewe unakaa hapa kijiweni kila siku unalalamika kuhusu hela.”
“…cha bure hakipo, hata mimi sina. Kinachotakiwa ni kuchapa kazi, na hata maandiko yanasema hivyo. Asiyefanya kazi na asile.”
“…umeme umefungwa hapa. Waliokuwa wanachimba mashimo si walikuwa wanalipwa hela? Lakini kuna waliokuwa wamekaa wanatazama tu. Wapo wanaochimba mitaro ya barabara, wapo wanaolima pamba...”
“…kalime hata viazi au matikiti maji, ukisimama hapa yataliwa tu hata mpaka Dar es salaam. Lakini kiukweli vya bure vimeisha na bado vitaisha zaidi...”
“…nenda hata kwenye machimbo. We unataka mkono wako uwe soft alafu unataka hela – haipo!”
“…kwahiyo ndugu zangu, mimi sijaja kuleta hela, nimekuja kuhimiza kufanya kazi...”
“…serikali inatafuta fedha kwa ajili ya huduma muhimu za jamii na si kwa ajili ya kukulisha wewe na mke wako...”
Rais yupo njiani kuelekea Shinyanga
Sasa basi, kufuatia hali ya kiuchumi kuendelea kuwa ngumu, mwananchi mmoja huko wilayani Igunga Mkoani Tabora, kwa nafasi adimu na adhimu aliyoipata ya kumweleza jambo Rais, amewasilisha malalamiko ya wengi.
“Maisha ni magumu fedha hakuna watu wana hali mbaya; akina mama wananyang’anywa televisheni, friji kwa ajili ya mikopo. Tunaomba mheshimiwa tuachie fedha mengine yote hatuna tatizo na wewe,” amesema mjasiriamali huyo.
Baada ya kutoa majibu ya matatizo mengine yanayowakumba wanaIgunga, Rais akajibu:
“Usipofanya kazi hela zitaisha tu. Ukitaka hela fanya kazi. Wapo wanaolima mpunga sasa hivi na baada ya miezi kadhaa watapata hela. Sasa wewe unakaa hapa kijiweni kila siku unalalamika kuhusu hela.”
“…cha bure hakipo, hata mimi sina. Kinachotakiwa ni kuchapa kazi, na hata maandiko yanasema hivyo. Asiyefanya kazi na asile.”
“…umeme umefungwa hapa. Waliokuwa wanachimba mashimo si walikuwa wanalipwa hela? Lakini kuna waliokuwa wamekaa wanatazama tu. Wapo wanaochimba mitaro ya barabara, wapo wanaolima pamba...”
“…kalime hata viazi au matikiti maji, ukisimama hapa yataliwa tu hata mpaka Dar es salaam. Lakini kiukweli vya bure vimeisha na bado vitaisha zaidi...”
“…nenda hata kwenye machimbo. We unataka mkono wako uwe soft alafu unataka hela – haipo!”
“…kwahiyo ndugu zangu, mimi sijaja kuleta hela, nimekuja kuhimiza kufanya kazi...”
“…serikali inatafuta fedha kwa ajili ya huduma muhimu za jamii na si kwa ajili ya kukulisha wewe na mke wako...”
Rais yupo njiani kuelekea Shinyanga