tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,859
- 18,282
Hata mbuyu ulianza kama mchicha, ndivyo unavyoweza kusema. Nipo kwenye basi natokea Songea kwenda Mwanza, safari nzima tunasikilizishwa nyimbo na video za kihuni za bongo flava mwanzo mwisho. Baadhi ya nyimbo zinazopigwa humu ni hizi:
1. Kila demu ana matako.
2. Nataka kunya
3. Nitongoze
4. Nipe tamu yangu
5. Finyia ndani
6. Hapo kati
Wewe fikiria nyimbo za kipumbavu na kipuuzi kama hizi zinapigwa na kuchezwa hadharani kwenye video. Maadili ya jamii yatabaki salama? Ukija kwenye video ndiko kwenye balaa zaidi. Mabinti wanacheza uchi huku wakishikwashikwa matiti na makalio hadi kero. Tukienda na mwendo huu hadi 2030, jamii itakuwa imeharibiwa sana na nyimbo hizi za ajabu ajabu.
Watu hadi tunashindwa kusafiri na watoto pamoja na wakwe zetu kwa sababu ya kuogopa kuaibika kutazamishwa video za kingono zinazochezwa kwenye mabasi haya. Chanzo kimojawapo cha kusambaza uharibifu wa maadili potovu yaliyomo kwenye nyimbo za bongo flava ni kupitia mabasi ya daladala na haya ya mikoani
Ifike wakati serikali ipige marufuku nyimbo na video hizi za kihuni kupigwa kwenye mabasi ili kuepuka kusambaza sumu ya uharibifu wa maadili katika jamii. Mwisho wa siku serikali itakuja kuwalaumu wazazi wakati yenyewe ndiyo imeshindwa kusimamia utaratibu wa kistaarabu na kimaadili ktk jamii.
Tujifunze kutokana na makosa ya wengine. Wazungu waliruhusu mfumo wa maisha huria kwa raia wa nchi zao lakini sasa wanalia baada ya maadili ya jamii kumomonyoka kwa kiwango kisichorekebika.
Hata kama vyama vya siasa vimekuwa vikiwatumia wasanii kuimba nyimbo hizi za ovyo kwenye kampeni za kisiasa, wakati umefika sasa serikali iache kuharibu maadili ya jamii kwa kisingizio chochote kile. Tusipiziba ufa ipo siku tutajenga ukuta.
1. Kila demu ana matako.
2. Nataka kunya
3. Nitongoze
4. Nipe tamu yangu
5. Finyia ndani
6. Hapo kati
Wewe fikiria nyimbo za kipumbavu na kipuuzi kama hizi zinapigwa na kuchezwa hadharani kwenye video. Maadili ya jamii yatabaki salama? Ukija kwenye video ndiko kwenye balaa zaidi. Mabinti wanacheza uchi huku wakishikwashikwa matiti na makalio hadi kero. Tukienda na mwendo huu hadi 2030, jamii itakuwa imeharibiwa sana na nyimbo hizi za ajabu ajabu.
Watu hadi tunashindwa kusafiri na watoto pamoja na wakwe zetu kwa sababu ya kuogopa kuaibika kutazamishwa video za kingono zinazochezwa kwenye mabasi haya. Chanzo kimojawapo cha kusambaza uharibifu wa maadili potovu yaliyomo kwenye nyimbo za bongo flava ni kupitia mabasi ya daladala na haya ya mikoani
Ifike wakati serikali ipige marufuku nyimbo na video hizi za kihuni kupigwa kwenye mabasi ili kuepuka kusambaza sumu ya uharibifu wa maadili katika jamii. Mwisho wa siku serikali itakuja kuwalaumu wazazi wakati yenyewe ndiyo imeshindwa kusimamia utaratibu wa kistaarabu na kimaadili ktk jamii.
Tujifunze kutokana na makosa ya wengine. Wazungu waliruhusu mfumo wa maisha huria kwa raia wa nchi zao lakini sasa wanalia baada ya maadili ya jamii kumomonyoka kwa kiwango kisichorekebika.
Hata kama vyama vya siasa vimekuwa vikiwatumia wasanii kuimba nyimbo hizi za ovyo kwenye kampeni za kisiasa, wakati umefika sasa serikali iache kuharibu maadili ya jamii kwa kisingizio chochote kile. Tusipiziba ufa ipo siku tutajenga ukuta.