KERO Idara ya Uhamiaji Arusha unaomba Pasipoti leo unaambiwa usubiri miezi mitano au 6, inaumiza sana hii!

KERO Idara ya Uhamiaji Arusha unaomba Pasipoti leo unaambiwa usubiri miezi mitano au 6, inaumiza sana hii!

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
654
Reaction score
1,598
Ofisi ya Idara ya Uhamiaji Mkoani Arusha mnatuumiza sana, pasipoti unaomba Januari unaambiwa usubiri Miezi 5 mpaka 6 sababu foleni ni kubwa.

Mara karatasi za ku-print zimeisha au kuna Maafisa wanakwambia utoe laki wakusaidie ku-push upate pasipoti kwa haraka.

Kuna nini kinaendelea hadi document hiyo ambayo ni haki kwa Mwananchi inachukua muda mrefu sana kukamilika, bora wangesema au kuwa wazi nini hasa ambacho kinaendelea.

Pia soma:
~ Uhamiaji wanakera kwa kuchelewa kutoa hati za kusafiria
~ Maafisa na Askari wa Uhamiaji tunateseka kwa uhamisho bila malipo
~ Kuna harufu ya rushwa Idara ya Uhamiaji kutumika kuhuisha vibali kwa raia wa China waliomaliza muda wa kuwepo nchini
~ Baadhi ya Maafisa wa Uhamiaji Wilaya ya Muleba wanatumia 'Road Barrier' kula rushwa
 
Mbona muda mrefu hivyo, wanataka rushwa au nini? Bora hata ingekuwa mwezi mmoja tu ingetosha
 
Mkuu ukiingia serikalini utaona jinsi rushwa ilivyo tamu sababu ya tamaa za wahusika. Pole kwa usumbufu
 
Connection mkuu. Mzee wa kulilia kushangiliwa akipiga simu moja tu document zote zinakamilika ndani ya masaa machache
Ila Simba na Yanga wakimbadilishia uraia mchezaji chap anapewa hati ndani ya muda mfupi
 
Duh inasikitisha sana. Na unalipia Tzs 150,000. Wakitoa passport 1000 kwa siku nchi nzima wanapata Tzs 150,000,000 hawaoni mapato yapo nje nje au gharama za kutengeneza zinazidi Tzs 150,000?
 
Duh inasikitisha sana. Na unalipia Tzs 150,000. Wakitoa passport 1000 kwa siku nchi nzima wanapata Tzs 150,000,000 hawaoni mapato yapo nje nje au gharama za kutengeneza zinazidi Tzs 150,000?
Ccm na disciples zake hawaja wahi kuwa na akili
 
Duh inasikitisha sana. Na unalipia Tzs 150,000. Wakitoa passport 1000 kwa siku nchi nzima wanapata Tzs 150,000,000 hawaoni mapato yapo nje nje au gharama za kutengeneza zinazidi Tzs 150,000?
Wanapaswa watoe passport hata Milioni 10 ili wapate pesa
 
Back
Top Bottom