Nimecheka kinoma! 😊
Kuna mwanetu aliomba msaada hapa ishu ya usikivu miaka imepita kidogo, basi na mimi nikaguswa na suala lake, nikamfuata PM, lengo lilikuwa ni kumwezesha aje mjini, akutane na specialist, ambaye pia ni mshikaji wangu na apate hearing aids. Nilipompa hilo wazo, hakulikataa ila akadai yupo bize anamuuguza mke wake, hivyo angekuja baadae, lakini hili la kuja halikuwahi tokea. Akanambia kuhusu situation yake kimaisha, ikabidi niwe nampiga kiume. Sasa akaja badae kuniambia amepata chance aje mjini, na kwamba familia yake anaipeleka Mwanza, hivyo atahitaji nauli, yake na familia yake n.k. Basi nikampa fedha ambayo niliona itamfaa kusafirisha familia, na yeye kuja mjini. 😊
Huo ndio ukawa mwisho wa mimi kuwasiliana nae. Hakupatikana hewani kwa namba zote, na ID yake hajawahi jibu sms mpaka hii leo. 😊
Na kweli tatizo la usikivu alikuwa nalo. Huwa nabaki tuu kucheka nikikumbuka hiki kisa.