IBTimes: Who is Maxence Melo arrested for not disclosing anonymous sources?

IBTimes: Who is Maxence Melo arrested for not disclosing anonymous sources?

Mkuu Barbarosa,

Labda tujiulize kwa pamoja, kwa nini kuna waandishi wa habari kutoka hayo mataifa (kwa wazungu) hapa nchini kwetu? Majukumu yao ni nini? Je, kwa upande wako, kwa uzito huu huu unaoona sio sawa kwa suala la Maxi kuhusisha wazungu, vipi viongozi wa serikali yetu wanapofanya nao mahojiano na taarifa za serikali kurushwa huko kwao? Mheshimiwa Rais wa awamu ya Tano, alipofanya mkutano na Wahariri pale Ikulu, miongon mwa waandishi waliohudhuria walikuwa ni wa vyombo vya habari kutoka kwa "wazungu", hili unalisemeaje?

Kaka ...


Kuna tofauti kubwa kati ya Wazungu kutuma Waandishi wao wa Habari ili kupata Habari zetu na sisi kuwatafuta na kuwapekea habari zinazotuhusu, hivyo vitu viwili tofauti!
 
Lkn mwisho wa siku tutapoteza wote kama unachukulia Libya au Iraki kama mfano hivyo hata hicho unachotaka kukipata hautakipata lkn ukizungumza na kutambua na kuheshimu Mamlaka ikiyopo uwezekano wa kufika mbali ni mkubwa!
Haya mambo hayataki hasira Serikali na Raisi wa JMTZ ndo walioshika mpini na huo ndio ukweli!

Hakuna mtu amepata negative press kama Mugabe lkn hao akina Tsvangirai wako leo hii? Wazungu wenyewe wameshawapotezea ...
Mkuu,

Mkuu wa nchi amewahi kutumia mifano ya nchi za Libya, Iraq, Syria akihusianisha na muktadha huo huo.

Kaka ...
 
Next year Melo atakuwa moja wa watu watakaopewa tuzo ya Nobel peace prize kwa ili tujisahihishe
 
Lkn mwisho wa siku tutapoteza wote kama unachukulia Libya au Iraki kama mfano hivyo hata hicho unachotaka kukipata hautakipata lkn ukizungumza na kutambua na kuheshimu Mamlaka ikiyopo uwezekano wa kufika mbali ni mkubwa!
Haya mambo hayataki hasira Serikali na Raisi wa JMTZ ndo walioshika mpini na huo ndio ukweli!

Hakuna mtu amepata negative press kama Mugabe lkn hao akina Tsvangirai wako leo hii? Wazungu wenyewe wameshawapotezea ...
Mkuu,

"Mpini" unaomaanisha ni sheria mama i.e. Katiba? Utaunga mkono "serikali" ikifanya lolote kinyume na Katiba?

Kaka ...
 
I wonder what is he doing in-here if he doesn't want people to speak-up to their government, no matter what they say! He should be banned from this forum b'cause he's against the forum's MOTTO "where we dare to talk openly". Mods, do we need these kind of people here esp. in times like these?
Mkuu,

Here (In this forum) is where we dare to "speak" openly. He, like anyone else, has the right to be here as well.

Kaka ...
 
nawashauri mods wawaondoe wanafiki wote wanaoshangilia hili jambo kama huyu BARBOSA,ISIS na wengineo,hawa ndio wanaoichongea jf kwa mabwana zao na wanalipwa kwa kazi hii tu.watu wabaya sana hawa!...ni wakua nao makini.
Mkuu,

Naomba nitofautiane na ushauri wako kwa mfano huu; Kwa nini tunafanya mitihani? Ili kujua kiwango cha uelewa cha mtihaniwa katika lile analofanyia mtihani. Basi wote tukiwa humu inasaidia pia kufahamu dhana, itikadi na mrengo wa kila mmoja wetu kwa namna tunavyojibainisha.

Kaka ...
 
Siku zote serikali za Africa huwa aziogopi wala kutikisika kwa vyombo vya habari vya nje tuombe mungu tu Melo wamwachie tu lakini kama serikali ikiamua JF ndo uwe mwisho wake hakuna kupinga wala kuzuia si CNN,FOX ,SKY NEWZ,DW,VOA,BBC na WikiLeaks kumbuka kuna wakina Julian Assange wanaishi kama digidigi kwa kutoa taarifa za serkali
 
Magufuli anahusika na hili? Hii Sheria ilipitushwa na Bunge ambapo Wapinzani walikuwepo sasa iweje uje kumlaumu Raisi kwa utekelezaji wa Sheria halali? Ndiyo maana hata Wazungu wenu wanawapuuzia kwa maana hamna hoja!
Mkuu Barbarosa

Naomba ufafanuzi (wako) wa kauli hii " hii sheria ilipitishwa na bunge ambapo wapinzani walikuwepo". Halafu nitarudi kujenga hoja baada ya kupata ufafanuzi wako.

Kaka ...
 
Lakini haijawahi kusaidia kitu, kama kuna chochote cha kujifunza basi mngejifunza kwa Maalimu Seifu amezunguka Miji Mikuu ya Wazungu karibia yote kutaka Nchi yetu iwekewe vikwazo na Wazungu, na nini kimetokea? Sasa hivi kajichokea kaamua kukaa zake nyumbani!
Mkuu,

"Nyerere" alizunguka nchi hizo hizo za wazungu na hatimaye tukapatiwa uhuru.

Kaka ...
 
1206446dfce8c144bf3c9753cdd9f6e9.jpg


Wahindishi wa habari wanatakiwa kuelimishwa sio kuwakamata.

Tukikosea tuelimishane. Huu ndio Utamaduni wetu.

Iran, Saudi Arabia, Rwanda, Misri, China na nchi nyingi duniani zinapingwa na Jumuia ya Kimataifa kwa tabia hizi za kuwakamata wahandishi wa habari. Tanzania yetu tusiingize kwenye orodha hiyo.


Tunayozungumza hapa sio lazima tuwe nchini Tanzania. Mahali popote pale kwenye Internet basi kutakuwa na sauti ya mwanaadamu.
Kumjua nani ni nani, haisaidii lolote maana wako wengine wako nchini Canada, Ungereza na hata Marekani, haya yanayozungumzwa hapa ni mazungumzo ya kawaida katika jamii na vyombo vikubwa vya habari.

Afrika tuwache uonevu wa wahandishi wa habari. Kupambana na vyombo vya habari vinavyosema uongo, polisi au jela sio dawa, tunatakiwa tujipange na ukweli na sisi pia.

Ukipewa kashfa, lazima uje mbele na kujisafisha.

Ndio maana katika vyou vikuu somo la "Digital Citizen" limeengezeka.

JF inatakiwa kutafuta wafadhili, lifanye shughuli zake nchini Canada hata JF iuzwe kwa Wazungu maana "Mzungu" haguswi.
Nani anadhubutu kumgusa raia wa Marekani au Uingereza?
Ni akina sisi tuu, ukizakiwa Mwafrika basi haki zako fulani zimeshavuliwa. Watu wanajua kuwaonea tuu Waafrika.

Mtanzania pia ni Binaadamu.
 
Njia mbadala ni sisi kutatua matatizo yetu wenyewe, hili mbona linaongeleka nilivyoona Max hajateswa wala kupigwa ina maana yuko mikono salama ni swala la kukaa na Serikali kutafuta muafaka na inawezekana lkn watu wanavyoanza kuzunguka kwa Wazungu kuisema Serikali hakuna watakachofanikiwa kwani Serikali nao watajibu na mwisho wa siku hakuna mshindi!

Mzungu hajawahi kutatua tatizo la Mwafrika hata siku moja bila kuanzisha lingine kubwa zaidi, hivyo kwangu mimi hii ni ishu ndogo na inazungumzika baina ya sisi wenyewe!
Kwa nini unaisemea serikal na hutak Maguful akosolewe hata km anastahili au mungu wenu huko ccm..... naomba unijib haraka kabla nami sijaanza kukufuatilia
 
Bahati mbaya hata zikisikika, mwisho wa yote inaangaliwa sheria za nchi zinasemaje. Ukweli ni kwamba sisi watumiaji wa JF tunaposhindwa kuitumia JF kwa misingi ya haki, usawa, utu na ukweli matokeo yake ndio haya. Binafsi simlaumu Maxence wala Serikali, bali nawalaumu watu wanaoona JF ni kijiwe cha matusi, uzushi na uongo kwa sababu tu wana access ya kuficha identity zao halisi. Binafsi nimetukanwa sana na watu humu hadi nilifika mahali nikataka niache JF. Nakumbuka miaka ya 2010 kurudi nyuma ilikuwa mtu kabla hujapot JF unajitafakari sana kama je hoja yako ina uzito na ukweli? Na hapo ndipo ilikuwa ile mantiki ya JF A HOME OF GREAT THINKERS. Nimekuwa mdau wa JF tangu kabla haijaitwa Jamii Forum, ila ilinichukua muda kujisajili kwa sababu nilijiona bado sina uwezo wa kupost hoja kama walizokuwa wanapost members wa kipindi hicho. Na wala JF haikuwa na matusi, ilikuwa ni hoja kwa hoja tena watu wakidai ushahidi, usipotoa ushahidi BAN ilikuwa inakuhusu. Hii JF ya sasa hivi utoto ni mwingi kuliko GREAT THINKERS

Mkuu,

Ilikuchukua muda kujisajili kwa kuwa "ulijiona huna uwezowa kupost hoja kama walizokuwa wanapost members wa kipindi hicho". Nikisoma bandiko lako najifunza zaidi.

Kaka ...
 
Lkn mwisho wa siku tutapoteza wote kama unachukulia Libya au Iraki kama mfano hivyo hata hicho unachotaka kukipata hautakipata lkn ukizungumza na kutambua na kuheshimu Mamlaka ikiyopo uwezekano wa kufika mbali ni mkubwa!
Haya mambo hayataki hasira Serikali na Raisi wa JMTZ ndo walioshika mpini na huo ndio ukweli!

Hakuna mtu amepata negative press kama Mugabe lkn hao akina Tsvangirai wako leo hii? Wazungu wenyewe wameshawapotezea ...
Typical "black" mind
 
Lkn mwisho wa siku tutapoteza wote kama unachukulia Libya au Iraki kama mfano hivyo hata hicho unachotaka kukipata hautakipata lkn ukizungumza na kutambua na kuheshimu Mamlaka ikiyopo uwezekano wa kufika mbali ni mkubwa!
Haya mambo hayataki hasira Serikali na Raisi wa JMTZ ndo walioshika mpini na huo ndio ukweli!

Hakuna mtu amepata negative press kama Mugabe lkn hao akina Tsvangirai wako leo hii? Wazungu wenyewe wameshawapotezea ...
Ndo tumeamua kupambana nao coz wanatupuuza. WE MJINGA NIMEANZA KUKUCHUKIA ZAID KULIKO HATA UPUUZ HUU UNAOUTETEA
 
Kuna tofauti kubwa kati ya Wazungu kutuma Waandishi wao wa Habari ili kupata Habari zetu na sisi kuwatafuta na kuwapekea habari zinazotuhusu, hivyo vitu viwili tofauti!
Mkuu,

Tofauti hiyo ni ipi?

Kaka ...
 
"They claim what has been posted, include the theft of fuel at the Dar es Salaam Port, corruption in public offices and tax evasion. Probably, those named in the reports complained to the police, wanting the disclosure of the names of subscribers," Ishabakaki said.


Kama kweli mwendokasi wote huu wa Polisi ni kwa Issue hii JP anatakiwa amtumbue mtu jibu cc. Mzee Mwanakijiji .Itakuwa aibu na mwisho wa Vita dhidi ya Ufisadi kufanikiwa.
 
Back
Top Bottom