Ibrahim Traore, Rais kijana, alovuviwa Roho ya Hayati Magufuli, anayepaswa kuigwa na Vijana wa Tanzania. Burkina Faso sasa inachanua

Carlos The Jackal

JF-Expert Member
Feb 6, 2017
24,090
71,562
Unaweza kudhani ni maajabu, ila huo ndio ukweli, Kijana alozaliwa 14/3/1988, aloamua kuchukua Nchi Kwa njia ya mapinduzi mnamo 30/9/2022 .. ni Mwaka mmoja na miezi 6 tuu ila Mzalendo huyu Kijana kaamua kuanzisha safari aloiachia HAYATI Thomasi Sankara.

Kwa watoto wa 2000, Thomas Sankara ni MAGUFULI alokuwepo miaka hiyo akiwa Rais wa Burkina Faso kuanzia 1983 mpaka pale alipouwawa 1988. Ndio Sababu MPINA LUAGA akasema, iundwe tume ya kuchungiza Kifo Cha HAYATI MAGUFULI!!.

Kwa Ufupi, Ibrahim Troure ,Kijana Msomi Kwa msukumo wa matendo ya kigaidi kutoka Kwa Magaidi waloteka maeneo makubwa yenye UTAJIRI wa dhahabu Nchini Burkina Faso, huku Wananchi wakizidi kua masikini ( yaan ni kama hapa Tanzania , tuna Madini ya Kila aina, misitu, mbuga, Sijui mafuta, Gesi , Ardhi, Sijui Milima na vivutio vingi vya utalii, maziwa makubwa , Chuma, makaa ya mawe... Ila bado tulivyo wajinga wapumbavu, tuko masikini wa kutupwa, ila Matajiri ni wachache watoto wa viongozi wa watoto wa walojiingiza siasani miaka ya 1950, Kama BABU YAKO hakuwa mwanasiasa, Wee Kaa kimya tu ).....

Ibrahim Traore, anajiunga na Jeshi ,anafanya ujeshi Kwa Bidii, kujituma ,na Kwa lengo la kuwaondoa Magaidi.

Traore na Rafiki yake Kipenzi DAMIBA , wanapewa jukumu la kuongoza mapambano dhidi ya Magaidi, wanakuta Jeshi limechokaa, halina vifaa, hamna morale, wanajeshi wanaishi Maisha magumu ,wanaamua Kumpindua Rais aliyepo Madarakani Kipenzi Cha wafaransa, na Traore anamruhusu DAMIBA kua Rais, Kwa ahadi ya kuja kuimarisha Jeshi na mapambano dhidi ya Magaidi.

DAMIBA anamsaliti Traore, anaendeleza aloyafanya Mtangulizi wake, mfaransa anazidi kula keki ya Burkina Faso.

Hatimaye sio Hila, Bali Kwa UCHUNGU alonao , IBRAHIM TRAORE anampindua DAMIBA na kua RAIS wa mpito.

Oyaaa, ni mwaka mmoja tu ila IBRAHIM TRAORE anafanya haya..

1👉Ujenzi wa uwanja mpya wa ndege wa kimataifa wa WAGADUGU .. Wasafiri takiriban Million Moja Kwa mwaka watapita hapa..... Maana yake Utalii huooooo.

2👉Ujenzi wa kiwanda cha kusafisha Mchanga wa dhahabu .... Kumbukeni kabla ya Hilo, Jamaa alipiga marufuku uuzaji wa mchanga wa dhahabu nje ( kama Magufuli tu) yeye anataka dhahabu iuzwe kama Dhahabu .

3👉Ujenzi wa Mabarabara, mkisikia Ujenzi wa barabara, basi Burkina Faso unafanya Ujenzi wa Mabarabara Nchini kote, Barabara za kuunganisha Nchi na Nchi, maeneo Kwa maeneo , watu wako saiti usiku na mchana.

4👉Umeme, Jamaa anachukua madaraka, Umeme ukiwa ni kilimo kikubwa..
Oyaaaa, wakati mnasema JPM alikosea kujenga Bwawa, JAMAA najenga SANDINI DAM na ZAGULI SOLAR PARK , miradi hii inaendaje kufuta kabisaa na kufanya kua msamiatu sahaulifu suala la UMEME.

5👉Train za Mwendokasi ( Umeme), Traore anajiona kachelewa, anaona akimbizane na muda, kule Ujenzi wa Umeme wa uhakika, huku Train Mwendokasi ambazo zitaunganisha Burkina Faso na Nchi Jirani, maana yake nini? UWEKEZAJI juu, biashara juu, Uzalishaji juu, utalii juu, Uchumi juuu .

6👉KILIMO ..uwiii hapa ndo usiseme, jamaa kaanzisha programs zake mbili
- Operation Agro-Pastoral Offensive

- The Presidential Initiative for Food Self-Sufficiency.
Lengo ni kua kufikia mwaka Huu 2024, Burkina Faso iwe imejiimarisha suala Zima la chakula.

7👉Ujenzi wa Kituo kipya Cha utalii ( WAGADUGU MUSEUM OF CIVILIZATION)

8👉Jamaa anarusha Satellite Angani itakayokua inafatilia masuala ya mabadiliko ya hali ya hewa kwenye kusapoti kilimo na kupambana na majanga.

9👉VITA DHIDI YA MAGAIDI , Jamaa kwakua Jeshi lilikua halina kitu, anaanzisha Kampeni ya KUOMBA Raia wachangie fedha za kununua vifaa.... Raia sisi tuna Moyo wa kutoa, ila tunataka TUONE tukitoa, vionekane, Oyaaa ,Jamaa kanunua Silaha nzito za kijeshi, kuanzia makombora, ndege vita, ndege zisizo rubani.. Sasa Magaidi wanaikimbia, Jeshi linazidi kuchukua maeneo , watu wanarudi kwenye makazi, Nchi imetulia

👉MIKOPO KWA VIJANA..jamaa anamwaga MIKOPO Kwa Vijana katika kubusti Maendeleo ya Vijana

👉Ujenzi wa Vyuo vikuu, Mahospitali, mashule ndo usiseme !!.

👉Mafisadi, wahujum Uchumi, wezi, Wala rushwa, wakwepa Kodi, kwasasa wanaipata, hao wamefungwa, wengine wanataifishwa Mali walozipata Kwa Jasho la masikin.

Jamaa kaamua kuegemea Mashariki ( Urusi na Uchina ).

Atatoboa? So far, kafanikiwa kukimbia Kifo Mara tano katika majaribio ya kuuawa.

Unakuja Bongo...unakutana na hivi vichwa vya Vijana ....👎

Kabwe....

Nnauye

Makamba

MACHAWA.

Mbowe...

Vijana wanaotafuta Uongozi Kwa sababu ya SIFA, MAGARI YA VING'ORA, UTAJIRI huku Wananchi wakizidi kua masikini.

Wakati huku kwetu, Anasifiwa.kwa.miaka mitatu Et kafanya mambo makubwaaaa, Ibrahim Traore ana mwaka nanusu

Hapo ndipo utaelew, Kuna kua Kiongozi alafu Kuna kua Kiongozi mzalendo, mwenye maono, UCHUNGU, mapenzi, ubunifu, maono, Kiongozi anayewaz Nchi na Wananchi wake kwanza!.

RIP JPM!!.
 
Haya tunawatakia Kila la kheri wafikishe nchi kwenye maisha Bora kwa Kila M burkinabe sisi acha tuendelee kumuongeza Mbowe miaka ili aje kuishinda ccm na upande mwingine tuendelee kumsifia mama kwa kuupiga mwingi na kukipongeza ccm kwa kudumu madarakani
KIGUMU CHAMA CHA MAPINTUSI
KIGUMU!KIGUMU SANA
 
Unaweza kudhani ni maajabu, ila huo ndio ukweli, Kijana alozaliwa 14/3/1988, aloamua kuchukua Nchi Kwa njia ya mapinduzi mnamo 30/9/2022 ...
Kuna Mijinga humiu imekaza mama kaupiga mwingi kaanzisha miradi ya kila namna kumbe moradi hewa,anakumbatia wapigaji na wakwepa kodi ingawa riport za CAG zinafumuka kila siku...Huyu Jamaa alitakiwa kuwa na damu nyingine huku Tamzania....
 
Mkuuu nbona una roho ya kichawi hivi?
Uzaliwe upya ili unielewe..gadafi...samora machel...mandela...sankara..mkapa..magu.,,nyerere..kikwete.,,kenyata...idd amin dada..odinga,,,kenyatta...samia suluhu...hawa wote ni wazalendo haswq...
 
Uzaliwe upya ili unielewe..gadafi...samora machel...mandela...sankara..mkapa..magu.,,nyerere..kikwete.,,kenyata...idd amin dada..odinga,,,kenyatta...samia suluhu...hawa wote ni wazalendo haswq...
Mtoe Samia hapo kwenye hiyo list Aseee.
 
Back
Top Bottom