Huyu dada ajengewe sanamu lake

Uko sahihi sana hapa, partnership ninayo izungumzia mimi siyo hii ya kugawana kila senti pasu kwa pasu (50/50), bali ni ile resource optimization.

Mwanaume yeyote mwenye akili hawezi kukubali mfumo wa aina hiyo ambao yeye anavuja jasho na mwenzake anachopata anahifadhi chake pembeni.

Mwanamke ninayemzungumzia mimi kwenye partnership ni yule anayechangia kwenye family wealth, kama anataka usawa, usawa uanzie kwenye kugawana mzigo wa majukumu ya nyumbani kulingana na uwezo wa kila mmoja, ukiona hataki hilo huyo siyo partner.

Mwanaume usikubali kuingia kwenye mtego wa complacency kama hataki kuchangia, hiyo inaku-qualify wewe kuwa na full control ya maamuzi ya kifedha.

Hauwezi kuleta usawa kwenye haki, halafu ukaacha usawa kwenye wajibu.
 
Hiyo sio partnership hiyo ni demolishing of masculinity, Alafu ndo silaha pekee wanao itumia feminists kumfanya mwanaume ajihisi yu sawa na mwanamke kuanzia psychologically mpk physically
Tupe definition ya partnership kama umeikataa hii.

Jamii ili i balance inahitaji mtawala na mtawaliwa, lakini kutumia mabavu sio practical na hakina afya na ndio matokeo yake huu mvutano.

Ili utawale jamii ya kisasa kama tuliyonayo sasa lazima uwe na nguvu ya ushawishi sio mabavu.

Tukisema usawa hatumaanishi sote tuvae sketi tunamaanisha ushirikishwaji.

Endeleeni kuburuzana tuone kama tupata matokeo chanya/ustawi walau kwa 20% Kikawaida binadamu huwezi mburuza maisha yake yote, Hata watoto wako waburuze uone kama hawaja kuhama nyumbani au angazia nyanja zote ambazo kuna ukandamizaji nitajie iliyofanikiwa walau kwa 50%

I’m more of a solutions na sio mivutano/lawama.
 
Patriarchy ni tofauti na ilivyo sasa. Patriarchy ilimpa fursa zote mwanaune hivyo ikamtaka awe main character.
Jamii za kiafrika bado ni jamii zinazotawaliwa na mfumo dume by far, walau asilimia zaidi ya nusu.
Kwa sasa fursa zimegawanywa na kwa wanawake pia lakini bado mwanaume hajaondolewa huo mzigo wa kuwa main character. Feminist mnataka usawa wa kijinsia kwenye vipengere vinavyowanufaisha, lakini usawa huo huo mnaukataa pale unapowataka muwajibike
Unayoyaona ni mabaki na madhara ya patriachy yenyewe, Jamii ina evolve bado hatujaifuta Patriarchy na hatujaifikia feminist walau kwa 70%
 
Gunner pia anataka fully masculinity dominance, with less wajibu… msome vizuri.
 
Sahihi kabisa, umeeleza nilicho kieleza kwenye post #164.
 
Jamii za kiafrika bado ni jamii zinazotawaliwa na mfumo dume by far, walau asilimia zaidi ya nusu.

Unayoyaona ni mabaki na madhara ya patriachy yenyewe, Jamii ina evolve bado hatujaifuta Patriarchy na hatujaifikia feminist walau kwa 70%
Mfume dume tayari umeshatokomezwa kwenye jamii nyingi zaidi Afrika. Kinachotokea kwa sasa ni wanaume kuwa-outperfom wanawake. Ndio maana tunaona wanawake mnataka upendeleo kwa kigezo cha usawa wa kijinsia mfano hizi harakati zenu za mwanamke akiwezeshwa anaweza. Ushapewa fursa sawa na mwanaume kwanini unataka upendeleo wa kiwezeshwa?

Kwenye harakati zenu za kutaka usawa kuna sehemu mnapotoka kidogo. Mnatafsiri usawa kama ulingano idadi ya wanaume na wanawake kwenye kila kitu. Kitu ambacho hampo sahihi. Usawa maana yake vigezo viwekwe wazi na kila mtu apate nafasi kulingana na uwezo wake.

Mfano kuna wanawake 50 na wanaume 50, na nafasi za kazi zipo 50. Nyie mmekalili usawa wa kijisnia ni lazima wanaume wawe 25 na wanawake 25.kitu ambacho sio sahihi. Usawa hapo ni kuweka vigezo vinavyohitajika na nafasi zitolewe bila kujali jinsia ya mtu. Kwa sababu wanaume wanawa-outperfom wanawake kwenye almost kila kitu sasa hapo wakipata nafasi wanaume 40 na wanawake 10 ndio mnasema ubaguzi wa kijinsia lakini unakuta hao wanaume wamepata nafasi kwa sababu ni competent zaidi.
 
Unajua ndo maana nikasema tuko pamoja, ila hao wenyewe (wanawake) wanaelewa vinginevyo, wao wanachukulia like it's a 50 kwa 50 na bado wao wasi wajibike!

Nakuambia this from experience na ndo wakina Baba levo walikuwa wanasema...

Hawa watu unapojaribu kuwa kind and partner kwao, ndo wanataka kutumia hii to their advantage.. Mwambie mwanamke pesa yake mgawane au asaidie kulipia watoto Karo uone. They don't give a damn, mfumo unawabeba.

Hivi unajua hii kitu chanzo wanasema ni sisi, ila Hapana... Mwanamke kiuhalisia sio provider, na hata akiingia kwenye jukumu hilo anakuwa anajiona kama anaonewa.

We have failed ourselves by not seeing this thing deeper

Unayo ongea wewe yapo sawa kabisa, ila kiuhalisia hawa viumbe hawawezi kukaa katika hiyo position.

Huyo ideal mwanamke imara ndo narcissist namba moja, ukimpa huo mzigo abebe
 
hamna lolote huyo naye anataka mjisikie kuonewa ili muwe inferior kama mfumo unavyotengeneza na kutaka wanaume wawe..
 
binti kiziwi atakuja kusema tena hapa ya kuwa mfumo dume hapa.

Hichi ulicho andika ndo mzizi wa fitina muulize kama ange kuwa yeye angekuwa natimiza hayo uloandika hapo.

The tell us to be that way, ila ukifika mda wa ku-step up wanakimbilia uanamke
 
Ni kweli unachokisema ndiyo maana watu wengi wanaona partnership ni ndoto ya mchana.

Tatizo walio wengi wakipewa hiyo nafasi wanaitumia kama advantage kwa sababu mfumo umewalea wakiwa na entitlement ya kupokea bila kutoa.

Tuseme tatizo siyo partnership yenyewe bali ni selection criteria, wanaume walio wengi pia huwa wanachagua wanawake kwa surface qualities halafu wanasahau ku-test character ya mwanamke kwenye mambo ya pesa na wajibu kabla ya kufunga ndoa au kuanzisha mahusiano.

Ukimchagua narcissist ambaye anaamini yeye ni malkia bila shaka atakuona unamuonea pale utakapomwambia sijui mambo ya kuchangia ada.

Ufumbuzi ninao uona mimi siyo kukataa partnership, bali ni tuwakatae parasites ambao wanatumia mgongo wa usawa ili ku drain rasilimali zetu.

Inatupasa tuwe makini kwenye vetting process.
 
Mkuu ukisoma post yake hapo #166 , kuna sehemu amegusia suala la ushirikishwaji ambalo mimi ndio ninalo lizingumzia, labda tuwe tunatofautiana maana.

Usawa unapaswa kuwa wa pande zote mbili (haki na wajibu).
 
Nyie ndio hamjaelewa mada. Ukitaka kutetea hoja kwa kufanyia rejea mfumo dume unakosea kabisa. Patriarchy is no relevant when we apply the vakues of equal opportunity for men and women.

Women want place of a man, privilege of a woman and responsibility of neither, and that have ruined society. Bila wanaume kusimama na kurudisha mambo kwenye mstari jamii lazima ipotee Mnang'ang'ania tu huruma huruma lakini hamna point yoyote.
 
Mkuu tatizo sio la mwanaume, tatizo ni la mwanamke. Ukiongelea patriarchy, feminism au hiyo collaboration ulioiita uko juu. Wajibu wa mwanaume haubadiliki, lazima awajibe na masuala ya provision and protection. Shida ipo upande wa mwanamke ambae bado anapinga patriarchy lakini anazitaka benefits zake kama lifetime provision and protection kutoka kwa mwanaume.

Hakuna mwanaume anaweza kukataa akisaidiwa na mkewe kulipa bill za nyumbani. Swali linakuja je wanawake hawa hawa na falsasa yao ya "hela ya mwanaume ni ya wote na ya mwanamke ni ya mwanamke pekee yake" wapo tayari na hiyo unayoiita collaboration?
 
Sahihi, na ndiyo maana sisi wanaume ni lazima tuwe na high standards kwenye vetting kabla hatujatangaza collaboration.

Tujitahidi kuchagua wanawake wenye investment mindset.

Usawa uwepo kwa upande wa haki na upande wa wajibu, hapa tutaenda sawa.
 
Kuogopa usawa ni ishara ya uanaume dhaifu unaohitaji support system ya unyonge wa mwanamke ili usimame.

Njoo na pointi nyingine ya msingi kwa sababu uanaume wa kweli hauwezi kubomolewa na usawa.
Mkuu unafikiri Rais anaheshimika na kuogopea kwa sababu ya uwepo wake tu kama binadamu? Bila shaka jibu ni hapana. Madaraka akiyonayo ndio yanampa hiyo sifa. Kiongozi ni lazima awe na dominance traits.

Dhana ya usawa wa kijinsia inaenda kinyume na asili ya uumbaji. Tutaitetea lakini ukweli ni kwabnba kuna sehemu tulikosea katika kuifanyia implementation.
 
Mkuu Rais anaheshimika kwa sababu ya institutional power kwa maana ya katiba na sheria, hiyo ni positional authority.

Uongozi wa familia haujengwi na katiba' au sheria ya mabavu isipokuwa unajengwa na relational authority.

Labda niseme hivi uongozi wa familia unahitaji dominance ya kifikra na kimkakati ukijaribu kuiongoza familia kama unavyoongoza nchi utaishia kupata mutiny tu.

Kuhusu implementation failure naungana na wewe, tumeshindwa ku-implement usawa kwa sababu tunajaribu kutumia mifumo ya bwana na mtumwa wake kwenye jamii inayohitaji synergy.

Uongozi wa mwanaume kwenye familia haupaswi kutokana na mke kuwa submissive kwa hofu, bali mke awe aligned na vision yako kwa hiari.
 
Nikisema hatujafika peak ya feminist ni pamoja na kutokuelewa suala la usawa wa fursa vs ubaguzi. Ni pamoja na kutokuelewa kuwa fursa zikiwa 20 na wakazipata wanaume tu sababu ya competence na wanawake tukakosa kwasababu ya incompetence si ubaguzi. Kwahivyo kama unaelewa ni kwamba hatujaweza bado kufikia kilele cha feminist, na jamii ambayo haijaelewa feminism to the core ni jamii ambayo inatawaliwa bado na Patriachy, au ina chembechembe hizo.

Hata wewe kuminimize feminist vs patriarchy katika aspect moja tu ya fursa ni proof kuwa bado hizi concept mbili hatujazielewa, leave alone kuzipractice by 100 au walau 90.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…