Mantiki ni ndogo sana hapa bado hauielewi, mfano wako wa tapeli na mtapeliwa, jibu langu ni rahisi tu.
Tapeli ni mhalifu, na mtapeliwa ni mtu aliyekosa due diligence. Wote wana sehemu yao ya lawama..
Kama mwanamke anaigiza ili aingie kwenye ndoa, ni mhalifu wa kimaadili na kama mwanaume naye anawekeza maisha yake kwa mtu bila kujua history yake wala kumpima kwa kumuweka kwenye hali ngumu ya maisha ili ajue uhalisia wake, naye ni financially/emotionally illiterate.
Katika kisa cha mwanaume kuanza manyanyaso baada ya ndoa kama ulivyosema, msimamo wangu ni ule ule:
Huyo mwanamke naye ni victim wa kushindwa kwake kufanya vetting ya kiume, hapa hakuna villain mmoja, wote wawili wamefeli.
Mimi siwapi pass wanawake, na wala siwapi pass wanaume lakini ukweli unabaki kuwa Kwenye maisha, huwezi kuizuia dunia isikudhuru, lakini unaweza kujiandaa ili isikudhuru.
Kushindwa kujiandaa siyo villainy kama unavyo ona wewe , hiyo ni weakness.