Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,024
- 1,616
Akizungumza katika 'Intavyuu' maalum na Mwananchi Feisal Salum maarufu Fei Toto amefunguka yafuatayo kuhusu mahusiano yake.
"Lile sakata liliniathiri kwenye mambo mengi sana sio kwa upande wa kucheza pekee, wakati niko kwenye wakati mgumu kama ule kila wakati unafikiria hii kesi itaishaje, nikakutana na pigo lingine la kukimbiwa na mpenzi wangu ambaye niliamini ningekuja kumuoa.
"Aliona kama maisha yangu ya soka tena basi ndio yameishia pale alishindwa kuvumilia na kuamua kutafuta mtu mwingine kitu kilichoniumiza zaidi ni hatua mbaya zaidi kwangu ikawa kwenda kuolewa tena nikiwa katikati ya lile sakata, sikuwa nimemuoa ila tulikuwa na mipango mingi ya maisha kati yetu, hakutaka kuvumilia kabisa nililazimika kuyapokea maamuzi yake hakukuwa na namna na sasa nimerudi uwanjani maisha mengine yataendelea tu."
HAKUMTAFUTA BAADA YA SAKATA KUMALIZIKA
"Hapana hakunitafuta na wala mimi sikumtafuta nilikubaliana na maisha au maamuzi aliyoyachukua na bahati mbaya sana mimi huwa sina hulka ya kuangalia nyuma eneo ambalo nimeondoka nilikubaliana naye maisha lazima yaendelee kwake na kwangu nikipata mwingine nitashukuru Mungu.
Chanzo: Mwanachi