Yimakatso
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 7,774
- 11,255
Sheria imetaja hairuhusiwi kuingia na simu haijataja simu aina gani.Kuna baadhi ya watu wamekosa kabisa ubinadamu na kujiona wao ni watu waliosahihi na hawatawahi kukosea.
Ipo hivi, Kuna dogo anasoma MUST mwaka wa tatu, alijisahau akaingia na simu ndogo (kiswaswadu) kwenye chumba Cha mtihani lakini inavoonekana atafukuzwa chuo Kwa kosa la kuingia na simu ndan ya chumba Cha mtihani.
Sasa nachojiuliza hivi ni kweli binadamu wamekuwa na roho mbaya kiasi hiki ambapo simu aliyoingia nayo Haina hata uwezo wa kufungua internet Wala PDF najiuliza hata kama ni sheria hio sheria haiangalii mazingira yanayopelekea kufanyika Kwa udanganyifu kwenye mtihani .
Wakuu naomba ushauri wa kumsaidia huyu bwana mdogo kwani ni mwaka wa mwisho na alikuwa anategemewa na walezi wake ambao kiukweli Wana Hali mbaya kiuchumi.
Sent from my Pixel 3a using JamiiForums mobile app
Hapo kujitetea kwamba sijui niliingia na kiswaswadu hoja haina mashiko.
Hata kiswaswadu unaweza kuandika majibu kwenye sehemu ya sms ukahifadhi draft.


