Huu sio ubinadamu kabisa

Huu sio ubinadamu kabisa

Mh ndio vyuo vilivyo skuhizi nakumbuka nikiwa chuo cha uhasibu hukaguliwi umeingia na simu au uchafu gani leo kiswaswadu kiachwe nyumbani😂😂😂 ila akaongee na uongozi watamsikiliza na sio waende wakalalamike wataharibu
 
Naimani walimu wake na uongozi wa chuo si wapumbavu hadi wafikie maamuz ya kumfukuza chuo huyo mtoto... Lazima kuna jambo huyo mtoto amekuficha ili umuonee huruma na uhisi kaonewa... Nikushauri nenda naye chuoni onana na Uongozi uliza kwa ustaarabu ilikuaje hadi dogo akafukuzwa shule kama utahisi sababu zao hazina mashiko mtoto na wewe mzazi mna haki kuandika barua ya kukata rufaa kwa DVC-A au DVC au bodi ya chuo...
Halafu hoja yako haina mashiko kwamba cm ya kitochi haina uwezo kwamba mtu akaitumia cm hiyo kama nyenzo ya majibu... Sisi tuliosoma chuo enzi za cm za vitochi, watu walikua wanaandika majibu (kama msg) ktk hizo cm, na kuna namna hiyo msg unaiseti ikitokea cm imekamatwa msg inafutika ikipekuliwa...
 
Kuna baadhi ya watu wamekosa kabisa ubinadamu na kujiona wao ni watu waliosahihi na hawatawahi kukosea.

Ipo hivi, Kuna dogo anasoma MUST mwaka wa tatu, alijisahau akaingia na simu ndogo (kiswaswadu) kwenye chumba Cha mtihani lakini inavoonekana atafukuzwa chuo Kwa kosa la kuingia na simu ndan ya chumba Cha mtihani.

Sasa nachojiuliza hivi ni kweli binadamu wamekuwa na roho mbaya kiasi hiki ambapo simu aliyoingia nayo Haina hata uwezo wa kufungua internet Wala PDF najiuliza hata kama ni sheria hio sheria haiangalii mazingira yanayopelekea kufanyika Kwa udanganyifu kwenye mtihani .

Wakuu naomba ushauri wa kumsaidia huyu bwana mdogo kwani ni mwaka wa mwisho na alikuwa anategemewa na walezi wake ambao kiukweli Wana Hali mbaya kiuchumi.

Sent from my Pixel 3a using JamiiForums mobile app
Pole kwake.
Kuna malecturer ni katili sana, wanasababisha elimu inakuwa kama vita.

Ilikuwaje na yeye akaingia na simu na ilikuwaje ikajulikana kama anayo?
 
Watu tulikuwa tunaiba booklete inajazwa kila kitu, unaingia nayo, ile unayoepewa unaipiga chini unaanza tumia uliyo ingia nayoo... then unaomba booklet ingine unapanga sasa majibu vizuri shule raha sanaaa
Mie sitaki kukumbukaa kabisaa, sio kwa nuksi ile, maisha yangu situmii nondo afu necta nitumie aaaah wapiiiii.
 
Dogo inabidi ajiandae kutafuta chuo kingine...uwezekano wa kuchomoka kwenye huo msala ni mdogo sana hasa kwa public universities... Ila dogo kazingua sana
 
Dogo Mwaka wa tatu alafu anafanya mambo kama First year.
Dogo afukuzwe, angekuwa Mwaka wa kwanza walau tungesema bado ni mdogo, lakini Mwaka wa tatu alafu anafanya vitu vya hivyo, huyo ni kubwa Jinga.
Tatizo letu ni kutofuata sheria. Ikitokea kitu tunakimbilia ubinadamu, tunasahau kuwa sheria ni msumeno. Watu wanadai simu yake ni kitechno kidogo haiwezi kutumika kuibia. Kuibia siyo lazima uwe na simu janja. Kuibia siyo lazima kwa intaneti. Unaweza ukahifadhi taarifa na notisi kwenye message na ukaibia saana. Wahusika wana haki ya ku"enforce examination rules and regulations". Mhusika atalazimika kuwajibika kwa makosa aliyoyafanya.
 
Pole kwake.
Kuna malecturer ni katili sana, wanasababisha elimu inakuwa kama vita.

Ilikuwaje na yeye akaingia na simu na ilikuwaje ikajulikana kama anayo?
Anavosema alifanya mtihani na akawa anaondoka mlangoni ndo akakuta jamaa anasachi mfukoni

Sent from my Pixel 3a using JamiiForums mobile app
 
Mie sitaki kukumbukaa kabisaa, sio kwa nuksi ile, maisha yangu situmii nondo afu necta nitumie aaaah wapiiiii.
Nyie magenious 😅😅😅.. sie tia maji tia maji suport document muhimu.. paper ya mwisho nakumbuka nilikuwa na smartphoneeeee.. booklet, kibomu pembeni kulikuwa na pisi ikatumika kama agent 🤣🤣🤣
 
Tatizo letu ni kutofuata sheria. Ikitokea kitu tunakimbilia ubinadamu, tunasahau kuwa sheria ni msumeno. Watu wanadai simu yake ni kitechno kidogo haiwezi kutumika kuibia. Kuibia siyo lazima uwe na simu janja. Kuibia siyo lazima kwa intaneti. Unaweza ukahifadhi taarifa na notisi kwenye message na ukaibia saana. Wahusika wana haki ya ku"enforce examination rules and regulations". Mhusika atalazimika kuwajibika kwa makosa aliyoyafanya.
Hatari

Sent from my Pixel 3a using JamiiForums mobile app
 
Nyie magenious .. sie tia maji tia maji suport document muhimu.. paper ya mwisho nakumbuka nilikuwa na smartphoneeeee.. booklet, kibomu pembeni kulikuwa na pisi ikatumika kama agent
sio zama hizi, sio genius ila mie hapana kwa Nondo. Bora nifeli tyuuh.

Sasa ndo km hivi Una kamatwaa, then?? Aaaah
 
sio zama hizi, sio genius ila mie hapana kwa Nondo. Bora nifeli tyuuh.

Sasa ndo km hivi Una kamatwaa, then?? Aaaah
wanakamatwa wasio na ushawishi.. usitumiee hayo makitu kama hujampanga msimamizi au msimaizi sio mwanaaa.. Mchezo unachewa nje, msimamizi ananunuliwa kabla ya kuingia chumba cha mtihani 😅😅😅 akiingia anakuwa kama msukule tu hadi mnapiga story.. naona ma lecture wakuda wanataka wanijue wafute degree na msc yangu 🤣🤣🤣🤣 acha nikaushe
 
Back
Top Bottom