mkumbwa junior
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 814
- 1,545
Huwa sipendi sana kuingilia imani ya mtu ila kwa jana nimeona kabisa MTUME na NABII Mwamposa kuna dalili za upigaji
Kuna mahali nilikuwepo wameweka ile chanel yake watu wanatoa ushuhuda jamaa mmoja akasema alienda kuomba apate hela akala na keki siku hiyo yupo nyumbani akashangaa sms kucheki amepokea milioni 10 hajui ilipotoka kwa hofu akamshirikisha jirani, jirani akamwambia katoe labda Mungu kakuona akaenda kwa wakala kutoa ilivyotoka ikaingia tano ingine akatoa
Najiuliza mtandao gani wa simu laini inaweza pokea milioni 15 na ikatoka ndani ya lisaa limojatena bora angekuwa mtu wa kutumia miamala jamaa anadai hakuwahi weka kwenye simu hata laki.
Jamaa akaendelea baada ya kutoa ile tano ikaingia mbili akatoa tena jumla akawa na milioni 17(sijui roho mtakatifu alilipia makato) jamaa anadai hakuwahi miliki milioni moja yake ila kwa mara ya kwanza akawa amepata milioni 17 akarudi home akaanza harakati za Ujenzi, mpaka sasa amefanikiwa kujenga, kununua pikipiki na kafungua biashara, anadai kuwa ule mtindo wa kupokea hela uliendelea hadi akakamilisha ujenzi wa nyumba ya Milioni 30 biashara na usafiri(pikipiki)sasa hivi ana mpango wa kununua gari.
Hela zote hajui zinatoka wapi.
Daah MUNGU anisamehe tu ila huu ni utapeli wa hadharani
Kuna mahali nilikuwepo wameweka ile chanel yake watu wanatoa ushuhuda jamaa mmoja akasema alienda kuomba apate hela akala na keki siku hiyo yupo nyumbani akashangaa sms kucheki amepokea milioni 10 hajui ilipotoka kwa hofu akamshirikisha jirani, jirani akamwambia katoe labda Mungu kakuona akaenda kwa wakala kutoa ilivyotoka ikaingia tano ingine akatoa
Najiuliza mtandao gani wa simu laini inaweza pokea milioni 15 na ikatoka ndani ya lisaa limojatena bora angekuwa mtu wa kutumia miamala jamaa anadai hakuwahi weka kwenye simu hata laki.
Jamaa akaendelea baada ya kutoa ile tano ikaingia mbili akatoa tena jumla akawa na milioni 17(sijui roho mtakatifu alilipia makato) jamaa anadai hakuwahi miliki milioni moja yake ila kwa mara ya kwanza akawa amepata milioni 17 akarudi home akaanza harakati za Ujenzi, mpaka sasa amefanikiwa kujenga, kununua pikipiki na kafungua biashara, anadai kuwa ule mtindo wa kupokea hela uliendelea hadi akakamilisha ujenzi wa nyumba ya Milioni 30 biashara na usafiri(pikipiki)sasa hivi ana mpango wa kununua gari.
Hela zote hajui zinatoka wapi.
Daah MUNGU anisamehe tu ila huu ni utapeli wa hadharani