UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,157
- 10,708
Nsikuchoshe na Usinchoshe,tusichoshane!.
Watanzania wengi wameshakata tamaa ya maisha na hii si kwa wasiyo nacho tu, bali hata kwa walionacho!.
Kila mtu anatafuta pesa kwa njia anayoifahamu yeye ilimradi tu kujijengea heshima kwa watu wake wa karibu na ukoo wake kutokana na dharau ambazo wamekuwa wakimuonyeshea.
Sasa kama mjuavyo ndugu zangu,mimi biashara yangu kubwa ni Bodaboda na jina langu ni kubwa sana hizi pande za Bunju ambapo mara nyingi ndipo kijiwe changu kilipo,sasa kuna mshikaji wangu mmoja ni Daktari hospitali fulani hapa mjini,jamaa mara zote huwa namchukuaga ile asubuhi mahali anapoishi na kumpeleka kazini kwake huko kwenye hiyo hospitali anayofanyia kazi,jamaa amekuwa zaidi ya rafiki kwasababu mambo kadhaa ambayo huwa anahitaji ushauri ananipigia simu namshauri kama brother.
Jamaa nadhani huwa hatumii JF kwasababu laiti kama angekuwa anatumia na akagundua mimi UMUGHAKA ninayembeba kila siku ndiye nilikuwa rafiki yake na Ally Mpemba tena nilikuwa napiga pesa kipindi fulani za mazonge mazonge,basi jamaa angenikomalia nimpeleke huko zenji au nimuunganishe na Ally kwa udi na uvumba.Kwakuwa hakufahamu chochote hivyo nikawa nimezikwepa bugudha zake.
Sasa haka ni kakisa kafupi ambako nasimulia ili kuwasanua wabongo waepukane na waganga wa kongo ambao wengi wao wamekuwa ni matapeli baada ya kuona watanzania wengi wanauhitaji wa kuwa matajiri.
Mwaka jana kati ya mwezi 8 - 11,jamaa yangu huyo au Bosi wangu huyo(Hapa nimuite Kamugisha)ingawa si jina lake halisi ili kuficha Identity yake,aliniambia mapema siku ya ijumaa nikiwa namtoa kazini kwake kwamba siku itakayofuatia yaani jumamosi tutafute mahali wanapochoma kitimoto angalau tule wakati huo tukipiga bia mbili tatu;Mi nilimwambia sitoweza kujumuika naye kwasababu kwanza Imani yangu hairuhusu mimi kula kitimonga,pili siku hiyo ya jumamosi ningekuwa kanisani nikimuabudu Mungu wangu.
Kamugisha "Ooh Mwanangu nisamehe sana nilikuwa nimesahau"
Aliendelea "Basi tufanye tu hata J'pili"
Mimi "Sawa bro hakuna tatizo ila mimi nitakula nyama choma ya kawaida tu,nguruwe situmii"
Kamugisha "Sawa mdogo wangu usijali,nathamini sana imani za watu wengine wala usiwe na shaka"
Kama nilivyosema,jamaa ni mshikaji ambaye tumefahamiana naye kwakuwa amekuwa mteja wangu,Pia amekuwa akinilipa pesa zangu kila mwisho wa mwezi ambazo ni Tsh 120000/=;Kwa maana kwamba kila siku ninapompeleka kazini kwake na kumfuata Jioni ni Tsh 4000/=,hivyo kwa mwezi ndiyo ananilipa kiasi hicho.
J'pili nilimcheki mshikaji akaniambia tuelekee mitaa ya river side pale Micasa lounge.
Mimi "Nichukue chombo yangu au tutapanda Daladala "
Kamugisha "Usijali mdogo wangu,leo ni wikiendi hivyo njia huwa ina mikosi ya walevi,pikipiki inaweza isiwe salama sana,nita-request Bolt"
Mimi "Sawa Bro"
Mimi "Tukutane wapi?"
Kamugisha "Nadhani tukutane hapo njia panda ya Goba"
Mimi ingawa nafanya kazi Bunju na ndipo kijiwe changu kilipo ila makazi yangu ni Mbezi - kwa Msuguri.Jamaa yeye anaishi Goba,hivyo ile asubuhi nikiwa natoka kituo cha kwanza ni kwake namchukua nampeleka kazini kwake kisha mimi naelekea kijiweni kwangu kama kawaida.
Kweli,hatimaye tulikutana jamaa aka-request Bolt tukaondoka zetu hadi Micasa Lounge,hili eneo kwangu haikuwa mara ya kwanza kufika kwasababu kuna abiria nishawapeleka hapo na kuwafuata pia,pia nikiwa ninapita mara kadhaa nikiwa kwenye mishemishe,nimekuwa nikiliona lilivochangamka.
Tulivyofika pale siku hiyo kulikuwa na live band ambayo ilikuwa inapiga kitu kama Karioke music na hiyo ilikuwa mida ya jioni saa 12 kuelekea saa 1 usiku.
Kila mmoja aliagiza kinywaji anachopiga akaletewa na muhudumu akaanza kupiga,jamaa Pombe ilipoanza kumuondolea aibu alianza kuongea bila uoga mambo ambayo nadhani ndiyo alitaka kuniambia.
Kamugisha "Mdogo wangu hivi huwa umeoa?"
Mimi "Ninaye mwanamke bro ila yeye yupo kikazi huko Moro"
Kamugisha "Sawa mdogo wangu,wewe nakupenda sana kama mdogo wangu kwakuwa ni mpambanaji sana na ninavyokuona utafika mbali sana"
Jamaa alipoaniambia nitafika mbali sana nikabaki namuangalia tu,angekuwa anajua huko mbali nilishafika kisha nikaamua kurudi tena nyuma wala asingeniambia hivyo bali nadhani angeshikwa na hasira sana kwanini niliamua kuacha mambo hayo.
Kamugisha "Mmebarikiwa watoto?"
Mimi "Nina mtoto mmoja tu kaka yupo na mama yake huko,huku huwa wanakuja wakati wa likizo tu"
Kamugisha "Ooh hongereni sana"
Aliendelea "Mimi kuishi na mwanamke nilishashindwa mdogo wangu,hivyo nikiona wewe una mwanamke napaswa kukupongeza sana"
Aliendelea "Wanawake ni manyang'au tu,mimi sasa hivi naangalia pesa tu,wanawake ndo kama hivi nikija sehemu kama hizi nikiwa na nyege nakamata li moja,naenda kulikung'uta mambo yanaisha kila mtu anaendelea na mishe zake".
Muda huo jamaa anaongea mimi natikisa kichwa tu kuonyesha tuko pamoja katika mazungumzo.
Kamugisha "Mdogo wangu mi ninataka hela tu kwa nguvu zote"
Mimi "Bora angalau wewe bro una ajira ya uhakika,sisi wengine tusipotoka hatuli"
Kamugisha "Ajira wapi mdogo wangu hizi kazi ni mateso tu,mshahara wenyewe ninaolipwa nikikwambia ni kituko cha karne"
Mimi "Bro mshahara ni mshahara tu,sisi wengine tusiyokuwa na mishahara ndiyo tunapata taabu"
Kamugisha "Mdogo wangu nalipwa milioni 1.2,hiyo hela nikikwambia kwa matumizi yangu na wategemezi kadhaa huwa nabaki na pesa ndogo sana"
Jamaa kile kitendo cha kuniambia analipwa milioni 1.2 halafu bado analia hana hela niliamaki kidogo kwasababu sisi wengine tunapambana kwa siku unapata hata elfu 10 unamshukuru Mungu.
Baada ya jamaa kuniambia vile,alizama kwenye mfuko wake wa jeans aliyokuwa amevaa akatoa simu yake kubwa aina ya I phone 12 kisha akaingia YouTube akanipatia na mimi nitazame,sasa nilikuwa nikiangalia YouTube kuna mshikaji mmoja alikuwa anaelezea namna alivyowahi kuwa tajiri kwa kwenda huko Congo na kupatiwa utajiri na mganga mmoja.
Kamugisha "Una muona huyo mshikaji?,jamaa amewahi kuwa tajiri mkubwa sana East Africa,kuna mshikaji niliongea nae akawa ameniambia hapo Congo kuna waganga hatari na hiyo kitu wanaitoa tena bure kabisa"
Mimi "Usiniambie kaka!"
Kamugisha "Kweli kabisa kwanini nikutanie!"
Jamaa wakati anaongea hakufahamu kabisa kwamba na mimi nimewahi kuwa na tuhela tudogo kwa kushikwa mkono na Ally Mpemba,nilitaka nimwambie lakini nikaamua kukausha tu.
Kamugisha "Nina taka siku moja niende kwa huyo mganga nasikia ni gwiji wa magwiji"
Aliendelea "Mdogo wangu haya siyo maisha,maisha ya kuendesha bodaboda na kupata hela ya kula tu siyo maisha kabisa,au wewe umeridhika nayo?"
Mimi "Bro nitafanye tena,ndo hivyo hivyo nasonga kibishi"
Kamugisha "Huwezi kujifariji kwa kusema unasonga kibishi mdogo wangu,tafuta hela uheshimike,dunia hii bila hela kwasasa hata kama uwe handsome vp bado utadhalaurika mdogo wangu,pesa ndiyo kila kitu"
Aliendelea "Mimi natafuta likizo halafu niende kwa huyo mtaalamu"
Kamugisha "Vp au mwenzangu hupendi hela nini!?"
Mimi "Kaka kuna mtu asiyependa hela?"
Kamugisha "Sasa mimi naona naongea peke yangu tu ndugu yangu na wewe huchangii chochote!"
Mimi "Bro napenda sana kuwa na pesa ila sasa hata ukisema niende huko kwasasa sina hela,labda mpaka nijipange"
Sikutaka kabisa hizo habari lakini niliamua kumtia moyo ili asijisikie vibaya,mimi nishapita huko na ninafahamu hali ilivyokuwa.
Kamugisha "Hela siyo tatizo dogo,wewe kama unataka tuungane twende niambie nitaomba likizo tusepe"
Mimi "Sawa kaka,kama ukinifadhiri nauli hakuna tatizo tutakwenda"
Kamugisha "Huo ndiyo uamuzi wa kiume dogo,hizi starehe zote ni hela,unaona watu walivyobaki mandinga hapo nje,hiyo yote ni hela bila hela utaonekana kibaka tu mbele ya watu wenye nazo hata kama unayoheshima"
Baada ya mazungumzo yale na vyombo kukolea kichwani kwa Kamugisha,jamaa aliamka akawa anacheza muziki bila aibu huku akimuita kila muhudumu wa kike aliyejipitisha mbele yake na kuanza kujichekesha chekesha bila sababu za msingi.
Naendelea................
Watanzania wengi wameshakata tamaa ya maisha na hii si kwa wasiyo nacho tu, bali hata kwa walionacho!.
Kila mtu anatafuta pesa kwa njia anayoifahamu yeye ilimradi tu kujijengea heshima kwa watu wake wa karibu na ukoo wake kutokana na dharau ambazo wamekuwa wakimuonyeshea.
Sasa kama mjuavyo ndugu zangu,mimi biashara yangu kubwa ni Bodaboda na jina langu ni kubwa sana hizi pande za Bunju ambapo mara nyingi ndipo kijiwe changu kilipo,sasa kuna mshikaji wangu mmoja ni Daktari hospitali fulani hapa mjini,jamaa mara zote huwa namchukuaga ile asubuhi mahali anapoishi na kumpeleka kazini kwake huko kwenye hiyo hospitali anayofanyia kazi,jamaa amekuwa zaidi ya rafiki kwasababu mambo kadhaa ambayo huwa anahitaji ushauri ananipigia simu namshauri kama brother.
Jamaa nadhani huwa hatumii JF kwasababu laiti kama angekuwa anatumia na akagundua mimi UMUGHAKA ninayembeba kila siku ndiye nilikuwa rafiki yake na Ally Mpemba tena nilikuwa napiga pesa kipindi fulani za mazonge mazonge,basi jamaa angenikomalia nimpeleke huko zenji au nimuunganishe na Ally kwa udi na uvumba.Kwakuwa hakufahamu chochote hivyo nikawa nimezikwepa bugudha zake.
Sasa haka ni kakisa kafupi ambako nasimulia ili kuwasanua wabongo waepukane na waganga wa kongo ambao wengi wao wamekuwa ni matapeli baada ya kuona watanzania wengi wanauhitaji wa kuwa matajiri.
Mwaka jana kati ya mwezi 8 - 11,jamaa yangu huyo au Bosi wangu huyo(Hapa nimuite Kamugisha)ingawa si jina lake halisi ili kuficha Identity yake,aliniambia mapema siku ya ijumaa nikiwa namtoa kazini kwake kwamba siku itakayofuatia yaani jumamosi tutafute mahali wanapochoma kitimoto angalau tule wakati huo tukipiga bia mbili tatu;Mi nilimwambia sitoweza kujumuika naye kwasababu kwanza Imani yangu hairuhusu mimi kula kitimonga,pili siku hiyo ya jumamosi ningekuwa kanisani nikimuabudu Mungu wangu.
Kamugisha "Ooh Mwanangu nisamehe sana nilikuwa nimesahau"
Aliendelea "Basi tufanye tu hata J'pili"
Mimi "Sawa bro hakuna tatizo ila mimi nitakula nyama choma ya kawaida tu,nguruwe situmii"
Kamugisha "Sawa mdogo wangu usijali,nathamini sana imani za watu wengine wala usiwe na shaka"
Kama nilivyosema,jamaa ni mshikaji ambaye tumefahamiana naye kwakuwa amekuwa mteja wangu,Pia amekuwa akinilipa pesa zangu kila mwisho wa mwezi ambazo ni Tsh 120000/=;Kwa maana kwamba kila siku ninapompeleka kazini kwake na kumfuata Jioni ni Tsh 4000/=,hivyo kwa mwezi ndiyo ananilipa kiasi hicho.
J'pili nilimcheki mshikaji akaniambia tuelekee mitaa ya river side pale Micasa lounge.
Mimi "Nichukue chombo yangu au tutapanda Daladala "
Kamugisha "Usijali mdogo wangu,leo ni wikiendi hivyo njia huwa ina mikosi ya walevi,pikipiki inaweza isiwe salama sana,nita-request Bolt"
Mimi "Sawa Bro"
Mimi "Tukutane wapi?"
Kamugisha "Nadhani tukutane hapo njia panda ya Goba"
Mimi ingawa nafanya kazi Bunju na ndipo kijiwe changu kilipo ila makazi yangu ni Mbezi - kwa Msuguri.Jamaa yeye anaishi Goba,hivyo ile asubuhi nikiwa natoka kituo cha kwanza ni kwake namchukua nampeleka kazini kwake kisha mimi naelekea kijiweni kwangu kama kawaida.
Kweli,hatimaye tulikutana jamaa aka-request Bolt tukaondoka zetu hadi Micasa Lounge,hili eneo kwangu haikuwa mara ya kwanza kufika kwasababu kuna abiria nishawapeleka hapo na kuwafuata pia,pia nikiwa ninapita mara kadhaa nikiwa kwenye mishemishe,nimekuwa nikiliona lilivochangamka.
Tulivyofika pale siku hiyo kulikuwa na live band ambayo ilikuwa inapiga kitu kama Karioke music na hiyo ilikuwa mida ya jioni saa 12 kuelekea saa 1 usiku.
Kila mmoja aliagiza kinywaji anachopiga akaletewa na muhudumu akaanza kupiga,jamaa Pombe ilipoanza kumuondolea aibu alianza kuongea bila uoga mambo ambayo nadhani ndiyo alitaka kuniambia.
Kamugisha "Mdogo wangu hivi huwa umeoa?"
Mimi "Ninaye mwanamke bro ila yeye yupo kikazi huko Moro"
Kamugisha "Sawa mdogo wangu,wewe nakupenda sana kama mdogo wangu kwakuwa ni mpambanaji sana na ninavyokuona utafika mbali sana"
Jamaa alipoaniambia nitafika mbali sana nikabaki namuangalia tu,angekuwa anajua huko mbali nilishafika kisha nikaamua kurudi tena nyuma wala asingeniambia hivyo bali nadhani angeshikwa na hasira sana kwanini niliamua kuacha mambo hayo.
Kamugisha "Mmebarikiwa watoto?"
Mimi "Nina mtoto mmoja tu kaka yupo na mama yake huko,huku huwa wanakuja wakati wa likizo tu"
Kamugisha "Ooh hongereni sana"
Aliendelea "Mimi kuishi na mwanamke nilishashindwa mdogo wangu,hivyo nikiona wewe una mwanamke napaswa kukupongeza sana"
Aliendelea "Wanawake ni manyang'au tu,mimi sasa hivi naangalia pesa tu,wanawake ndo kama hivi nikija sehemu kama hizi nikiwa na nyege nakamata li moja,naenda kulikung'uta mambo yanaisha kila mtu anaendelea na mishe zake".
Muda huo jamaa anaongea mimi natikisa kichwa tu kuonyesha tuko pamoja katika mazungumzo.
Kamugisha "Mdogo wangu mi ninataka hela tu kwa nguvu zote"
Mimi "Bora angalau wewe bro una ajira ya uhakika,sisi wengine tusipotoka hatuli"
Kamugisha "Ajira wapi mdogo wangu hizi kazi ni mateso tu,mshahara wenyewe ninaolipwa nikikwambia ni kituko cha karne"
Mimi "Bro mshahara ni mshahara tu,sisi wengine tusiyokuwa na mishahara ndiyo tunapata taabu"
Kamugisha "Mdogo wangu nalipwa milioni 1.2,hiyo hela nikikwambia kwa matumizi yangu na wategemezi kadhaa huwa nabaki na pesa ndogo sana"
Jamaa kile kitendo cha kuniambia analipwa milioni 1.2 halafu bado analia hana hela niliamaki kidogo kwasababu sisi wengine tunapambana kwa siku unapata hata elfu 10 unamshukuru Mungu.
Baada ya jamaa kuniambia vile,alizama kwenye mfuko wake wa jeans aliyokuwa amevaa akatoa simu yake kubwa aina ya I phone 12 kisha akaingia YouTube akanipatia na mimi nitazame,sasa nilikuwa nikiangalia YouTube kuna mshikaji mmoja alikuwa anaelezea namna alivyowahi kuwa tajiri kwa kwenda huko Congo na kupatiwa utajiri na mganga mmoja.
Kamugisha "Una muona huyo mshikaji?,jamaa amewahi kuwa tajiri mkubwa sana East Africa,kuna mshikaji niliongea nae akawa ameniambia hapo Congo kuna waganga hatari na hiyo kitu wanaitoa tena bure kabisa"
Mimi "Usiniambie kaka!"
Kamugisha "Kweli kabisa kwanini nikutanie!"
Jamaa wakati anaongea hakufahamu kabisa kwamba na mimi nimewahi kuwa na tuhela tudogo kwa kushikwa mkono na Ally Mpemba,nilitaka nimwambie lakini nikaamua kukausha tu.
Kamugisha "Nina taka siku moja niende kwa huyo mganga nasikia ni gwiji wa magwiji"
Aliendelea "Mdogo wangu haya siyo maisha,maisha ya kuendesha bodaboda na kupata hela ya kula tu siyo maisha kabisa,au wewe umeridhika nayo?"
Mimi "Bro nitafanye tena,ndo hivyo hivyo nasonga kibishi"
Kamugisha "Huwezi kujifariji kwa kusema unasonga kibishi mdogo wangu,tafuta hela uheshimike,dunia hii bila hela kwasasa hata kama uwe handsome vp bado utadhalaurika mdogo wangu,pesa ndiyo kila kitu"
Aliendelea "Mimi natafuta likizo halafu niende kwa huyo mtaalamu"
Kamugisha "Vp au mwenzangu hupendi hela nini!?"
Mimi "Kaka kuna mtu asiyependa hela?"
Kamugisha "Sasa mimi naona naongea peke yangu tu ndugu yangu na wewe huchangii chochote!"
Mimi "Bro napenda sana kuwa na pesa ila sasa hata ukisema niende huko kwasasa sina hela,labda mpaka nijipange"
Sikutaka kabisa hizo habari lakini niliamua kumtia moyo ili asijisikie vibaya,mimi nishapita huko na ninafahamu hali ilivyokuwa.
Kamugisha "Hela siyo tatizo dogo,wewe kama unataka tuungane twende niambie nitaomba likizo tusepe"
Mimi "Sawa kaka,kama ukinifadhiri nauli hakuna tatizo tutakwenda"
Kamugisha "Huo ndiyo uamuzi wa kiume dogo,hizi starehe zote ni hela,unaona watu walivyobaki mandinga hapo nje,hiyo yote ni hela bila hela utaonekana kibaka tu mbele ya watu wenye nazo hata kama unayoheshima"
Baada ya mazungumzo yale na vyombo kukolea kichwani kwa Kamugisha,jamaa aliamka akawa anacheza muziki bila aibu huku akimuita kila muhudumu wa kike aliyejipitisha mbele yake na kuanza kujichekesha chekesha bila sababu za msingi.
Naendelea................