LESIRIAMU
JF-Expert Member
- Feb 12, 2008
- 8,721
- 13,959
Maneno mujarabu, kwa maana nyingine, Ccm ina ongozwa na CHADEMA, means hata serikali ya Ccm inaongozwa na Chadema ndio maana hata Baba lao amefuata sera za Chadema. Acha hao malala nje wapayuke tuu maana hawajielewiVIJANA WA CCM TUKAE KWA KUTULIA.
Na Thadei Ole Mushi.
Kila nikiangalia hii picha ya Joshua Nasari, nikikumbuka na swali lililoulizwa na Mjumbe Wa NEC toka Songwe kuhusu wahamiaji kupewa Vyeo badala ya vijana waliopo CCM nacheka Sana.
Definitely tuache Hawa vijana wajinafasi kwa kuwa sioni ndani ya UVCCM mwenye uwezo wa kuwazidi. Nilipokuwa nasema Sana kuhusu hili miaka ya kuanzia 2017 Hakuna waliokuwa wanaunga mkono Hoja hiyo kila mtu alikuwa anaimba litania, Ngonjera,Pambio za Masifu, kupiga Manyanga nk.
Niliwaambia ifikapo 2020 mtakumbuka haya niliyokuwa nawaandikia na niliwaambia CCM Asilia itakuwa imetekwa na kutiwa mfukoni. Ni Dhahiri baada ya chuo Cha kivukoni kushindwa kupika vijana wa CCM Chadema inatusaidia jukumu Hilo.
Huwa nawaambia mnapata wapi ujasiri wa kuwaita Chadema Nyumbu? Hahahahah tutulie infact hatuna vijana wanaofikia viwango vya Hawa watu. Tutulie tuendelee na kujifua.
Ukiona baba yako anawagawia watoto wa Jirani Urithi ujue wewe ni mvuta bangi na mla Unga. Akikupa Urithi utauza upate hela ya kulamba Unga.
Ole Mushi
0712702602