US walianza kwa ZTE, wakaja kwa Huawei!! Hivi bado unaamini kampuni zingine za China zitaendelea kujihisi zipo salama dhidi ya US kwa kuona hayo yaliyowakuta ZTE na Huawei wao hayawezi kuwakuta?!
Kukujibu swali lako kitakachofanya waachane na Android ni kwa sababu hakuna hata mmoja anayeweza kujiona yupo salama kibiashara ikiwa ataendelea kutegenea US Tech kwa 100%!!
Aidha, serikali ya China pia inaweza kutoa incentives kubwa kwa kampuni za ndani zitakazotumia Chinese made OS na kuzifanyia figisu zile zitakazoendelea kutumia Android!! Kwa serikali ya China hilo linawezekana kabisa unless Huawei waamue hiyo OS waitumie peke yao kama ilivyo kwa Apple, jambo ambalo sitarajii kwa sababu nadhani wanafahamu kwamba hii vita si ya kupigana peke yao halafu watarajie ushindi!
Kwamba mazingira ya soko yanategemea Android sio sahihi bali usahihi ni kwamba, majority ya Smartphones zinaingia sokoni zikiwa na Android! Ni kama hoja aliyoileta mdau mmoja hapa kwamba Waafrika hatuelewi na matokeo yake tumeng'ang'ana na Windows wakati kuna Linux! Huyu amesahau kwamba majority ya PCs zinakuja na Windows, na kwavile majority ya watumiaji wa PCs ni watu wa kawaida (contrary to watu wenye ABC za IT), there's no way hao watu wanaweza kuhangaika ku-install Linux bila kujali kama muhusika ni Mwafrika, Mchina, Mzungu or whoever! Na ndivyo ilivyo kwa Android! Leo hii inaonekana Android haikwepeki kwa sababu majority ya smartphones zinakuja na Android! Endapo Apple wasingekuwa wanaibania iOS, probably the story could be different now!!
So, it's up to kwa Huawei. Ikiwa watafanikiwa kutengeneza OS iliyosimama, keep this post, within 5 years, Android itaanza kupumulia mashine hasa kwa kwa kuziangatia manufacturers wakubwa wa affordable smartphones (by units produced) wapo China, na wataendelea kuibuka kila mwaka!
Kwamba Huawei wamesema wataendelea kutumia Android; kumbe ulitarajia waanze kuwa na nyodo kabla OS yao haijasimama?! Hivi hata mpangqji aliyeamua kujenga baada ya kuchoka manyanyaso ya Baba/Mama Mwenye Nyumba, unadhani ataanza kumletea nyodo mwenye nyumba wakati nyumba anayojenga ndo kwanza ni boma tu?! Hiyo kauli ya Huawei ni lugha tu ya kibiashara ili waendelee ku-maintain customers' confidence. There's no way Mchina ataacha kuhangaika kutafuta OS ya kwake mwenyewe wakati anafahamu, there's no way Mchina atakuja kuongea lugha moja na Mmarekani at least in the next 25 years!!