Karibia kila kampuni kubwa za uzalishaji wa simu Duniani zina Operating Systems zao na zipo sokoni. Issue ya kuja na OS mpya na kuiweka sokoni si kitu kirahisi kama wengi wanavyozungumza hapa. Ni jambo linalohitaji uwekezaji mkubwa sana hasa katika issue ya App Ecosystem. Kutengeneza OS tu bila kuwa na Support ya Apps na Developers wa kutosha hilo ni tatizo kubwa sana. Unapomuona Xi Jinping anahangaika kwenda Urusi kutafuta App Store mbadala ama unapowaona Huawei wanakwenda Ureno huko kushughulikia App Store mbadala kwa ajili yao usidhani kuwa ni jambo rahisi tu la kusema "OS imekamilika".
Unasema kuwa Serikali ya China itazifanyia figisu kampuni za ndani zitakazogoma kuachana na Android;
Hilo la 'Figisu' unalosema halijaanza leo na lipo. China wameshazipiga 'Ban' kampuni nyingi tu za Kimarekani nchini humo na hata zilizopo humo mfano hata Apple wameshasumbuliwa vya kutosha na wako tayari hata kuhamisha viwanda vyao na kuvipeleka mahali pengine, ikibidi. Katika mazingira kama hayo ya kuzibana kampuni za nje na kuweka upendeleo ndani ya China pekee unafikiri ni App Developers wangapi wa Kimataifa watakaofanya kazi katika mazingira hayo kwa ajili ya hiyo OS yao na waachane na Android? Unafikiri hali ya kampuni hizo za ndani itakuwaje katika soko la kimataifa licha ya kuwa soko lao la ndani ni kubwa?
"Mazingira ya soko yanategemea Android" ?? Sidhani kama hii 'Statement' niliisema na pamoja na hilo bado haipishani sana na ukweli wenyewe sababu Android si OS tu peke yake. Kuna watu wanachanganya hapa na pengine hawafahamu nyuma yake kuna kitu gani. Android kama OS nyuma yake kuna App Ecosystem (yenye Apps za kutosha, App Developers wa kutosha) iliyojijenga kwa muda mrefu na imejitosheleza kwa ujumla wake kwa kiasi cha kufikia kuliteka soko la Dunia. Ni kwamba tayari walishatengeneza mazingira ambayo hata kama kuna kampuni zitakazoibuka na kuanzisha uzalishaji wa simu 'leo hii' hawana budi kujiunga katika 'Ecosystem' yenye nguvu zaidi kwa sasa.
Huawei wanadai kuwa wamekamilisha OS yao hiyo (Harmony). Well, Huawei wamekuwa wakifanyia kazi OS yao muda mrefu na hata sasa wana kazi ya kuhakikisha kwamba inafanya kazi ndani ya soko la China kwanza na ndicho kitakachofanyika na hata hivyo bado kama nilivyosema awali, wanahitaji kuja na kitu bora zaidi cha kuitikisa Android na kuwashawishi App Developers kutoka sehemu mbalimbali Duniani kufanya kazi nao, hicho si kitu rahisi. Na hata wanachosema Huawei ni kuwa hiyo OS haitatumika kwenye simu (Smartphones) bali katika vifaa vinginevyo kama vile Smart Displays, Watches n.k.
Na kama unavyosema, endapo Serikali ya China ikiziendeleza hizo 'Figisu' kwa sura nyingine, huenda ndipo tutakaposhuhudia uhalisia wa 'vita' yenyewe ya kiuchumi itakayo muathiri hata China mwenyewe kuliko kilichopo hivi sasa. Wachina wanalifahamu hilo na hawatopenda 'kukurupuka' na kuachana tu na Android kisa wana OS yao na ndiyo maana wanasema hivyo kwamba hawataachana na Android na wataendelea nayo kama kawaida mpaka hapo mazingira yatakapokuwa magumu kwao kuendelea kufanya hivyo.