Huawei tayari wamekamilisha Operating System (OS) yao

Huawei tayari wamekamilisha Operating System (OS) yao

Kila siku mnasema China katengeneza ya kwake kumbe horaaa
 
Jenga hoja, majadiliano lazima yawe na pande mbili kwa hoja sio ushabiki, mvutano ndio unaongeza uelewa
Mkuu humu utaumia, unajadiliana na mataahira ambayo hayajengi hoja badala yake yanaleta ushabiki na mapenzi kwenye mambo ya kitaalam. Hapa utaumia. Kuna mengine humu yanatamani yanatamani marekani ife kwa sababu zao za kidini, hayo unafikiri kuna chochote yanachowaza cha maana?

Utaumia kujadiliana na wavaa vipedo na mataahira wengine inapokuja swala la Marekani.
 
FED na Trump wana mpango wa kushusha dollar ili waanze export zaidi.

Yuan imeshuka na hii itawasaidia Wamarekani kununua zaidi
Mkuu yuan ikishuka viwanda vya china.% kubwa vina nunuwa material ndani ya Nchi adi viwanda vetu vina nunuwa material china je hujuwi kuwa iyo ni nafuu kwa viwanda vya china na hapa kwetu!!
Na jambo ambalo lina waumiza wa marekani ni hilo wanataka yuan ipande ndio itakuwa faida kwao!
Dollar ikishuka izo us anazoziita high-tech zitakuwa rahizi hataweza kumudu kulipa watu wake na mambo mengine mengi yani mambo bado ni kisaanga kwa US hapa ni hesabu anayeweza kumaliza hesabu kwa haraka ndie atakaye fungal ndie mshindi bila shaka china ameshamaliza hesabu zake ama ameshajuwa kanuni!
 
Jenga hoja, majadiliano lazima yawe na pande mbili kwa hoja sio ushabiki, mvutano ndio unaongeza uelewa
Hoja unajenga kwa watu wanaoelewa hoja. Huwezi kujenga hoja kwa watu ambao wametambuliza mapenzi na hisia zao kwenye hilo jambo ukaeleweka.

I can argue with anyone about anything based on facts not on assumptions and personal feelings.

So I better sit back, relax and watch hyenas tearing themselves apart.
 
Android ndio google wenyewe uzi acha product iliyo juu ulimwenguni kisa mgogoro china juzi tu ndo ameacha ujinga ila china alikua anatumia os yao ambayo ilikua na lugha yao kabs zilipoanza fanya vizur devices zao na kuanza kutoka nje ya taifa lao wakaona waingie deal na android leo devices za china zinafanya vizur sababu hiyo sasa uwezi kusifia kitu ambacho akipo sokoni izo ni sarakasi kama mpira kabla amjacheza mtajisifu mmejiandaa na mtashinda alafu ukifungwa unaanza tafuta sababu ila mmarekani nae sio kama anataka huawei afe mana zaid ya 70% ya chips set za huawei ni za viwanda vya kimarekani china wana assemble tu na few chip set mana vingine vinatika korea na ndo mana leo new updates kwenye huawei inapatikana
Sijui kama umeelewa kilichoandikwa.

Google sasa ivi ana focus kwenye Fuschia OS ni mbadala wa OS yake ya Android. Wachina hapo mwanzo walikuwa wanatumia OS ipi kwani kabla ya android? kabla ujio wa IOS na Android, OS iliokuwa iko top ni Symbian ya Nokia, na hii kama sikosei ilikua distributed kwa kampuni nyengine kwa kulipa license fee. Simu nyengine zilikuwa ni mp4 player tu. Usibabaike na Lugha ukafiri kuwa eti ni OS, ukienda Settings tu unaweza kuchange language na kuweka kichina.

Yaani kabla ya ujio wa Android na OS, hapo mwanzoni kitaa unakuta watu wana nokia na sony ericsson ndo zilikuwa na chat, kina samsung na wengine hawakua na ishu yoyote. Sasa sijui huawei aliwezaje kuuza devices zake nje wakati unasema alikuwa anatumia OS yao ambayo ipo kwenye lugha yao tu, halafu ndio wakaingia deal na Android.
 
Usicheze na waChina a.k.a Vimacho vidogo, Google wameanza kujuta huko, Inaonyeshea Plan B ya hawa vimacho itafanikiwa kwa kiasi kikubwa ndani ya mda mfupi tu, waafrica na Asia watatumia tu bidhaa ya vimacho hamna namna coz ni rahisi sana, Ulaya wote sasaivi wanatumia 5G ya mchina, Marekani anaanza kubwabwaja na kulalamikia nchi za ulaya kuwa zinamsaliti, Yaani mpaka UK anasema hawawezi kuhairisha mfumo wa 5G wa huawei coz taari mkataba umeshafanyika
View attachment 1176635View attachment 1176636
Afrika nayo ya kutegemea hata chupi tu na brezia wananunua mitumba (Kafa Ulaya) leo waje wanunue simu ya laki nne.

Uchumi wa China baada ya September 2 wakishawekewa zile tariffs ndio utaanza kuelekea rasmi makaburini. China hawezi ku-survive economically kwani kutegemea masoko ya nje kwa asilimia 70 ndio itakuwa kifo chake.
 
Nadhani inabidi ifike mahali binadamu tuheshimiane.
Katika hali ya kupambana kibiashara na Us ..China kaanza kumjibu Us kimya kimya.
Thaman ya Yuan imeshushwa.
Rare mineral hakuna kuuza Us.
Hakuna kununua soya beans toka Us.
Taka toka Us zimepigwa marufuku kwa nchi nyingi Asia.
China wamejipanga kupambana na Us bilashaka.
Haisaidii google na apple walikuwa wa kwanza first to arrive first to be served na ubaya wa wachina wanaiga sana na ni wawivu kwenye kufanya research. Sasa hivi big westerners wanafanya research on Artificial Intelligence na Big Data analysis
 
Haisaidii google na apple walikuwa wa kwanza first to arrive first to be served na ubaya wa wachina wanaiga sana na ni wawivu kwenye kufanya research. Sasa hivi big westerners wanafanya research on Artificial Intelligence na Big Data analysis
Lakin hatua moja ni sehemu ya hatua 1000
 
US walianza kwa ZTE, wakaja kwa Huawei!! Hivi bado unaamini kampuni zingine za China zitaendelea kujihisi zipo salama dhidi ya US kwa kuona hayo yaliyowakuta ZTE na Huawei wao hayawezi kuwakuta?!

Kukujibu swali lako kitakachofanya waachane na Android ni kwa sababu hakuna hata mmoja anayeweza kujiona yupo salama kibiashara ikiwa ataendelea kutegenea US Tech kwa 100%!!

Aidha, serikali ya China pia inaweza kutoa incentives kubwa kwa kampuni za ndani zitakazotumia Chinese made OS na kuzifanyia figisu zile zitakazoendelea kutumia Android!! Kwa serikali ya China hilo linawezekana kabisa unless Huawei waamue hiyo OS waitumie peke yao kama ilivyo kwa Apple, jambo ambalo sitarajii kwa sababu nadhani wanafahamu kwamba hii vita si ya kupigana peke yao halafu watarajie ushindi!

Kwamba mazingira ya soko yanategemea Android sio sahihi bali usahihi ni kwamba, majority ya Smartphones zinaingia sokoni zikiwa na Android! Ni kama hoja aliyoileta mdau mmoja hapa kwamba Waafrika hatuelewi na matokeo yake tumeng'ang'ana na Windows wakati kuna Linux! Huyu amesahau kwamba majority ya PCs zinakuja na Windows, na kwavile majority ya watumiaji wa PCs ni watu wa kawaida (contrary to watu wenye ABC za IT), there's no way hao watu wanaweza kuhangaika ku-install Linux bila kujali kama muhusika ni Mwafrika, Mchina, Mzungu or whoever! Na ndivyo ilivyo kwa Android! Leo hii inaonekana Android haikwepeki kwa sababu majority ya smartphones zinakuja na Android! Endapo Apple wasingekuwa wanaibania iOS, probably the story could be different now!!

So, it's up to kwa Huawei. Ikiwa watafanikiwa kutengeneza OS iliyosimama, keep this post, within 5 years, Android itaanza kupumulia mashine hasa kwa kwa kuziangatia manufacturers wakubwa wa affordable smartphones (by units produced) wapo China, na wataendelea kuibuka kila mwaka!

Kwamba Huawei wamesema wataendelea kutumia Android; kumbe ulitarajia waanze kuwa na nyodo kabla OS yao haijasimama?! Hivi hata mpangqji aliyeamua kujenga baada ya kuchoka manyanyaso ya Baba/Mama Mwenye Nyumba, unadhani ataanza kumletea nyodo mwenye nyumba wakati nyumba anayojenga ndo kwanza ni boma tu?! Hiyo kauli ya Huawei ni lugha tu ya kibiashara ili waendelee ku-maintain customers' confidence. There's no way Mchina ataacha kuhangaika kutafuta OS ya kwake mwenyewe wakati anafahamu, there's no way Mchina atakuja kuongea lugha moja na Mmarekani at least in the next 25 years!!
Karibia kila kampuni kubwa za uzalishaji wa simu Duniani zina Operating Systems zao na zipo sokoni. Issue ya kuja na OS mpya na kuiweka sokoni si kitu kirahisi kama wengi wanavyozungumza hapa. Ni jambo linalohitaji uwekezaji mkubwa sana hasa katika issue ya App Ecosystem. Kutengeneza OS tu bila kuwa na Support ya Apps na Developers wa kutosha hilo ni tatizo kubwa sana. Unapomuona Xi Jinping anahangaika kwenda Urusi kutafuta App Store mbadala ama unapowaona Huawei wanakwenda Ureno huko kushughulikia App Store mbadala kwa ajili yao usidhani kuwa ni jambo rahisi tu la kusema "OS imekamilika".

Unasema kuwa Serikali ya China itazifanyia figisu kampuni za ndani zitakazogoma kuachana na Android;

Hilo la 'Figisu' unalosema halijaanza leo na lipo. China wameshazipiga 'Ban' kampuni nyingi tu za Kimarekani nchini humo na hata zilizopo humo mfano hata Apple wameshasumbuliwa vya kutosha na wako tayari hata kuhamisha viwanda vyao na kuvipeleka mahali pengine, ikibidi. Katika mazingira kama hayo ya kuzibana kampuni za nje na kuweka upendeleo ndani ya China pekee unafikiri ni App Developers wangapi wa Kimataifa watakaofanya kazi katika mazingira hayo kwa ajili ya hiyo OS yao na waachane na Android? Unafikiri hali ya kampuni hizo za ndani itakuwaje katika soko la kimataifa licha ya kuwa soko lao la ndani ni kubwa?

"Mazingira ya soko yanategemea Android" ?? Sidhani kama hii 'Statement' niliisema na pamoja na hilo bado haipishani sana na ukweli wenyewe sababu Android si OS tu peke yake. Kuna watu wanachanganya hapa na pengine hawafahamu nyuma yake kuna kitu gani. Android kama OS nyuma yake kuna App Ecosystem (yenye Apps za kutosha, App Developers wa kutosha) iliyojijenga kwa muda mrefu na imejitosheleza kwa ujumla wake kwa kiasi cha kufikia kuliteka soko la Dunia. Ni kwamba tayari walishatengeneza mazingira ambayo hata kama kuna kampuni zitakazoibuka na kuanzisha uzalishaji wa simu 'leo hii' hawana budi kujiunga katika 'Ecosystem' yenye nguvu zaidi kwa sasa.

Huawei wanadai kuwa wamekamilisha OS yao hiyo (Harmony). Well, Huawei wamekuwa wakifanyia kazi OS yao muda mrefu na hata sasa wana kazi ya kuhakikisha kwamba inafanya kazi ndani ya soko la China kwanza na ndicho kitakachofanyika na hata hivyo bado kama nilivyosema awali, wanahitaji kuja na kitu bora zaidi cha kuitikisa Android na kuwashawishi App Developers kutoka sehemu mbalimbali Duniani kufanya kazi nao, hicho si kitu rahisi. Na hata wanachosema Huawei ni kuwa hiyo OS haitatumika kwenye simu (Smartphones) bali katika vifaa vinginevyo kama vile Smart Displays, Watches n.k.

Na kama unavyosema, endapo Serikali ya China ikiziendeleza hizo 'Figisu' kwa sura nyingine, huenda ndipo tutakaposhuhudia uhalisia wa 'vita' yenyewe ya kiuchumi itakayo muathiri hata China mwenyewe kuliko kilichopo hivi sasa. Wachina wanalifahamu hilo na hawatopenda 'kukurupuka' na kuachana tu na Android kisa wana OS yao na ndiyo maana wanasema hivyo kwamba hawataachana na Android na wataendelea nayo kama kawaida mpaka hapo mazingira yatakapokuwa magumu kwao kuendelea kufanya hivyo.
 
Humu kuna watu wengi sana huna haja ya kuumiza kichwa chagua watu ambao wanasoma na kufatilia mambo hapo utafurah wewe, comments zingine unapita juu tuu. Ndege wa rangi moja uruka pamoja
Hoja unajenga kwa watu wanaoelewa hoja. Huwezi kujenga hoja kwa watu ambao wametambuliza mapenzi na hisia zao kwenye hilo jambo ukaeleweka.

I can argue with anyone about anything based on facts not on assumptions and personal feelings.

So I better sit back, relax and watch hyenas tearing themselves apart.
 
Nadhani inabidi ifike mahali binadamu tuheshimiane.
Katika hali ya kupambana kibiashara na Us ..China kaanza kumjibu Us kimya kimya.
Thaman ya Yuan imeshushwa.
Rare mineral hakuna kuuza Us.
Hakuna kununua soya beans toka Us.
Taka toka Us zimepigwa marufuku kwa nchi nyingi Asia.
China wamejipanga kupambana na Us bilashaka.
China hata afurukute vipi hatoweza shinda vita dhidi ya USA hata siku moja na mwenyewe anajua hilo.
Tatizo la marekani ni kwamba wanaweza pambana kwa muda mrefu bila madhara kuwakumba mana wao ndio wanaratibu shughuli nyingi za kiuchumi Duniani kote.
 
Karibia kila kampuni kubwa za uzalishaji wa simu Duniani zina Operating Systems zao na zipo sokoni. Issue ya kuja na OS mpya na kuiweka sokoni si kitu kirahisi kama wengi wanavyozungumza hapa. Ni jambo linalohitaji uwekezaji mkubwa sana hasa katika issue ya App Ecosystem. Kutengeneza OS tu bila kuwa na Support ya Apps na Developers wa kutosha hilo ni tatizo kubwa sana. Unapomuona Xi Jinping anahangaika kwenda Urusi kutafuta App Store mbadala ama unapowaona Huawei wanakwenda Ureno huko kushughulikia App Store mbadala kwa ajili yao usidhani kuwa ni jambo rahisi tu la kusema "OS imekamilika".



Unasema kuwa Serikali ya China itazifanyia figisu kampuni za ndani zitakazogoma kuachana na Android;



Hilo la 'Figisu' unalosema halijaanza leo na lipo. China wameshazipiga 'Ban' kampuni nyingi tu za Kimarekani nchini humo na hata zilizopo humo mfano hata Apple wameshasumbuliwa vya kutosha na wako tayari hata kuhamisha viwanda vyao na kuvipeleka mahali pengine, ikibidi. Katika mazingira kama hayo ya kuzibana kampuni za nje na kuweka upendeleo ndani ya China pekee unafikiri ni App Developers wangapi wa Kimataifa watakaofanya kazi katika mazingira hayo kwa ajili ya hiyo OS yao na waachane na Android? Unafikiri hali ya kampuni hizo za ndani itakuwaje katika soko la kimataifa licha ya kuwa soko lao la ndani ni kubwa?



"Mazingira ya soko yanategemea Android" ?? Sidhani kama hii 'Statement' niliisema na pamoja na hilo bado haipishani sana na ukweli wenyewe sababu Android si OS tu peke yake. Kuna watu wanachanganya hapa na pengine hawafahamu nyuma yake kuna kitu gani. Android kama OS nyuma yake kuna App Ecosystem (yenye Apps za kutosha, App Developers wa kutosha) iliyojijenga kwa muda mrefu na imejitosheleza kwa ujumla wake kwa kiasi cha kufikia kuliteka soko la Dunia. Ni kwamba tayari walishatengeneza mazingira ambayo hata kama kuna kampuni zitakazoibuka na kuanzisha uzalishaji wa simu 'leo hii' hawana budi kujiunga katika 'Ecosystem' yenye nguvu zaidi kwa sasa.



Huawei wanadai kuwa wamekamilisha OS yao hiyo (Harmony). Well, Huawei wamekuwa wakifanyia kazi OS yao muda mrefu na hata sasa wana kazi ya kuhakikisha kwamba inafanya kazi ndani ya soko la China kwanza na ndicho kitakachofanyika na hata hivyo bado kama nilivyosema awali, wanahitaji kuja na kitu bora zaidi cha kuitikisa Android na kuwashawishi App Developers kutoka sehemu mbalimbali Duniani kufanya kazi nao, hicho si kitu rahisi. Na hata wanachosema Huawei ni kuwa hiyo OS haitatumika kwenye simu (Smartphones) bali katika vifaa vinginevyo kama vile Smart Displays, Watches n.k.



Na kama unavyosema, endapo Serikali ya China ikiziendeleza hizo 'Figisu' kwa sura nyingine, huenda ndipo tutakaposhuhudia uhalisia wa 'vita' yenyewe ya kiuchumi itakayo muathiri hata China mwenyewe kuliko kilichopo hivi sasa. Wachina wanalifahamu hilo na hawatopenda 'kukurupuka' na kuachana tu na Android kisa wana OS yao na ndiyo maana wanasema hivyo kwamba hawataachana na Android na wataendelea nayo kama kawaida mpaka hapo mazingira yatakapokuwa magumu kwao kuendelea kufanya hivyo.
Man, sijasema China itazifanyia figisu kampuni za nje, rudia kusoma nilichoandika! Aidha, sijasema hiyo OS ipo okay to take OFF, na wala sijasema hiyo kazi ni rahisi kama unavyojaribu kunilisha maneno! Nilichosema ni kwamba, Huawei WAKISHAFANIKIWA KUWA NA OS ILIYOSIMAMA, basi kuna uwezekano mkubwa serikali ya China encourages kampuni ZA NDANI kutumia a Chinese made OS! Na nikasema China wanaweza hata kufanya figisu kwa kampuni (ZA NDANI) zitakazoendelea kung'ang'ana na Android! Na tunaposema figisu haimaanishi kutaka kuziua hizo kampuni bali zinaweza kukosa favors fulani kutoka serikalini!

Kuhusu kuwekeza, I wish ningekuwa natumia PC nikupe data uone ni namna gani China hivi sasa ina-invest in R&D! Na serikali ya China inazipiga tafu sana hizi tech companies especially Huawei ambayo ni kama national flagship!

Kwamba kampuni nyingi zina OS Yake lakini bado hazijatoboa, wote hao bado walikuwa wanatengeneza za kwao in laxity kwa sababu wanajua tayari ipo OS iliyo operational, kwahiyo hawakuwa na sababu ya ku-~invest a lot of time and money! It's like mtu anayejenga huku anaishi nyumba ya serikali.

Kuhusu Developers hiyo ni issue ndogo sana! Developers wanachohitaji ni platform, PERIOD! Leo hii hiyo OS yao ikishakuwa okay, App Developers wata-develop tu apps cuz all they need is easy to entry platform! Na hivyo wameshasema itakuwa ni open source, utashangaa na kujiuliza na-apps yote haya yametokea wapi!

But all in all, wakati ukisisitiza kwamba kutengeneza OS sio jambo rahisi nami ningependa kukukumbusha Wachina usiwachukulie poa!!
 
Huyo Mwafrika unayemwongelea ni Mwafrika wa aina gani?! Mwafrika wa kawaida ambae ni mtumiaji wa bidhaa au Mwafrika mwenye uelewa na mambo ya IT? Hivi unadhani PCs zingekuwa zinakuja zikiwa na Linux, huyo Mwafrika unayemsema angehangaika kuitafuta Windows?

Hiyo OS ya Huawei kama itakuwa finalized, itakuwa haikwepeki kama isivyokwepeka Windows kwa watumiaji wa kawaida ambao ndio wengi maradufu! Itakuwa haikwepeki, kwa sababu inafahamika simu za Mchina ndizo simu za bei nafuu huku zingine zikiwa na specs mzuri tu! Sasa let's assume hiyo OS ipo okay, kisha simu za Huawei zinakuja na hiyo OS! Na ninaamini simu zingine za Kichina kama Honor, Xiaomi, One Plus, Oppo, Tecno, Infinix na wengine huenda wakafuata kwa sababu, none of them anaweza kujihisi yupo salama dhidi ya figisu figisu za US!

Niliwahi kuongea siku za nyuma, na hapa narudia! Kama hiyo OS itakuwa iko poa, mteja mkubwa wa kuaminika wa Google atabaki Samsung!
Samsung
HTC
Google Pixel
Motorola
Nokia
Sony
One Plus
LG
N.k

Kumbuka kuna zaidi ya device 24.000 zinatumia android. Za china hazifiki hata nusu ya hiyo.
 
Soko kubwa la iPhone lipo China na si US au Europe.

Inaonesha jinsi gani wachina wenyewe hawakubali bidhaa zao hasa Huawei.

Hiyo OS itawavuruga wachina na hawataitumia kama mnavyofikiri.

Ni ngumu kuacha kutumia bidhaa za US kwa jinsi walivyozifunga na Eco system zao.

Itakuwa ngumu ku-intergrate hiyo OS na products nyingi tu toka US.
 
Wachina wangetengeneza complete ecosystem ya Harmony OS. Kuanzia kwenye simu, tablets, PCs na products nyingine independent kama Adobe n.k.
 
Back
Top Bottom