Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Mimi msimamo wangu utakuwa ni kama ulivyo. Sigeuki nyuma nikawa jiwe. Hawa watu wanaubaguzi wa hali juu tena kibaya zaidi wanaufanya kwetu dhidi ya wazawa, lakini watu hawataki kuuona huo wala kuuzungumzia wanataka kuzungumzia ubaguzi aliofanyiwa yeye tu!

Ubaguzi kivipi Bro?

Hatutibiwi kwenye hospitali "zao", i.e Aga Khan, Hindu Mandal, Burhani, TMJ etc?

Walituzuia kwenye majumba "yao" ya sinema? Empire, Odeon, Empress, Drive inn etc?

au kwenye mahoteli "yao" Seacliff, White sands, The courtyard etc?

Tataizo "letu", kujieleza ndio shughuli, kubaguliwa kivipi?

Sidhani kama tunaweza kuwaita Azim Dewji & Mohammed Dewji-Simba, Mar Abbas Gulamali-Yanga, Shaffi & Moh'd Bora-Majimaji, Naushad Moh'd -Malindi (tena huyu ana mke Mswahili), etc kuwa hawa jamaa walikuwa wabaguzi...

Kuna watanzania wenye asili ya kihindi-wagoa wanaojihusisha na mambo ya dini, si wabaguzi, kuna wagoa wanaojihusisha na muziki mf; INAFRIKA Band, si wabaguzi...

Kuna watanzania wenye asili ya kihindi-masinga singa wanaojishughulisha na ufundi pale gerezani, si wabaguzi...

Ubaya wa wachache wetu (watanzania wazawa-wabantu) ni tabia za utoro kazini & uvivu, udokozi, fitna & majungu , na kukubali Rushwa (tena za kipuuzi i.e fulana, kofia, na wale vibosile kwenda kwenye maduka "yao" kuomba tv, mafriji etc) ndio maana hawa jamaa wanatudharau, sio kutubagua.

Hapa nilipo, kuna wahindi nane kutoka East africa, wana heshima na adabu, tena wanasema "wewe ndugu yetu, tumetoka wote nyumbani!", na kiingereza hawataki kukizungumza, kiswahili tu!.
 
Ubaguzi kivipi Bro?

Hatutibiwi kwenye hospitali "zao", i.e Aga Khan, Hindu Mandal, Burhani, TMJ etc?

Walituzuia kwenye majumba "yao" ya sinema? Empire, Odeon, Empress, Drive inn etc?

au kwenye mahoteli "yao" Seacliff, White sands, The courtyard etc?

Tataizo "letu", kujieleza ndio shughuli, kubaguliwa kivipi?

Sidhani kama tunaweza kuwaita Azim Dewji & Mohammed Dewji-Simba, Mar Abbas Gulamali-Yanga, Shaffi & Moh'd Bora-Majimaji, Naushad Moh'd -Malindi (tena huyu ana mke Mswahili), etc kuwa hawa jamaa walikuwa wabaguzi...

Kuna watanzania wenye asili ya kihindi-wagoa wanaojihusisha na mambo ya dini, si wabaguzi, kuna wagoa wanaojihusisha na muziki mf; INAFRIKA Band, si wabaguzi...

Kuna watanzania wenye asili ya kihindi-masinga singa wanaojishughulisha na ufundi pale gerezani, si wabaguzi...

Ubaya wa wachache wetu (watanzania wazawa-wabantu) ni tabia za utoro kazini & uvivu, udokozi, fitna & majungu , na kukubali Rushwa (tena za kipuuzi i.e fulana, kofia, na wale vibosile kwenda kwenye maduka "yao" kuomba tv, mafriji etc) ndio maana hawa jamaa wanatudharau, sio kutubagua.

Hapa nilipo, kuna wahindi nane kutoka East africa, wana heshima na adabu, tena wanasema "wewe ndugu yetu, tumetoka wote nyumbani!", na kiingereza hawataki kukizungumza, kiswahili tu!.

Angalia maswali yangu kwa Mkjj ukishayajibu tutaweza kuendelea na mjadala vinginevyo hakuna umuhimu wa kuendelea na mjadala huu.
 
nyinyi wote mnazungumzia "hawa watu" sijui "wahindi vile au hivi" huo ni mjadala mwingine, hamjajieleza vya kutosha kwanini binti huyu specifically, asiwe miss Tanzania? Msianze kusema makosa ya jamii nzima mumwadhibu yeye? Je, binti huyu amewahi kuwabagua watu weusi, je binti huyo alikuwa anajitenga kwenye mashindano n.k mtaendelea kupiga kelele "wahindi hivi au vile" haifanyi kuwa hoja yenu ya kumbagua huyu binti iwe na nguvu!

Mnaweza kusema "wahindi walitunyima mihogo" au "wahindi hawakutupa maji ya kunywa" kuwa ni wabaguzi wakubwa hilo lote sawa na mimi naelewa na ninafahamu kuna wahindi ambao wana tabia hizo za kibaguzi tena si kidogo! Hilo wala siyo mjadala, mjadala ni Richa Adhia amefanya nini cha kibaguzi ambacho kinamfanya asistahili kuwa Miss Tanzania? Hadi hivi sasa hakuna aliyethubutu kutuonesha japo kitu kimoja isipokuwa porojo za "wahindi wako hivi ohh wahindi wako vile"

Give me some undisputable facts kwamba Richa Adhia hastahili kuwa Miss Tanzania kwa vile amefanya hivi au vile au hakufanya hivi au vile!! haya ya 'wahindi wabaguzi' I have had enough.. stick to the topic..

Kwa nini Richa Adhia, aliyekuzaliwa na kukulia Tanzania anayezungumza Kiswahili, Kiingereza, Na Kisukuma (sijui alijifunza shule gani Kisukuma!!) ambaye hakuna hata mahali pamoja ametoa kauli za kibaguzi (at least not in public) au amefanya kitendo chochote cha kuwadhalilisha watu weusi, asiwe Miss Tanzania? Can i make this question more pointed than that?

Unathubutu kuwaita hata dada zetu maimuna pamoja na kujua wazi mfumo wetu wa elimu unavyolegalega kwenye ufundishaji wa Kiingereza. Huoni walakini wowote wa dada zetu kukosa ushindi wa Miss Tanzania kwa kuwa 'walijikanyaga' katika kujibu swali kwa kiingereza. Wakati huo huo huoni mapungufu aliyokuwa nayo huyo mdosi ambayo hayakustahili yeye kupewa ubingwa huo!
 
Unathubutu kuwaita hata dada zetu maimuna pamoja na kujua wazi mfumo wetu wa elimu unavyolegalega kwenye ufundishaji wa Kiingereza. Huoni walakini wowote wa dada zetu kukosa ushindi wa Miss Tanzania kwa kuwa 'walijikanyaga' katika kujibu swali kwa kiingereza. Wakati huo huo huoni mapungufu aliyokuwa nayo huyo mdosi ambayo hayakustahili yeye kupewa ubingwa huo!

Hata Richa ni dada yetu!! Kama alikuwa na mapungufu ya sifa zilizokuwa zinahitajika basi tujadili na tupinge ushindi wake katika parameters hizo. Mnapotoka nje na kuanza kuingiza asili yake na kuanza kumuita majina kama "mdosi"n.k., huo ni ubaguzi na mimi naupinga kwa nguvu zangu zote. Two wrongs don't make a right. Wahindi ambao ni wabaguzi na wao nawapinga kama ninavyowapinga Waafrika weusi walio wabaguzi na mtu/ watu wengine wote walio wabaguzi. Ubaguzi ni ubaguzi tu. Mimi kubaguliwa na Mhindi hakuhalalishi mimi kumbagua Mhindi mwingine asiye na makosa na ambaye hajanibagua na hakuhalalishi mimi kuchukia jamii nzima ya Kihindi. Ndugu zangu humu mnanitisha na hizo feelings zenu za kibaguzi. Nilidhania Tanzania hatuna mambo haya but I guess I was wrong!!!!!!
 
Hata Richa ni dada yetu!! Kama alikuwa na mapungufu ya sifa zilizokuwa zinahitajika basi tujadili na tupinge ushindi wake katika parameters hizo. Mnapotoka nje na kuanza kuingiza asili yake na kuanza kumuita majina kama "mdosi"n.k., huo ni ubaguzi na mimi naupinga kwa nguvu zangu zote. Two wrongs don't make a right. Wahindi ambao ni wabaguzi na wao nawapinga kama ninavyowapinga Waafrika weusi walio wabaguzi na mtu/ watu wengine wote walio wabaguzi. Ubaguzi ni ubaguzi tu. Mimi kubaguliwa na Mhindi hakuhalalishi mimi kumbagua Mhindi mwingine asiye na makosa na ambaye hajanibagua na hakuhalalishi mimi kuchukia jamii nzima ya Kihindi. Ndugu zangu humu mnanitisha na hizo feelings zenu za kibaguzi. Nilidhania Tanzania hatuna mambo haya but I guess I was wrong!!!!!!

Wako wadosi wengi tu wenyewe wanajiita wadosi wala hawaoni noma, iweje wewe uone noma zaidi yao? Dada zetu kuitwa maimuna hukuona ubaya wowote! Mimi wahindi sio dada zangu wala kaka zangu hata siku moja, siwaoni sehemu za starehe zilizojaa waswahili, siwaoni kwenye sherehe zetu kama vile harusi n.k. mpaka zile za vingunge wa chama na serikali. Siwaoni kwenye vilio vya watu weusi, hata kwenye misiba ya Kitaifa kama ajali ya meli ziwa victoria na ajali ya treni pale TRC wadosi sikuwaona hivyo kwangu mimi siwaoni kama kaka au dada zangu.
 
Juzi juzi tu tulikuwa na msiba wa dada yetu Amina Chifupa, pamoja na kuwa alikuwa na umaarufu mkubwa lakini hao 'dada zako na kaka zako' hatukuwaona kwenye msiba huo hilo wewe hulioni. Angalieni vizuri mjue ni nani mbaguzi!
 
Wako wadosi wengi tu wenyewe wanajiita wadosi wala hawaoni noma, iweje wewe uone noma zaidi yao? Dada zetu kuitwa maimuna hukuona ubaya wowote! Mimi wahindi sio dada zangu wala kaka zangu hata siku moja, siwaoni sehemu za starehe zilizojaa waswahili, siwaoni kwenye sherehe zetu kama vile harusi n.k. mpaka zile za vingunge wa chama na serikali. Siwaoni kwenye vilio vya watu weusi, hata kwenye misiba ya Kitaifa kama ajali ya meli ziwa victoria na ajali ya treni pale TRC wadosi sikuwaona hivyo kwangu mimi siwaoni kama kaka au dada zangu.

Na kuna weusi wengi tu wajiitao "nigger" au "nigga" bila noma yoyote lakini ukweli unabaki palepale kuwa neno "mdosi" ni la dhihaka au tusi. Kwa vile umewakataa wao kuwa kaka na dada zako hiyo inaonyesha mizizi ya chuki yako dhidi yao imejijenga na iko imara na si rahisi kunyofolewa. Haya kaka wewe endelea kuwa hivyo.
 
Juzi juzi tu tulikuwa na msiba wa dada yetu Amina Chifupa, pamoja na kuwa alikuwa na umaarufu mkubwa lakini hao 'dada zako na kaka zako' hatukuwaona kwenye msiba huo hilo wewe hulioni. Angalieni vizuri mjue ni nani mbaguzi!

Wewe ulikuwepo kwenye huo msiba? Unajuaje kama hakukuwepo na watu wenye asili ya Kihindi? Uliangalia rangi na asili ya kila mtu aliyekuwepo? Je, wasukuma walikuwepo wangapi? Na Watanzania wenye asili ya Kisomali walikuwepo? Wapemba je?
 
51ad580f.jpg


This is Richa Adhia Miss Earth Tanzania 2006
 
Five queens picked for world contests

2006-08-21 07:53:45
By Majuto Omary

Five queens won chances to represent Tanzania in various miss world beauty contests over the weekend.

The beauties are Jamillah Munisi, who will represent Tanzania in Miss Globe International, Upendo Mpanda (Miss Intercontinental) and Angella Kileo (Miss International).

Others are Edna Audax (Miss Top Model of the World) and Richa Adhia (Miss Earth).

The queens won the local titles at the Beauty Queen of Tanzania Contest held at the Dar es Salaam Holiday Inn last Saturday.

The contestants competed wearing clothes designed by three local designers - Farouque Abdelah from Zanzibar, Angelo-Elly Mlaki of Neith Fashions and up and coming designer Loveness Mpanda of Dar es Salaam.

Other awards went to Siah Lyimo, who won Miss Talent, Aziza Mbogga (Miss Punctuality), Nora Alex (Miss Personality) and Sarah Martin (Miss Photogenic).

Other queens who contested at the event organized by Maria Sarungi but did not win any award are Anna Mshana, Halima Mandari, Kaneza Kapfunsi, Neema Chembe and Sherehe Abdallah.

The contest was sponsored by Holiday Inn Hotel, Golden Tough Salon and Valley Springs.

Rehema Sudi last year represented Tanzania at the Miss Earth, Magreth Wilson Chacha (National Costumes in Miss International), Joan Cassian (Miss Intercontinental) and Tetemaria Mallya (Miss Top Model).
  • SOURCE: Guardian
 
ndugu yangu kada tafadhali punguza munkari! baba wataifa alisha sema tusibaguane kwa dini,rangi, kabila, jinsia eneo unalotoka au nanmna nyingine yeyote ile.

namuheshimu sana hayati baba wa taifa, but do "i" have to base everything on him ? not me, that i know of !
 
wee hata ungeangalia video za miss tz jamaa mmoja hivi (sio huyo miss ) wa kihindi nadhani ndio alikuwa nchaji wa hayo mambo ! wenyewe wanakwambia binti kapachikwa ! ni kama miss wa mwaka wa jana, watu walisema weeeeeeeeeeeeeee mwishowe kimyaaaaaaaaaaaaa, same thing will go on here !
 
wewe ndio umetumia neno wazawa.. so wewe ulidefine! ili nijue unazungumzia nini. Mmetoka kwenye rangi, mnaenda kwenye kupachikwa... si mseme tu hakuzaliwa TAnzania tujue! na wazazi wake siyo raia!

Bubu, hujaniambia Richa amekosea nini? WEwe umeng'ang'ania wahindi hivi wahindi vile.. je we unaendaga kwenye misiba yao!? Unaendaga kwenye harusi zao? HIvi kuna mtu humu ambaye anarafiki wa kihindi na aliwaalika kwenye harusi au sherehe fulani na hawakutokea?
 
There is a very thin line here and I think pple need to walk on it with a lot of cautious. This kind of talk is dangerous.....though both sides have good points!!. Mie binafsi sifagilii ubaguzi wa aina yeyote ile kwani nina ukabili almost everyday in the last 10yrs, wahindi wazawa ni sehemu ya TZ na lazima tulikubali hilo. Kuna matatizo ktk community ya wahindi na wapo wabaya tena sana lakini hiyo haitoshi kumkandamiza huyu dada kwani kuna nafasi kubwa si miongoni mwa wale wabaya. Mpeni nafasi yake ya kuipeperusha Flag ya bongo kwani ameshinda fair and square!!. Kuna politics mingi sana ktk mjadala huu......nadhani kwamba watu wanao mbagua huyu dada wapo motivated na hilo pamoja na economic issues lakini wana shindwa ku-drive hiyo point home. Chuki iliyopo juu ya RA anayesemekana na mhindi, mkataba mpya wa reli na mengineyo yana changia fikra hizi za kibaguzi juu ya dada huyu. Lazima tujue kwamba yeye ni mrembo tu na hayo mengine hayamhusu....tujifunze kudili na kila mtu kama individual na sio kama group la race flani........naiacha hapo kwa sasa.
 
Ngoja niulize swali hapa lakini mfano.SWALI: Je akitokea mchezaji soka mzuri wa kihindi,akachaguliwa timu ya taifa na akawa anafunga magoli mengi kiasi cha kuifikisha timu yetu labda kwenye kombe la dunia je watu watasemaje??. Usije kusema, ooooooh wahindi huwa hawachezi soka kwani utachemsha. Kumbuka France kwenye squad lao la mwaka 2006, walikuwa na mchezaji wa kihindi ingawa alikuwa hapati minutes nyingi.
 
Ile ya sherehe na misiba ilikuwa haijatulia kabisa kaka nanilii, kusema kweli I was shocked for a cheap shot like that esp from you (unajijua).
 
Mynameisyours, binafsi nimejaribu kutwa nzima kusteer mjadala huu kwenye hoja moja tu, nayo ni Binti huyo hajamkosea Mtanzania mwingine jambo lolote kiasi cha kustahili kutendewa anavyotendewa hivi. Wabaguzi wetu kwa vile wanamalalamiko juu ya WAhindi basi wamepata nafasi yao ya kuonesha wahindi "makosa yao". Hoja zote zinazozungumzwa dhidi ya wahindi hakuna aliyeonesha hata kidogo ni jinsi gani Richa anahusika. Hakuna aliyeonesha kuwa Richa amewahi kumuita mtanzania mweusi "mbwa", hakuna aliyeonesha kama Richa hawajawahi kuwa bf mweusi, hakuna aliyeonesha kuwa huyu binti hazungumzi Kiswahili (as a matter of fact she does), hakuna mtu anayeweza kuonesha kuwa huyu binti hajui lugha nyingine yoyote ya watanzania (anazungumza Kisukuma), hakuna aliyeonesha hata mara moja kuwa jirani zake walipofiwa huyu binti hakutokea, na hakuna aliyeonesha kuwa wakati Amina anafariki huyu binti hakusikia uchungu au kuguswa na msiba ule! None!! HAKUNA.

Bla bla bla zote hazihusiani na binti huyu. Ndiyo maana nimetoa ushauri wanataka kuzungumzia matatizo ya jamii ya Wahindi waanzishe mada, ila wakiendelea na maneno yao ya kibaguzi tutaendelea kuwaonesha ubaguzi wao (na wala haina haja kwani wengine wameshakubali kuwa wao ni wabaguzi).

Richa ameshinda Umiss Tanzania 2007, atawakilisha TAifa letu, and I'm so proud that Tanzania hatimaye imeweza kufanya kile ilichokuwa inahubiri enzi zile "Binadamu wote ni sawa, na Afrika ni moja!" Tuliwapinga wabagauzi weusi, tukawaimbia nyimbo za kuwakana, vivyo hivyo tutawapinga wabaguzi weusi.

Wakati Nelson Mandela anahitimisha ile hotuba yake maarufu katika mahakama ya Makaburu, alimaliza kwa kusema hivi na natumaini itawasha moto wa usawa ndani yenu:

During my lifetime I have dedicated myself to this struggle of the African people. I have fought against white domination, and I have fought against black domination. I have cherished the ideal of a democratic and free society in which all persons live together in harmony and with equal opportunities. It is an ideal which I hope to live for and to achieve. But if needs be, it is an ideal for which I am prepared to die.

Hotuba yake hiyo ilitolewa siku tano tu kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Na ndani yake ukiisoma utaona anawataja kina Nyerere na Kawawa jinsi walivyosaidia katika harakati za ukombozi kule Afrika KUsini.
 
Mimi siangalii hili kama ubaguzi wa rangi bali ubaguzi wa kijamii. Nina imani kuwa huyu hakuwa mrembo kuliko wote, ingawa sikusikia wale wangine walivyojibu maswali yao. Ninadhani kuwa alikuwa kipezwa uzito sana hata kwa mambo madogo tu kulingana na position yake kijamii.
 
Back
Top Bottom