How GOD is smart

How GOD is smart

Yule Mwana wa mariam (YESU) alikuwa ni chombo tu cha Mungu kufanyia kazi zake hapa duniani yule alikuwa na Vyeo (TITLES) Mbalimbali ndio-maana aliitwa Nabii,Mwana wa Adam,Mwalimu,Mtume,mwana kondoo,Mwana wa Mungu,Kristo,masihi wa bwana,
,Pia hujawahi kusoma andiko linasema atazaliwa mtoto mwanaume jina lake ataitwa Emmanuel maana yake ni "MUNGU PAMOJA NASI" ? (Isaya 7:14,Matayo 1:23),kivipi Mungu pamoja nasi??,inamaana bikira mariamu alimzaa MUNGU?? HAPANA! kwanini Hapana? kwa sababu
> Mungu hazaliwi (Yesu kristo alizaliwa),wala
>Mungu hana Baba wala hana mama (Yesu kristo alikuwa nao)
>Mungu Hakui kiumri na maarifa(Yesu alikua kiumri na maarifa Luka 2:52)
>Mungu Hana mwanzo na hana Mwisho(Mwana wa adamu mwanzo wake alizaliwa na mama yake na mwisho wake alisulubiwa msalabani)
>Mungu Alikuwepo kabla ya vyoote(mwana wa adamu alikuja baadaye),
>Mungu Ni wa milele na milele (mwana wa adamu alikufa msalabani)
>Mungu hafi (Mwana wa Adam alikufa)
Sasa KIVIPI EMMANUELI MUNGU PAMOJA NASI?? Jibu lipo 2 Wakolinto 5:19 inasema hivi "yaani, 'Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho"
kumbe Yule mtoto aliyezaliwa na Bikira mariamu akaitwa Yesu hakuwa Mungu ila Mungu alikaa ndani yake,Mungu alijificha ndani yake,Mungu huwaga anajificha (ISAYA 45:15)!,
Yesu alisema "ukiniona mimi Umemuona Mungu" (Yohana 14:9) Kivipi umemuona Mungu wakati Mungu ni Roho na haonekani?,kivipi wakati Mungu sio mwanadamu Yesu alikuwa mwanadamu??,alikuwa anamaanisha Kupitia Kazi anazozifanya sababu yeye hafanyi chochote isipokuwa Mungu ambaye yupo ndani yake ndio anafanya!,yeye anatumika tu kama chombo (Yohana 14:10)!,
>Kwahiyo Mungu akiingia kwa kitu hicho kitu hakiwi Mungu bali Mungu anakuwa kajidhihirisha kupitia hicho kitu
>Yesu ni Mungu sasa na alikuwa Mungu kabla ila yule binadamu aliyezaliwa na Bikira mariam akaitwa Yesu hakuwa Mungu bali alikuwa Mwana wa Mungu ,kwakuwa alikuwa mwana wa Mungu alirithi jina la Mungu Baba ambalo ni Yesu,Mungu alikuwa ndani yake
>Hiyo yohana 17:3 ,nikweli Yesu alitumwa na Mungu kivipi? ndio nimekuelezea hapo juu,sasa ili umjue Mungu unatakiwa ukubali matendo ya mwili ya mwanaye wa pekeealiyoyafanya hapa duniani kwasababu yalikuwa kama mfano kwetu namna gani tufanye hapa duniani ili kuurithi ufalme wa Mungu,ndiomaana tunabatizwa,sababu Yesu alibatizwa,tunajawa na roho mtakatifu sababu Yesu alijawa na roho mtakatifu nk..

1. Tatizo lako maneno mengi halafu huelewi unachokiongea. Sasa hayo maelezezo uliyotoa juu umethibitisha kuwa yesu alikuwa ni binadamu tu ila Mungu ndiye alikuwa ndani ya Yesu ili Yesu aweze kufanya jambo.

2. ili Yesu nae awe Mungu inabidi ukiri ya kwamba kulikuwa na Yesu wawili kwamaana aliyekuwa duniani kufundisha waisrael na kisha akafa kifo cha laana alikuwa ni Yesu, na pia aliyekuwa mbinguni kipindi Yesu akiwa duniani ambapo Yesu alimwita kuwa ni baba; naye alikuwa ni Yesu huyo huyo kwahiyo Yesu alikuwa anajiomba mwenyewe.

3. Nimekwambia utoe andiko linalosema Yesu ni Mungu tangu mwanzo wa dunia. Umenipa 1wakorintho (10:1-4) kwenye hilo andiko hakuna mahali paliposema kuwa Yesu ni Mungu tangu mwanzo wa dunia.
Andiko lako hilo hapo ulilotoa
1 Wakorintho 10:1-4

1 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;

2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;

3 wote wakala chakula kile kile cha roho;

4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Well, vyote ulivyoandika hapo juu ni very illogical, since natumia logic nichangiapo mijadala(bila shaka kila mtu anapaswa kutumia pia), kipingele hiki pekee ndicho angalau kinaweza fanyiwa majadiliano, ili niweze kuendelea kuchangia, naomba unijibu swali nitakalo kuuliza ili niweze kuchanganua kama kipengele hiki nacho kina at least chembe za logic ama nachenywe ni pumba tu. Swali langu ni, tangua niwe na akili zangu timamu, sijawahi kumuomba mungu anisaidie kitu chochote kile, lakini nina mafanikio makubwa kuliko wakeshao wakimuomba(moja wapo ni bado napumua{natumia point yenu kuu ya kuwa mungu ndio mgawaji wa pumzi}), kwanini mungu ni mnafiki kiasi kwamba anawanyima wafuasi wake waaminifu na watiifu pumzi na mafanikio mengine, ila ananipa mimi nisiye hata na muda nae?
Mungu alishagawa rizki kwa kila kiumbe hadi panya na kiroboto na alisha gawa uhai mpaka muda maalum alioamua yeye ufe. Haijalishi ni jambazi au padri au mchawi
 
Hakuna binadamu anayefikia u-smart alionao Mungu, kwanza kabisa Mungu hawezi vunja sheria aliyojiwekea tofaut na mwanadamu, pili Mungu sio muongeaji ongeaji hovyo, huwa ana maneno machache Kwa sababu kila neno lake ni sheria.

Watu wengi tumekua tukijiuliza Kwa nin Mungu aliruhusu shetani amdanganye hawa, jibu ni kwamba Mungu alimpa mwanadamu option mbili ya kumkata au kumkubali, bahati mbaya Adam akamkataa Mungu, na Mungu bila hiana akakubaliana na adamu kwa-sababu angeingilia angevunja sheria aliyojiweka yeye. Na shetan anamjua Mungu Kwa sababu ameshakaa naye ndo maana alijiamini alivyomfuata hawa.

Ndo maana hata wanadamu wanamtukana Mungu na haingilii, jibu ni kwamba hawez kukulazimisha umtumikie/umfuate, yaan wanafamu tuna Uhuru wa kumkataa Mungu, ndo maana ni Hatar sana kulazimisha watu kumfuata Mungu.

Mungu hawez kuja kuishi duniani Kwa sababu in roho (spirit), ili uishi duniani lazima uwe na mwili (dead body), ndo maana hata majini lazima yamwingilie MTU yaishi ndani yake Kwa sababu ili uishi dunian ni lazima uwe na mwili.

Shetani ilimbidi amuombe nyoka mwili ili autumie mwili wake kumdanganya Adam na hawa Kwa sababu na yeye ni roho

Hata binadamu akifa kinachokufa ni mwili na sio roho, ndo maana baada ya kufa roho haiwez ishi duniani Kwa sababu ni illegal Kwa roho kuish duniani, kwa hy lazima iondoke, ndo maana Mungu alimtuma YESU aje na mwili wa binadamu ili atimize lengo lake.

Ndo maana dhana nzima ya maombi ikaja, Kwa sababu ukitaka kitu lazima umuombe Mungu Kwa sababu ana uhakika unataka jambo fulani au hulitaki, Kwa sababu kabla ya mwanadamu kuasi kulikua na fellowship na sio maombi.
Kwas sababu kila neno lake ni sheria nimependa iyoo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Tatizo lako maneno mengi halafu huelewi unachokiongea. Sasa hayo maelezezo uliyotoa juu umethibitisha kuwa yesu alikuwa ni binadamu tu ila Mungu ndiye alikuwa ndani ya Yesu ili Yesu aweze kufanya jambo.

2. ili Yesu nae awe Mungu inabidi ukiri ya kwamba kulikuwa na Yesu wawili kwamaana aliyekuwa duniani kufundisha waisrael na kisha akafa kifo cha laana alikuwa ni Yesu, na pia aliyekuwa mbinguni kipindi Yesu akiwa duniani ambapo Yesu alimwita kuwa ni baba; naye alikuwa ni Yesu huyo huyo kwahiyo Yesu alikuwa anajiomba mwenyewe.

3. Nimekwambia utoe andiko linalosema Yesu ni Mungu tangu mwanzo wa dunia. Umenipa 1wakorintho (10:1-4) kwenye hilo andiko hakuna mahali paliposema kuwa Yesu ni Mungu tangu mwanzo wa dunia.
Andiko lako hilo hapo ulilotoa
1 Wakorintho 10:1-4

1 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;

2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;

3 wote wakala chakula kile kile cha roho;

4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.



Sent using Jamii Forums mobile app
Shida unachukulia concept ya Mungu ki-binadamu
1.Yesu alikuwa Mungu na ni Mungu sasa lakini mwana wa Adam hakuwa Mungu ila Mungu alikaa ndani yake,Yule mwana wa adamu aliyeitwa Yesu Kristo alirithi Jina,nguvu,uweza,mamlaka,nk kutoka kwa baba yake ambaye ni Mungu,ndiomaana hata sisi tukifanyika kuwa wana wa Mungu basi tunarithi hivyo vyoote

2.Hapa ndio unachukulia Concept ya Mungu kibinadamu,Mungu mwenyewe kasema yeye sio mwanadamu!,Yohana anasema Mungu ni Roho (Yohana 4:24),kama ni Roho inamaana Yuko kila mahali kwa wakati mmoja,(Yeremia 23:23-33,mithali 15:3,zaburi 139:7-10).Angalia maajabu mengine ya Mungu kipindi Yesu kristo kaenda kubatizwa na Yohana mbatizaji ,
>Mungu huyo huyo alikuwa ndani ya Yohana Mbatizaji (Sababu yohana mbatizaji alizaliwa tayari kajaa roho mtakatifu Mungu alikuwa ndani yake),
>Mungu huyo huyo alikuwa ndani ya Yesu kristo (sababu imeandikwa Mungu alikuwa ndani ya kristo kuupatanisha ulimwengu na yeye)
>Mungu huyo huyo alisikika mbinguni akisema "Huyu ni mwanangu mpendwa nimependezwa naye"
Shughuli zoote hizi alikuwa anazifanya mwenyewe kwa njia mbalimbali,umeniuliza kama Yesu alikuwa anajiomba mwenyewe
inamaana hujui Yesu alikuja dunian kufanya nini!,biblia inasema hivi Yesu alikuja duniani kuacha mfano wa sisi wanadamu kuufuata (Yohana 13:13-16,1wakolinto 11:1).Alibatizwa na sisi tunabatizwa,alimuomba Mungu na sisi tunamuomba Mungu,hakutenda dhambi na sisi tunatakiwa tusitende dhambi,alifunga na sisi tunafunga,alishiriki meza ya bwana na sisi pia tunashiriki,alijawa na roho mtakatifu na sisi pia tunatakiwa kujawa na roho mtakatifu,nk ,kwahiyo alikuwa anamuomba Mungu ambaye alikuwa ndani yake,na Muda huo alikuwa mbinguni!

3.Hilo andiko nimekupa umeliandika na huo mstari wa 4 inamaana haujauelewa au ulitaka waseme Yesu kabisa na sio kristo??,ngoja nikupe na hili,umesahau Yesu mwenyewe aliulizwa yeye ni nani na akajibu Kabla ya Abraham kuwako alikuwako (Yohana 8:58) na hii (1 Wakorintho 10:1-4) huo mstari wa 4 unasema Mwamba wa Roho uliokuwa umewafuata akina Musa ni Kristo! (Yesu),
Kinacho kuchanganya ni huyu Yesu aliyekuwapo kabla na yupo sasahv na yule Yesu aliyezaliwa na bikira mariam wewe unawaona ka Yesu wawili tofauti wakati ni mmoja isipokuwa alipokuja duniani alitengeneza mwili akakaa ndani ya huo mwili ambao ulipewa jina lake YESU,Hujawahi kujiuliza kwanini hakuitwa Emmanuel kama Isaya alivyosema?
>Isaya alisema ataitwa Emmanuel (lakini akaitwa Yesu) isaya 7:14 kwanini?
>isaya huyo huyo alisema Ataitwa "Mshauri wa ajabu" "Mungu mwenye nguvu" "Baba wa milele" "Mfalme wa amani" (lakini akaitwa Yesu) kwanini hakuitwa hata moja kati ya hayo majina yoote aliyoyasema isaya?(isaya 9:6)
Jibu nikwamba Yesu hakuitwa hayo majina yoote sabau hayo sio majina bali ni Title (vyeo) au kazi za Mungu ambazo angezitenda kupitia huyo mtoto wa Kiume,badala yake Malaika alivyomtokea mariam alimwagiza mtoto aitwe YESU,kwanini Yesu kwasababu Yesu ndilo Jina la Mungu,kwahivyo kwakuwa yeye alikuwa ni mwana wa Mungu alirithi Jina la Baba yake,Kwa hivyo Jina Yesu ni jina la urithi alilopewa mwana wa Adamu "Waebrania 1:4",wafilipi 2:9-11,sasa kazi ya Yesu Kristo duniani ilikuwa ni nini? kuzaliwa,kutuonyesha binadamu kuishi maisha ya kitakatifu bila ya kutenda dhambi mpaka kufa,then pale msalabani kutolewa kafara ili kuukomboa ulimwengu kupitia ile damu na maji vilivyo mwagika pale! Biashara ikaishia hapo aliyefufuka hapo ule mwili alikuwa ni Mungu(Yesu) sasa Yule aliyekuwa ndani ya yule mtu kabla hajafa akiwa na mwili wa utukufu wake,ndio huyo atakuja tena kulichukua kanisa lake na kuhukumu Ulimwengu na ndio huyo huyo MUNGU!!

complicated eeh? Jawa na roho mtakatifu utanielewa
 
Mwanadamu alipowekwa pale bustani ya Eden (Adam na Hawa) walizuiliwa wasile mti wa ujuzi wa mema na mabaya,Adam kupitia mkewe wakala kwahiyo wakapata ujuzi wa kutambua jema na Baya lakini madhara yake nikwamba kifo kikaingia ( (Mwanzo 2:17, 3:22),huoni baada ya kula lile tunda Biblia inasema macho yao yakafunguka wakajiona wapo uchi!
(Mwanzo 3:7-19)
Kwahiyo kila binadamu anajua analolifanya kama ni jema au ni baya,kama ni jema Nafsi yake itamshuhudia kuwa ni jema na kama ni baya pia nafsi yake itamshuhudia kuwa ni baya,Yohana anasema kila anayefanya baya anachukia mwanga ndiomaana anafanyia mafichoni (Yohana 3:20)
Huu utashi wa kutambua jema na baya ndio unatutofautisha binadamu na Viumbe wengine
Senkiyuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Neno "Mungu Baba" ni cheo (TITLE)" kinachotumika kuelezea shughuli za Mungu,kwanini aitwe Baba na sio Mama,Anaitwa Baba kwanza kwasababu Yeye ndio muumba wa vitu vyoote vinavyoonekana na visivyoonekana (1 wakolinto 8:6),Pili anaitwa Baba kwasababu hapo mwanzo aliumba mtu kwa mfano wake na aliumba Mwanaume kwanza na sio mwanamke,sasa kama aliumba mwanaume kwa mfano wake hawezi kuitwa Mama inamaana yeye ni Baba.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
maada nzuri na mimi kukikazia kazia kidogo ni hivi
1.Asili ya Mungu ni nini? Asili (Nature) ya Mungu ni Roho (YOHANA 4:24).Sasa kama Mungu asili yake ni Roho na kuna roho aina mbali mbali Roho ya mungu ni ya aina gani??,Roho ya Mungu ni TAKATIFU (HOLY).sasa kwa asili ya Mungu kuwa Roho inamaana anapatikana kila mahali,Duniani,chini ya dunia,angani,mbinguni na ulimwenguni koote kwa wakati mmoja!

2.Mungu Hakumtuma Yesu aje na mwili wa Binadamu,kilichofanyika nikwamba Mungu mwenyewe aliumba mwili then akaingia ndani yake,yaani Mungu alijificha kwenye ule mwili ambao ulizaliwa na Mariam,Mungu Mwenyewe alikuwa ndani ya YESU Kristo! angalia maajabu ya Mungu,Muda huo huo alikuwa ndani ya Yesu,Muda huo huo alikuwa Mbinguni kwenye kiti cha enzi,Muda huo huo alikuwa ndani ya Yohana mbatizaji kwakuwa yohana mbatizaji alizaliwa tayari amejaa roho mtakatifu(roho wa Mungu)!,hukusoma andiko lilikuwa linatabiri kuja kwa Yesu na likasema ataitwa Emmanuel maana yake MUNGU PAMOJA NASI?,(ISAYA 7:14),Na pia kuna andiko linasema Mungu alijidhihirisha katika mwili akakaa kwetu? (1Timotheo 3:16) maana yake Mungu alitengeneza mwili then akaingia ndani yake then akaja kwa binadamu,alijidhihirisha katika mwili,kama vile wewe unavyoweza kujidhihirisha kwenye mavazi mbalimbali,ukavaa suti,au jens,au ukajidhihirisha na nguo za cadet nk..zile ni nguo tu ila wewe uko ndani ya zile nguo,na kwakuwa Mungu alikuwa anakuja kukomboa wanadamu ilimbidi aje kwa sura ya kibinadamu aishi na binadamu,awaonyeshe binadamu namna ya kuishi bila kutenda dhambi sasa Mungu ni roho ilimpasa aende kwenye nyumba ya daudi atengeneze MWILI halafu auvae huo mwili azaliwe kwa njia ya mwanamke kama binadamu wengine then atufundishe namna ya kuishi maisha matakatifu na hatimaye kafara ifanyike msalabani kuukomboa ulimwengu woote
Astaghafulahi...hizi kufuru ebu zitubie kiongozi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aliekosea ni adamu Kwa sababu Mungu alikua ameumba mti wa uzima na ubaya, maanaa yake mti wa uzima na ubaya in mfumo wa shetan, Na mti wa uzima in mfumo wa mungu lakin Adam akachagua mfumo wa shetani, ndo kosa alilolifanya adamu

Na pia kumbuka shetan Tayar alikuwa ameshahukumiwa baada ya jaribio lake LA mapinduz kufeli
Unaweza kunipata tarehe na mwaka wa hayo matukio
 
.............His spiritual qualities kept pace with his personal charm, for God had fashioned his soul with particular care. She is the image of God, and as God fills the world, so the soul fills the human body; as God sees all things, and is seen by none, so the soul sees, but cannot be seen; as God guides the world, so the soul guides the body; as God in His holiness is pure, so is the soul; and as God dwells in secret, so doth the soul.(COPIED FROM THE LEGEND OF THE JEWS).

Kwa maelezo hayo MUNGU YUPO SIRINI KAMA VILE ROHO YAKO ILIVYO SIRINI NA IMEJAZA MWILI WAKO.

Ni kuulize swali mkuu,je unaweza kumwonyesha MTU software ya Simu,computer au calculator?
Je hizo software zipo au ni hadithi tu za kutunga kama ambavyo unaita habari za MUNGU MWENYEZI kuwa ni za kutunga?

Sent using Jamii Forums mobile app
Umesema kweli lkn hayo matukio Mungu aliyafanya wakat gani unaweza kunitajia mwaka ? na kwann vitabu vitakatifu havitaji miaka ya matukio mbalimbali yaliyotokea wakati huo?
 
Umesema kweli lkn hayo matukio Mungu aliyafanya wakat gani unaweza kunitajia mwaka ? na kwann vitabu vitakatifu havitaji miaka ya matukio mbalimbali yaliyotokea wakati huo?
Sijui Ni kwa sababu gani miaka haijaandikwa Wala Sijui Ni mwaka gani MUNGU MWENYEZI aliyafanya haya.Wanaojua watasema.
Ninachoweza kusema Ni kuwa hayo matukio yalitokea kipindi ambacho Adam anaumbwa.
Nimetumia source niliyonayo kufafanua kwa nini hatuwezi kumwona MUNGU MWENYEZI kwa macho yetu(Kumwona live).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini uliandika kwa lugha usiyoielewa?

Ulimaanisha nini kwa Kiswahili Hilo bichwa lako la habari?
Na we sasa unakuwa mtoto wakati ni bibi, soma maelezo yake inatosha, Kwan mtu akisema Arusa badala ya Arusha unashindwaje kuelewa kuwa alikusudia Arusha!!?
 
Shida unachukulia concept ya Mungu ki-binadamu
1.Yesu alikuwa Mungu na ni Mungu sasa lakini mwana wa Adam hakuwa Mungu ila Mungu alikaa ndani yake,Yule mwana wa adamu aliyeitwa Yesu Kristo alirithi Jina,nguvu,uweza,mamlaka,nk kutoka kwa baba yake ambaye ni Mungu,ndiomaana hata sisi tukifanyika kuwa wana wa Mungu basi tunarithi hivyo vyoote

2.Hapa ndio unachukulia Concept ya Mungu kibinadamu,Mungu mwenyewe kasema yeye sio mwanadamu!,Yohana anasema Mungu ni Roho (Yohana 4:24),kama ni Roho inamaana Yuko kila mahali kwa wakati mmoja,(Yeremia 23:23-33,mithali 15:3,zaburi 139:7-10).Angalia maajabu mengine ya Mungu kipindi Yesu kristo kaenda kubatizwa na Yohana mbatizaji ,
>Mungu huyo huyo alikuwa ndani ya Yohana Mbatizaji (Sababu yohana mbatizaji alizaliwa tayari kajaa roho mtakatifu Mungu alikuwa ndani yake),
>Mungu huyo huyo alikuwa ndani ya Yesu kristo (sababu imeandikwa Mungu alikuwa ndani ya kristo kuupatanisha ulimwengu na yeye)
>Mungu huyo huyo alisikika mbinguni akisema "Huyu ni mwanangu mpendwa nimependezwa naye"
Shughuli zoote hizi alikuwa anazifanya mwenyewe kwa njia mbalimbali,umeniuliza kama Yesu alikuwa anajiomba mwenyewe
inamaana hujui Yesu alikuja dunian kufanya nini!,biblia inasema hivi Yesu alikuja duniani kuacha mfano wa sisi wanadamu kuufuata (Yohana 13:13-16,1wakolinto 11:1).Alibatizwa na sisi tunabatizwa,alimuomba Mungu na sisi tunamuomba Mungu,hakutenda dhambi na sisi tunatakiwa tusitende dhambi,alifunga na sisi tunafunga,alishiriki meza ya bwana na sisi pia tunashiriki,alijawa na roho mtakatifu na sisi pia tunatakiwa kujawa na roho mtakatifu,nk ,kwahiyo alikuwa anamuomba Mungu ambaye alikuwa ndani yake,na Muda huo alikuwa mbinguni!

3.Hilo andiko nimekupa umeliandika na huo mstari wa 4 inamaana haujauelewa au ulitaka waseme Yesu kabisa na sio kristo??,ngoja nikupe na hili,umesahau Yesu mwenyewe aliulizwa yeye ni nani na akajibu Kabla ya Abraham kuwako alikuwako (Yohana 8:58) na hii (1 Wakorintho 10:1-4) huo mstari wa 4 unasema Mwamba wa Roho uliokuwa umewafuata akina Musa ni Kristo! (Yesu),
Kinacho kuchanganya ni huyu Yesu aliyekuwapo kabla na yupo sasahv na yule Yesu aliyezaliwa na bikira mariam wewe unawaona ka Yesu wawili tofauti wakati ni mmoja isipokuwa alipokuja duniani alitengeneza mwili akakaa ndani ya huo mwili ambao ulipewa jina lake YESU,Hujawahi kujiuliza kwanini hakuitwa Emmanuel kama Isaya alivyosema?
>Isaya alisema ataitwa Emmanuel (lakini akaitwa Yesu) isaya 7:14 kwanini?
>isaya huyo huyo alisema Ataitwa "Mshauri wa ajabu" "Mungu mwenye nguvu" "Baba wa milele" "Mfalme wa amani" (lakini akaitwa Yesu) kwanini hakuitwa hata moja kati ya hayo majina yoote aliyoyasema isaya?(isaya 9:6)
Jibu nikwamba Yesu hakuitwa hayo majina yoote sabau hayo sio majina bali ni Title (vyeo) au kazi za Mungu ambazo angezitenda kupitia huyo mtoto wa Kiume,badala yake Malaika alivyomtokea mariam alimwagiza mtoto aitwe YESU,kwanini Yesu kwasababu Yesu ndilo Jina la Mungu,kwahivyo kwakuwa yeye alikuwa ni mwana wa Mungu alirithi Jina la Baba yake,Kwa hivyo Jina Yesu ni jina la urithi alilopewa mwana wa Adamu "Waebrania 1:4",wafilipi 2:9-11,sasa kazi ya Yesu Kristo duniani ilikuwa ni nini? kuzaliwa,kutuonyesha binadamu kuishi maisha ya kitakatifu bila ya kutenda dhambi mpaka kufa,then pale msalabani kutolewa kafara ili kuukomboa ulimwengu kupitia ile damu na maji vilivyo mwagika pale! Biashara ikaishia hapo aliyefufuka hapo ule mwili alikuwa ni Mungu(Yesu) sasa Yule aliyekuwa ndani ya yule mtu kabla hajafa akiwa na mwili wa utukufu wake,ndio huyo atakuja tena kulichukua kanisa lake na kuhukumu Ulimwengu na ndio huyo huyo MUNGU!!

complicated eeh? Jawa na roho mtakatifu utanielewa

Hakuna ulipojibu maswali yangu zaidi ya kuleta mahubiri tu tena yote pumba tupu eti nijawe na roho mtakatifu nitakuelewa, hakuna swala la kujawa roho mtakatifu bali ni huko ni kujilazimisha kuamini bila kuhoji.

Hapa tunazungumzia uungu wa Yesu wewe umesema "
"Yesu alikuwa Mungu na ni Mungu sasa lakini mwana wa Adam hakuwa Mungu ila Mungu alikaa ndani yake,Yule mwana wa adamu aliyeitwa Yesu Kristo alirithi Jina,nguvu,uweza,mamlaka,nk kutoka kwa baba yake ambaye ni Mungu,ndiomaana hata sisi tukifanyika kuwa wana wa Mungu basi tunarithi hivyo vyoote"

Ndio maana nakwambia huelewi unachokiamini bali umekariri juu ya uungu wa yesu bila kufanya reasoning eti kisa tu eti unajawa roho na mtakatifu.

Mpaka hapo kwenye bold umeshaonesha kuna wawili tofauti (kuna Yesu na pia kuna baba yake Yesu ambaye ni Mungu)



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaweza kunipata tarehe na mwaka wa hayo matukio
Kama kalenda tunaotumia ni ya warumi, fahamu kwamba kila jamii ilikua na kalenda yake mfano waislamu wana kalenda yao, sawa Kwa wachina, waethiopia, na jews na hata wanascience na jinsi yao ya kuhesabu siku. Kwa hy kukutajia mda exactly ni ngumu sababu hata Mungu ana kalenda yake tofauti na sis
 
Sijui Ni kwa sababu gani miaka haijaandikwa Wala Sijui Ni mwaka gani MUNGU MWENYEZI aliyafanya haya.Wanaojua watasema.
Ninachoweza kusema Ni kuwa hayo matukio yalitokea kipindi ambacho Adam anaumbwa.
Nimetumia source niliyonayo kufafanua kwa nini hatuwezi kumwona MUNGU MWENYEZI kwa macho yetu(Kumwona live).

Sent using Jamii Forums mobile app
Aliyeleta hizi habari za Adam kuumbwa ni nani ?
 
Kama kalenda tunaotumia ni ya warumi, fahamu kwamba kila jamii ilikua na kalenda yake mfano waislamu wana kalenda yao, sawa Kwa wachina, waethiopia, na jews na hata wanascience na jinsi yao ya kuhesabu siku. Kwa hy kukutajia mda exactly ni ngumu sababu hata Mungu ana kalenda yake tofauti na sis
Sawa tutumie basi hiyo ya Mungu
 
Aliekosea ni adamu Kwa sababu Mungu alikua ameumba mti wa uzima na ubaya, maanaa yake mti wa uzima na ubaya in mfumo wa shetan, Na mti wa uzima in mfumo wa mungu lakin Adam akachagua mfumo wa shetani, ndo kosa alilolifanya adamu

Na pia kumbuka shetan Tayar alikuwa ameshahukumiwa baada ya jaribio lake LA mapinduz kufeli
Mbona haujamjibu? Why aumbe huo mti wa ubaya ilihali anajua fika kuwa Adamu atauchagua huo wa ubaya? Na kabla ya hapo why amuumbe shetani aliejua kabisa atamsaliti one day?
 
Mfumo aliochagua Adam ndo umeleta vurugu zote hizi tunazoziona
Why alaumiwe Adamu wakati alieumba vitu hivyo ni Mungu mwenyewe? Na hata kabla ya kuviumba alijua fika mwisho vitaleta shida na akaandaa na Jehanam kabisa.

Yaani hii ni sawa na unampa mtoto mtihani unaojua fika ataushindwa ili mwisho wa siku umuadhibu.
 
2.Hapa ndio unachukulia Concept ya Mungu kibinadamu,Mungu mwenyewe kasema yeye sio mwanadamu!,Yohana anasema Mungu ni Roho (Yohana 4:24),kama ni Roho inamaana Yuko kila mahali kwa wakati mmoja,(Yeremia 23:23-33,mithali 15:3,zaburi 139:7-10).Angalia maajabu mengine ya Mungu kipindi Yesu kristo kaenda kubatizwa na Yohana mbatizaji ,
>Mungu huyo huyo alikuwa ndani ya Yohana Mbatizaji (Sababu yohana mbatizaji alizaliwa tayari kajaa roho mtakatifu Mungu alikuwa ndani yake),
>Mungu huyo huyo alikuwa ndani ya Yesu kristo (sababu imeandikwa Mungu alikuwa ndani ya kristo kuupatanisha ulimwengu na yeye)
>Mungu huyo huyo alisikika mbinguni akisema "Huyu ni mwanangu mpendwa nimependezwa naye"
Shughuli zoote hizi alikuwa anazifanya mwenyewe kwa njia mbalimbali,umeniuliza kama Yesu alikuwa anajiomba mwenyewe
inamaana hujui Yesu alikuja dunian kufanya nini!,biblia inasema hivi Yesu alikuja duniani kuacha mfano wa sisi wanadamu kuufuata (Yohana 13:13-16,1wakolinto 11:1).Alibatizwa na sisi tunabatizwa,alimuomba Mungu na sisi tunamuomba Mungu,hakutenda dhambi na sisi tunatakiwa tusitende dhambi,alifunga na sisi tunafunga,alishiriki meza ya bwana na sisi pia tunashiriki,alijawa na roho mtakatifu na sisi pia tunatakiwa kujawa na roho mtakatifu,nk ,kwahiyo alikuwa anamuomba Mungu ambaye alikuwa ndani yake,na Muda huo alikuwa mbinguni!

hapa umejibu tofauti na ulichoulizwa, acha mahubiri jenga tabia ya kujibu maswali kulingana na ulichoulizwa, unaulizwa yesu alikuwa anajiomba mwenyewe wewe unazunguka zunguka kwa mahubiri. ili mimi niweze kukubaliana na wewe ya kwamba Yesu ni Mungu, naomba ukiri ya kwamba aliyekuwa duniani kuokoa wana wa Israel alikuwa ni Yesu, na pia aliyekuwa mbinguni, kipindi hiko hiko Yesu akiwa duniani alikuwa ni Yesu huyo huyo. Na aliyeingia ndani wa mwili wa Yesu na Yohana alikuwa ni ni huyo huyo Yesu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom