Mwl Mwakujonga
JF-Expert Member
- Jun 29, 2023
- 368
- 735
Maana ya Neno Uzinifu
Mtu ambaye hana ndoa lakini anafanya tendo la ndoa huyo anaitwa mzinifu.
Maana ya Pili
Mtu ambaye ameoa au kuolewa anapofanya uzinifu anaitwa mwasherati
Inawezekana watu wengi tuna amini kwamba ndoto zenye kuambatana na vitendo vya uzinzi ni kitu cha kawaida tu , na mara nyingi hatutilii maananu juu ya ndoto hizi
Wakati mwingine tunaona ni sawa tu, kuota unazini na wako wengine wamekwenda mbali zaidi na kuwa wanaona ni furaha kuota ndoto unazini ?
Ndoto ni nini
Kitabu cha Ayu. 33: 13-14, kinatwambia ndoto ni njia ambayo Mungu anatumia kuongea na mtu akiwa usingizini
Kama Mungu anaongea na Mtu kwa njia ya Ndoto, na kwa mujibu wa maandiko Mungu ni Roho maana yake Mungu kama ni Roho anapozungumza nasi kwa njia ya ndoto anasema nasi kwa njia ya kiroho hivyo ni sawa na kusema ndoto ni mlango wa Mungu kusema na roho yangu /nafsi yangu
Ndoto ni mlango ambao Mungu anautumia kwa lengo la kumsaidia mwanadamu kumwondoa katika makusudi yake Ayu 33:17
Kama tulipojifunza hapo juu ndoto ni mlango na mlango hauchagui nani aingie nani asingie , mlango unaweza kutumiwa na mwizi au mchungaji , kadhalika ndoto inaweza kutumiwa na Mungu au shetani
Kuna madhara gani ya kuota ndoto ya uzinifu
Biblia inasema adamu na mkewe walikuwa mtu mmoja kupitia ndoa , kwa hiyo ndoa ni muunganiko wa kimwili na sio wa kiroho
Rom 7:2 Kifungo cha ndoa kati ya Mwanamke na Mwanaume ni pale tu wakiwa katika Mwili ndio maana maandiko yanasema mwanamke amefungwa na sheria ya mume akiwa hai kwa hiyo ndoa ni ya mwili na sio ya rohoni
Kwa hiyo mtu anapoota anafanya uzinzi katika ndoto maana yake anashiriki tendo la ndoa katika ulimwengu wa roho kwa sababu ndoto ni mlango wa kupitisha mambo ya rohoni kwa mwanadamu
Maana ya kuota ndoto za uzinifu / uasherati
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalo mwanga miza nafsi yake. Mit 6:32
Kwa hiyo mtu anapoota ndoto anafanya uzinzi maana yake , shetani amekusudia kuangamiza nafsi yake
Nini maana ya nafsi kuangamizwa
Kuangamizwa maana yake ni kuhua.
Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga.Kut 17:13
Kwa hiyo kupitia ndoto ya uzinzi shetani amekusudia kuua nafsi yako
Madhara ya nafsi iliyokufa
Mtu ambaye nafsi yake imekufa ni mtu ambaye matendo yake yanafananishwa na mtu ambaye hana akili
Madhara mengine ya nafsi yanakwenda kwa kiini cha nafsi ambayo ni kufa kwa fikra, akili na hekima pia
Ndo maana mtu ambaye nafsi yake imekufa ni kawaida kutenda mambo yafuatayo.
ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu. 2 Kor 4:4
Mtu ambaye nafsi imekufa ni mbishi sana kwa mambo ya Mungu ni mpinga Kristo
ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao; EFe 4:18
Madhara mengine ya nafsi iliyokufa ni pamoja na kukosa akili , unatenda mambo ya aibu
Ushuhuda
Kijana mmoja ambaye alikuwa anasumburiwa na ndoto za uzinifu akaniambia Mwl natamani sana kuacha zinaa lakini nashindwa kuna wakati nakuwa kama nachanganyikiwa nikimwona mwanamke natamani kulala naye , nimelala ma wanawake wengi na wakati napo jaribu kufunga ili nivuke nashindwa
Madhara makubwa ambayo mtu atapata kwa kuota ndoto za uzinifu ni pamoja na kushindwa kujizuia juu ya dhambi ya uzinzi kwanini?
Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
Mathayo 19:6
Kwa hiyo ndoa ni Muunganiko wa kiroho na uzinzi ni hivyo hivyo, unapofanya uzinzi kwenye ndoto maana yake nafsi yako inaungana na roho ya uzinifu ndio maana watu wengi ambao wamekuwa na tabia za kuota ndoto za uzinzi sio rahisi kuhepuka uzinzi kwa sababu nafsi yao inakuwa imefungwa na roho ya uzinzi
Roho ya uzinzi ina ambatana na pepo la uzinzi ndio maana mara zote wale ambao wamekuwa wakufanya uzinzi kwa njia ya ndoto hata maisha yao ya mwili ni hivyo hivyo wamekuwa wakifanya na watu hata ambao uwezi kuzania
Mtu ambaye hana ndoa lakini anafanya tendo la ndoa huyo anaitwa mzinifu.
Maana ya Pili
Mtu ambaye ameoa au kuolewa anapofanya uzinifu anaitwa mwasherati
Inawezekana watu wengi tuna amini kwamba ndoto zenye kuambatana na vitendo vya uzinzi ni kitu cha kawaida tu , na mara nyingi hatutilii maananu juu ya ndoto hizi
Wakati mwingine tunaona ni sawa tu, kuota unazini na wako wengine wamekwenda mbali zaidi na kuwa wanaona ni furaha kuota ndoto unazini ?
Ndoto ni nini
Kitabu cha Ayu. 33: 13-14, kinatwambia ndoto ni njia ambayo Mungu anatumia kuongea na mtu akiwa usingizini
Kama Mungu anaongea na Mtu kwa njia ya Ndoto, na kwa mujibu wa maandiko Mungu ni Roho maana yake Mungu kama ni Roho anapozungumza nasi kwa njia ya ndoto anasema nasi kwa njia ya kiroho hivyo ni sawa na kusema ndoto ni mlango wa Mungu kusema na roho yangu /nafsi yangu
Ndoto ni mlango ambao Mungu anautumia kwa lengo la kumsaidia mwanadamu kumwondoa katika makusudi yake Ayu 33:17
Kama tulipojifunza hapo juu ndoto ni mlango na mlango hauchagui nani aingie nani asingie , mlango unaweza kutumiwa na mwizi au mchungaji , kadhalika ndoto inaweza kutumiwa na Mungu au shetani
Kuna madhara gani ya kuota ndoto ya uzinifu
Biblia inasema adamu na mkewe walikuwa mtu mmoja kupitia ndoa , kwa hiyo ndoa ni muunganiko wa kimwili na sio wa kiroho
Rom 7:2 Kifungo cha ndoa kati ya Mwanamke na Mwanaume ni pale tu wakiwa katika Mwili ndio maana maandiko yanasema mwanamke amefungwa na sheria ya mume akiwa hai kwa hiyo ndoa ni ya mwili na sio ya rohoni
Kwa hiyo mtu anapoota anafanya uzinzi katika ndoto maana yake anashiriki tendo la ndoa katika ulimwengu wa roho kwa sababu ndoto ni mlango wa kupitisha mambo ya rohoni kwa mwanadamu
Maana ya kuota ndoto za uzinifu / uasherati
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalo mwanga miza nafsi yake. Mit 6:32
Kwa hiyo mtu anapoota ndoto anafanya uzinzi maana yake , shetani amekusudia kuangamiza nafsi yake
Nini maana ya nafsi kuangamizwa
Kuangamizwa maana yake ni kuhua.
Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga.Kut 17:13
Kwa hiyo kupitia ndoto ya uzinzi shetani amekusudia kuua nafsi yako
Madhara ya nafsi iliyokufa
Mtu ambaye nafsi yake imekufa ni mtu ambaye matendo yake yanafananishwa na mtu ambaye hana akili
Madhara mengine ya nafsi yanakwenda kwa kiini cha nafsi ambayo ni kufa kwa fikra, akili na hekima pia
Ndo maana mtu ambaye nafsi yake imekufa ni kawaida kutenda mambo yafuatayo.
ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu. 2 Kor 4:4
Mtu ambaye nafsi imekufa ni mbishi sana kwa mambo ya Mungu ni mpinga Kristo
ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao; EFe 4:18
Madhara mengine ya nafsi iliyokufa ni pamoja na kukosa akili , unatenda mambo ya aibu
Ushuhuda
Kijana mmoja ambaye alikuwa anasumburiwa na ndoto za uzinifu akaniambia Mwl natamani sana kuacha zinaa lakini nashindwa kuna wakati nakuwa kama nachanganyikiwa nikimwona mwanamke natamani kulala naye , nimelala ma wanawake wengi na wakati napo jaribu kufunga ili nivuke nashindwa
Madhara makubwa ambayo mtu atapata kwa kuota ndoto za uzinifu ni pamoja na kushindwa kujizuia juu ya dhambi ya uzinzi kwanini?
Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
Mathayo 19:6
Kwa hiyo ndoa ni Muunganiko wa kiroho na uzinzi ni hivyo hivyo, unapofanya uzinzi kwenye ndoto maana yake nafsi yako inaungana na roho ya uzinifu ndio maana watu wengi ambao wamekuwa na tabia za kuota ndoto za uzinzi sio rahisi kuhepuka uzinzi kwa sababu nafsi yao inakuwa imefungwa na roho ya uzinzi
Roho ya uzinzi ina ambatana na pepo la uzinzi ndio maana mara zote wale ambao wamekuwa wakufanya uzinzi kwa njia ya ndoto hata maisha yao ya mwili ni hivyo hivyo wamekuwa wakifanya na watu hata ambao uwezi kuzania