maada nzuri na mimi kukikazia kazia kidogo ni hivi
1.Asili ya Mungu ni nini? Asili (Nature) ya Mungu ni Roho (YOHANA 4:24).Sasa kama Mungu asili yake ni Roho na kuna roho aina mbali mbali Roho ya mungu ni ya aina gani??,Roho ya Mungu ni TAKATIFU (HOLY).sasa kwa asili ya Mungu kuwa Roho inamaana anapatikana kila mahali,Duniani,chini ya dunia,angani,mbinguni na ulimwenguni koote kwa wakati mmoja!
2.Mungu Hakumtuma Yesu aje na mwili wa Binadamu,kilichofanyika nikwamba Mungu mwenyewe aliumba mwili then akaingia ndani yake,yaani Mungu alijificha kwenye ule mwili ambao ulizaliwa na Mariam,Mungu Mwenyewe alikuwa ndani ya YESU Kristo! angalia maajabu ya Mungu,Muda huo huo alikuwa ndani ya Yesu,Muda huo huo alikuwa Mbinguni kwenye kiti cha enzi,Muda huo huo alikuwa ndani ya Yohana mbatizaji kwakuwa yohana mbatizaji alizaliwa tayari amejaa roho mtakatifu(roho wa Mungu)!,hukusoma andiko lilikuwa linatabiri kuja kwa Yesu na likasema ataitwa Emmanuel maana yake MUNGU PAMOJA NASI?,(ISAYA 7:14),Na pia kuna andiko linasema Mungu alijidhihirisha katika mwili akakaa kwetu? (1Timotheo 3:16) maana yake Mungu alitengeneza mwili then akaingia ndani yake then akaja kwa binadamu,alijidhihirisha katika mwili,kama vile wewe unavyoweza kujidhihirisha kwenye mavazi mbalimbali,ukavaa suti,au jens,au ukajidhihirisha na nguo za cadet nk..zile ni nguo tu ila wewe uko ndani ya zile nguo,na kwakuwa Mungu alikuwa anakuja kukomboa wanadamu ilimbidi aje kwa sura ya kibinadamu aishi na binadamu,awaonyeshe binadamu namna ya kuishi bila kutenda dhambi sasa Mungu ni roho ilimpasa aende kwenye nyumba ya daudi atengeneze MWILI halafu auvae huo mwili azaliwe kwa njia ya mwanamke kama binadamu wengine then atufundishe namna ya kuishi maisha matakatifu na hatimaye kafara ifanyike msalabani kuukomboa ulimwengu woote