Mtanzania,
Hapana mkubwa wangu hujanipata kabisa kwani umeshindwa kutofautisha kati ya dira ya kitaifa, mrengo wangu, mawazo ya Mwalimu na reality.
Mkubwa umetoa mifano ya nchi kama Marekani, Uingereza jinsi zinavyoendesha Biashara zake na nchi kama Saudia na China. bahati mbaya ni kwamba Tanzania hatuendeshi biashara ila tunaomba msaada..
Tofautisha kati ya yule maskini anayekaa mlangoni msikitini akisubiri kuomba na mbangaizaji (mlalahoi) anayechapuka kila asubuhi kuingia mitaani ktafuta deal iwe ktk maofisi ama hata Machinga.
Tanzania kwa kukosa mrengo tumekuwa kama masikini anayesubiri mitaani akipiga gita na kucheza sana mnenguo akisubiri kusikia sauti za sarafu zaikimwagika ktk kopo lake. Yaani kifupi ni kwamba aidha milango ya uchumi wa nchi yetu ni ile ya Kitalii na kufanywa ma Charle Chaplin, nchi nzima tunacheza ngwasuma na kutegemea kuwa kivutio kwa nchi za Ulaya. Ama sisi ni sawa na jamaa zetu nyumbani ambao kila siku hutegemea sisi tulioko Ulaya tutawatumia mallioni ya fedha wapate kuendesha maisha yao ya kila siku.
Na kwa bahati mbaya mfano yetu wenyewe tumeiona sana kuwa hata siku moja huwezi kumkomboa ndugu ama jamaa yako kwa kumtumia dollar, atakufilisi wewe na yeye bado ataendelea kuwa maskini...
Haya ndio maisha tunayoishi na kweli nakubaliana nawe kuwa ndio reality ya Tanzania. Ni reality inayoppatikana Tanzania tu wala sio nje ya mipaka yake. Tanzania hata ukimkopa mtu kurudisha hizo fedha ni ngoma, yaani wengi hutegemea kupewa msaada zaidi ya kukopeshwa. Na reality ni kwamba unapoombwa fedha basi ni vizuri kufikiria kumpa bure usitegemee malipo kuliko kumkopa mdanganyika... utakesha!..
Hii ndiyo reality ya Tanzania (only in Tanzania) reality ambayo haiwezi kutuvuta hata hatua moja isipokuwa kutuweka ktk utumwa na kutudidimiza zaidi ktk dimbwi la Umaskini.
Nasema hivi kwani hata Kitaifa, viongozi wetu na wananchi kwa ujumla hutegemea kuona hiyo mikopo yetu tumesamehewa kiasi gani!.. na tunaposiukia tumesamehewa hupiga makofi na kumpa hongera kiongozi wakati tunashindwa kujiuliza hizo fedha zilijenga kitu gani?...
Hivyo basi mkuu wangu kwa mzee Bush nasema hivi,
Ni ujinga mkubwa kuendelea kumpa fedha mvuta unga ukitegemea utaweza badilisha maisha yake, hizo fedha zitaenda nunua unga zaidi na kumfanya awe teja la kutupwa...Misaada ya Bush ya vyandarua utakuja sikia vimeuzwa kwa wananchi. Na huwezi kuondoa maleria kwa viandarua mkuu wangu hilo halina reality!... ni ujuha wetu kujisifia kupata viandarua tunashindwa kufukia madimbwi ambayo hayana cost kubwa kama huduma na jitihada zote zinazofanywa kuzuia Maleria...