Hotuba za Rais kila mwezi

Hotuba za Rais kila mwezi

Je unaridhika na hotuba za Rais Kikwete?

  • Ndio

    Votes: 13 15.5%
  • Hapana

    Votes: 71 84.5%
  • SIJUI

    Votes: 0 0.0%
  • Sina jinsi

    Votes: 1 1.2%

  • Total voters
    84
  • Poll closed .
Katika uchambuzi wangu wa hotuba ya JK, nimekiona kipengele hiki ambacho kidogo kimenipa taabu sana kukielewa.

Mheshimiwa Jk Alisema:- Rais Bush alikuja kuwathibitishia wananchi wa Marekani kuwa sera yao ya misaada Afrika ni sahihi na kwamba mafanikio yaliyotarajiwa yanapatikana. Kwa ajili hiyo, aliamua kukaa hapa kwetu kwa siku nyingi kwa sababu, katika misaada yao ya kupambana na malaria na UKIMWI barani Afrika, hapa Tanzania kumekuwepo na mafanikio ya kutolewa mfano.

Nachotaka kufahamu hiyo sera mwanzoni tulipewa kiasi gani kiasi kwamba aje kwa siku tatu kuonyesha mafanikio?
Je, ni mafanikio yapi yamepatikana ktk kuondoa maradhi haya HIV na hasa Maleria toka mradi huu umeanzishwa. Nilichokiona zaidi hapa ni rais wetu kuwashukuru baadhi ya watu kwa maandalizi mazuri ya kumpokea Bush... kazi ambayo nchi za Kiafrika ni mahodari sana ktk maandalizi ya kumfumba mtu ukweli na hali halisi. Ni katika mtililiko wa mazingaombwe haya Hospital kama Amana zilipigwa soap soap na huduma kuboreshwa ktk siku hizo tatu, hivyo hivyo sehemu zote walizotembelea kuna kila dalili kuwa watu waliandandaliwa kuonyesha mafanikio badala ya hali halisi.

Jambo jingine ningependa kuelewa nalo ni kwamba hivi kama sio ziara ya Bush na ahadi alizotoa ina maana sisi wenyewe hatukuwa na mpango wala hesabu za kutengeneza barabara, umeme wala viwanja vyetu isipokuwa kwa msaada wa Millenium?..

Nje ya misaada hii ya Millenium ni kiasi gani cha fedha za misaada toka nchi nyinginezo ambazo zimeweza jenga miundombinu yetu na kwa gharama inayokubalika kimahesabu. Kwa sababu tusiwe tunazungumzia figures yaani dollar millioni 700 macho yakatutoka kwa uroho, kumbe wazee wanavuta karibu nusu yake. Tukazungumzia matukio ya jirani zetu, Ujio wa Bush na maswala ya EPA hali kuna mambo mengine mazito zaidi yanazidisha chuki ya wananchi kwa serikali yao. Chanzo cha vurugu zozote zile ni ubadhilifu wa serikali iliyopo madarakani. Ubaguzi wa rangi ama kikabila hutokana na kutokuwepo kwa haki ama uongozi bora wa serikali inayo tawala laa sivyo viamsho hivi ubakia kama volcano iliyolala (dormant).
Ni rahisi sana kuwadanganya wageni kuhusu maendeleo yetu lakini sii rahisi kuwadanganya raia wenyewe ambao wanafahamu uchovu wa serikali ama viongozi wao. Tatizo la Kenya halikutokana na makabila, laa hasha limetokana na ushindi ama uongozi wa Mwai Kibaki. Nina hakika kabisa kuwa kama Mwai Kibaki angekubali kushindwa na kuachia ngazi haya matatizo ya Ukabila Kenya yasingetokea...
Hivyo basi ni muhimu kutazama chanzo cha kila tukio badala ya kutibu gonjwa, matatizo ya Kenya yataendelea ikiwa Mwai ataendelea kuwa rais wa nchi hiyo sawa na tatizo la aMaleria nchini haliwezi kwisha kwa viandarua millioni 5 ama 10 ila litakwisha ikiwa madimbwi ya maji machafu na yaliyosimama yatafukiwa kuhakikihsa MBU hawapati sehemu za kuzaliana.


Mwisho, nimeona ktk Youtube, kumbe Bush aliwahi kuja TZ kabla ya safari hii (sio kama mgeni rasmi).
Tazama Youtube:- President Bush remembers Tanzania

Komredi Mkandara:

Wewe sasa masikini jeuri. Maswali mengi kama vile tushawahi kujitegemea miaka iliyopita.
 
Tutakuwa tunatoka nje ya mada.

Mkuu Bin Maryam

Alichotaka kuonyesha ni kuwa kujulikana siyo tu kuja Bush Tanzania, kwa kipindi Bush amefika Bongo inawezekana kuna watu lukuki ambao hawakujua suala hilo, na baada ya miaka mitano ijayo linaweza lisiwe katika kumbukumbu za watu.

Hila huyu anatuonyesha ni jinsi gani mambo mbalimbali kama riadha, Kandanda, Mashirika ya ndege, na vitu vingine vidogo vidogo vinavyoweza kuchangia kusababisha nchi kujulikana.
 
NInajua hilo kuwa Tanzania katika ulimwengu haijulikani kabisa hata huna haja ya kwenda ulaya-Amerika-China- Japan nk. Tanazania hata haijulikani kwa baadhi ya nchi za Kiafrica.

Sijui sasa hivi umeisha faya analysis ukajua kuwa Baada ya Bush kututembelea tumeisha julikana kama unavyotaka tuamini?

Kakindomaster,

Hapo ndipo unapokosea, unapotaka kuniweka maneno yako mdomoni mwangu. hakuna hata sehemu moja nilipoandika sasa wanadunia wanaijua Tanzania na wala jambo hilo haliwezi kufanywa na ziara moja.

Kinachofanyika ni process nzima na kuja kwa Bush ni kitu kimoja tu kwenye hiyo process. Sasa ukiunganisha mambo yote kwa pamoja, mwisho wake ni kwa Tanzania kujulikana duniani.

Naona unafikisha conclusions zako kwa data kidogo sana, matokeo yake unapata garbage, si unajua garbage in garbager out? Sijaandika popote kwamba baada ya Bush kuja, basi sasa watu wakitaka kufungua ofisi, watafungua Dar. Mkuu, soma tena hoja na kama kuna kitu hujaelewa, basi uliza. Hii ya moja jumlisha moja ni tatu, yalimponza Jumbe. Nilichomaanisha ni kwamba hiyo image ya a democratic and stable Tanzania ambayo inakuja kwa kujumlisha mambo chungu nzima, kukiwemo kuja kwa Bush, mafanikio ya JK Kenya, ndio inaleta hiyo perception ya vyombo vya dunia ku prefer Dar kuliko Nairobi wakati huko nyuma ilikuwa ni kinyume chake.
 
Kakindomaster,

Hapo ndipo unapokosea, unapotaka kuniweka maneno yako mdomoni mwangu. hakuna hata sehemu moja nilipoandika sasa wanadunia wanaijua Tanzania na wala jambo hilo haliwezi kufanywa na ziara moja.

Kinachofanyika ni process nzima na kuja kwa Bush ni kitu kimoja tu kwenye hiyo process. Sasa ukiunganisha mambo yote kwa pamoja, mwisho wake ni kwa Tanzania kujulikana duniani.

Naona unafikisha conclusions zako kwa data kidogo sana, matokeo yake unapata garbage, si unajua garbage in garbager out? Sijaandika popote kwamba baada ya Bush kuja, basi sasa watu wakitaka kufungua ofisi, watafungua Dar. Mkuu, soma tena hoja na kama kuna kitu hujaelewa, basi uliza. Hii ya moja jumlisha moja ni tatu, yalimponza Jumbe. Nilichomaanisha ni kwamba hiyo image ya a democratic and stable Tanzania ambayo inakuja kwa kujumlisha mambo chungu nzima, kukiwemo kuja kwa Bush, mafanikio ya JK Kenya, ndio inaleta hiyo perception ya vyombo vya dunia ku prefer Dar kuliko Nairobi wakati huko nyuma ilikuwa ni kinyume chake.
Mkuu Mtanzania
Nafikiri kwa la kwanza sasa tunaelekea kuelewana mimi nilikuwa nakupinga baada ya kuona unashikilia suala la Bush kama ndo Basi tumeisha piga bao, ungeeleza vizuri mwanzoni tusingelitofautiana.

Lakini sasa tunaweza kuelewana baada ya kuonyesha kuwa hili suala la kujulikana linachangiwa na vitu vingi sana. Kwa Mfano wakati nasoma watu waliijua Kenya na Nigeria kwa sababu kulikuwa na Walimu kutoka Kenya na Nigeria basi. Hapa naona tunaelewana kuwa siyo Bush tu hila ni process kama nilivyoweka hata pale juu.

Suala la Dar umelitolea Mfano sina haja ya kuelezea hili Mkuu.

Ni vizuri sasa baada ya kukuulizia sana na kukupinga umeliweka vizuri. Nafikiri pia pale ambapo hujaelewa unaweza kupoint naweza kukutolea ufafanuzi Mkuu.

Hapa hatugombani Mkuu.
 
Bin Maryam,

Hapana mkuu wangu sio masikini jeuri ila kama umenielewa mimi nayaweka maslahi ya Taifa mbele...
Bush kesha kuja na ahadi zimetolewa sawa! tunazipokea lkwa mikono miwili akini humu ndani mwetu kweli hizo fedha zinapewa huduma na thamani inayotakiwa!... hatujawahi jitegemea lakini sii ndio malengo yenyewe mkuu?..
Inakuwaje vibaya kujiuliza kama huko nyuma tumeweza tambua matatizo yanayotukwamisha ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya fedha hizi za misaada. Vijimila vya kuwa wasafi anapokuja mgeni ama mtu kuvaa suti yake siku ya harusi, kula chakula kizuri siku za harusi na maulidi..is this healthy kweli ktk maendeleo ya nchi yetu?
Watatupa hadi lini ikiwa sisi wenyewe hatuna malengo zaidi ya kutegemea misaada ambayo haiwafikii wananchi. Trust me, Bin Maryam, fedha za mabarabara na Umeme ambazo tumewahi pewa.. ni billion of dollars lakini tazama tumefanya nini?...na imekuwaje tumekuwa wazuri sana ktk kupokea misaada ya kuponya magonjwa yaliyokwisha ingia badala ya kuzuia magonjwa hayo!

I mean vyandarua millioni 5 bure kwa watoto kweli vinaweza kusaidia ikiwa mbu watazidi kuzaliana?...hivi kweli Maleria hupatika tu pale watu wanapolala ama ni swala la mazingira mazima. Je ni kiasi gani kati ya fedha hizo zimetengwa ili kuboresha mazingira yanayohusiana na chanzo cha maradhi hayo?.. zero!
Hata hivyo sina maana Bush hakufanya la maana isipokuwa nionavyo mimi hii ni biashara zaidi ya kusaidia.
 
Mkuu Bin Maryam

Alichotaka kuonyesha ni kuwa kujulikana siyo tu kuja Bush Tanzania, kwa kipindi Bush amefika Bongo inawezekana kuna watu lukuki ambao hawakujua suala hilo, na baada ya miaka mitano ijayo linaweza lisiwe katika kumbukumbu za watu.

Hila huyu anatuonyesha ni jinsi gani mambo mbalimbali kama riadha, Kandanda, Mashirika ya ndege, na vitu vingine vidogo vidogo vinavyoweza kuchangia kusababisha nchi kujulikana.

Nadhani kabla ya posti hiyo nilitoa mfano jinsi vitu vidogo kama riadha vinavyoweza kutangaza nchi. Na jamaa akata nieleze tena ujio wa Bush na Serikali yetu inavyoweza kuwasaidia wanariadha.

British system of Education kwa kiwango fulani inalazimisha watu kufahamu mambo ya kidunia. Lakini nchi nyingi dunia hazifuati mfumo huo.

Ujio wa Bush umetangaza nchi kwa namna fulani lakini momentum ya kutangaza nchi iendelee. Na kesho mtanzania akishinda marathon Boston au New York ni lazima kutakuwa na watu wanajiuliza kuna nini huko Tanzania.
 
Mkuu Mtanzania
Nafikiri kwa la kwanza sasa tunaelekea kuelewana mimi nilikuwa nakupinga baada ya kuona unashikilia suala la Bush kama ndo Basi tumeisha piga bao, ungeeleza vizuri mwanzoni tusingelitofautiana.

Lakini sasa tunaweza kuelewana baada ya kuonyesha kuwa hili suala la kujulikana linachangiwa na vitu vingi sana. Kwa Mfano wakati nasoma watu waliijua Kenya na Nigeria kwa sababu kulikuwa na Walimu kutoka Kenya na Nigeria basi. Hapa naona tunaelewana kuwa siyo Bush tu hila ni process kama nilivyoweka hata pale juu.

Suala la Dar umelitolea Mfano sina haja ya kuelezea hili Mkuu.

Ni vizuri sasa baada ya kukuulizia sana na kukupinga umeliweka vizuri. Nafikiri pia pale ambapo hujaelewa unaweza kupoint naweza kukutolea ufafanuzi Mkuu.

Hapa hatugombani Mkuu.


Ujio wa Bush ni sehemu moja tu. Nilipokuwa ulaya miaka ya 90 wakenya na Waethiopia walijulikana sana kwa sababu ya mbio. Na hicho sio kitu cha gharama sana kwa sababu mwariadha alishafikia kiwango fulani kutakuwepo na wadhamini watakaokuwa tayari kulipa gharama zote.
 
Bin Maryam,

I mean vyandarua millioni 5 bure kwa watoto kweli vinaweza kusaidia ikiwa mbu watazidi kuzaliana?...hivi kweli Maleria hupatika tu pale watu wanapolala ama ni swala la mazingira mazima. Je ni kiasi gani kati ya fedha hizo zimetengwa ili kuboresha mazingira yanayohusiana na chanzo cha maradhi hayo?.. zero!
Hata hivyo sina maana Bush hakufanya la maana isipokuwa nionavyo mimi hii ni biashara zaidi ya kusaidia.

Kadiri yangu, msaada wa vyandarua ni wa aibu. lakini hii Bongo bwana. Watawala wetu wamesifia, wadanganyika tumepiga makofi, maisha yanaendelea.

Ninavyoamini misaada hutumika tu kama daraja au stepping stone kuelekea kwenye sustainable something(maendeleo).

Nchi inapoendeshwa kwa misaada miaka nenda rudi, hii ndio nini?
 
Komredi Mkandara:

Wewe sasa masikini jeuri. Maswali mengi kama vile tushawahi kujitegemea miaka iliyopita.

Mimi na Mkandara tunafanana kwa moja, wote naona tulikuwa waumini wazuri wa ujamaa na wapenzi wa Mwalimu Nyerere. Ila sasa tofauti inakuja, Mkandara hataki kukubali kwamba yule mpenzi wake wa utotoni sasa hayupo tena, inatakiwa aachane naye na kutambua reality iliyopo. Amheshimu mpenzi wake wa sasa na kuacha kukumbushia mambo yake ya nyuma, vinginevyo atawakosa wote.

Mimi naona ndugu yangu tukubaliane na the reality ya dunia tunayoishi sasa na kwamba kujikomba kwenye maslahi ndio reality ya dunia ya leo. Mmarekani akitaka mafuta Saudi, basi huenda na kila lugha ya kusifia. Mwingereza akitaka kuwavuta wawekezaji wa Kichina anaenda kuwaona bila hata kutaja neno human right. Sisi tukitaka 600M za Mmarekani inabidi tukubali kumweka Bush matakoni kwetu (According to Chemi Che-Mponda)na pia tutabasamu mpaka magego yaume. Nani anajali? Ni siku tatu tu, baada ya hapo unaweza kwenda Ruvuma ukawaambia wananchi dawa ya ukimwi inakuja, barabara inakuja, una uhakika wa makofi na kura 2010. Hiyo ndio reality ya dunia ambayo kama tunataka kufanikiwa inabidi tuikubali.
 
Bin Maryam,

Hapana mkuu wangu sio masikini jeuri ila kama umenielewa mimi nayaweka maslahi ya Taifa mbele...
Bush kesha kuja na ahadi zimetolewa sawa! tunazipokea lkwa mikono miwili akini humu ndani mwetu kweli hizo fedha zinapewa huduma na thamani inayotakiwa!... hatujawahi jitegemea lakini sii ndio malengo yenyewe mkuu?..
Inakuwaje vibaya kujiuliza kama huko nyuma tumeweza tambua matatizo yanayotukwamisha ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya fedha hizi za misaada. Vijimila vya kuwa wasafi anapokuja mgeni ama mtu kuvaa suti yake siku ya harusi, kula chakula kizuri siku za harusi na maulidi..is this healthy kweli ktk maendeleo ya nchi yetu?
Watatupa hadi lini ikiwa sisi wenyewe hatuna malengo zaidi ya kutegemea misaada ambayo haiwafikii wananchi. Trust me, Bin Maryam, fedha za mabarabara na Umeme ambazo tumewahi pewa.. ni billion of dollars lakini tazama tumefanya nini?...na imekuwaje tumekuwa wazuri sana ktk kupokea misaada ya kuponya magonjwa yaliyokwisha ingia badala ya kuzuia magonjwa hayo!

I mean vyandarua millioni 5 bure kwa watoto kweli vinaweza kusaidia ikiwa mbu watazidi kuzaliana?...hivi kweli Maleria hupatika tu pale watu wanapolala ama ni swala la mazingira mazima. Je ni kiasi gani kati ya fedha hizo zimetengwa ili kuboresha mazingira yanayohusiana na chanzo cha maradhi hayo?.. zero!
Hata hivyo sina maana Bush hakufanya la maana isipokuwa nionavyo mimi hii ni biashara zaidi ya kusaidia.

Kuna rais mmoja wa Philipines (Ferdinand Marcos) alifanya utapeli na raia mmoja wa ujerumani.

Philipines ina visiwa vingi basi Ferdinand Marcos na rafiki yake wa kijerumani walichagua kisiwa kimoja na wakawaita waigizaji wa ki-philipines kuigiza kama primivites wa mwisho duniani. Wakachukua filamu za waigizaji hao na kuzionyesha kwenye TV za ujerumani kuomba misaada. Walipata kama 20 Millioni USD na wakagawana.

Kwa mtaji huu kama tunategemea misaada hili ijaze mifuko ya viongozi hatutakwenda popote. Lakini hilo sio swali la kuwauliza wanaotusaidia.
 
Kadiri yangu, msaada wa vyandarua ni wa aibu. lakini hii Bongo bwana. Watawala wetu wamesifia, wadanganyika tumepiga makofi, maisha yanaendelea.

Ninavyoamini misaada hutumika tu kama daraja au stepping stone kuelekea kwenye sustainable something(maendeleo).

Nchi inapoendeshwa kwa misaada miaka nenda rudi, hii ndio nini?

Katika mijadala mingi nilikuwa napigania uimalishaji wa soko la ndani. Kwa mfano kuna vipindi mbalimbali wakulima wa mahindi wa mikoa ya Rukwa, Mbeya, Ruvuma na Iringa wanakosa sehemu za kuuza masoko yao lakini katika vipindi hivyo mikoa ya kaskazini ina upungufu mkubwa wa chakula.

Nadhani kama tungeimalisha barabara na nguvu za umeme basi wananchi wengi wangejiinua wenyewe bila kutegemea sana serikali. Lakini kwa miaka mingi tulikubali misaada ya chakula ambayo imevunja soko la ndani.

Vyandarua navyo vinaanguka katika kundi hili. Pamba ni moja ya malighafi ya kutengeneza vyandarua. Hivyo kama kungekuwepo na uwiano mzuri wa mzalishaji wa pamba, viwanda vya nguo basi tungeweza kuua ndege wengi kwa dongo moja. Mtanzania ni lazima awe na chandarua maishani mwake, na chandarua kitokane na uzalishaji wa nchini.
 
Muafaka wa Kenya JK did nothing labda la kukaa na Bush na kuchekacheka naye

Tibwilitibwili,

Soma hii na je bado unaamini JK hakufanya lolote?

How JK salvaged Kenya peace talks

By Tom Mosoba, Dar and Emman Omari, Nairobi

The inside story of how the Kenyan political deal was finally clinched on Thursday can be revealed today by The Citizen.

Sources said that Tanzanian model, where the President and the Prime Minister amicably share State responsibilities is what eventually won the hearts of the hardliners on the Government side.

The revelations emerged as the talks mediated by former UN secretary-general Kofi Annan resumed at the Serena Hotel in Nairobi yesterday, but conspicuously missing was Justice and Constitutional Affairs Minister Martha Karua, who leads the four-member PNU mediation team.

Her colleague at the talks, Foreign Affairs minister Moses Wetangula, said the minister was engaged in another assignment.

But sources from inside the shuttle diplomacy that culminated into the signing of the power sharing agreement between President Mwai Kibaki and his erstwhile rival, opposition leader Raila Odinga, said that it was only after the Tanzanian system was fully explained that the Government side agreed to salvage the deal.

President Jakaya Kikwete, it was revealed, was particularly instrument in persuading his Kenyan counterpart to accept creation of the post of executive premier.

"Kibaki was adamant on not relenting on ceding power to his rival but Kikwete thoroughly explained to him the Tanzanian model while giving his own experience," the sources said.

"It is not an easy job being in power. It is not a luxurious experience to shoulder the burden alone," President Kikwete was reported to have told Mr Kibaki, in an effort to convince the Kenyan leader to agree to the creation of the office for prime minister as his principal assistant in government.

This was during the Wednesday meeting between the two leaders without any of the government negotiators.

"This actually appeared to be the turning point and Kibaki only made one request. He asked Kikwete to make sure that the prime minister's office was not immediately entrenched in the constitution," said another source.

"Kibaki appeared to have understood Kikwete and actually from then on it was like a big step had been taken towards drawing the final document," the sources explained.

Only after this icebreaking, did President Kikwete agree to bring in Vice-President Kalonzo Musyoka and the government negotiators, namely ministers Martha Karua, Sam Ongeri and Mutula Kilonzo.

Yesterday, a source close to President Kibaki said: "A time comes when a leader must take the hard decisions on his own and what happened yesterday (Thursday) was one such moment. The President rose above party interests to make a decision for Kenya."

In Nairobi Mr Annan resumed the talks on what is commonly known as Agenda Four on long-term resolutions. They include comprehensive constitutional review within a year. His job will, however, be driven forward by Nigerian negotiator, Prof Oliweni Abenije.

Earlier on, President Kikwete, who is the African Union (AU) chairman, had held talks with Mr Raila Odinga and his team of negotiators at Grand Regency Hotel, where he was staying. Those present were Mr Musalia Mudavadi, Mr William Ruto, Dr Sally Kosgei and Mr James Orengo.

The Raila team, it was said, pleaded with President Kikwete to force a deal through as they feared worse violence would break out if his intervention failed.

"The ODM (Orange Democratic Movement) team reported that the Government was arming the dreaded Mungiki militia to cause mayhem across the country," explained the source.

Members of the government team had also their own worries and immediately sought President Kikwete's help as soon as he arrived at Jomo Kenyatta International Airport on Tuesday.

An official in the entourage confirmed that Kenya's foreign minister Moses Wetangula almost begged Mr Kikwete at the airport to have Mr Annan rescind his earlier decision to suspend the talks.

Mr Annan had called off consultations with the two negotiating teams after Justice minister Karua, criticised him and fellow mediator, former Tanzanian President Benjamim Mkapa. She reportedly accused them of alleged incompetence when they argued the case for an executive prime minister.

Mr Wetangula conceded that the suspension of the talks had caught the Government off-guard and was not good for its image. "The minister told Kikwete to convince Annan to rescind his decision and resume negotiations."

In Dar es Salaam on Thursday, while addressing the media on his arrival from Nairobi, President Kikwete said he was not aware the talks had been put off when he arrived in Nairobi. He said: "On arrival at the JKIA, this minister (Wetangula) came announcing that things had taken a different twist with Mr Annan calling off the talks."

President Kikwete said from there on, he knew the Kenyan crisis was taking a dangerous turn. "Annan had, of course, called and asked me to join him. He said things were not comfortable but he abruptly ended the talks," said the AU chairman.

Revealing the negotiations that unlocked the stalemate, President Kikwete said he met Mr Annan and his predecessor, Mr Mkapa, to get a proper briefing.

In the meeting, Mr Annan insisted that the intervention of his team and President Kikwete revolve around the six-point agreement by PNU and ODM before the talks were cancelled.

"We looked at the document and put together the agreed areas and separated the sticking points that we were to hold talks around with Kibaki and Odinga," explained Kikwete.

The Tanzanian leader said the major problem was how to create the prime minister's office and powers he should enjoy in government and whether these powers should be entrenched in the constitution.

He said they embarked on the delicate mission to assure the two teams that it was possible to have both the president and prime minister working harmoniously.

"It is really like our case here with Mizengo Pinda (Tanzanian prime minister). The office bearer has the power to oversee control, supervise day to day functions of the government," President Kikwete said on Thursday at the airport.

In the negotiated deal, the new-look Kenyan government will have the president, vice-president, prime minister and two prime ministers.

The only difference between the Tanzanian and Kenyan prime ministers, he said, is that the former has the word control added while in Kenya they chose to only have one who would coordinate and supervise the functions and execution of government function.

President Kikwete said he had been moved by pleas from the many Kenyans he came across in the corridors of state and in the streets, who beseeched him to stay until a deal was struck.

He said he would be shocked if any of the Kenyan leaders reneged on any part of the long-drawn agreement.

Source: The Citizen
 
Mimi na Mkandara tunafanana kwa moja, wote naona tulikuwa waumini wazuri wa ujamaa na wapenzi wa Mwalimu Nyerere. Ila sasa tofauti inakuja, Mkandara hataki kukubali kwamba yule mpenzi wake wa utotoni sasa hayupo tena, inatakiwa aachane naye na kutambua reality iliyopo. Amheshimu mpenzi wake wa sasa na kuacha kukumbushia mambo yake ya nyuma, vinginevyo atawakosa wote.

Mimi naona ndugu yangu tukubaliane na the reality ya dunia tunayoishi sasa na kwamba kujikomba kwenye maslahi ndio reality ya dunia ya leo. Mmarekani akitaka mafuta Saudi, basi huenda na kila lugha ya kusifia. Mwingereza akitaka kuwavuta wawekezaji wa Kichina anaenda kuwaona bila hata kutaja neno human right. Sisi tukitaka 600M za Mmarekani inabidi tukubali kumweka Bush matakoni kwetu (According to Chemi Che-Mponda)na pia tutabasamu mpaka magego yaume. Nani anajali? Ni siku tatu tu, baada ya hapo unaweza kwenda Ruvuma ukawaambia wananchi dawa ya ukimwi inakuja, barabara inakuja, una uhakika wa makofi na kura 2010. Hiyo ndio reality ya dunia ambayo kama tunataka kufanikiwa inabidi tuikubali.

Hata mimi niliamini mengi ya Nyerere kwa sababu sikuwa na nafasi ya kupata zaidi ya kile alichosema yeye.

Dunia ina migogoro mingi na nafasi kwa nchi ndogo kama Tanzania ni nadra na zinapopatikana ni lazima tuzitumia kwa maslahi ya taifa na vilevile tuzitumie kama vile ni nafasi yetu ya mwisho.

Wakati siasa za Ujamaa zimepamba moto duniani, nchi za Scandinavia zilitupa misaada bila kutuuliza tunafanyia nini. Na sisi tukachukulia kama misaada hiyo ilitoka kwa watu wanaotupenda kwa sababu siasa zao zilikuwa zinakaribiana na zetu.

Lakini nchi nyingi za Scandinavia zilikuwa na uhusiano na Urusi na zilifanya biashara na nchi za kikomunisti ambayo ilikuwa na faida kubwa kwao. Wao walikuwa ni proxy kati ya nchi za komunisti na nchi za kibepari. Na nchi hizi hazikuona faida za kujiunga na Umoja wa nchi za Ulaya.

Baada kuvunjika kwa ukomunisti uchumi wa nchi za Scandinavia ukadorora. Ukosefu wa kazi uliongezeka mpaka 15% na wakaanza kusaidia nchi za ndugu zao zilizojikwamua kutoka katika shirikisho la Kisovieti.

Kutokana na majukumu ya ndani ya nchi zao na kusaidia ndugu zao wa Lithuania, Latvia wakaanza kutuuliza jinsi tunavyotumia misaada yao. Na walivyopigia kelele misaada yao, watanzania tukaanza kusema kuwa hadhi yetu imeharibika nje ya nchi na ni lazima Ikulu aingie mtu atayerudisha hadhi yetu.

Ukweli wa mambo hatukuwa na hadhi yoyote nje ya Tanzania. Tulisaidiwa kwa sababu za kisiasa ambazo wao nao walizitumia katika maslahi yao ya kisiasa.

Kwa sasa hivi tunasaidiwa kwa sababu za kisiasa na mambo yanayotokea duniani. Itafika mahali watakata misaada hii. Watakapokata kuna watanzania watafikiri kuwa imekatwa kwa sababu ya kupungua kwa hadhi ya Ikulu. Itakatwa kwa sababu hawana maslahi tena na sisi.

Nilisikiliza hotuba za Reagan akigombea urais 1964. Alisema serikali iache kusaidia nchi kama Ethiopia ambayo viongozi wao pesa kununua private yatch. Alipopata Urais 1979 alichofanya ni kuendelea kumtajirisha Mobutu Sese Seko.

Hivyo ni lazima watanzania tujue siasa za kimataifa na sababu gani misaada inakuja kwetu.
 
SafeRedirect.aspx


Haya ndiyo matunda ya Safari ya Bush Tanzania!
 
Nimekaa chini tena na kujiuliza baada ya kuona kideo cha Bush na tamko la vyandarua. Je kutupa hivyo vyandarua pamoja na nia yake ambayo siihoji au kutilia shaka, hivi hatuoni aibu?

Tumenunua Ma VX mengi kila baada ya uchaguzi mkuu, tumeongeza masurufu na matumizi ya viongozi lakini tunashindwa kununua hata Chandarua?

Ni sawa na mtu aliyepiga suti na moka la nguvu huku ndani kinasa chake kimebakia nyuzi?

It is time we need to stop prouding ourselves on receiving aid or assistance on things that we are capable to control! Hili la vyandarua limenisikitisha.

Bush kasema, kaangalia kushoto halafu kulia akasema what the heck, let me pay for all vyandarua so these kids who are the future of this country grow safe at least for a year, safe of Malaria! Ni sawa na mgeni kununua Chumvi unapomkaribisha mlo!
 
Kadiri yangu, msaada wa vyandarua ni wa aibu. lakini hii Bongo bwana. Watawala wetu wamesifia, wadanganyika tumepiga makofi, maisha yanaendelea.

Ninavyoamini misaada hutumika tu kama daraja au stepping stone kuelekea kwenye sustainable something(maendeleo).

Nchi inapoendeshwa kwa misaada miaka nenda rudi, hii ndio nini?
Mkuu

Kweli hata mimi naona hili la vyandarua kutolewa mtu kama Bush ni aibu kwa taifa.

Hili ni sawa sawa na mgeni kuja nyumbani kwako akaamua kukununulia shuka za kulalia.

Sijui kama kweli wamarekani wanaweza kujisikia vizuri kuwa rais wao ametoa msaada wa vyandarua kwa nchi maskini yenye Utajiri.

Kuna siku nilishawahi kuulizwa hivi Tanzania iko wapi? Nikasema iko karibu na Nairobi na tuna mbuga ya wanyama ya serengeti, jamaa akajua Nairobi na pia akajua serengeti. Suala la Pili akauliza hivi mnawezaje kuishi na wanyama? Ilikuwa patashika kujibu suala hili maana jamaa lilikuwa halitaki kuelewa kuwa Watanzania hatuishi na wanyama wa serengeti.

Sasa baada ya hili nina wasiwasi Suala litageuka na kuwa vipi Mbu wameisha pungua? Au nikununulie neti?.

Kama suala la Neti ni muhimu sana nafikiri ifike wakati Serikali iliweke kwenye bajeti zake maana nasikia VX moja inaweza kufikia milioni 60 na ushee hivi Je tunaweza kununua vyandalua ngapi? Je Tunahitaji Bush aje kutununulia vyandarua hivi?

Ningependa kama Bush angetupa Msaada wa Elimu kuliko vyandarua.
 
Niliandika "anaweza kudeliver" nikiwa na maana the jury is still out. Anaweza kuwa ana struggle mpaka sasa lakini kuna uwezekano akafanikiwa kwenye baadhi ya mambo labda kuliko hao walimtangulia na mifano ni hilo la Kenya na kumleta Bush.

..the jury is way out!. mwaka 2010 si huo hapo?
Huenda mpaka sasa haya mambo hayatusaidii kama taifa maana hayaongezi pato wala shibe ya Mtanzania lakini pia yanaweza kuwa nguzo kubwa ya kuiletea baraka TZ siku za mbele through employment na investments zingine. Message kubwa hapo ni kwamba Tanzania ni democratic and stable, vitu viwili ambavyo ni muhimu mno kwa investors wa maana.

..hizi siasa nyingine hizi! unafikiri uwekezaji ni suala linaloota kama magugu shambani? u need some coordinated efforts to pull that one off! unaweza kusema currently tuna miundombinu inayovutia uwekezaji? achilia mbali costs of production!


Sikuwa na maana JK amedeliver maana mambo mengi aliyosema atafanya, hajafanikiwa kuyafanya mpaka sasa.

..god willing atafanya!. maana ndio lililobakia hilo!
 
Mkuu,

Naamini dunia na watu wengi wa dunia akiwemo Annan, wanaamini JK kasaidia.

..and i wonder,when reading western news,he is not mentioned anywhere,hata kwa neno moja tu.

..annan ndio anaonekana shujaa.
 
Back
Top Bottom