Hotuba za Rais kila mwezi

Hotuba za Rais kila mwezi

Je unaridhika na hotuba za Rais Kikwete?

  • Ndio

    Votes: 13 15.5%
  • Hapana

    Votes: 71 84.5%
  • SIJUI

    Votes: 0 0.0%
  • Sina jinsi

    Votes: 1 1.2%

  • Total voters
    84
  • Poll closed .
Halmashauri Kuu inaona kuwa sahihi za Maalim Seif na Mzee Makamba au za viongozi tu pekee hazitoshi. Ridhaa ya wananchi ni muhimu na hili ni jambo la msingi na la kawaida katika mifumo yote ya kidemokrasia..

JK msanii at his best,

mi ningepata muda ningemuuliza tu kwamba (kutokana na niliyoyaquote hapo juu) kama sahihi za Makamba na Maalim Seif hazikutosha/zisingetosha inakuwaje basi sahihi za Nyerere na Karume Sr. zilitosha kuua utaifa wa Tanganyika na Zanzibar back in time?Nilifikiri kuwa Makamba na Maalim walikuwa wanawasilisha matakwa ya wanachama wao (ambao ni raia wa Visiwani),pili kuhusu ushirikishwaji wa wananchi Kikwete ningemuuliza wakati Tanganyika na Zanzibar zilipokuwa zinapokonywa utaifa wazo Nyerere na Karume Sr. waliwashirikisha kivipi wananchi wa nchi hizi mbili?Na wakati ule Aboud Jumbe "akishikishwa" adabu kule Dodoma je wananchi wa Zanzibar walishirikishwa kinamna gani?

No wonder Mkapa alikataa kwenda Butiama kupoteza busara zake bure.Isipokuwa tu kwa ufisadi alioshiriki kuufanya kipndi chake,Mkapa remains the best ever kwa Kikwete come a million years.
 
"Jambo la kwanza linahusu kuwashirikisha wananchi katika kufanya uamuzi huu mkubwa. Halmashauri Kuu ya Taifa inaamini kuwa mabadiliko yanayopendekezwa ni makubwa sana na ya msingi. Yanahusu kuubadili kabisa mfumo wa sasa wa utawala na uendeshaji wa shughuli za Serikali Zanzibar. Halmashauri Kuu ya Taifa inaona kuwa ipo haja ya msingi ya kuwashirikisha wananchi wa Zanzibar kuamua.

Halmashauri Kuu inaona kuwa sahihi za Maalim Seif na Mzee Makamba au za viongozi tu pekee hazitoshi. Ridhaa ya wananchi ni muhimu na hili ni jambo la msingi na la kawaida katika mifumo yote ya kidemokrasia.. Kama suala ni muda, napenda kuwahakikishia kuwa hata CCM inapenda mambo hayo yaishe mapema iwezekanavyo. "

Wenye akili walijua hili toka zamani. Kuna posts nyingi tu huko nyuma zilisema hili ndio litakalotokea, na kweli again JF imeendelea kuwa jukwaa la Ukweli.

Dhana ya kusema wananchi waamue ina matata sana, kuna baadhi ya mambo yanaamuliwa na wananchi na baadhi yanaamuliwa na wananchi kwa kupitia viongozi wao. Ukimuuliza lay man wa Kojani kuhusu mambo mengi yenye umuhimu wa kitaifa na kiusalama, au ukimuuliza mtu yoyote kule Kibanda maiti kuhusu umuhimu wa serikali ya Muungano hawezi kusema lolote la maana. Hili Suala lilitakiwa kuendelea kama lilivyokubaliwa kwenye muafaka. Kama CCM wakienda kinyume na uamuzi uliowekwa saini na katibu wake CUF watakuwa na haki ya kutowaamini tena.

Kwa mara nyingine JK, ameshindwa kuprovide leadership, Karume ameonesha udhaifu mkubwa. Kuna haja ya moja kwa moja kuanza kuinusuru Tanzania kwa kuunusuru uongozi wa CCM.
 
Nawapa pole kwa msiba uliowapata wa kumpoteza mwenzao mmoja aliyezama majini pale Kisiwani Mwali siku moja kabla ya majeshi yetu kuondoka kuelekea Nzuani. Ajali haina kinga..

Hii statement ya AJALI HAINA KINGA haitofautiani sana na ile aliyoitoa kule Mererani juzi, ninaweza kumuelewa mtu yoyote akisema hivi mitaani but for Gods sake- Not a president! How can he say anything like this and get away with it? This attitude has got to change! Mr. President-accidents can be prevented,vyanzo vya ajali nyingi sehemu za kazi,majumbani, barabarani, etc zinatokana na uzembe na lack of training au enough knowledge kuhusu sources mbalimbali za accidents.Serekali inatakiwa i introduce mandatory risk analysis na kuwe na policies za health and safety kila sehemu ya kazi.

Madereva kibao hadi leo hii wanaendesha magari bila leseni, hawajui hata sheria ndogondogo za barabarani.Maofisi yamejaa fire extinguishers lakini im sure ni wachache sana wenye knowledge ya kuizitumia kama kutakuwa na fire incidents.Kule Mererani kama kungekuwa na risk analysis na health and safety measures in place,sidhani kama haya yaliyotokea juzi yangetokea!Its not a rocket science kujua kwamba mvua ikinyesha itaingia kwenye hayo mashimo, even a nursery kid know what has to be done!Fun enough, kuna strategies za kupambana na mauaji ya albinos- fine, but where are the measures kuhakikisha kwamba kilichotokea Mererani hakitokei tena hapo au kwenye machimbo mengine yoyote nchini?Does the government know how many miners are trapped down there?

Tukiendelea na hii attitude za 'ajali haina kinga' na 'kazi ya mungu' tutaisha, our leaders need to act now.
 
Jamaa anasema hata kuweka sahihi it took him ages hadi Bush akawa amekaa anangoja amalize kuweka sahihi .

Mizuka ya IPTL, Richmond na mikataba mibovu ilikuwa inamfanya aweweseke, hazikuwa mbwembwe bali alikuwa anasoma vipengele kwenye maandishi mnayoyaita fine print!🙁
 
Hivi hii ni hotuba kwa wana CCM au kwa wananchi? Kwanini kwenye mtiririko huo hapo juu kama kweli hii ni hotuba kwa wananchi na sio kwa wana CCM neno "Ndugu Wananchi" lisitangulizwe juu? Hivi ni lazima aitaje CCM kwenye hizi hotuba? Na mwishoni anamalizia na kidumu Chama cha Mapinduzi!
Maelezo ya wanajeshi kupelekwa Comoro yangepaswa kutolewa kwa wananchi kabla hata hiyo oporesheni ya demokrasia iliyotumia mtutu haijaanza na sio mwishoni.

Kana ka Nsungu,

Ukisoma alichoandika Halisi mwanzoni mwa thread hii utagundua kwanini mpangilio ulikuwa hivyo.

TAARIFAKWA VYOMBO VYA HABARI


Rais Jakaya Mrisho Kikwete keshotarehe 2 April, 2008, saa kumi jioni,
atalihutubia taifa kupitia wana CCM na viongozi wa Jumuiya za Chamakatika ukumbi wa
Diamond Jubilee.

Rais hakuweza kutoa hotuba yake yamwisho wa mwezi wa tatu (Machi) kutokana na maafa yaliyotokea katika machimboya Tanzanite, Mererani katika mkoa wa Manyara ambapo ilimlazimu kwendakutembelea eneo la maafa ili kujionea hali na kutoa pole kwa wananchi nawachimbaji wa Mererani.

Hotuba hiyo itatangazwa moja kwa mojakupitia redio na Televisheni mbalimbali hapa nchini.

ImetolewaIkulu, Dar-es-salaam,
Tarehe1, April, 08
 
Hii statement ya AJALI HAINA KINGA haitofautiani sana na ile aliyoitoa kule Mererani juzi, ninaweza kumuelewa mtu yoyote akisema hivi mitaani but for Gods sake- Not a president!
Madereva kibao hadi leo hii wanaendesha magari bila leseni, hawajui hata sheria ndogondogo za barabarani.

Kikwete anajua kabisa jinsiw atendaji wanavyokula rushwa lakini he is slugish in acting. ni huyuhuyu aliyewahi kusema kuwa anawajua wala rushwa kwa majina, lakini cha ajabu akatia muda eti wajirekebishe! akili kweli hii.
Bado tunahitaji kiongozi nchi hii, kwa usanii huu tutachukua muda kupata kile tunachokihitaji katika maendeleo
 
Mie Naomba kuuliza .
Hivi RAIS wa jamhuri ya muungano wa tz anamamlaka ya kumfukuza kazi Rais wa ZAnzibar???

mfano kama JK kakubaliana na CUF kuunda serikali ya mseto kule zenji harafu Karume akaimtolea nje JK na akamwambia kama wewe unataka serikali ya mseto basi waingize CUF ktk serikali yako ya DAR.

Je? JK anaubavu kikatiba kumun'goa Karume ama itakuaje
 
Mie Naomba kuuliza .
Hivi RAIS wa jamhuri ya muungano wa tz anamamlaka ya kumfukuza kazi Rais wa ZAnzibar???

mfano kama JK kakubaliana na CUF kuunda serikali ya mseto kule zenji harafu Karume akaimtolea nje JK na akamwambia kama wewe unataka serikali ya mseto basi waingize CUF ktk serikali yako ya DAR.

Je? JK anaubavu kikatiba kumun'goa Karume ama itakuaje
Mkamap,Mhe. Jk hana Ubavu wa kumng'oa Rais wa Zanzibara ambaye ni kiongozi wa zanzibar.
tuangalie ibara ya 104 ya katika ya Jamhuri ya Muungano.
1)atachaguliwa na wananchi katika Tanzania Zanzibar kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya Zanzibar, na kwa kufuata utaratibu
uliowekwa kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi la Zanizibar inayohusu uchaguzi kwa ujumla au uchaguzi wa Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, kiti cha Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kitakuwa ki wazi,
na uchaguzi wa Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar utafanyika ili kujaza nafasi hiyo kila mara litokeapo lolote kati yamambo yafuatayo.
(a) baada ya Baraza la Wawakilishi kuvunjwa;
(b) baada ya Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kujiuzulu bila ya kulivunjwa Baraza la Wawakilishi kwanza;

(c) baada ya kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupoteza sifa za kushika nafasi ya madaraka ya kuchaguliwa;

(d) baada ya Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kushtakiwa katika Baraza la Wawakilishi kwamujibu wa Katiba ya Zanzibar 1984 na kuondolewa katika madaraka.

(e) baada ya kuthibitishwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar 1984 kwamba Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hawezi kumudu kazi na shughuli zake;

(f) baada ya Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi yaZanzibar kufariki.




 
Mkamap,Mhe. Jk hana Ubavu wa kumng'oa Rais wa Zanzibara ambaye ni kiongozi wa zanzibar.
tuangalie ibara ya 104 ya katika ya Jamhuri ya Muungano.
[/LEFT]
[/FONT]

Gembe,

Anaweza kumng'oa inderectly kupitia CCM, kitu ambacho kwasasa hawawezi kufanya.

Huko nyuma walishamng'oa Jumbe lakini ilikuwa kupitia vikao vya chama.

Akijifanya mjanja, wanaweza kuvua uanachama wa CCM na hapo atakuwa amepoteza hata urais wa zanzibar.
 
Gembe,

Anaweza kumng'oa inderectly kupitia CCM, kitu ambacho kwasasa hawawezi kufanya.

Huko nyuma walishamng'oa Jumbe lakini ilikuwa kupitia vikao vya chama.

Akijifanya mjanja, wanaweza kuvua uanachama wa CCM na hapo atakuwa amepoteza hata urais wa zanzibar.

hili linawezekana kama kuvuliwa uanachama,ila kumvua uanachama Rais wa CCM ni sawa na kukivua nguo chama cha Mapinduzi.

Karume hana kiburi cah kuwaachia CUF ili kwa pamoja waunde serikali ya Mseto ila wale wafahidhina ndio balaa.Yeye anamalizia muda wake tu wa kutawala.Mie nadhani ile sera ya Chadema ya Majimbo ingekuwa dawa ya tatizo hili.Pemba ingekuwa jimbo na Unguja ingekuwa poa sana..CUf wanajinyakulia Jimbo lao na CCM hivyo hivyo.na tunakuwa na Rais Mmoja Tanzania nzima..<Je itawezekana??>.
 
Guys,

This' so educative. Thanks on behalf of unregistered members.

Mkamap,Mhe. Jk hana Ubavu wa kumng'oa Rais wa Zanzibara ambaye ni kiongozi wa zanzibar.
tuangalie ibara ya 104 ya katika ya Jamhuri ya Muungano.

Gembe,

Anaweza kumng'oa inderectly kupitia CCM, kitu ambacho kwasasa hawawezi kufanya.

Huko nyuma walishamng'oa Jumbe lakini ilikuwa kupitia vikao vya chama.

Akijifanya mjanja, wanaweza kuvua uanachama wa CCM na hapo atakuwa amepoteza hata urais wa zanzibar.

hili linawezekana kama kuvuliwa uanachama,ila kumvua uanachama Rais wa CCM ni sawa na kukivua nguo chama cha Mapinduzi.

Karume hana kiburi cah kuwaachia CUF ili kwa pamoja waunde serikali ya Mseto ila wale wafahidhina ndio balaa.Yeye anamalizia muda wake tu wa kutawala.Mie nadhani ile sera ya Chadema ya Majimbo ingekuwa dawa ya tatizo hili.Pemba ingekuwa jimbo na Unguja ingekuwa poa sana..CUf wanajinyakulia Jimbo lao na CCM hivyo hivyo.na tunakuwa na Rais Mmoja Tanzania nzima..<Je itawezekana??>.
Gembe,

Sera ya majimbo mwenyewe nilikuwa naiona kama haifai lakini kwa namna hii inaweza kupendeza japo pia ikasababisha nchi mbili za ziada, Zanzibar & Pemba ambazo zipo katika Taifa la Tanzania na huenda hilo likapelekea jina la Tanzania kubadilika endapo Pemba wanaweza kudai (demand) kutambuliwa kama nchi ndani ya nchi na hivyo kutaka uwepo wa muungano wa Tanganyika, Pemba na Zanzibar.

Hili suala la Muungano ni gumu sana. Wasiwasi wangu watu wengi wa bara wakiambiwa wapige kura endapo tuendelee kuwa na Muungano huu wanaweza kusema "Hapana" wengine bila hata kufikiria.

Suluhu ya Zanzibar ni kuwepo kwa vyama zaidi vyenye nguvu zaidi ya CUF na CCM. Kitendo cha kuwepo vyama viwili vyenye nguvu zaidi ndiko kunapelekea haya (kwa hisia zangu).
 
majimbo? thubutu
Haya Mawazo ya watu kama Mpita njia ndio yaliyomo katika mioyo ya watu wafahidhina wasiotaka muungano wa Serikali kati ya CCM na CUF.JK ameshandwa kwasabu hana ubavu wa kuingilia hili na anjua madhara yake ni yapi.

Mhe. Zitto naomba uiweke sera ya Majimbo hapa tuijadili!!hii ikiboreshwa nadahni itakuwa ndio suluhu ya Migongano hii
 
Kana Kasungu ulitaka asemeje??

Ni Msemo wakiswahili na una maana,tuache kujenga hoja zisizo za msingi!!
 
Haya Mawazo ya watu kama Mpita njia ndio yaliyomo katika mioyo ya watu wafahidhina wasiotaka muungano wa Serikali kati ya CCM na CUF.JK ameshandwa kwasabu hana ubavu wa kuingilia hili na anjua madhara yake ni yapi.

Mhe. Zitto naomba uiweke sera ya Majimbo hapa tuijadili!!hii ikiboreshwa nadahni itakuwa ndio suluhu ya Migongano hii

Nawashukuru wote kwa majibu yenu mazuri
Mimi binafsi ktk swala hili kama nilivyopata kutoka kwenu waelewa kama kweli wajumbe wa zanzibar pamoja na karume walikua na msimamo mkali kumlaumu JK hapo si kumtendea haki.

SWala la Majimbo kwa kweli mie naliunga mkono kwa 100% kwa mtazamo wangu ni kitu kinacholeta maendeleo kwa haraka na kusogeza huduma karibu kwa wananchi.
Mfano siwezi kusafiri toka Mwanza na treni na kuchukua siku tatu njiani kwenda kutafuta passport tena kwa kirasimu DAR hii inamaana kusitisha shughuri karibu za mwezi kwa ajiri ya kutafuta hicho kitu maendeleo yatakuja kweli kwa haraka??

kitu chochote kizuri ukikichukulia kwa nia mbaya na kinakua haramu ,mfano Mtu hawezi leta idea kua kusokata kamba ya kufungia mbuzi si vyema na haramu maana kamba za namna hiyo watu hujitundika na kuzitoa roho zao
 
Mie Naomba kuuliza .
Hivi RAIS wa jamhuri ya muungano wa tz anamamlaka ya kumfukuza kazi Rais wa ZAnzibar???

mfano kama JK kakubaliana na CUF kuunda serikali ya mseto kule zenji harafu Karume akaimtolea nje JK na akamwambia kama wewe unataka serikali ya mseto basi waingize CUF ktk serikali yako ya DAR.

Je? JK anaubavu kikatiba kumun'goa Karume ama itakuaje


NO rais wa Zanzibar kachaguliwa na wananchi Rais wa muungano wana uwezo wa kufukuza.Kama vile asivyo na mamlaka kwa wabunge kwa kuwa wamechaguliwa na wananchi.Rais wa muungano ana mamlaka juu ya wale walio waajiliwa wa kawaida wa serikali na walioteuliwa na rais mwenyewe .
Duh kumbe jamaa alitoa jibu hilo tehe tehe tehe.
 
Gembe,

Anaweza kumng'oa inderectly kupitia CCM, kitu ambacho kwasasa hawawezi kufanya.

Huko nyuma walishamng'oa Jumbe lakini ilikuwa kupitia vikao vya chama.

Akijifanya mjanja, wanaweza kuvua uanachama wa CCM na hapo atakuwa amepoteza hata urais wa zanzibar.

kaka UBAVU HUO ALIKUWA NAO MCHONGA[MWALIMU NYERERE]..SIO HUYU AMBAYE HAWEZI HATA KUFUKUZA SHAMBA BOY KAZI....ANAOGOPA LAWAMA..KAMA KILA SIKU ALIVYOKUWA AKIWEWESEKA BAADA YA KUMFUKUZA AFISA MMOJA PALE ELIMU KIMAKOSA ....JAMBO AMBALO KWA MTAWALA SI LA AJABU...SIMPLY ANGEAMUA TU KUMRUDISHA NA KUMLIPA FIDIA ..BADALA YA KUKAA KUWEWESEKA..

HANA UBAVU WA KUMWAMBIA LOLOTE KARUME SEMBUSE KUMFUKUZA...MMESAHAU HATA KUMFUKUZA BALALI ..ALINGOJA MWENYEWE AANDIKE BARUA ...NA HATA KUMFUKUZA ALITANGAZA WAKATI BALALI ALIWA MAUTI UTI..ICU.....

LOWASSA NDIO KABISA ALISHINWA KUMKEMEA AKABAKI ANAMNUNIA....KAMA MKE MWENZA!!
 
Kana Kasungu ulitaka asemeje??

Ni Msemo wakiswahili na una maana,tuache kujenga hoja zisizo za msingi!!

Ingekuwa vyema kama Mh. Raisi badala tu ya kusema 'ajali haina kinga' angesema serekali ina mikakati gani kuhakikisha kwamba janga kama hilo halitokei tena mahali hapo au kwenye machimbo mengine yoyote nchini.Utakuwa mvivu wa kufikiri Gembe kama unaamini kwamba ajali nyingi zinazotokea bongo haziwezi kuzuilika.Ni msemo wa kiswahili ndio lakini kwangu hauna maana,every accident can be prevented.
 
Waungwana,

Mwezi wa saba huo ndiyo unaelekea ukingoni. Kama mnavyofahamu JK alijiwekea utaratibu wa kutoa hotuba kila mwisho wa mwezi. Miezi miwili iliyopita, May na June, hakutoa hotuba hizo. Sasa sijui kama mwezi huu atatoa hotuba atazungumza kuhusu nini. Labda itakuwa ni mafanikio yake ya ziara aliyoifanya hivi karibuni huko Tanga, au atazungumza kuhusu safari yake kwenda kwa swahiba wake US mwezi wa nane lakini kamwe tusitegemee kabisa azungumze yale ambayo sasa hivi yanachukua sehemu kubwa katika mazungumzo ya watanzania walio ndani na nje ya nchi kuhusiana na ufisadi unaoiangamiza nchi yetu.

Hawezi kabisa kuzungumzia uchunguzi wa EPA umefikia wapi na mpaka sasa hivi wameshakusanya kiasi gani toka kwa mafisadi. Mara ya mwisho tuliambiwa wamekusanya shilingo 60 billioni ingawaje walishindwa kutupa majina ya akina nani waliorudisha pesa hizi na kiasi cha kila aliyerudisha na zimewekwa katika bank ipi, si ajabu nazo zimeshatafunwa. Kamwe hatazungumzia kuhusiana na ufisadi uliofanywa na fisadi Mkapa wa kutupora mgodi wetu wa Kiwira. Kamwe hatazungumzia jitihada zinazofanywa kuwadai Richmond/Dowans waturudishie mabilioni yetu waliolipwa bila kufanya kazi yeyote ile, kama mnavyofahamu bado wanalipwa shilingi 152 millioni kwa siku. Kamwe hatazungumzia mikataba mibovu kuhusiana na madini yetu mbali mbali.

Huyu ndiye Rais ambaye baadhi yetu walimwita ni changuo la Mungu!!!! Sijui kama Mungu anatuchukia kiasi hichi Watanzania wa kutuchagulia mtu ambaye hana uwezo wa kuendesha hata mtaa achilia mbali kuendesha nchi!! Tusubiri Watanzania labda dua zetu zitasikika na hatimaye 'chaguo la mungu' aanze kuzungumza yale tunayotaka kuyasikia. Pia tusishangae akiamua kuingia mitini tena kwa mwezi wa tatu mfululizo.

Alutta Continua!

Mungu ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom