Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Barrick nimeitolea kama mfano tu,lakini hapa Tanzania kuna kampuni nyingi tu za nje ambazo zimewekeza na kusema FDR imeshuka sio kweli.-Umegusia kampuni moja tu ya barrick lakini foreign direct investment imeshuka nchini kwetu,
-wahisani wanatoa misaada lakini lazima ujuwe kwamba wana masharti yao ikiwemo haki za binadamu na ndiyo maana WB walishikilia Mkopo wetu kwa kipindi Fulani kutokana na barua ya malalamiko ya zitto na hata WB walipotoa ule mkopo ukatolewa kwa masharti
-kusema watu hawapigi kura kwa huruma au wanapiga kwa huruma hilo sasa litategemea na usikae kwenye akili za watu na kuwasemea kwamba hawatapiga kura za huruma (usisemee mioyo ya watu unless una research findings kama za TWAWEZA zinazothibtisha hilo) kwa sababu watu pia wanaweza kupiga kura za huruma kama kumthamini kwa ujasiri na magumu aliyopitia na kumpa kura za ushindi kama zawadi ya kipigania haki ndani na nje ya bunge.
Kama haki za binadamu zinakiukwa sidhani kama Usaid wangekuwa wanatoa misaada. Tukio la Lissu kushambuliwa isiwe sababu ya kusema haki za binadamu zinavunjwa.
Tungekuwa tunaona watu wanapigwa risasi kama mbwa mabarabarani na polisi hapo tungesema kuna tatizo. Ndio maana watu hawamchagui mtu kwa kumhurumia bali kwa uchapa kazi wake na uzalendo.