Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,069
10,012
Mara ya kwanza nilioona suala hili Royal Village, nimekuta wapiga picha kibao, ukikaa sura wazi wanakukochoa, na mtu umeshalipa hela nyingi kukaa kwa amani, ukitaka picha utawaita mwenyewe ila kule hali ni tofauti.

Niko hoteli nyingine leo, the same sh*t, jamaa kakomaa na kamera lake anataka kupiga picha ikabidi nimkumbushe sheria ya taarifa binafsi. Tabia hii siioni kwenye hoteli nyingi za Dar ambapo mtu unakuwa na amani unakaa kwa kutulia.

Nadhani hii ni tabia ya kijinga sana, na nitaanza kutumia sheria kwa yeyote atakayeleta za kuleta ili wajifunze kuwa na adabu. Mwendo ni kama waliofanyiwa CRDB tu kulipa mamilioni
 
Wabongo bana yani take home yako 500k unavimbaaa na dharau
Acha dharau anachoongea mtoa mada ni kweli,Binafsi niliona mwaka fulani pale Dar Live,wapiga picha wamejaa kila kona na mtu umeenda kufanya starehe zako kwa faragha,bpia Jangwani Sea breeze nilishindwa sababu hiyo hiyo, Nimekanyaga ufukweni tu na warembo wawili nikashtuka tayari nipo kwenye kurasa yao ya Instagram.

Ilibidi niwasiliane na Admin akagoma kutoa zile picha,nikatafuta namba za meneja ni Mhindi ndio akasema watazitoa.

Next weekend nimeenda tena Nikapigwa picha wakaweka tena Instagram,nikawasiliana tena na meneja kumuomba atoe.

Wametoa zile picha kwenye Instagram siku tatu mbele wakapost tangazo la kuvuta wateja weekend na mie tena nikawepo kwenye lile Tangazo,Sijawahi kanyaga tena pale.
 
Mkuu hebu fafanua kidogo,maana sijakuekewa!

Yaani hao wapiga picha huwa wapo nje ya Hotel zote Dodoma na kila mgeni akiingia au kutoka wanakukimbilia na kukulazimisha wakupige picha au imekaaje?,Au wewe ni mtu maarufu sasa baada ya kukuona mapaparazi wakahitaji wakupige picha?,Hebu fafanua kidogo maana ni kama sijakuelewa!
 
Acha dharau anachoongea mtoa mada ni kweli,Binafsi niliona mwaka fulani pale Dar Live,wapiga picha wamejaa kila kona na mtu umeenda kufanya starehe zako kwa faragha,pia Jangwani Sea breeze nilishindwa sababu hiyo hiyo,Nimekanyaga ufukweni tu na warembo wawili nikashtuka tayari nipo kwenye kurasa yao ya Instagram. Ilibidi niwasiliane na Admin akagoma kutoa zile picha,nikatafuta namba za meneja ni Mhindi ndio akasema watazitoa. Next weekend nimeenda tena Nikapigwa picha wakaweka tena Instagram,nikawasiliana tena na meneja kumuomba atoe. Wametoa zile picha kwenye Instagram siku tatu mbele wakapost tangazo la kuvuta wateja weekend na mie tena nikawepo kwenye lile Tangazo,Sijawahi kanyaga tena pale.
ukimani ni shida sana. kuna models kazi yao nini? sijui wanaona ubahili mbuzi hawa. dawa yao next time usiwashtue wewe ka file legal case.
 
Acha dharau anachoongea mtoa mada ni kweli,Binafsi niliona mwaka fulani pale Dar Live,wapiga picha wamejaa kila kona na mtu umeenda kufanya starehe zako kwa faragha,pia Jangwani Sea breeze nilishindwa sababu hiyo hiyo,Nimekanyaga ufukweni tu na warembo wawili nikashtuka tayari nipo kwenye kurasa yao ya Instagram. Ilibidi niwasiliane na Admin akagoma kutoa zile picha,nikatafuta namba za meneja ni Mhindi ndio akasema watazitoa. Next weekend nimeenda tena Nikapigwa picha wakaweka tena Instagram,nikawasiliana tena na meneja kumuomba atoe. Wametoa zile picha kwenye Instagram siku tatu mbele wakapost tangazo la kuvuta wateja weekend na mie tena nikawepo kwenye lile Tangazo,Sijawahi kanyaga tena pale.
Mkuu kwanini usingewachukulia sheria?

Hivi watanganyika tutaendelea kulalamika hadi lini na sheria zipo?
 
Mkuu hebu fafanua kidogo,maana sijakuekewa!

Yaani hao wapiga picha huwa wapo nje ya Hotel zote Dodoma na kila mgeni akiingia au kutoka wanakukimbilia na kukulazimisha wakupige picha au imekaaje?,Au wewe ni mtu maarufu sasa baada ya kukuona mapaparazi wakahitaji wakupige picha?,Hebu fafanua kidogo maana ni kama sijakuelewa!
Sina umaarufu, ila wakikuona tu, tayari wanakupiga picha.
 
Viposho hivyo na jeuri lipa bana....picha kumbukumbu ya viposho
Kumbukumbu inaamuriwa na mwenyewe. Ingia matukio ya watu wakubwa mtaambiwa mna uhuru wa kuchagua kupigwa picha au kutopigwa picha. Hii nimeiona maeneo mengi. Zipo hoteli zinazuia wapiga picha unless amepewa tenda na mteja. Yote ni kulinda taarifa binafsi za wateja wao. Hali haiko hivyo Dodoma, wapiga picha wanakaa kaa tu kupiga picha
 
Mara ya kwanza nilioona suala hili Royal Village, nimekuta wapiga picha kibao, ukikaa sura wazi wanakukochoa, na mtu umeshalipa hela nyingi kukaa kwa amani, ukitaka picha utawaita mwenyewe ila kule hali ni tofauti.

Niko hoteli nyingine leo, the same sh*t, jamaa kakomaa na kamera lake anataka kupiga picha ikabidi nimkumbushe sheria ya taarifa binafsi. Tabia hii siioni kwenye hoteli nyingi za Dar ambapo mtu unakuwa na amani unakaa kwa kutulia.

Nadhani hii ni tabia ya kijinga sana, na nitaanza kutumia sheria kwa yeyote atakayeleta za kuleta ili wajifunze kuwa na adabu. Mwendo ni kama waliofanyiwa CRDB tu kulipa mamilioni
Kama haya uliyoandika yana ukweli, basi Wamiliki wa Hoteli hiyo wanapaswa kukomesha hali hii. Wajitahidi kuwaondoa wapiga picha hao kwenye maeneo ya jirani na Hoteli yao, waende mbali kabisa na eneo hilo la hoteli. Hiyo ni breach of personal privacy, ni mbaya sana. Itaharibu biashara ya hoteli yenyewe kwa kukimbiwa na wateja na hata itasababisha taarifa za binafsi za wateja kuvuja sambamba na kuhatarisha usalama wao binafsi kwani Wapiga picha wengi pamoja na Waandishi wa Habari wengi wao ni Majasusi au Mawakala wa Siri wa Makundi na Magenge ya Uhalifu, ni watu wanaohusika na Secret Physical Surveillance of their Targets. Not only that, but also some of the Photo-Journalists are the Secret/Undercover Agents for Abduction Squads and/or Hit Squads groups.
 
Wait for the day nikienda kwenye hizo hotel, incase nikikutana na hiyo changamoto nitarudi kuwaletea mrejesho 🤒😎
 
Back
Top Bottom