Hoja za Mawakili wa Serikali dhidi ya Adamoo

Sorry tunamwangalia mheshimiwa Jaji na tuna Imani naye ya kuwa atatenda haki. Ushahidi ameusikia na vilevile amepata faida ya kuwaona mashaidi kwa mamma walivyokuwa wakitoa ushahidi wao(deameaner of witnesses). Tumwombee Mungu amtangulie na atende haki.

Mahakama ni mahala pa wazi. Tunacho andika hapa ni vyote tulivyovisikia ambavyo tunaamini kila mtu kasikia akiwamo mheshimiwa Jaji.

Tunaamini si zaidi si pungufu labda utuonyeshe wapi tumepwaya.

Hatuna taabu na Jaji wala hatukuwa na taabu na hata yule aliyemwaga manyanga mapema.

Tuna taabu na mfumo. Tungefarijika mno kama tungekuwa kwenye mazingira ya katiba bora zaidi kuliko tuliyomo.

Kilio chetu kuhusu katiba mpya ni halisi.
 
ushahidi wa Adamoo ni maneno ya mfa maji, hayana maana hata kidogo, maneno yake yamejaa uzushi na uongo wa kunuka, yanafaa yapuuuzwe kabisaaaa.

Maneno ya Adamoo yamesikika. Yanathibitishwa kamili na shahidi wa 2 na wa 3 wa utetezi.

Adamoo alivamiwa RAU Moshi akatekwa. Waliomteka walichukua vyote alivyokuwa akapigwa na kuwekewa bastola, madawa ya kulevya na kuchukuliwa kikuku kupelekwa cental polisi Moshi.

Central polisi Moshi alipata kipigo kikali:

Utesaji wa Dola - Agenda kubwa Uchaguzi ujao

Yaliyomo humo yalimsibu Adamoo.

Kingai na Mahita hawajasema walichukua nini kwa Adamoo wala Ling'wenya.

Haiingii akilini kuwa walizunguka na mtuhumiwa Adamoo mitaani ambaye alikuwa mgeni Moshi kumtafuta Lijenje.

Mahita kathibitisha kuwa haijawahi kutumia PGO kwenye ukamataji wake wala haoni umuhimu wake.

Kwamba mbweni polisi ni salama zaidi kuliko central, Mahita kajikanyaga.

Haya ya kabatini si maelekezo ya akina Kingai? Yuko wapi Lijenje? Yuko wapi Luteni Urio?

Kuna mhalifu mzoefu hapa.

Kweli hao si Kingai na Mahita?
 
Je, wahuni ndani ya hii Serikali haramu hawatamtisha Ili kuingilia uhuru wake na kufanya maamuzi watakayo hao Wahuni!?
Ukitaka "utakatifu" ungali hai hapa duniani, hakuna wa kuuzidi huo wa huyu Jaji na kesi hii.

Kapewa fursa ya chee kuonyesha 'utakatifu' wake hata kama yeye siyo mtakatifu.

Ni shetani wa namna gani huyo anayeweza "kushinikiza" na kubadili jambo linaloonekana wazi kiasi hiki mbele za macho ya watu, sio hapa nyumbani tu, hata huko nje kupitia kwa mabalozi.
Hapa hakuna namna, bali ni kuachia tu.

Walisahau kuzuia aibu hii isifike mbele ya macho ya dunia. Sijui ilikuwaje wakajisahau kiasi hiki!
 
Mawakili wa Serikali wanadai Adamoo alikamatwa kwa mujibu wa sheria na tena akatoa maelezo kwa kina Kingai kwa mujibu wa sheria na bila shinikizo. Hivyo wanaitaka mahakama kuyapokea maelezo hayo kama ushahidi wa kuaminika dhidi ya watuhumiwa kwenye shauri la msingi.

Adamoo kaeleza mwenyewe namna alivyokamatwa. Yaliyotokea Moshi, alivyojikuta Tazara, hadi polisi Mbweni.

Shahidi #2 wa utetezi kaeleza mazingira ya ukamatwaji. Kilichotokea Moshi, alivyojikuta Tazara hadi Mbweni.

Shahidi wa pili alimwona Adamoo akipelekwa kwenye kinyumba cha mateso Moshi. Alimsikia sauti ya zege akilia. Alimwona akikokotwa kurejeshwa mahabusu. Kama alivyohisi zamu yake ya mateso na vipigo ilifuata baada tu ya Adamoo kurejeshwa mahabusu.

Shahidi wa pili aliambiwa na mmoja wa watesi wao kuwa kipigo cha Adamoo kilikuwa kikali zaidi kuwa bahati yake yeye alipata mwokozi.

Aliporudishwa rumande kwake alisema na Adamoo ambapo Adamoo alijibu - Mikazo (code ya kijeshi kuwa kateswa sana).

Kabla ya safari ya Dar shahidi #2 alimwona Adamoo akikokotwa kuletwa kwenye gari.

Tazara, shahidi wa pili alimsikia akilia na kumwona na kujiridhisha kuwa alikuwa ni luteni Urio ambaye alikuwa naye akiteswa.

Njiani kwenda Mbweni Shahidi wa pili akigongwa gongwa kichwani kwa bastola aliambiwa na Inspekta Mahita kuwa asipokubaliana na yao watamtupa pia kama walivyomtupa Moses Lijenje.

Mbweni Shahidi #2 anasema yeye na bila shaka Adamoo hawakupata chakula chochote rasmi kwa siku 10.

Adamoo na Shahidi wa 2, kote Tazara na Mbweni waliandikishwa kwa majina tofauti na yao. Johnson John alikuwa Commando Ling'wenya shahidi #2.

Mashahidi wote hawa wanasema waliletewa maelezo wakatakiwa kuyasaini wakiwa kwenye vitisho.

Shahidi #3 wa utetezi mke wa Adamoo anasema nyumbani kulisachiwa akiwa hayupo na baadhi ya vitu vikachukuliwa. Yeye na wenzake walifika vituo kadhaa vya polisi kuwatafuta wenza wao kwa utambulisho wa majina yao bila mafanikio.

Mama Ling'wenya angejua vipi mumewe ni Johnson John kama ile chanjo ya yetu pendwa ya J&J?

Segerea, shahidi wa tatu alisikia askari magereza wakisema mumewe yaani Adamoo ni yule mtu kwenye kabati.

Alipokuja Adamoo alikuwa kadhoofu, macho yamemdumbukia, akichechemea, akiwa na makovu mapya mikononi.

Adamoo alimwambia shahidi wa tatu kuwa alikuwa kateswa na kupigwa sana Moshi.

Mashahidi wa serikali wameshindwa kuieleza mahakama ni kwa nini washitakiwa walipelekwa Mbweni Polisi.

Mawakili wa serikali hawakatai kuwapo mtu akiteswa Moshi. Wanatilia shaka kuwa Ling'wenya anaweza kuwa alisikia mtu mwingine.

Pamoja na kuwa waliomba kesi kuahirishwa kumsubiria shahidi wao #4 Jumanne, katika hali ya kushangaza pamoja na kuwa Jumanne alionekana kwenye viunga vya mahakama siku ya shauri, mawakili wa serikali waliamua ghafla kufunga sehemu yao ushahidi.

Macho yote sasa kwa Jaji. Akitupilia mbali pingamizi hili maana yake kakubaliana na upande mashtaka kuwa yote ilikuwa kwa mujibu wa PGO.

Yuko wapi Moses Lijenje?
Kazi ipo .
 
Maneno ya Adamoo yamesikika. Yanathibitishwa kamili na shahidi wa 2 na wa 3 wa utetezi.

Adamoo alivamiwa RAU Moshi akatekwa. Waliomteka walichukua vyote alivyokuwa akapigwa na kuwekewa bastola, madawa ya kulevya na kuchukuliwa kikuku kupelekwa cental polisi Moshi.

Central polisi Moshi alipata kipigo kikali:

Utesaji wa Dola - Agenda kubwa Uchaguzi ujao

Yaliyomo humo yalimsibu Adamoo.

Kingai na Mahita hawajasema walichukua nini kwa Adamoo wala Ling'wenya.

Haiingii akilini kuwa walizunguka na mtuhumiwa Adamoo mitaani ambaye alikuwa mgeni Moshi kumtafuta Ling'wenya.

Mahita kathibitisha kuwa haijawahi kutumia PGO kwenye ukamataji wake wala haoni umuhimu wake.

Kwamba mbweni polisi ni salama zaidi kuliko central, Mahita kajikanyaga.

Haya ya kabatini si maelekezo ya akina Kingai? Yuko wapi Lijenje? Yuko wapi Luteni Urio?

Kuna mhalifu mzoefu hapa.

Kweli hao si Kingai na Mahita?
Adamo ndio kamtaja Mzee Mbowe kumtumia ktk Ugaidi.
ndio maana anapapatua ili maelezo yake yasipokelewe, ila kazidisha uongo hadi unanuka!!
eti anadai hajala siku 10!! hiyo ni dalili ya mtu muongo! na mzushi!
 
Ndiyo maana mwendazake hakutaka kuipeleka hii kesi mahakamani...alijua haitoboi..

Sijui nini kimewapata hawa jamaa kuisukuma mahakamani wakati hata mi wa la saba nishajua mzani umeegemea wap.

Kesi hii imeacha maswali mengi kuliko majibu - Wapi Komandoo Moses? Kwa nini JWTZ haina protocol ya kuwa protect askari wao..?

Ningependa sana kama adhabu hizi zingetolewa na JWTZ yenyewe kama wamekiuka viapo vyao. Comandoo si mtu wa kumtesa hovyo hovyo namna hii.
 
Hii kesi itaibua mengi sana. By now I think wanajuta kwanini mpaka leo bado inaendelea
watajuta walio kuwa wanapanga mipango haramu ya kuchafua Amani ya nchi.
vipo vya kuchezea kama kitambi chako, kidevu n.k lkn kamwe usijaribu kuchezea Amani ya nchi.
Amani ya nchi ni zaidi ya mboni ya jicho.
 
Amani ya nchi hii itaendelea kulindwa na kizazi na vizazi.....kamwe hatotokea wa kuchezea Amani ya nchi na akaachwa tu.
Amani ni ya watanzania wote wapenda amani na tutailinda kwa nguvu zetu zote.
 
Mawakili wa Serikali wanadai Adamoo alikamatwa kwa mujibu wa sheria na tena akatoa maelezo kwa kina Kingai kwa mujibu wa sheria na bila shinikizo. Hivyo wanaitaka mahakama kuyapokea maelezo hayo kama ushahidi wa kuaminika dhidi ya watuhumiwa kwenye shauri la msingi.

Adamoo kaeleza mwenyewe namna alivyokamatwa. Yaliyotokea Moshi, alivyojikuta Tazara, hadi polisi Mbweni.

Shahidi #2 wa utetezi kaeleza mazingira ya ukamatwaji. Kilichotokea Moshi, alivyojikuta Tazara hadi Mbweni.

Shahidi wa pili alimwona Adamoo akipelekwa kwenye kinyumba cha mateso Moshi. Alimsikia sauti ya zege akilia. Alimwona akikokotwa kurejeshwa mahabusu. Kama alivyohisi zamu yake ya mateso na vipigo ilifuata baada tu ya Adamoo kurejeshwa mahabusu.

Shahidi wa pili aliambiwa na mmoja wa watesi wao kuwa kipigo cha Adamoo kilikuwa kikali zaidi kuwa bahati yake yeye alipata mwokozi.

Aliporudishwa rumande kwake alisema na Adamoo ambapo Adamoo alijibu - Mikazo (code ya kijeshi kuwa kateswa sana).

Kabla ya safari ya Dar shahidi #2 alimwona Adamoo akikokotwa kuletwa kwenye gari.

Tazara, shahidi wa pili alimsikia akilia na kumwona na kujiridhisha kuwa alikuwa ni luteni Urio ambaye alikuwa naye akiteswa.

Njiani kwenda Mbweni Shahidi wa pili akigongwa gongwa kichwani kwa bastola aliambiwa na Inspekta Mahita kuwa asipokubaliana na yao watamtupa pia kama walivyomtupa Moses Lijenje.

Mbweni Shahidi #2 anasema yeye na bila shaka Adamoo hawakupata chakula chochote rasmi kwa siku 10.

Adamoo na Shahidi wa 2, kote Tazara na Mbweni waliandikishwa kwa majina tofauti na yao. Johnson John alikuwa Commando Ling'wenya shahidi #2.

Mashahidi wote hawa wanasema waliletewa maelezo wakatakiwa kuyasaini wakiwa kwenye vitisho.

Shahidi #3 wa utetezi mke wa Adamoo anasema nyumbani kulisachiwa akiwa hayupo na baadhi ya vitu vikachukuliwa. Yeye na wenzake walifika vituo kadhaa vya polisi kuwatafuta wenza wao kwa utambulisho wa majina yao bila mafanikio.

Mama Ling'wenya angejua vipi mumewe ni Johnson John kama ile chanjo ya yetu pendwa ya J&J?

Segerea, shahidi wa tatu alisikia askari magereza wakisema mumewe yaani Adamoo ni yule mtu kwenye kabati.

Alipokuja Adamoo alikuwa kadhoofu, macho yamemdumbukia, akichechemea, akiwa na makovu mapya mikononi.

Adamoo alimwambia shahidi wa tatu kuwa alikuwa kateswa na kupigwa sana Moshi.

Mashahidi wa serikali wameshindwa kuieleza mahakama ni kwa nini washitakiwa walipelekwa Mbweni Polisi.

Mawakili wa serikali hawakatai kuwapo mtu akiteswa Moshi. Wanatilia shaka kuwa Ling'wenya anaweza kuwa alisikia mtu mwingine.

Pamoja na kuwa waliomba kesi kuahirishwa kumsubiria shahidi wao #4 Jumanne, katika hali ya kushangaza pamoja na kuwa Jumanne alionekana kwenye viunga vya mahakama siku ya shauri, mawakili wa serikali waliamua ghafla kufunga sehemu yao ushahidi.

Macho yote sasa kwa Jaji. Akitupilia mbali pingamizi hili maana yake kakubaliana na upande mashtaka kuwa yote ilikuwa kwa mujibu wa PGO.

Yuko wapi Moses Lijenje?
Plc mnawafanyia hv wtz mwenzen ili mpate nn? Nadhan tunahitaji katiba mpya tuondokane na ccm
 
Mawakili wa Serikali wanadai Adamoo alikamatwa kwa mujibu wa sheria na tena akatoa maelezo kwa kina Kingai kwa mujibu wa sheria na bila shinikizo. Hivyo wanaitaka mahakama kuyapokea maelezo hayo kama ushahidi wa kuaminika dhidi ya watuhumiwa kwenye shauri la msingi.

Adamoo kaeleza mwenyewe namna alivyokamatwa. Yaliyotokea Moshi, alivyojikuta Tazara, hadi polisi Mbweni.

Shahidi #2 wa utetezi kaeleza mazingira ya ukamatwaji. Kilichotokea Moshi, alivyojikuta Tazara hadi Mbweni.

Shahidi wa pili alimwona Adamoo akipelekwa kwenye kinyumba cha mateso Moshi. Alimsikia sauti ya zege akilia. Alimwona akikokotwa kurejeshwa mahabusu. Kama alivyohisi zamu yake ya mateso na vipigo ilifuata baada tu ya Adamoo kurejeshwa mahabusu.

Shahidi wa pili aliambiwa na mmoja wa watesi wao kuwa kipigo cha Adamoo kilikuwa kikali zaidi kuwa bahati yake yeye alipata mwokozi.

Aliporudishwa rumande kwake alisema na Adamoo ambapo Adamoo alijibu - Mikazo (code ya kijeshi kuwa kateswa sana).

Kabla ya safari ya Dar shahidi #2 alimwona Adamoo akikokotwa kuletwa kwenye gari.

Tazara, shahidi wa pili alimsikia akilia na kumwona na kujiridhisha kuwa alikuwa ni luteni Urio ambaye alikuwa naye akiteswa.

Njiani kwenda Mbweni Shahidi wa pili akigongwa gongwa kichwani kwa bastola aliambiwa na Inspekta Mahita kuwa asipokubaliana na yao watamtupa pia kama walivyomtupa Moses Lijenje.

Mbweni Shahidi #2 anasema yeye na bila shaka Adamoo hawakupata chakula chochote rasmi kwa siku 10.

Adamoo na Shahidi wa 2, kote Tazara na Mbweni waliandikishwa kwa majina tofauti na yao. Johnson John alikuwa Commando Ling'wenya shahidi #2.

Mashahidi wote hawa wanasema waliletewa maelezo wakatakiwa kuyasaini wakiwa kwenye vitisho.

Shahidi #3 wa utetezi mke wa Adamoo anasema nyumbani kulisachiwa akiwa hayupo na baadhi ya vitu vikachukuliwa. Yeye na wenzake walifika vituo kadhaa vya polisi kuwatafuta wenza wao kwa utambulisho wa majina yao bila mafanikio.

Mama Ling'wenya angejua vipi mumewe ni Johnson John kama ile chanjo ya yetu pendwa ya J&J?

Segerea, shahidi wa tatu alisikia askari magereza wakisema mumewe yaani Adamoo ni yule mtu kwenye kabati.

Alipokuja Adamoo alikuwa kadhoofu, macho yamemdumbukia, akichechemea, akiwa na makovu mapya mikononi.

Adamoo alimwambia shahidi wa tatu kuwa alikuwa kateswa na kupigwa sana Moshi.

Mashahidi wa serikali wameshindwa kuieleza mahakama ni kwa nini washitakiwa walipelekwa Mbweni Polisi.

Mawakili wa serikali hawakatai kuwapo mtu akiteswa Moshi. Wanatilia shaka kuwa Ling'wenya anaweza kuwa alisikia mtu mwingine.

Pamoja na kuwa waliomba kesi kuahirishwa kumsubiria shahidi wao #4 Jumanne, katika hali ya kushangaza pamoja na kuwa Jumanne alionekana kwenye viunga vya mahakama siku ya shauri, mawakili wa serikali waliamua ghafla kufunga sehemu yao ushahidi.

Macho yote sasa kwa Jaji. Akitupilia mbali pingamizi hili maana yake kakubaliana na upande mashtaka kuwa yote ilikuwa kwa mujibu wa PGO.

Yuko wapi Moses Lijenje?
Mkuu naomba kuuliza. Kama ikibainika hawakukamatwa kwa mujibu wa sheria na yale maelezo ya polisi sio yao nini kitafuata? Je kesi itafutwa au wataandika maelezo upya??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom