- Thread starter
- #21
Sorry tunamwangalia mheshimiwa Jaji na tuna Imani naye ya kuwa atatenda haki. Ushahidi ameusikia na vilevile amepata faida ya kuwaona mashaidi kwa mamma walivyokuwa wakitoa ushahidi wao(deameaner of witnesses). Tumwombee Mungu amtangulie na atende haki.
Mahakama ni mahala pa wazi. Tunacho andika hapa ni vyote tulivyovisikia ambavyo tunaamini kila mtu kasikia akiwamo mheshimiwa Jaji.
Tunaamini si zaidi si pungufu labda utuonyeshe wapi tumepwaya.
Hatuna taabu na Jaji wala hatukuwa na taabu na hata yule aliyemwaga manyanga mapema.
Tuna taabu na mfumo. Tungefarijika mno kama tungekuwa kwenye mazingira ya katiba bora zaidi kuliko tuliyomo.
Kilio chetu kuhusu katiba mpya ni halisi.