Hoja ya Wasomi Kusoma VETA, Japo ni Hoja Chungu, Ndio Ukweli Wenyewe Kama Kidonge Kichungu, Ndicho Kinachotibu Homa!. VETA Ndio Tiba ya Joblessness!

Hoja ya Wasomi Kusoma VETA, Japo ni Hoja Chungu, Ndio Ukweli Wenyewe Kama Kidonge Kichungu, Ndicho Kinachotibu Homa!. VETA Ndio Tiba ya Joblessness!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,723
Wanabodi,
Hii hoja ya wasomi wahitimu wa vyuo vikuu kwenda kusoma VETA.
Shuhudia hizi Testimonials....

View: https://youtu.be/Rzr6coD9ihs?si=ZKYzt1V9FZFITszQ

kauli ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa, kuwa wahitimu wa Chuo Kikuu, wakasome VETA, imepokelewa kwa hisia tofauti, zenye sintofahamu fulani fulani.

Kauli hiyo imepokelewa vibaya na wasomi wa vyuo vikuu, wanaoringia usomi wao, hata kama usomi huo, hauwasaidii kitu, hivyo kitendo cha kuambia wakasome VETA, wanajiona kama wamedharauliwa!.

Wahadhiri wa vyuo vikuu nao wameipokea vibaya kauli hiyo, kwa kuona Waziri Mkuu, ni kama ametangazia taifa kuwa elimu ya chuo kikuu kwa sasa, ni kama haina maana tena, mambo yote ni elimu ya ufundi stadi inayotolewa na VETA, hivyo kuogopa kuitikiwa kwa wanafunzi badala ya kuomba udahili wa vyuo vikuu, bora waende VETA!.

Ukweli utabaki kuwa ukweli, watu wanaongoza kwa kutegemea ajira za maofisini, ni wasomi wa vyuo vikuu, wanaojiona wao ni wasomi sana, wamesema sana, na wanastahili kazi za maana, huku wakuwaona wahitimu wa VETA kama ni wale Darasa la saba, waliofeli na kushindwa kujiunga sekondari ndio wanategemea VETA!.

Hapa ukumbini, zimetolewa shuhuda 10 za wahitimu wa vyuo vikuu, waliokosa kazi baada ya kuhitimu, na walipoamua kujiunga VETA kusomea ufundi standi, sasa ni matajiri wakubwa, sio tuu kwa kujiajiri, bali pia kwa kuajiri wengine.

Ukweli mchungu kuhusu elimu yetu ya chuo kikuu inawafundisha watu kutegemea ajira, hivyo wahitimu wa vyuo vikuu wanaweza kukosa ajira kwa vile hazipo, lakini wahitimu wa VETA, hakuna kabisa hoja ya kukosa ajira, kwasababu wahitimu wa VETA, hawahitaji kuajiriwa, bali VETA inawajengea uwezo wa kujiajiri!.
Pascal
 
Nchi ya kufanya maamuzi kimihemko ya kisiasa na uchawa.

Sera ya serikali ni kuwa na wasomi wengi wenye level ya degree.

Hayo ndiyo yalikuwa malengo ya milenia 2025.

Sasa leo hii mmeshikia kidedea hoja ya hawa degree holders warudi VETA.

Kile walichonacho kichwani hawajakitumia, the mnataka wakaongeze kingine kichwani, for what purpose?
 
Vijana wengi wamepita veta bado hawana ajira. Inabidi hata gharama za kuanzisha kiwanda kwa vijana ipunguzwe. Pawe na bei ndogo elekezi maalum kwa ajili ya kununua kiwanja cha kiwanda. Bei iliyopo ipo juu mno


 
Vijana wengi wamepita veta bado hawana ajira. Inabidi hata gharama za kuanzisha kiwanda kwa vijana ipunguzwe. Pawe na bei ndogo elekezi maalum kwa ajili ya kununua kiwanja cha kiwanda. Bei iliyopo ipo juu mno


Msingi wa VETA ni kujiajiri sio kuajiriwa.

Kuajiriwa ni ziada.
 
Vijana wengi wamepita veta bado hawana ajira. Inabidi hata gharama za kuanzisha kiwanda kwa vijana ipunguzwe. Pawe na bei ndogo elekezi maalum kwa ajili ya kununua kiwanja cha kiwanda. Bei iliyopo ipo juu mno


Malaysia walikua wakiwapa graduates pesa wafanye kilimo na uwekezaji mwingine, maana msomi ukimfundisha kilimo atafanya kwa ufanisi mkubwa,kuwa graduate hakukufanyi uwe na misuli ya kifedha kuanza uwekezaji
 
Kama suala la Wahitimu wa Elimu ya Juu kuendelea kupewa uzito wa kulazimika kwenda VETA, ninashauri yafuatayo.

Wengi wa hao Wahitimu wa Degree wamesoma Kwa Mkopo.

Kwa aliyesoma degree ya miaka 3, wengi hujikuta wamekopeshwa sio Chini ya milioni 10.5

Aliyesoma degree ya miaka 4, sio Chini ya milioni 16.

Nashauri, badala ya kuwapa hiyo Mikopo na kuwapotezea muda wao, vyema wapewe hizo fedha kama Mkopo na wautumie kwa biashara.

Haipendezi Kijana amalize Chuo na kuendelea kuisotea ajira Kwa miaka 10 ama zaidi.

Ni kumchosha na kufanya wasomi wetu kuishi Kwa stress pasipo matumaini
 
Bado ni band aiding a leg which needs amputation..., Tatizo kubwa ni buying power kwahio no matter skill uliyonayo au huduma unayotoa kama watoaji wapo wengi na wanunuzi ni wachache na hawana hizo pesa mwisho wa siku ni kugawana umasikini na wala hicho utakachofanya hakitakidhi mahitaji...

The system is so rotten inahitaji overhaul na ushirikiano wa sekta zote ili kuhakikisha sustainability na mbaya zaidi tupo katika cross roads (Ni kama kipindi cha utumwa kilivyoisha baada ya industrial revolution), Ndio sasa hivi teknolojia inavyo overhaul capitalism as we know it (man power is no longer needed) na mbaya zaidi tunaongeza machungu hata kwa madogo ambayo tungeweza kuyatackle kwa urahisi kwenye hii dunia ambayo imekuwa kijiji....

 
Back
Top Bottom