Hivi kwanini kila jambo linajadiliwa kisiasa, tuache siasa. ukweli ni kwamba biashara ya ndege ni ngumu sana kwakuwa kampuni inahitaji kuwa na watumishi ww kutosha na wenye ujuzi ambao wanalipwa mshahara kila mwezi , lakini hakuna uhakika wa wateja ni mdogo, hapa nchini ni watu wachache sana wanaopanda ndege , kuwa na kampuni 3 za huduma hiyo inaweza kupelekea mojawapo kufa. Pia ni ukweli kuwa taasisi za serikali kufanya biashara ni gharama zaidi kuliko kampuni binafsi inatokana na taratibu za ajira ndani ya serikali, watumshi wanaajiriwa wengine na wanatakiwa kulipwa bila kujali tija inayopata kampuni, mfano hadi sasa kuna watumishi takribani 200 wa ATC wanalipwa japo hakuna ndege inayoruka, haya masuala yanatakiwa yaangaliwe sana. Mashirika ya ndege hata kwenye nchi zenye uchumi mkubwa huwa yanaendeshwa kwa hasara ila serikali inayalea kwa heshima tu ya nchi.