Hizi ndio ndege za Magufuli

Hizi ndio ndege za Magufuli

Biashara ya ndege ngumu, ilitakiwa labda serikali iingize mtaji PrecisionAir na kuwaachia wakurugenzi na wafanyakazi kuenesha shirika la ''kitanzania '' kibiashara. PrecisionAir wameonesha wanaweza lakini hawa Air Tanzania kuna mashaka makubwa.

Lakini hili la kununua ndege na kuikabidhi Air Tanzania nina shaka kubwa kama mradi huu utafanikiwa maana watatokea viongozi ''wanalazimisha wapewe ofa ya usafiri wa bure'', kutoa amri ndege isiruke kwa ratiba stahiki iwasubiri wao ''viongoz'i maana walichelewa kuamka na bado wapo nyumbani n.k

HAYA YAPO TZ TU! SIJUI KWANINI WATU HAWAJIFUNZI WABADILIKE.
 
Air Tanzania wanaweza kabisa iwapo serikali itakuwa makini kwa uongozi wa ATCL. Pia serikali ikubali shirika lijiendeshe lenyewe kibiashara ucwe ni mradi wa chama Tawala. Kukopa ticket kila kukicha.
 
Badala ya hizo mbili ndogo angenunua moja kubwa kuliko hivyo vitoroli
24f2a5420ec83b78c30ee9023a29f4fd.jpg
74ffbbd76ee1568c3c6b3a66ef7536cc.jpg
Picha ya juu na ya chini hazina uhusiano. A320 ni single aisle narrow bodied.
 
Yani kumbe ndege zlzokua znapigiwa makelele ndo izi zenye hadi panga boi kama helicopter?
 
Safari Ndefu Sana Hii Kuelekea Nchi Ya Asali Na Maziwa
 
Biashara ya ndege ngumu, ilitakiwa labda serikali iingize mtaji PrecisionAir na kuwaachia wakurugenzi na wafanyakazi kuenesha shirika la ''kitanzania '' kibiashara. PrecisionAir wameonesha wanaweza lakini hawa Air Tanzania kuna mashaka makubwa.

Lakini hili la kununua ndege na kuikabidhi Air Tanzania nina shaka kubwa kama mradi huu utafanikiwa maana watatokea viongozi ''wanalazimisha wapewe ofa ya usafiri wa bure'', kutoa amri ndege isiruke kwa ratiba stahiki iwasubiri wao ''viongoz'i maana walichelewa kuamka na bado wapo nyumbani n.k
Hayo matatizo yalishakuwepo siku za nyuma.
Ni kuyadhibiti tu kama tulivyothibiti safari za nje za watumishi hao hao wa serikali.
 
Badala ya hizo mbili ndogo angenunua moja kubwa kuliko hivyo vitoroli
24f2a5420ec83b78c30ee9023a29f4fd.jpg
74ffbbd76ee1568c3c6b3a66ef7536cc.jpg
Hii Jet engines ingebaguwa viwanja.Ndege kabila hii wanazo Fastjet,matokeo yake inatuwa katika viwanja vitano tu Tanzania.

Bombardier ina uwezo wa kutua Iringa,Kigoma,Tabora,Arusha,Songea,Mtwara,Mpanda,Nachingwea,Lindi na Dodoma.Hivyo kuongeza coverage ya utuwaji.Bombardier ndio haswaa mujarabu kwetu
 
Hii Jet engines ingebaguwa viwanja.Ndege kabila hii wanazo Fastjet,matokeo yake inatuwa katika viwanja vitano tu Tanzania.

Bombardier ina uwezo wa kutua Iringa,Kigoma,Tabora,Arusha,Songea,Mtwara,Mpanda,Nachingwea,Lindi na Dodoma.Hivyo kuongeza coverage ya utuwaji.Bombardier ndio haswaa mujarabu kwetu
Asante kwa ufafanuzi wenye maarifa
 
Ivi watu wanawashauri kweli?? Kwa dunia ya leo ya ushindani wa airbus na boeing nyie mnaleta ivi helcopter vya watoto ivyo nani atapanda kwa shirika kama air tanzania lililokufa? Badala mlete ndege za maana kushindana na soko dahhh mnaleta mchezo, sasa uko ni kupoteza pesa tuuuuu
kwa ushindani wa soko lip mkuu?
 
Kuwa na airbus sio shida, shida iko kwenye idadi ya viwanja ambavyo airbus itatua, kwa hapa nchini. Ni vichache sana, na ingi havina viwango. Airbus hazitui kwenye vile vya vumbi kama hizi bombadier amd ATR za Precision. Airbus ni kama hizi Fastjet, ambazo zinatua KIA, Songwe, Dar, Zanzibar na Mwanza tu. Labda zoezi la kuagiza ndege hizo liendane na upanuzi na uwekaji lami viwanja vyetu vilivyosalia, ili angalau kila Mtanzania atumie usafiri huu kufika kwake ama karibu na kwake. Ni hayo tu
Fastjet wenyewe hzo airbus znawachosha had wanampango wa kuziuza ili wanunue ndege ndogo zenye operation cost ndogo.
 
Safari Ndefu Sana Hii Kuelekea Nchi Ya Asali Na Maziwa

Lets wait and see ila uwezekano ni mkubwa sana kodi zetu zitapotea bure kwenye hili pia. Siamini kwamba tatizo la ATCL ni ukosefu wa ndege.

Kwa makusudi au kwa kutokuelewa wanasiasa wanadhani usafiri wa anga ni huduma kama zilivyo huduma za kijamii kama afya, elimu na nyinginezo kwamba ni wajibu wa serikali. Hilo ni kosa kubwa sana, Precision air wanapumulia mashine kwa sasa na sababu kubwa ni ushindani wa fast jet. Kenya airways walikuwa na kila aina ya ndege kabla hawajaanza kuziuza. Wameuza mpaka eneo lao Heathrow airport.

State haipaswi kufanya biashara ya usafiri wa anga bali ilipaswa kuwezesha private sector ili iweze kuwekeza zaidi kwenye hilo eneo. Model nzuri wa uwekezaji kwetu ilipaswa kuwa Ethiopin Airlines model na si Rwanda. Wengine yetu macho ila tunaomba shirika likiendeshwa kwa ruzuku (kodi zetu) tupewe taarifa.
 
Kuwateua tu mapilot waliobobea na wazoefu kuziendea hizo ndege uchakachuaji ulitokea hapo hapo bila kujali ambayo yangeweza kutokea.Nani mwenye uchungu na hii nchi na wananchi wake?Niliwahi kushuhudia ndege ikicheleweshwa uwanjani kumsubiri kibosile wa chama aliechelewa.Rubani kulazimishwa kurusha ndege ilhali masaa yake ya kuruka yakiwa yameisha na wakati mwingine matairi yakitakiwa kubadilishwa rubani analazimishwa kuwapeleka wajumbe wa chama Dodoma au Dar.Serikali kuchelewesha au kutolipa madeni ya kuwasafirisha maofisa wao waliosafirishwa kwa mikopo.Shirika kulazimishwa kuchangia masuala yasiyo na faida kwa shirika kama mwenge na wakati mwingine kukopwa bila mikopo hiyo tena isiyo rasmi kurejeshwa.Kwa ujumla sioni shirika lolote la serikali ya hii nchi lililopiga hatua zaidi ya kufa na kuuzwa kwa hela ya kununulia simu tatu za maana.
Mkuu kwa serikal hii, hyo nafasi hakuna, watu watalipa hakuna mkopo, na kumbuka ktk awam hii hainaga kibosile...

So hyo changamoto ya nan kacjelewa au den cjui makorokoro gani yalizikwa rasim oct.25 2015...

Baada ya hapo utawala huu hutasikia tena huo uzembe....
 
Lets wait and see ila uwezekano ni mkubwa sana kodi zetu zitapotea bure kwenye hili pia. Siamini kwamba tatizo la ATCL ni ukosefu wa ndege.

Kwa makusudi au kwa kutokuelewa wanasiasa wanadhani usafiri wa anga ni huduma kama zilivyo huduma za kijamii kama afya, elimu na nyinginezo kwamba ni wajibu wa serikali. Hilo ni kosa kubwa sana, Precision air wanapumulia mashine kwa sasa na sababu kubwa ni ushindani wa fast jet. Kenya airways walikuwa na kila aina ya ndege kabla hawajaanza kuziuza. Wameuza mpaka eneo lao Heathrow airport.

State haipaswi kufanya biashara ya usafiri wa anga bali ilipaswa kuwezesha private sector ili iweze kuwekeza zaidi kwenye hilo eneo. Model nzuri wa uwekezaji kwetu ilipaswa kuwa Ethiopin Airlines model na si Rwanda. Wengine yetu macho ila tunaomba shirika likiendeshwa kwa ruzuku (kodi zetu) tupewe taarifa.
Usafiri wa ndege ni muhim sn ktk maendeleo ya Nchi kaka .
Hasa hapa kwetu TANZANIA kutokana na ukubwa wa Nchi yetu na kaasi ya maendeleo tunayo taka kuyapata .

Nawametumia busara ATCL sn kutaka kuimarisha usafiri wa ndani kwa aina hii ya Ndege BOMBARDIER hizi ni Affordable na zinauwezo wa kufika sehem kubwa ya Nchi .

Chukua kaka mfano rahisi ww unafanya kazi DAR unataka kwenda KIGOMA unashughuli yako na Leo hii na urudi DAR leo .

Na ATCL wanatoa huduma ya usafiri every few Hours kwenda MIKOANI na affordable huoni ni njia sahihi ya kimaendeleo kaka.
 
Biashara ya ndege ngumu, ilitakiwa labda serikali iingize mtaji PrecisionAir na kuwaachia wakurugenzi na wafanyakazi kuenesha shirika la ''kitanzania '' kibiashara. PrecisionAir wameonesha wanaweza lakini hawa Air Tanzania kuna mashaka makubwa.

Lakini hili la kununua ndege na kuikabidhi Air Tanzania nina shaka kubwa kama mradi huu utafanikiwa maana watatokea viongozi ''wanalazimisha wapewe ofa ya usafiri wa bure'', kutoa amri ndege isiruke kwa ratiba stahiki iwasubiri wao ''viongoz'i maana walichelewa kuamka na bado wapo nyumbani n.k

Wambie waliokutuma ile hiyo post, waache upuuzi,.
 
N


Nimesoma vizuri and I still have the same comment! Viongozi kuomba kupanda Ndege Ni issue ya policies tu!!! Hakuna point hapo....
Vizuri umesimamia kile unachoamini, wanasahau hata hiyo staff ya Precision air ni zao la staff kutoka ATC, watz wanaweza ila tumejiweka katika pozi la hatuwezi maana haingii akilini, Mtz huyo huyo akiwa serikalini anakuwa chini ya performance alafu huyo huyo akienda sehemu nyingine anafanya (kinachotakiwa n watu wafanye kazi kwa mujibu wa taratibu na kusimamia maadili ya kazi)
 
Back
Top Bottom