Hivi vitu vina maana gani?

Hivi vitu vina maana gani?

Kinyume na hizo zinazo fanywa. Japo Biblia siamini, hakuna mafundisho ndani ya Biblia yanaelekeza namna ya uponyaji mnao fanyiwa na hao wanao itwa manabii.

Kingine mnatakiwa mjua Shetani anafanya vipi kazi, uwezo huo amepewa.

Huwezi kiwatibu watu katika mchanganyiko na wako uchi, ukasema hiyo ni tiba sahihi, sababu inaenda kinyume na mafundisho sahihi ya Mola.
We Kuna mtu umemuona uchi kwenye kongamano la Mwamposa?au neno UCHI limepoteza maana?
 
nikiomba mwenyewe nitaupata huonuponyaji?? au kuna watu maalum
Swali mujarabu, nami nitajaribu kukujibu.

Ili maombi yako yapokelewe, ni lazima uwe na imani kuwa hakika uliyoyaomba yamepokelewa. Ukisoma Marko 11:24 inasema 'Kwa hiyo nawaambieni, mnaposali na kuomba kitu, aminini kwamba mmekipokea, nanyi mtapewa'.

Kwa hiyo lazima uwe na uhakika wa kuwa maombi yako yatajibiwa. Usiweke shaka yeyote.

Kama una imani na umejiunganisha katika jina la Yesu Kristo, katika yote uombaye naye atakujibu.

Kwa nini Kuna watu wakikuombea unapona au kufanikiwa katika jambo lako?
Ukweli ni kuwa unaweza kujiombea mwenyewe na usifanikiwe katika hitaji lako. Ila Kuna watu wa Mungu wakikuombea hapo hapo tatizo lako linatatuliwa. Je, kwa nini? Ni kwa sababu watu wamepewa vipawa na Mungu. Na kukemea pepo wachafu nao wakawatii. Lakini pia, watu hao wamejiunganisha karibu zaidi na nguvu za Mungu. Na ndivyo, maombi Yao husikika kwa uharaka zaidi. Wana elimu ya ufahamu wa neno na imani yao i thabiti. Wanafahamu ni namna Gani waenende katika Kila tatizo.

Mungu hapokei maombi ya wenye dhambi. Ila mwenye dhambi akikubali na kumkiri Yesu kuwa Mwokozi wake, naye humsamehe dhambi zake zote na kumfanya mwana wake. Na ukishakuwa mwana wa Mungu, yote uombaye kwa imani utapata.
 
a087f448ba647cc5248401fe5674a7e9.jpg
 
sasa kwa comment yako hi unatakabkusema mwamposa anatumia nguvu za giza je ukipona unakua kundi gani, mbona watu kutwa wanatoa ushuhuda
Swali zuri.

Huo unakuwa umepewa mtihani, kutokana na mapito unayo pitia.

Shetani yupo kwa ajili ya kuwapoteza watu, na alipewa uwezo wa kufanya maajabu, ndiyo maana Kuna marafiki wa shetani na Marafiki wa Allah. Ukisoma vitabu utakutana na habari zao.

Mchawi anatibu na anaponya, ila ukimuamini unakuwa umepotea na kukufuru, hapa ndipo Kuna mtihani na kunahitaji Elimu.

Kwenye kutoa ushuhuda, hapa hakuna hoja na Watu wame yaongelea sana, waja wema au watu wakweli hawana mambo ya ushuhuda na huwa hawataki kujulikana wakitenda maajabi waa hawajitangazi, bali wapo na wafanya haya mambo.
 
Back
Top Bottom