Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,231
- 113,609
Rais wetu huyu mpya majuzi katangaza kuwa ataunda sijui kamati ya Corona. Bado sijaelewa hasa lengo na madhumuni ya hiyo kamati yatakuwa ni yepi. Sasa ni zaidi ya mwaka na ushee tokea dunia ikumbwe na hili janga.
Kwa jinsi mwelekeo wa hali unavyoonekana, janga hili ni kama vile linaelekea elekea ukingoni sasa hususan baada ya upatikanaji wa ‘chanjo’.
Licha ya hivyo, nadhani kwa sasa nitakuwa sawa nikisema kuwa ‘tunajua’ kiasi cha kutosha kuhusu ugonjwa huo.
Sasa, kama kweli Rais Samia ana nia ya dhati ya kuunda kamati ya corona, kwa nini mpaka sasa walau haonyeshi mfano kuwa kweli anautilia maanani ugonjwa huo kwa kuzingatia hata zile tahadhari zilizo za msingi kama kuvaa barakoa na kukaa ama kusimama mbalimbali na watu?
Leo kampokea waziri Amina Mohammed kutoka Kenya aliyekuwa katumwa na Rais Kenyatta. Bi. Amina kaingia ikulu ya Dar akiwa amevaa barakoa. Samia yeye hakuwa kavaa.
Waziri Mulamula naye mwanzoni alionekana kavaa. Baadaye wote walipokuwa wanaongea na waandishi wa habari, wote wakaonekana hawajazivaa.
Hivi ni kweli Rais Samia yupo serious au alikuwa anaongea tu siku ile ili kuridhisha baadhi ya watu kwa maneno tu lakini hakuwa na nia ya dhati kuonyesha kimatendo kuwa anamaanisha anachokisema?
Yeye kama raia namba moja si ndo anapaswa kuonyesha mfano wa kimatendo, au nakosea? Au Watanzania walio wengi hawana muda na matendo bali wanapenda tu kusikia maneno yawapendezayo masikioni mwao?
Kwa jinsi mwelekeo wa hali unavyoonekana, janga hili ni kama vile linaelekea elekea ukingoni sasa hususan baada ya upatikanaji wa ‘chanjo’.
Licha ya hivyo, nadhani kwa sasa nitakuwa sawa nikisema kuwa ‘tunajua’ kiasi cha kutosha kuhusu ugonjwa huo.
Sasa, kama kweli Rais Samia ana nia ya dhati ya kuunda kamati ya corona, kwa nini mpaka sasa walau haonyeshi mfano kuwa kweli anautilia maanani ugonjwa huo kwa kuzingatia hata zile tahadhari zilizo za msingi kama kuvaa barakoa na kukaa ama kusimama mbalimbali na watu?
Leo kampokea waziri Amina Mohammed kutoka Kenya aliyekuwa katumwa na Rais Kenyatta. Bi. Amina kaingia ikulu ya Dar akiwa amevaa barakoa. Samia yeye hakuwa kavaa.
Waziri Mulamula naye mwanzoni alionekana kavaa. Baadaye wote walipokuwa wanaongea na waandishi wa habari, wote wakaonekana hawajazivaa.
Hivi ni kweli Rais Samia yupo serious au alikuwa anaongea tu siku ile ili kuridhisha baadhi ya watu kwa maneno tu lakini hakuwa na nia ya dhati kuonyesha kimatendo kuwa anamaanisha anachokisema?
Yeye kama raia namba moja si ndo anapaswa kuonyesha mfano wa kimatendo, au nakosea? Au Watanzania walio wengi hawana muda na matendo bali wanapenda tu kusikia maneno yawapendezayo masikioni mwao?