Hivi pesa inapatikana wapi?

Hivi pesa inapatikana wapi?

Jirani yangu hapa ni Mbrazil alikuwa anabeba box miaka

Akapata mchongo huo kapiga trip tatu kafanikiwa zote
Ile nyumba aliyopanga kainunua na amenunua Pub na Hotel
Amesema kama maisha ndio haya basi nimeyafikia
Harudi tena kwenye sembe
Watoto wamekuwa sasa
Maisha haya
Pm namba ya huyo jirani yako mkuu
 
Hivi unaelewa kwanza ninachokiongelea wewe kwenye mpira huwezi kutoboa Kwa huo umri we umekazana mtafutaji mara sijui nini wewe nenda Kabebe sembe
Hapo nimekutolea mfano wa umri

Miaka 30 ni mingi sana kuna baadhi ya madili huwezi fanya ndio maana nikasema umri unanitupa mkono nikiwa fukara hohehahe
 
Nimeenda migodini nimepiga veni na kanyero za kutosha sijapata pesa

Nimeingia porini kata miti na mbao sikupata pesa

Nimesoma hadi chuo pia olaa

Biashara ya uwakala, mitumba, viatu, viwanja, nyumba kote sijapata pesa

Oya pesa inapatina wapi mazee
Kosa lako ulikuwa unatumia nguvu bila mipango ndipo ulipokuwa unafeli.
Yaani wewe ulikuwa unafanya kitu kwa kukariri au kwa kusikia watu wengine kwamba mgodini kuna pesa sana kisha unakurupuka unaenda baadae unagundua hakuna hela.
Kumbe pesa iko mahali popote ulipo ukiweza kuchekecha ni kitu gani ni changamoto katika maeneo ulipo.
 
Naomba nijibiwe hili swali kwa weledi bila kejeli wala mzaha

Hakuna mtu hapendi pesa wadau na kila siku watu hujituma kutafuta pesa sasa pesa huwa inapatikana wapi?

Naomba nieleweke nikisema pesa simaanishi vipesa vya kula namaanisha pesa nyingi

Karibuni
Sio kila mwenye Pesa ni pesa zingine ni za mashetani .
 
Kwahiyo kaacha biashara ya sembe
Zamani sana, ukimuona ana Bentley lake na wife anasukuma Range
Alipofanikiwa tu akanunua hizo biashara
Arudi tena adakwe wakati kaishafikia malengo

Wengine huwa wana tamaa mpaka washikwe, kila mara anasema hii ya mwisho
Anachezea hela zikiisha anarudi tena mwisho ananyongwa
 
Zamani sana, ukimuona ana Bentley lake na wife anasukuma Range
Alipofanikiwa tu akanunua hizo biashara
Arudi tena adakwe wakati kaishafikia malengo

Wengine huwa wana tamaa mpaka washikwe, kila mara anasema hii ya mwisho
Anachezea hela zikiisha anarudi tena mwisho ananyongwa
Yaani kweli ata tapeli anakamatwa Kwa ajili ya tamaa tu
 
Kosa lako ulikuwa unatumia nguvu bila mipango ndipo ulipokuwa unafeli.
Yaani wewe ulikuwa unafanya kitu kwa kukariri au kwa kusikia watu wengine kwamba mgodini kuna pesa sana kisha unakurupuka unaenda baadae unagundua hakuna hela.
Kumbe pesa iko mahali popote ulipo ukiweza kuchekecha ni kitu gani ni changamoto katika maeneo ulipo.
Kwenye kusaka pesa nguvu na akili vyote hutumika na lazima uingie kwenye bato uone kama kweli
 
Utatoboa kama ukituliza kichwa.
Wewe unaonekana ni aina ya watu wenye pupa au kwa lugha nyingine mihemko ukiwa mtu wa hivi kutoboa ni ngumu.
Kutoboa kunahitaji watu wenye creativity,focus,consistency sio kurukia mambo juu kwa juu.
Kwahiyo wanihakikishia baada ya miaka kumi mbele nitakuwa nimetoboa
 
Back
Top Bottom