Hivi pesa inapatikana wapi?

Hivi pesa inapatikana wapi?

Utatoboa kama ukituliza kichwa.
Wewe unaonekana ni aina ya watu wenye pupa au kwa lugha nyingine mihemko ukiwa mtu wa hivi kutoboa ni ngumu.
Kutoboa kunahitaji watu wenye creativity,focus,consistency sio kurukia mambo juu kwa juu.
Nifungulie makufuli ya hazina mkuu nishakua creative sana badala yake napata vicent vya kula tu
 
Nipe mfano wa creativity uliyoifanya na ulidumu nayo kwa muda gani kisha nitakwambia ulikosea wapi
Mimi ni miongoni mwa waanzilishi wa vibanda vya tigo pesa na huduma mtandao kijijini kwetu hadi saizi sijatoboa

Ukija ofisini utagundua ubunifu wangu wa ofisi na utoaji huduma lakini kutusua ni ndoto, ni nyingi sana mkuu
 
Kwenye hicho kijiji ulichoweka kina wakazi wangapi kwa makadirio?na shughuli zao za kiuchumi zinazowaingizia kipato ni zipi?Kama shughuli zao ni kilimo tu cha kawaida means pesa zao zitakuwa ni za msimu hapo kutoboa ni ngumu
Mimi ni miongoni mwa waanzilishi wa vibanda vya tigo pesa na huduma mtandao kijijini kwetu hadi saizi sijatoboa

Ukija ofisini utagundua ubunifu wangu wa ofisi na utoaji huduma lakini kutusua ni ndoto ni nyingi sana mkuu
 
Kwenye hicho kijiji ulichoweka kina wakazi wangapi kwa makadirio?na shughuli zao za kiuchumi zinazowaingizia kipato ni zipi?Kama shughuli zao ni kilimo tu cha kawaida means pesa zao zitakuwa ni za msimu hapo kutoboa ni ngumu
Kwa sasa nipo mjini mkuu naendelea na ubunifu kijijini niliona ni ngumu kutoboa
 
Nmeanza kwa kutatua changamoto, nlienda huo mtaa una shule tatu ila hamna stationery nlihitaji copy hakuna yani stationery ipo mbali mno kwahiyo nikaweka stationery hapo.....cha kwanza hicho.
Pia hakukuwa na biashara za miamala kabisa huduma ipo mbali nikaweka pia, Naendelea na kutatua changamoto zingine pia ambazo ndio fursa zenyewe.

Umeelewa sasa nlichoandika pale juu???
Wewe ni genius
 
Nataka pesa halisi either paper money au salio ziwe nyingi mkuu
Hata hizo za ndagu ni pesa halisi lakini zina masharti yake, humu watu watakupiga porojo nyingi lakini pesa nyingi unazozitaka kuzipata sio rahisi kiivyo.

Nina mifano mingi tu lakini uwe tayari kujikana nafsi na usiwe na roho ya huruma hapo ndo utazikuta hizo hela nyingi unazozitaka... Kama ww ni muoga na huna roho ngumu endelea kutafuta hela za kula tu!
 
Naomba nijibiwe hili swali kwa weledi bila kejeli wala mzaha

Hakuna mtu hapendi pesa wadau na kila siku watu hujituma kutafuta pesa sasa pesa huwa inapatikana wapi?

Naomba nieleweke nikisema pesa simaanishi vipesa vya kula namaanisha pesa nyingi

Karibuni
Pesa utaipata ulipoiweka, kama uliweka kwenye kibubu utaikuta kwenye kibubu, kama uliiweka benki utaikuta benki.
 
Back
Top Bottom