Hivi ni majukumu au ubinafsi unaofanya watu wasiwe karibu kama zamani?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,784
Leo nimewaza sana,
Nakumbuka miaka ya zamani tunakua, kulikuwa na ukaribu mkubwa sana baina ya watu. Ilikuwa inafika kipindi watu wa mtaa mzima tulikuwa tunafahamiana vizuri kabisa hata kutembeleana. Hili lilikuwepo kuanzia mitaa ya uswahilini, hadi uzunguni.

Kuanzia shuleni, tulikuwa tunasoma na watoto wa wakubwa, na hata siku za sherehe kama Brithday, Eid, Christmas, Easter, New-Year n.k tulikuwa tunakutana bila kuangalia mtoto wa nani ni nani. Lakini mbali na watoto, hata wazee walikuwa na ukaribu sana. Unaweza kumuona mtu kwenye taarifa ya habari, lakini siku za mwisho wa wiki unakuta kaja kwenu kusalimiana na wazazi wako na wanaongea hata masaa.

Nakumbuka utoto wangu tulikuwa tukienda kwenye nyumba za wakubwa fulani hivi, weusi, wahindi, waarabu hata wazungu na kucheza na watoto wao bila kuzuizi chochote kile. Huu uhusiano haukuwa kamili (There were prejudices, here and there) lakini watu tuliweza kuvumiliana na kuchukuliana sana. Tumecheza mpira wote, tumeangalia televisheni wote, tumecheza michezo wote, tumejisomea wote n.k

Hili lilitusaidia kutengeneza ukaribu, urafiki na kufahamiana ambako kwa namna moja au nyingine kumekuwa na manufaa sana hadi leo hii. Tumesaidiana na kubebana kama ndugu kwenye shida na raha. Nadhani hili ndilo lengo kubwa la ujirani mwema.

Kinachonishangaza kidogo ni kwamba, leo hii ambako watu wengi wameelimika na kuwa na vipato vya kati ilitegemewa kwamba ndiyo tutakuwa na ukaribu na mahusiano mazuri. Lakini imefikia kipindi jirani wa nyumba moja hamfahamu hata mwingine, watu tunaogopana na kukwepana. Kila mtu anataka kuwa kivyake na watoto wake. Hata ndugu wa damu kila mtu anakufa kivyake. NO FAMILY REUNIONS, NO FIDELITY, NO FRATERNITY.

Mtoto anatoka International School tokea asubuhi mpaka jioni, akifika nyumbani anapewa Ipad, Video Game, Laptop au TV imeunganishwa na Netflix tayari anakaa peke yake hadi kesho tena. Huu ndiyo unakuwa mfumo wake wa maisha 24/7/365. Kibaya zaidi watoto wetu siku hizi hata KISWAHILI hawajui vizuri kabisa lakini wazazi hatustuki kabisa.

Wazazi tunafurahia (We are very proud) maisha ambayo watoto wetu wanaishi, tunaona haya ndiyo mafanikio yenyewe kwasababu wengi hatukuishi haya maisha. Wengi wetu tuliishi maisha ya kidumu, jembe, ufagio, viboko na kufanya kazi za nyumbani, hivyo tunahisi yale maisha hayakuwa mazuri. Kanuni nzima ya adhabu na nidhamu kwa mtoto limekuwa jambo la kishamba kabisa(Antiquated Medieval Madness). Mtu anayewaza kutoa adhabu ni mshezi tu.
HAPA NAWAZA TU, NAWEZA NISIWE NIKO SAHIHI.

Mwisho kabisa, watoto wetu wanasoma mitaala ya GCSE, moja ya mitaala mizuri kabisa ambayo inawawezesha kuwa na vyeti vizuri mbavyo huwapa nafasi nzuri kwenye soko la ajira. Lakini nimeangalia kwa macho yangu kama mzazi na kufahamu kwamba mbali na watoto kufahamu mambo mengi sana (General Knowledge), Ufahamu na Uelewa sahihi(Proper Understanding & Comprehension) kuhusu mazingira yao wanakuwa hawana. THEY'RE SIMPLY DETACHED FROM REALITY.....

Nawaza sana hiki kizazi tunachokitengeneza kitakuwaje huko mbele na sipati majibu. Aidha ni woga wangu tu, AU uelewa wangu mdogo, AU bado naishi siku za kale bila kukubali kwamba dunia imebaridika (Nostalgic and Trapped in the past). Lakini yote tisa, kizazi hichi cha kisasa ni cha kisasa haswaaaaa.
 
Mingine ni mitego,Tena mitego haswaaa,familia zinajichanganya bila kufahamu...
Hii ni tanzu haswa lakini nadhani madhara yake tutakuja kuyaona siku za mbeleni huko. Kibaya zaidi ni kwamba hata sehemu kubwa ya malezi mtoto inafanywa na mwalimu wa shule na siyo mzazi. Kuna dada moja siku tunapeleka watoto shule amekuja asubuhi anahema kavaa nigh-dress yake anatafuta watoto. Huyu mwanamke na mume wake ni moja kati ya watu wenye kazi nzuri na mishahara minono.

Kilichotokea ni kwamba yeye alirudi nyumbani katoka kazini, kama kawaida akapita moja kwa moja akaenda kulala. Asubuhi anamwambia dada wa kazi hebu waandae watoto, dada wa kazi kajibu mbona jana hukuwaleta nyumbani. Mama akaanza kukaripa kwa dada wa kazi, kumbe alipigiwa sana simu shuleni lakini haipatikani, dada wa kazi naye hajui chochote kile.

Bahati nzuri kule shuleni baada ya kuona wale watoto hawajachukuliwa na wanalia sana na simu za wazazi hazipatikani, Mkurugenzi akaamua kuwapeleka watoto kwenye mabweni ya shule wakalala huko. Mama yao ndiyo kaja asubuhi kachanganyikiwa, anasema alikuwa ametingwa sana na majukumu. Siku ile baada ya kuona lile tukio nikawaza sana na kuwaonea wivu watu wanaoishi maisha ya kawaida lakini wako na familia zao wakicheka.

Nikajisemea kama Mfalme Suleimani, MAISHA YETU NI MAFUPI NA YEMAJAA UBATILI MTUPU.
 
Leo nimewaza sana,
Nakumbuka miaka ya zamani tunakua, kulikuwa na ukaribu mkubwa sana baina ya watu. Ilikuwa inafika kipindi watu wa mtaa mzima tulikuwa tunafahamiana vizuri kabisa hata kutembeleana. Hili lilikuwepo kuanzia mitaa ya uswahilini, hadi uzunguni.

Kuanzia shuleni, tulikuwa tunasoma na watoto wa wakubwa, na hata siku za sherehe kama Brithday, Eid, Christmas, Easter, New-Year n.k tulikuwa tunakutana bila kuangalia mtoto wa nani ni nani. Lakini mbali na watoto, hata wazee walikuwa na ukaribu sana. Unaweza kumuona mtu kwenye taarifa ya habari, lakini siku za mwisho wa wiki unakuta kaja kwenu kusalimiana na wazazi wako na wanaongea hata masaa.

Nakumbuka utoto wangu tulikuwa tukienda kwenye nyumba za wakubwa fulani hivi, weusi, wahindi, waarabu hata wazungu na kucheza na watoto wao bila kuzuizi chochote kile. Huu uhusiano haukuwa kamili (There were prejudices, here and there) lakini watu tuliweza kuvumiliana na kuchukuliana sana. Tumecheza mpira wote, tumeangalia televisheni wote, tumecheza michezo wote, tumejisomea wote n.k

Hili lilitusaidia kutengeneza ukaribu, urafiki na kufahamiana ambako kwa namna moja au nyingine kumekuwa na manufaa sana hadi leo hii. Tumesaidiana na kubebana kama ndugu kwenye shida na raha. Nadhani hili ndilo lengo kubwa la ujirani mwema.

Kinachonishangaza kidogo ni kwamba, leo hii ambako watu wengi wameelimika na kuwa na vipato vya kati ilitegemewa kwamba ndiyo tutakuwa na ukaribu na mahusiano mazuri. Lakini imefikia kipindi jirani wa nyumba moja hamfahamu hata mwingine, watu tunaogopana na kukwepana. Kila mtu anataka kuwa kivyake na watoto wake. Hata ndugu wa damu kila mtu anakufa kivyake. NO FAMILY REUNIONS, NO FIDELITY, NO FRATERNITY.

Mtoto anatoka International School tokea asubuhi mpaka jioni, akifika nyumbani anapewa Ipad, Video Game, Laptop au TV imeunganishwa na Netflix tayari anakaa peke yake hadi kesho tena. Huu ndiyo unakuwa mfumo wake wa maisha 24/7/365. Kibaya zaidi watoto wetu siku hizi hata KISWAHILI hawajui vizuri kabisa lakini wazazi hatustuki kabisa.

Wazazi tunafurahia (We are very proud) maisha ambayo watoto wetu wanaishi, tunaona haya ndiyo mafanikio yenyewe kwasababu wengi hatukuishi haya maisha. Wengi wetu tuliishi maisha ya kidumu, jembe, ufagio, viboko na kufanya kazi za nyumbani, hivyo tunahisi yale maisha hayakuwa mazuri. Kanuni nzima ya adhabu na nidhamu kwa mtoto limekuwa jambo la kishamba kabisa(Antiquated Medieval Madness). Mtu anayewaza kutoa adhabu ni mshezi tu.
HAPA NAWAZA TU, NAWEZA NISIWE NIKO SAHIHI.

Mwisho kabisa, watoto wetu wanasoma mitaala ya GCSE, moja ya mitaala mizuri kabisa ambayo inawawezesha kuwa na vyeti vizuri mbavyo huwapa nafasi nzuri kwenye soko la ajira. Lakini nimeangalia kwa macho yangu kama mzazi na kufahamu kwamba mbali na watoto kufahamu mambo mengi sana (General Knowledge), Ufahamu na Uelewa sahihi(Proper Understanding & Comprehension) kuhusu mazingira yao wanakuwa hawana. THEY'RE SIMPLY DETACHED FROM REALITY.....

Nawaza sana hiki kizazi tunachokitengeneza kitakuwaje huko mbele na sipati majibu. Aidha ni woga wangu tu, AU uelewa wangu mdogo, AU bado naishi siku za kale bila kukubali kwamba dunia imebaridika (Nostalgic and Trapped in the past). Lakini yote tisa, kizazi hichi cha kisasa ni cha kisasa haswaaaaa.
Sisi tunaishi kwenye heavily gated affluent neighborhood tunapenda sana faragha na hii inazuia na kuwadhibitisana mitambo ya umbea kutufuatiliafuatilia maisha yetu.
 
Kwa zamani ilikua wote mmekua pamoja na wengi wazawa wa hapo ndio maana ikawa rahisi kufahamiana kiundani + kushirikiana tofauti na saivi pilika ni nyingi watu wengi wanahangaika kutafuta maisha wengine wamehama mtaa/mkoa na huko walikohamia wamekutana na watu wapya na inakua ngumu kuleta mazoea mengi kwa stranger.
 
Sisi tunaishi kwenye heavily gated affluent neighborhood tunapenda sana faragha na hii inazuia na kuwadhibitisana mitambo ya umbea kutufuatiliafuatilia maisha yetu.
Nimekaa Oyster-bay na Masaki, and I tell you it doesn't get affluent than here. Kama ni umbeya, huku kuna umbeya hatari, tena First-Class, (Top-Notch) siyo ule wa vijiwe vya kahawa, maana serikali yote ilikuwa huku. Lakini mbali na yote haya, miaka ya 80's na 90's tulikuwa na ujirani mwema sana, iwe ni kwenye jumuiya za kidini, sherehe au misiba.

We have just grown selfish........
 
Kwa zamani ilikua wote mmekua pamoja na wengi wazawa wa hapo ndio maana ikawa rahisi kufahamiana kiundani + kushirikiana tofauti na saivi pilika ni nyingi watu wengi wanahangaika kutafuta maisha wengine wamehama mtaa/mkoa na huko walikohamia wamekutana na watu wapya na inakua ngumu kuleta mazoea mengi kwa stranger.
Inawezekana, japo naomba niongelee mimi kwa upande wangu. Nakumbuka niliwahi kwenda kuishi mkoa mmoja hivi na wazazi wangu, tukawa tunaishi kwenye mtaa wa uzunguni kidogo. Ulikuwa umejaa watu wengi wenye asili ya kiashia. Lakini baada ya muda mfupi walikuwa ni marafiki wakubwa sana wa mama yangu.

Wanawake wa kiarabu huwa hawatoki sana kwao, lakini ikifika wikendi walikuwa wanakuja nyumbani kwa maza na wanapika misosi ya hatari. Watoto wao nimecheza nao sana na walikuwa wakitoka tu shule, hao hapo nyumbani kwetu. Siku za Eid wamama wa mtaani wanapika chakula cha pamoja na mtaa mzima tunakaribishana. Krismasi nayo vivyo hivyo.....

Nadhani kuna sehehmu tumepotoka na kujikwaa......
 
Kweli maisha yanabadilika sana nakumbuka zamani sikukuu hiz xmass mtu kupika na kuita majirani mkale pamoja ilikuwepo sana,ila siku hizi dah kila mtu kivyake.

Nadhani pia matumizi ya simu janja yamechangia sana maana unaweza kuwa mtaani huna rafiki lakini kwenye social network una washkaji wengi balaa ambao hujawahi hata kuonana nao na tunaona cool tu.
Maana hata mkikutana sasa hivi hamna kinachoendelea mmekaa watu watano kila mtu ameinamia simu anachat au anaperuzi tafrani kwa kweli.
 
Nimekaa Oyster-bay na Masaki, and I tell you it doesn't get affluent than here. Kama ni umbeya, huku kuna umbeya hatari, tena First-Class, (Top-Notch) siyo ule wa vijiwe vya kahawa, maana serikali yote ilikuwa huku. Lakini mbali na yote haya, miaka ya 80's na 90's tulikuwa na ujirani mwema sana, iwe ni kwenye jumuiya za kidini, sherehe au misiba.

We have just grown selfish........
Wengi hawajui zamani O'bay nyumba nyingi hazikuwa na fence,unakatiza nyumba kwa nyumba mitaa mitatu....watoto,wazee wote wanafahamiana. Sasa hivi kuna maukuta kama gereza na watu wanaona sifa kutokufahamiana.
 
Inawezekana, japo naomba niongelee mimi kwa upande wangu. Nakumbuka niliwahi kwenda kuishi mkoa mmoja hivi na wazazi wangu, tukawa tunaishi kwenye mtaa wa uzunguni kidogo. Ulikuwa umejaa watu wengi wenye asili ya kiashia. Lakini baada ya muda mfupi walikuwa ni marafiki wakubwa sana wa mama yangu.

Wanawake wa kiarabu huwa hawatoki sana kwao, lakini ikifika wikendi walikuwa wanakuja nyumbani kwa maza na wanapika misosi ya hatari. Watoto wao nimecheza nao sana na walikuwa wakitoka tu shule, hao hapo nyumbani kwetu. Siku za Eid wamama wa mtaani wanapika chakula cha pamoja na mtaa mzima tunakaribishana. Krismasi nayo vivyo hivyo.....

Nadhani kuna sehehmu tumepotoka na kujikwaa......
Zamani maisha yalikua mazuri watu walisocialize vzuri na mkijenga urafiki unakua ni urafiki hasa na wenye faida tofauti na sasa.

Pia siku za sherehe mtajumuika familia + marafiki wamama watapika tutakula na kuenjoy + stories kibao but nowdays sijui ndio utandawazi kukiwa na sherehe mtu atabebana na familia yake anaenda kuenjoy restaurant/hotelin basi imetoka.

I miss the good old days kwakweli.
 
Back
Top Bottom