Wazazi mngejua adha wanazopata watoto wenu katika daladala mngetamani kuwahamisha shule za karibu

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
3,520
6,503
Huenda wakati mwingine kama wazazi huwa tunapenda wenetu wasome katika shule zenye majina makubwa au zile ambazo ni maarufu hapa jijini dar es salaam, lakini kiukweli maumivu ya usafiri wa daladala wanapata watoto wetu.

Huwa wananyanyaswa Sana na makondakta, huzuiwa kupanda Magari,kama tunavyojua sio makonda wote ni wenye kujali, wengi wao hawana huruma Kwa hawa malaika wa Mungu, inafika kipindi watoto wanalazimisha kupanda hivyo hivyo na kuhatarisha usalama wao.

Jana nikiwa posta mida ya saa kumi na moja jioni, watoto wakiwa wanapanda magari ya kwenda gongo la mboto, niliona watoto wadogo wakilazimisha kupanda daladala huku likiwa linaondoka na kuhatarisha usalama wao, huwezi ukawalaumu hawa watoto kwakuwa wamechoka na wanataka kwenda nyumbani kupumzika.

Kutokana na changamoto wanazo kutana nazo kila siku imewafanya wawe ngangali kama watu wazima vile, unakuta vitoto vya darasa la kwanza au la pili vinakomaa na watu wazima kupanda katika daladala na wakati huo huo wanapambana na roho mbaya za makondakta wasio na huruma.

Utavikuta maskini vinakimbilia basi hili mara lile na kote huko saa nyingine vinakataliwa, utaviona vinyonge na vyenye kukata tamaa.

Wazazi, serikali ilipoamua kujenga shule za kata lengo lilikuwa kuwapunguzia watoto adha ya kwenda kusoma mbali na kuleta ahueni katika harakati nzima za kutafuta elimu yao , walau basi wangekuwa watoto wa sekondari sio mbaya kwanza ni wakubwa na wanajielewa, lakini hawa wa msingi ni mtihani sana kwao.

Ebu tuwaonee huruma hawa wenetu kwa kuwatafutia shule za karibu ili kuwapunguzia adha ya usafiri ukichukulia wengi wetu hatuna uwezo wa kulipia mabasi maalumu ya wanafunzi.

Mbona wengi wetu huko miaka ya nyuma tulisoma shule za kawaida tu na tulimaliza shule za msingi na kuendelea na elimu ya sekondari bila shida yoyote?

Ukitaka uyaamini haya ninayosema kwa wewe mzazi ambaye hujapata ona adha ya usafiri ambayo wanapata wenetu ebu siku moja nenda kituo cha daladala uone Show yake, ndo utajua purukushani ambazo wanakutana nazo watoto wetu.

Ngoja niishie hapa naona kama kalamu yangu inaisha wino na bahati mbaya usiku huu maduka mengi yamefungwa hivyo si rahisi kupata peni nyingine.

Ni hayo tu!
 
Huenda wakati mwingine kama wazazi huwa tunapenda wenetu wasome katika shule zenye majina makubwa au zile ambazo ni maarufu hapa jijini dar es salaam, lakini kiukweli maumivu ya usafiri wa daladala wanapata watoto wetu.

Huwa wananyanyaswa Sana na makondakta, huzuiwa kupanda Magari,kama tunavyojua sio makonda wote ni wenye kujali, wengi wao hawana huruma Kwa hawa malaika wa Mungu, inafika kipindi watoto wanalazimisha kupanda hivyo hivyo na kuhatarisha usalama wao.

Jana nikiwa posta mida ya saa kumi na moja jioni, watoto wakiwa wanapanda magari ya kwenda gongo la mboto, niliona watoto wadogo wakilazimisha kupanda daladala huku likiwa linaondoka na kuhatarisha usalama wao, huwezi ukawalaumu hawa watoto kwakuwa wamechoka na wanataka kwenda nyumbani kupumzika.

Kutokana na changamoto wanazo kutana nazo kila siku imewafanya wawe ngangali kama watu wazima vile, unakuta vitoto vya darasa la kwanza au la pili vinakomaa na watu wazima kupanda katika daladala na wakati huo huo wanapambana na roho mbaya za makondakta wasio na huruma.

Utavikuta maskini vinakimbilia basi hili mara lile na kote huko saa nyingine vinakataliwa, utaviona vinyonge na vyenye kukata tamaa.

Wazazi, serikali ilipoamua kujenga shule za kata lengo lilikuwa kuwapunguzia watoto adha ya kwenda kusoma mbali na kuleta ahueni katika harakati nzima za kutafuta elimu yao , walau basi wangekuwa watoto wa sekondari sio mbaya kwanza ni wakubwa na wanajielewa, lakini hawa wa msingi ni mtihani sana kwao.

Ebu tuwaonee huruma hawa wenetu kwa kuwatafutia shule za karibu ili kuwapunguzia adha ya usafiri ukichukulia wengi wetu hatuna uwezo wa kulipia mabasi maalumu ya wanafunzi.

Mbona wengi wetu huko miaka ya nyuma tulisoma shule za kawaida tu na tulimaliza shule za msingi na kuendelea na elimu ya sekondari bila shida yoyote?

Ukitaka uyaamini haya ninayosema kwa wewe mzazi ambaye hujapata ona adha ya usafiri ambayo wanapata wenetu ebu siku moja nenda kituo cha daladala uone Show yake, ndo utajua purukushani ambazo wanakutana nazo watoto wetu.

Ngoja niishie hapa naona kama kalamu yangu inaisha wino na bahati mbaya usiku huu maduka mengi yamefungwa hivyo si rahisi kupata peni nyingine.

Ni hayo tu!
Kina J Mhagama wanadai bado ma DED na viongozi wengine serikalini hawana V8 za kutosha!
Ukumbuke karibu watoto wote wa hawa vigogo hawatumii usafiri wa daladala!
Tuna viongozi wabinafsi sana TZ!
 
Kina J Mhagama wanadai bado ma DED na viongozi wengine serikalini hawana V8 za kutosha!
Ukumbuke karibu watoto wote wa hawa vigogo hawatumii usafiri wa daladala!
Tuna viongozi wabinafsi sana TZ!
Na hilo ndo tatizo kubwa, kitanda usicho lalia hujui kunguni wake, hivyo hawawezi kujali hata Kidogo sana sana watajali maslahi yao tu
 
Hivi tatizo ni nini wakati shule zimetapakaa kila mahali? Au akisoma shule zilizoko mbali anakuwa na elimu bora zaidi? Mimi hata sielewi kwa kweli. Kuna shule iliyopo walking distance from home, unampeleka ya Km 30 why? Na ndio sababu kubwa ya mimba za utotoni. Makondakta na bodaboda wana take advantage ya hili gap.
 
Inasikitisha sana
Mzazi hapangi mtoto wake asome shule ya Mfano akimaliza la saba mtoto anapangiwa shule ya kwenda .Kivumbi kinakuja Kila kata Ina shule ya sekondari moja.Shule za msingi kwenye kata ziko Nne Zina wanafunzi 400 Darasa la saba .Form one sekondary ya kata uwezo wake kuchukua wanafunzi 50 waliofaulu kwenda sekondary kwenye kata 350 hao mia tatu inabidi wapangiwe shule za mbali huko za kata zingine ndio shida inaanzia hapo .Mtoto Kila siku umpe nauli ya mabasi mawili au matatu na Hela ya chakula .Ukipiga Hesabu hizo pesa na usumbufu mtoto anaopata kuanzia kuamka alfajiri sana kuwahi usafiri na kurudi usiku sana ni Bora angeenda tu shule ya Bweni ya Private

Watoto wengi wamekuwa Hadi ma matusi ya nguoni kutukana makondakta wakigoma kuwapakia wanawaporomoshea Hadi matusi nguoni wakitukana na konda anawatukana vinaanza kuwa na tabia mbovu Bado vidogo tu

Kwa kweli mzazi anatakiwa awe na huruma na mtoto na aangalie ni kumsaidia mtoto kwenye hilo
 
Hivi tatizo ni nini wakati shule zimetapakaa kila mahali? Au akisoma shule zilizoko mbali anakuwa na elimu bora zaidi? Mimi hata sielewi kwa kweli. Kuna shule iliyopo walking distance from home, unampeleka ya Km 30 why? Na ndio sababu kubwa ya mimba za utotoni. Makondakta na bodaboda wana take advantage ya hili gap.
Wewe unaishi nchi Gani mzazi Mfano sekondary mzazi hapangi hiyo shule ya secondary mtoto anayotakiwa kwenda

Angeenda ya karibu lakini Kunakuwa hakuna nafasi

Wanaopanga wanampangia ya mbali
 
Wewe unaishi nchi Gani mzazi Mfano sekondary mzazi hapangi hiyo shule ya secondary mtoto anayotakiwa kwenda

Angeenda ya karibu lakini Kunakuwa hakuna nafasi

Wanaopanga wanampangia ya mbali
Kwa iyo na shule za msingi nazo mtoto anapangiwa na serikali kwenda shule ya mbali?

Tatizo ni la wazazi kutokujali watoto wao.
Kwa mfano pale kkoo gerezeni stendi mida ya saa kumi na moja jioni utawakuta watoto wa shule ya msingi wapo wengi wanagombea kupanda gari za temeke.
 
Back
Top Bottom